KWA
NINI WATU WANABATIZWA KWA KUTUMIA BENDERA?
BWANA YESU ASIFIWE, hapa tutajifunza siri
ya ufalme wa shetani ambayo baadhi wakristo wanabatizwa kwa kutumia bendera.
Ukisoma Biblia, ubatizo uliopo na unaotambulika ni wa Yohana tu, japo zikaja batizo
nyingine ambazo zote ni tofauti na Yohana alivyobatiza, ambazo hizi zote ni za
uongo. Ninaposema ni za uongo nataka uelewe kwamba batizo hizo ni za mapokeo ya
wanadamu. Hivyo basi yakupasa uelewe ya kwamba hata ukibatizwa kwa jinsi hiyo, bado
YESU hakutambui kama umebatizwa, haijalishi lilitumika jina lake. Soma Mathayo 15: 5-9, mnaniabudu bure, ni
wanafiki; haya maneno YESU aliyasema ili watu wajue unapofuata mapokeo, hata
uombeje ni kazi bure, hata kama umeokoka yeye hakutambui, zaidi unabakia kuwa kama
mnafiki kwake japo wewe unakua haujui ukweli; au unajijua umetekwa na shetani
au mpinga kristo pasipo kupenda au kujua.
UBATIZO
WA BENDERA (FLAG)
Huu ni ubatizo ambao umeshaingia katika
dunia hii, haujatokea mbinguni kabisa, kwanza hawatumii maji yoyote hata tone, bali
inawekwa bendera mbele yako na mchungaji
(pastor) anayekubatiza anaitwa captain. Kitu cha ajabu jiulize, YESU
hakuleta captain ndiyo liwe jina la
mchungaji, bali mchungaji ni mchungaji. Hapo tayari si sahihi (it’s wrong). Pia
nataka mjue kwamba kazi ya bendera ni kwa ajili ya ufalme wa kidunia, ndiyo hutumia
bendera kimwili, ila kiroho kanisa halipaswi kuwa na bendera yoyote ile, na
kanisa linapokuwa na bendera uwe makini sana na bendera hiyo, kwa sababu inakujulisha
ni huduma ambayo mwanzilishi wake alipewa afanye hivyo kama agano na anapoweka
bendera basi shetani anaimarisha hilo kanisa na mapepo na majeshi yake.
Sasa watu wanashindwa kuelewa na kujiuliza,
mbona Biblia inatumika na jina la YESU linatajwa mahali hapo? YESU mwenyewe
alishasema, tena watawateka hata wateule wakitumia jina langu; wateule ni watu
wanaopenda kuokoka, wengi wameshatekwa na shetani wasiende mbinguni ila
kiongozi au mwanzilishi yeye anajua anachokifanya. Mtu anapobatizwa kwa kutumia
bendera na anayeitwa captain
(mchungaji) hushika bendera na anayebatizwa hupita mbele ya bendera na kusimama
na kupiga saluti akiangalia bendera,
na mengineyo; eti hapo tayari anakuwa amebatizwa, naomba usicheke, hivi ni
vituko au masaibu ya kumchezea YESU. Inasikitisha na mimi nawaeleza kila aliyebatizwa
kwa kiapo cha bendera hataenda mbinguni bali anaenda jehanamu na zaidi
ameshajiingiza katika maagano asiyoyajua ambayo yatamtesa maisha yake kwa sababu
ametii kiapo cha miungu na miungu inakua na uhalali naye. Hivyo basi, ili upone
ubatizwe haraka ubatizo wa Yohana na achana na madhabahu hizo kabisa.
Ujumbe huu ni YESU ndiye aliyenipa ruhusa
niulete kwa mataifa yote na wewe unapoupata utume kwa wengine ili wasije
wakapelekwa jehanamu kwa sababu hata wanaobatizwa hivyo baadhi yao
wamefundishwa kuamini hivyo na wala hawajui kuwa kilicho mbeleni ni jehanamu,
na siku ile ya mwisho hakuna cha kujitetea. Toka sasa utubu, upate neema ya
kuokolewa na ujitenge na huu ubatizo, ubatizwe kama YESU kwa maji mengi
yanayotembea, zaidi soma kitabu cha “Ubatizo wa Kweli kwa Ulimwengu Wote”. Fungua
www.prophethebron.or.tz na ingia
katika blog na YouTube ujifunze mengi.
Sema; BWANA YESU, naomba unisamehe, dhambi
zangu zote nilizozitenda, unisamehe na dhambi hii ya kubatizwa kwa bendera
ambayo nimejidanganya kabisa, kwa sababu neno ubatizo ni kuzamishwa na mimi
hata sijazamishwa ninakuwa mpinzani, nilisimama kama askari akipiga saluti
pasipokujua au kwa kujua. Uandike jina langu, katika kitabu chako cha uzima wa
milele, ulitoe kabisa kweye jina la mapokeo ya wanadamu. Uniongoze nikabatizwe
kama wewe ili niwe mwanafunzi wako ambaye si mnafiki. Amen.
NABII
HEBRON.