BILA KUZIKWA NA
KUFUFUKA KWA NJIA YA UBATIZO WA MAJI MENGI; HUWEZI KUFUFUKA KAMA
YESU
Bwana YESU asifiwe, katika somo hili la
kufufuka kama YESU utasoma katika kitabu cha Warumi 6:1-6 neno linasema je damu
katika dhambi, mstari wa 4, tunapobatizwa kwa maji mengi hapo ndipo linapotokea
tendo la kuzikwa na kufufuka na YESU na ufufuko huu ninao waelezea ni kufufuka
kiroho na kimwili, unaweza ukapata ufufuko wa giza bila kujua au kupenda,
badala ya kupata ufufuko wa nuru ya kweli ambao aliuagiza MUNGU ili watu wote
ili ufuatwe na watu wote ili siku moja wamuone yeye na wafufuke na kupaa
mbinguni.
Aliponiita YESU, alinieleza na kusisisitiza
“ukafundishe kuhusu ubatizo, wa kweli kwa wote na watu wabatizwe,ili wawe watu
wangu na kwa sababu watu wengi wanao ubatizo wa giza, na wanajiita wakristo na
hawafuati njia zangu katika ubatizo wengine hawajui na wengine wanajua kabisa
kuwa wanafanya makosa na wapo upande wa mpinga kristo.
Neno linasema mkabatizwe kwa mfano wangu mimi
niliobatizwa sasa jiulize! Je ni mfano upi? Je! YESU alibatizwa ubatizo upi?
Mataifa hebu jiulizeni. YESU yeye alibatizwa katika maji yanayotembea tena ya
mtoni, ukisoma biblia hutaona kuwa kama kuna aina yeyote ya mfano wa ubatizo
ambao YESU alibatizwa nao, na MUNGU alijua kuwa neno lake litabadilishwa, na
mwanae YESU alisema watatuumia jina langu kuwapoteza hata wateule wake
kwa kufundisha mambo ya uongo, na yasiyo ya mfano wake, mimi Hebron
hapo awali kabla sijapata neema hii, nilishabatizwa kwa mfano ambao
haukuwa wa YESU, na sijui mfano huo ulitokea wapi na nilikuwa mtoto mchanga na
sikuwa na ufahamu na nilimwagiwa maji kichwani.
Ninajua kuwa watu wengi ni wasomi “maana ya Neno
Ubatizo ni Kuzamishwa” sasa inakuwaje leo unamwagiwa maji kichwani na uitwe
kuzamishwa? Hauni kuwa huo ni uongo na kama ni uongo basi unakuwa unapokea nuru
ya ufufuko wa giza, utafufuliwa na hilo giza na hatima yake unapokea nuru ya
ufufuo wa giza na giza hilo litakufufua na ila siku ya mwisho utaenda kwenye giza
la shetani kwa sababu unacho kiapo hicho. Tafuta kwenye biblia, hakuna mfano
wowote ambao ambao unaeleza ubatiizo mbadala wa ule ambao alibatizwa YESU,
hakuna. Soma 2 Wakorintho 4:2,4 jambo lingine baadhi ya watu katika Mataifa
mengine wanabatiza wakifuata madhaifu ya baadhi ya Mitume, badala ya kufuata
yale mazuri tu na hao walikuwa ni wanadamu na wapo waliokosea kama YESU
alivyotaka katiba baadhi ya Mambo, mfano: Paulo alipobatiza ndugu zake kwa
vumbi lile ni kosa, na natumaini alitubu ndio maana yuko mbinguni. MUNGU
anataka dunia yote ifuate kama vile
alivyoonyesha YESU katika ubatizo na sio kamaa mwingine yeyote, na
ndio sababu yeye YESU aliitwa njia ya kweli.
