JINSI
GANI MTU ANAWEZA KUMPA SHETANI MAISHA YAKE BILA KUJUA WALA KUPENDA?
(KWA
KUOKOKA)
BWANA YESU ASIFIWE! Nafikiri wengi
watashangaa haya ninayoyaelezea, zipo njia nyingi ambazo mwanadamu anaweza
akampa shetani maisha yake huku akijua kabisa, kwa mfano, kujiunga na freemason
na mengineyo. Ila hapa naelezea kumpa shetani maisha yako kupitia kutumia jina
la YESU. Hata YESU mwenyewe alishasema watakuja watumishi wengi wa uongo na
watatumia Jina lake kuwapoteza hata wateule. Hapa nitaelezea jambo moja, japo mengine
mengi nitaendelea kuyaelezea jinsi YESU alivyonifundisha na kunijulisha njia
zao ili niwaeleze mataifa wakapate kupona.
Njia yenyewe ni hii, shetani na yeye
anatumia neno hili hili kuwateka wateule. Wateule ni watu ambao wanapenda
kuokoka au wameokoka. Maana ya kuokoka ni kumpa YESU maisha yako awe BWANA na
mwokozi wa maisha yako, ukisoma katika kitabu cha Warumi 10: 9-10.
“9Kwa sababu, ukimkiri YESU kwa
kinywa chako ya kuwa ni BWANA, na kuamini moyoni mwako ya kuwa MUNGU alimfufua
katika wafu, utaokoka. 10Kwa maana kwa moyo mtu huamini hata kupata
haki, na kwa kinywa hukiri hata kupata wokovu.”
Sasa kupitia neno hili hili ndio njia
aliyoileta YESU kwa ajili ya mwanadamu kwa kumpa maisha yake kwa kuokoka, na
kuokoka huja kwa kikiri kwa kinywa chako yale maneno ya toba unayoongozwa na
mtumishi wa MUNGU wa kweli, ikiwa unaongozwa sala hiyo ya toba kikweli na Mtumishi
ambaye MUNGU amemchagua na anamtumia, hapo utakuwa unampa YESU maisha yako kuwa
BWANA na mwokozi wako. Ila ikiwa umeongozwa sala ya toba na mtumishi freemason
kupitia sala ile ambayo ndio kiapo, unakua umemkiri shetani, haijalishi
limetumiwa jina la YESU, kimsingi bado utakuwa haujaokoka bali utakua umeokoka
ili uende jehanamu au unakuwa umempa
shetani maisha yako, na ndio sababu Biblia inasema wengi watalia siku ile
wakisema niliokoka na atawaambia siwajui ninyi. Hii ni sababu moja wapo.
Sababu nyingine ni kuongozwa sala ya toba
na mtumishi aliyegeuza nyumba ya MUNGU ni sehemu ya biashara, anatoza watu pesa
za maombezi, kubatiza kwa kisima au kubatiza kwa maji ya kikombe au kubatiza
kwa jina la mchungaji au kubatizwa kwa bendera. Haijalishi hata ukibatizwa na
maji mengi kama YESU wakati kanisa linatoza watu pesa na kwenda kinyume na YESU
bado hao watu wote watakuwa wameunganishwa maisha yao na shetani, sababu jinsi
alivyo kuhani ndivyo muumini alivyo.
Yapo mambo mengi yaliyoingizwa katika
kanisa na wanadamu huku wakiyatoa yale au kuyapunguza yale yaliyopigwa muhuri
na MUNGU kwa sababu shetani anajua watu wanakimbilia kuokoka ili waende mbinguni.
Shetani na yeye amezaa watumishi wengi na kuwapa wokovu wa kupeleka watu
jehanamu. Asilimia kubwa ya wahubiri duniani kote wengi wametengenezwa na
waganga wa kienyeji kwa njia za masharti. Sasa jiulize toka lini Mtumishi wa
MUNGU akatengenezwa na mganga wa kienyeji? Jibu umelipata. Yamkini hata baadhi ya
mnaosoma ujumbe huu mnaenda kwa waganga, adhabu ya MUNGU inawasubiri na zile
Ole zote. Unaweza ukaongozwa sala hii na mtumishi ambaye labda hapo mwanzoni
kweli alikuwa anatumiwa na MUNGU lakini baadaye akaasi akaenda upande wa
shetani na bado anashika biblia na anahubiri sasa uelewe hiyo injili yote
anayoihubiri hata kuwaongoza watu sala za toba kwa njia hiyo anakuwa anawaunganisha
wanadamu kumpa shetani maisha yao sababu roho iliyopo ndani yake siyo ya MUNGU
ni roho nyingine itendayo kazi, kama ni hivyo basi watu wote wanaongozwa sala
hizo majina yao yanakuwa yanaandikwa
katika kitabu cha uzima na mateso ya milele na mahali jina lako lilipo ndipo
utakapoenda.
