Pages

Friday, March 2, 2018


JE NI SAHIHI KUABUDU KABURI LA YESU?

BWANA YESU WA NAZARETI ASIFIWE!

Swali, Je ni sahihi kuabudu kaburi la YESU, au kufanya ibada ndani ya kaburi lake? Kila mtu anajua kaburi la YESU siyo YESU, kaburi ni nyumba ya kuhifadhia mwili mpaka uoze na usionekane tena. Ninawaeleza hii ulimwengu wote kwa sababu hata YESU mwenyewe anawashangaa wanadamu hapa duniani wakiliabudu kaburi lake, wakati hilo kaburi siyo YESU. Shetani naye akiendelea kuwashtaki kila anayeenda kuabudu hapo kaburini huko Israel na kufanya ibada kama vile hilo kaburi ndiyo YESU. Mkumbuke moja ya amri kumi usiabudu chochote zaidi ya MUNGU na wala usiabudu vitu alivyoviumba, na imeandikwa MUNGU yeye siyo MUNGU wa wafu. Sasa mtu anapoimba kaburini na kutoa sadaka na kupeleka maombi yake, katika ulimwengu wa roho yapo mapepo kaburi yanameza na zaidi unakuwa unapata dhambi kwa sababu umevunja amri ya MUNGU.

Kitu kingine cha kujiuliza, je ibada ya kaburini ikoje? Jibu ni ibada ya kusindikiza mwili, sasa swali, je bado YESU anazikwa hata leo? YESU amefufuka yu hai, hivyo unayependa kujua ukweli, usifanye hivyo. Unapoenda kwenye kaburi la YESU, wewe nenda kutembea tu kwa kujifunza au kama mtalii, YESU hayupo kaburini, yupo mbinguni. Msitende tena dhambi hii, kama ulikuwa hauelewi sasa umeelewa na utubu na kuacha. Wakati mwingine nitaelezea kwa undani zaidi kuhusu kaburi la mfalme wetu BWANA YESU aliye hai. Hata kibinadamu kwa wale wanaoenda makaburini kupeleka matatizo yao katika familia pale kufanya ibada kwa yule aliyekufa awasaidie jambo fulani kwa sababu ni mzoga upo pale na mizimu. Sasa jiulize, je YESU ni mzimu au ni mzoga? Jibu hapana, YESU yupo hai wala hayupo kaburini tena, yupo mbinguni na BABA yake, yaani MUNGU. MUNGU ni MUNGU wa wenye uhai na siyo MUNGU wa wafu.

Yapo madhara makubwa na mabaya endapo utaabudu katika kaburi lolote lile likiwemo la YESU. Madhara yake ikiwemo kupata dhambi na mengineyo. Na zaidi yupo mungu aitwaye kaburi huyu ni aina ya miungu ambaye huwasaidia wanaofanya ibada za makaburi na ndiye anayekuwa kiongozi wao na kuharibu maisha ya wanadamu. Pia wapo wachungaji wengi wanaotumia nguvu za giza huongozwa pia na aina ya huyu mungu kaburi, na zaidi utashangaa utaona baadhi ya watumishi wanajijengea makaburi au minara katika nyumba zao au katika makanisa yao, na wala hakuna mtu amezikwa hapo. Sasa jiulize, kwa nini wanajenga na hata wanaweza wakasema tujenge kaburi la YESU au la mtume yeyote, mfano Daudi, Eliya na wengineo, waulize je kazi ya injili waliyotumwa ni kujenga makaburi ya watoto wa MUNGU? Hawana jibu, kazi ya makaburi hayo ni nyumba za miungu kaburi, unapoona hayo mwenye akili na aelewe na apone nafsi yake. Watu wanaoenda hapo wanamezwa katika ulimwengu wa roho na hayo makaburi, na usishangae imeandikwa kaburi limenimeza na anayeandika yupo hai. Makaburi hayo ni masharti anayopewa mtumishi ili kuwapeleka watu kwa shetani, na kwa kufanya hivyo yeye hufanikiwa hapa duniani, ila mwisho wake ni jehanamu.

Wapo wengi ambao tayari wanajijua, wote watachomwa tu kwa sababu wamekubali kuwa wakala wa shetani. Hivyo usithubutu kuomba/kufanya ibada katika hayo makaburi wala kutoa sadaka hata kupeleka mguu wako. Unapoenda kufanya ibada mahali hapo, huyo mungu kaburi anakumeza na vitu vyako vyote na unabakia na matatizo lukuki (full).

NABII HEBRON.

USISAHAU KUSUBSCRIBE YOUTUBE CHANNEL
 YETU YA PROPHET HEBRON KWA KUBONYEZA LINK HII https://www.youtube.com/prophethebron?sub_confirmation=1 KUTAZAMA

 VIDEO ZAIDI