Pages

Friday, March 30, 2018



HAPPY PASSOVER 2018
HERI YA PASAKA 2018

Siku ya kukumbuka kufufuka kwake BWANA wetu na mwokozi wa maisha yetu kwa wanadamu wote, kwa wale ambao watamuamini na kuokoka na kuishi katika maisha matakatifu hao wataurithi ufalme wa mbinguni na siku moja atawapokea mahali pa paradiso alipo yeye. Zaidi napenda kukumbushia kwa ulimwengu wote wamrudie YESU watubu na kuokoka YESU anarudi wakati wowote na akirudi akikuta haujaokoka kwa kweli hatakuchukua utabakia katika mateso na Jehanamu sababu Jehanamu imeandaliwa kwa ajili ya shetani na malaika zake pamoja na wale wanadamu  wote ambao watakataa kuokoka, kumpokea YESU. Basi YESU aliniambia niwaeleze na yeye atawakataa siku ile mbele ya BABA yake, hivyo wakati huu ni wa neema.

Kipindi cha pasaka ni kwa ajili ya ukombozi wa wanadamu lakini cha ajabu hata binadamu hawa wengi sana hawataki wokovu wanabakia kujiita wakristo jina tu, yaani hawaokoki, hawamkiri na kufuata njia zake, watu hao jehanamu ndio sehemu yao, sasa rejea kwake ipo siku utayakumbuka maneno haya na neema itakuwa imeshapita, milango imefungwa hata ukitubu hausikiki tena.

Napenda mkumbuke kuwa pasaka haiitwi Easter haya ni makosa makubwa zaidi soma katika blog hii nimeelezea kuhusu neno Easter ni nini. Easter ni mungu wa kike aina ya sungura. Sisi wakristo hatupaswi kumsherekea yeye na katika biblia hakuna neno easter ndio pasaka bali pasaka ni pasaka na kwa kingereza ni Passover. Hata waisraeli wenyewe hawasemi Happy easter wanasema Happy Passover.

Muepuke chachu ya Mafarisayo ujumbe mkuu aliouacha YESU.

Nawatakia Pasaka njema, Happy Passover.

APOSTLE HEBRON.