Jambo hili linauma sana na YESU akiangalia
dunia hii anajikuta hana watu wengi wanaoenda mbinguni. Aliponiita mwaka 2010
aliniambia 98% ya watu wote wapo chini ya ufalme wa shetani, ni asilimia mbili
(2%) tu ndio watu wake, sasa fikiria mikutano ya injili ilivyo mingi dunia
yote, watu wanavyookoka na wanaongozwa sala ya toba, lakini ni asilimia mbili
tu. Sasa mwenye akili na ufahamu na uelewe, uwe makini. Sio kila mtu
anayekuongoza sala ya toba atafanya jina lako liandikwe mbinguni. Hata
kibinadamu, hauwezi kwa mfano ukaenda kukata ticket ya ndege kwenye ofisi ya
baiskeli wakati wao wanahusika na baiskeli tu, hiyo ticket ukienda nayo uwanja
wa ndege (airport) watakurudisha nje kwa sababu hawamjui huyo wakala na hivyo ndivyo
ilivyo, watumishi wengi zaidi kwa kipindi hiki cha mwisho siyo mawakala wa MUNGU
na kama siyo mawakala wake basi ni mawakala feki (batili) kwa hivyo kila
utakachofundishwa ni feki (batili), hautaupata uhalisia wa MUNGU na badala yake
utakuwa mwana wa miungu. Kama ni sadaka utakuwa unawapa miungu na kukufanya
uzidi kumkosea MUNGU zaidi pasipo wewe kupenda wala kujua, ndio sababu
amenituma Nabii wake niwaeleze mambo haya ambayo najua shetani na kila roho
iliyopo ndani ya mawakala wa shetani hawafurahii bali wale mawakala wa MUNGU wanafurahi
na kumtukuza MUNGU kwa sababu wanazidi kuujua ukweli. Ukiongozwa sala ya toba
na mchungaji ambaye anadai watu pesa za kumwona ofisini, au pesa za kupangiwa
sehemu za kukaa mbele, au kutozwa pesa ili uombewe na tena unapangiwa kiasi cha
kutoa jua tayari umeunganishwa na safari ya jehanamu. Jamani mataifa, someni Biblia,
mawakala wa shetani wamejaa kila mahali. Wenye MUNGU hawatozi pesa kwa ajili ya
maombi, atakuombea bure kwa sababu juu yake ipo roho ya MUNGU ina upako wa
mafuta, ila wenye kutoza pesa juu yao ipo roho ya miungu, roho ya ulafi, wizi
na unyang’anyi, na ndiyo roho itendayo kazi ikitumia jina la YESU kuwapoteza na
kuiba mali za watu.
Hivyo basi kama una uelewa, uelewe zaidi na
upime, tokea lini roho ya giza ikampeleka mtu mbinguni? Jibu ni kwamba itakupeleka
gizani na hata sasa inabidi watu wengi waokoke upya, watafute mchungaji wa
kweli ili majina na maisha yao waliyokiri pasipokujua au kupenda walipo ongozwa
sala hizo na kumpa shetani maisha yao na miili yao itoke huko la sivyo watabakia
katika mahekalu ya mateso na shida badala ya baraka na ushindi. Na hii ndio
sababu unakuta mtu ameokoka lakini analogeka au ameporomoka maisha yake na yupo
katika wokovu.
Angalizo:
Ujumbe
huu na maneno haya aliyonieleza YESU yawasaidie mnaompenda YESU mkawekwe huru.
Ikiwa ulitubishwa sala za toba na watumishi wa jinsi hiyo uelewe hauendi
mbinguni, ticket yako ni feki. Yakupasa kutubu upya.
Sema,
BWANA YESU, naomba unisamehe, dhambi zangu zote, ukiondoa jina langu kwa
miungu, uondoe maisha yangu niliyompa shetani pasipokujua au kwa kujua
nikaongozwa sala ya toba na mtumishi ambaye wewe unamjua siyo wako akaniapisha
kiapo cha wokovu wa shetani, nayafuta maneno yote ya toba hiyo, hivyo naanza
upya mimi kwa jina langu (taja jina
lako), natubu naomba rehema, nakupenda YESU, nakukabidhi maisha yangu na
mwili wangu kuanzia sasa na milele, wewe ndiye BWANA na mwokozi wa maisha
yangu, uandike jina langu katika kitabu chako cha uzima wa milele, nikae kwako
milele. Najitenga na sala za toba za kuniteka niwe mfuasi wa shetani. Asante
YESU, Amen.
Ubarikiwe,
nakuombea kila mara ufunikwe kwa Damu ya YESU.
NABII
HEBRON.
USISAHAU KUSUBSCRIBE YOUTUBE CHANNEL
YETU YA PROPHET HEBRON KWA KUBONYEZA LINK HII https://www.youtube.com/prophethebron?sub_confirmation=1 KUTAZAMA
VIDEO ZAIDI