Pages

Saturday, August 4, 2018


KUFANYA SHEREHE ZA MAZAO KANISANI NI KUMKUFURU MUNGU, YESU, ROHO MTAKATIFU NA MBINGU!

BWANA YESU ASIFIWE, MUNGU anayewapenda watu wake aliowaumba amenituma niwaeleze ili wale watakaopenda kusikia wapone na watakao kaza shingo watakutana naye kwa mapigo ajuavyo Yeye. Kama nilivyokwisha kusema awali, YESU alishasema watakuja waongo ili kuwapoteza hata wale wanaoenda mbinguni ili waende jehanamu pasipo kujua kwa sababu shetani na yeye anazo mbinu zake na mipango yake ya siri ambayo imefichika katika nchi zote ambapo jina la YESU na hata jina la MUNGU linakuwa likitumiwa vibaya, wakati hata MUNGU mwenyewe hasikii. Nataka muelewe unapofanya kitu ambacho MUNGU amekataa halafu mkamtaja Yeye haji na badala yake shetani ndio anakuja kwa sababu ndilo lake.

Nataka uelewe kuhusu sherehe za mavuno zinazofanyika baada ya watu kuvuna mazao yao na kwa nini sherehe hizi hazifanyiki kipindi cha masika. Katika sherehe hizi wanakuwepo pia madalali (ambao ni wazee wa kanisa). Kufanya sherehe hiyo ni dhambi kwa sababu mnamnyima mkulima uhuru wake wa kumtolea MUNGU fungu lake la kumi, na badala yake mnalinadia fungu lake la kumi. Hii haina tofauti na mfanyakazi au mfanya biashara fungu lako la kumi unalomtolea MUNGU sadaka ukalipeleka kanisani halafu akaja dalali akaanza kusema, kwa mfano umetoa 10,000 igombaniwe na atakayeibuka kwa pesa zaidi mfano hiyo 10,000 ukapanda mpaka 20,000 ikabakia hapo kanisani, hapo bado utakuwa haujamtolea MUNGU fungu la kumi.

Mkulima anavuna mazao yake na akatenga kiasi fulani ni cha MUNGU anauza na atapeleka kanisani, sasa ukipeleka hayo mazao yakafanyiwa mnada uelewe ya kwamba haukumpelekea MUNGU bali ulipeleka sokoni kwa hiyo usimdai MUNGU. Huo ndio ukweli, neno lifuatwe kama lilivyo, kanisa halipaswi kufanya mnada kwenye mafungu ya kumi ya watu, ila kama ni mpinga kristo, wao wataendelea kwa sababu hiyo ni sheria ya roho iwaongozavyo. YESU alikataa, mbona sasa inafanywa kuwa ni sherehe? Ina maana YESU anapuuzwa (Soma Marko 11:15-18). MUNGU analiangalia Neno lake, MUNGU anapaona hapo ni sokoni na siyo ibadani, bali mpinga kristo yeye anapaona ni kanisani.

Angalizo:
Jiulize tokea lini sadaka ya mtu anayemtolea MUNGU ikaletewa dalali ainadi? Pia zipo sadaka ambazo ni zakupandia kiwango au dau ambazo wanasema ni sadaka za sanduku la agano, hizo hutembezwa katika baadhi ya nyumba za watu halafu atakayetoa sadaka za kiwango au pesa nyingi kama mashindano ndiye anayepewa hicho kisanduku cha agano ila pesa yote inachukuliwa na mtumishi, huu ni wizi na ni utapeli, hata mnaotoa mjue ni kama mmetupa kwenye choo. Hizo ni mbinu za baadhi ya watumishi ambao wapo kinyang’anyi na siyo kwa mapenzi ya MUNGU, wakitumia jina lake YESU. Kwa wale ambao hawakujua, sasa mpone na uwatumie na wengine ujumbe huu au elimu hii ya kweli kwa sababu hawajui ukweli. Na sadaka hizo hutengenezewa visanduku na kila mwisho wa wiki (weekends) hukutanika kwenye nyumba za waumini wakifanya huu utapeli eti mashindano na atakayetoa kiwango cha juu zaidi yeye atabakia na sanduku la agano kama lile la wana wa Israeli na eti atafanikiwa kwa kila jambo.

NABII HEBRON WILSON KISAMO.