Pages

Tuesday, August 7, 2018


HIKI NDICHO KIPINDI ANACHOTUMIA SHETANI NA WATUMISHI WAKE KUPIMA MAENDELEO YA KIROHO YA MUUMINI AMBAYO MWISHO WAKE NI JEHANAMU

Katika nyakati hizi baadhi ya makanisa au watumishi wengi hupenda kujua taarifa za watoaji, njia zao wanazotolea na viwango vyao wanavyovitoa tofauti na Mwenyezi MUNGU anavyoelekeza, ambaye Yeye anasema kumtolea ni siri kati Yake na mtu anayemtolea.

Soma Mathayo 6: 2-4; Kwa sababu hiyo wakati unapotoa zawadi za rehema, usipige tarumbeta mbele yako, kama vile wanafiki wanavyofanya katika masinagogi na barabarani, ili watukuzwe na watu. Kwa kweli ninawaambia ninyi, Wanapata thawabu yao kwa ukamili. Lakini wewe, unapotoa zawadi za rehema, usiache mkono wako wa kushoto ujue lile ambalo mkono wako wa kuume unafanya,  ili zawadi zako za rehema zitolewe katika siri; ndipo Baba yako anayetazama akiwa mahali pa siri atakulipa.

Ni lazima ujiulize ni kwa nini watu katika baadhi ya makanisa na sehemu za ibada wanaambiwa waandike majina na kiasi walichotoa, wakati MUNGU ameeleza bayana unapomtolea iwe siri, sasa hao watumishi wanaowaeleza waumini waandike majina na kiasi walichotoa, je wao ni zaidi ya MUNGU au wao ndio wanamfundisha MUNGU njia yao wanayoitaka? Jibu analo afanyayo hayo. Mtu huyo imeivunja sheria ya MUNGU hadharani na ikawekwa sheria ya shetani ndani ya kanisa, huko ndiko kumfukuza MUNGU katika ibada. Na jambo hili limeanzishwa na baadhi ya watumishi waliotokea kuzimu au wenye asili ya uchawi ili kuibia watu pesa zao na nguvu zake siyo Roho Mtakatifu.
Cha kujiuliza, kama Kamanda mwaminifu kwa Jemedari wake ameteuliwa kufanya kazi fulani na amepewa maelekezo, Kamanda huyo mwaminifu hufanya hivyo hivyo kwa uaminifu kama alivyoelekezwa, lakini cha ajabu baadhi ya makamanda wa kanisa siyo waaminifu kwa Jemedari wao ambaye ni YESU, wengi ni waasi na wanyang’anyi kwa kutumia jina la YESU.

Mimi nimetumwa na aliyeumba kila kitu niyaseme haya na mengineyo ili ukweli ujulikane katika yeye. Hii siyo njia ya kumpima muumini kiroho kwa kuangalia vipato vyake kwa njia ya sadaka na kumpa risiti, na pale asipotoa mchungaji huangalia taarifa (report) yake na akiona anachokipata kimepungua hivyo anarudi kwenye daftari au computer zilipoandikwa taarifa (reports) za sadaka akikuta watu hawajatoa viwango vilivyozoeleka unapigiwa simu au kufuatiliwa na hatimaye utaelezwa eti roho anaumia kwa nini haumtolei, kumbe anakua ameshaangalia taarifa zako na matoleo ya jinsi hiyo. Napenda muelewe hizo zote siyo sadaka na wala hazipokelewi na MUNGU, Yeye anaangalia Neno lake, haijalishi Biblia itasomwa. Hizo siyo sadaka tena, soma Neno linaeleza bayana.

Katika hizi theolojia yapo mambo mengine ni mabaya ambayo watumishi wanafundishwa na kuyapokea ili yazidi kuwafanya waangamie wakifuata mapokeo ya wanadamu. Soma Biblia, YESU ameshatoa sheria ili ifuatwe kwa nini haifuatwi? Elewa kwamba hizo ni roho nyingine. Na sehemu nyingine ukiacha kutoa mwezi mmoja wanaangalia ripoti yako unaambiwa umezimia kiroho na usipotoa tena mwezi wa pili fungu la kumi hapo unaambiwa umekufa na sasa wewe ni maiti na watu wanaamini hayo ni kweli kwa sababu Biblia inasomwa na YESU anatajwa. Sasa pasipo kujua au kuelewa wanadanganywa na wanafanyika kama vitega uchumi vya mtumishi kwa sababu yeye anayo maagano yake ya nguvu ya kishetani hivyo ili kanisa liendelee ni lazima ijulikane na mchungaji umetoa ngapi.

Napenda muelewe hakuna mtumishi yeyote anapaswa kukufuatilia umetoa kiasi gani, sadaka ni ibada yako na ni siri yako kati yako na MUNGU tu. Ukitoa kwa jinsi hiyo bado umetupa kwa shetani na hata kama umetoa bila kuandika jina katika madhabahu hiyo bado utakuwa unampa shetani kwa sababu hiyo ni madhabahu yenye roho ya kumpinga MUNGU kwa kupindua Neno lake au kwa lugha nyingine ni madhabahu ya kumpinga MUNGU atakavyo Yeye, hivyo MUNGU hana uhusiano kabisa na sehemu hiyo. Zaidi fuatilia masomo ya Nabii Hebron katika blog yangu ufunguliwe zaidi na utakuwa huru. Sasa unafunguka, ubarikiwe na YESU.

NABII HEBRON WILSON KISAMO.