Ubatizo mwingine ambao utafanya watu wasiende
mbinguni ni ubatizo wa kisima au shimo huo bado sio ubatizo wa mfano
YESU mwana wa MUNGU, sasa cha kujiuliza je! Mnafuata ubatizo wa mfano ule ule
wa YESU au ubatizo wa mifano ambayo hajabatizwa YESU? Jibu unalo na ni
demokrasia yako ila kama ulikuwa hujui sasa
sasa uelewe na upate uponyaji. Japo upo ubatizo wa maji mengi ya mtoni lakini
kabatizwa kwa jina la YESU na la mchungaji kwa jina lake(mfano. Mchungaji
anaitwa X na muumini A, mchungaji anakubatiza “Nakubatizwa A, kwa jina la baba,
mwana na roho mtakatifu na kwa jina lake X) huo ni ubatizo wa giza , imeandikwa kwa jina
la YESU tu na sio la mtu yeyote.
Shetani aliwapofusha watu wasiielewe biblia,
na wanaofundisha hivi ni sawa na mwanafunzi anayesoma sana halafu asiielewe
anachokisoma katika kitabu, biblia watu wanazo lakini baadhi hawaelewi na
shetani na shetani anatumia njia hiyo kama mlango wa kuwafelisha Wakristo, ili
wasiende mbinguni na zaidi wapo mawakala wa shetani wakijiita kuwa ni watumishi
wa MUNGU, ila wametumwa kuiharibu hii dunia, na watu wake waangamie kwa
kulipindua neno la MUNGU, na kama Neno lilivyoandikwa
linapobadilishwa au kuongezwa, na watu tayari linakuwa sio lile alilosema
MUNGU, sasa maneno ya watu yakachanganywa na ya MUNGU, hapo ndipo
palipo haribika na mtu akiamini neno lililoharibika na yeye ndipo anapoharibika
sababu anapokea uharibifu, na analazimika au kulazimishwa kuona ndio sahihi.
Sasa ili ukamilishe mpango wako wa kufa na
kufufuka na YESU kwanza ni lazima uokoke yaani umpokee yeye awe BWANA NA
MWOKOZI WAKO na pili, ubatizwe kwa mfano wake na kuwa na uhuru, mtu mzima anayo
akili timamu; lakini mtoto mdogo mchanga yeye haelewi, hajui chochote,
ingelikuwa ni mpango wa MUNGU kuwa watoto ndio wabatizwe basi YESU
angebatizwaga na maji ya kumwagiwa kwa kikombe lakini siyo mpango wa MUNGU na
mapenzi yake Mwenyezi MUNGU, hayo ni makosa na ni dhambi na ndipo Warumi 1:7
inaongea na wewe. Mamilioni wamebatizwa kwa uongo; baadhi wakijua na baadhi
hawajui kuwa ni wa uongo, sasa hiki ni kipindi chako cha Neema, ijue kweli nayo
itakuweka huru, Fuata ubatizo wa kweli na kwa mfano ule ule ili siku ya mwisho
utafufuliwa na wewe utafufuka na utakuwa unajiunganisha na ile nguvu ya kupaa
katika unyakuo
Sasa cha ajabu shetani anajua siri hii na
kuamua kuwatumia baadhi ya watumishi kuwaongoza watu jehanamu pasipo
wao kujua, wapo Wakristo kwa kuwadanganya kama anavyofanya, kiasi
kikubwa , mtafufuka lakini hamtapaa mawinguni sasa ufanye maamuzi kuwa Mkristo
tu bila wokovu ni bure, na pili bila kubatizwa kwa maji mengi ya
mtoni bado ni kazi bure,(unapobatizwa tofauti unauchafua tu mwili wako) kama
unataka kupona fuata kama yeye njia (YESU ) ya kweli.
Kwa kweli itakuwa ni siku ya kilio kwa wengi,
kwa ambao hamtaendelea kubatizwa kama YESU, na cha ajabu ni pepo gani hilo ambalo linawafunga
watu ufahamu wasimtii YESU na kuamua kutengua njia zake? Amenituma kwa mataifa
yote, ili mbadilike, mje mbatizwe kama yeye, na sio kwa mfano wa tofauti na
yeye, ili mpone yeye anawapenda, mrejee, hiki ni kipindi cha neema(Grace
Period) itafika wakati mtatafuta neno la kweli hamtaliona, wala mafundisho ya kweli
hayataonekana, ndipo watu watakumbuka haya maneno, mda uliobakia ni mchache
sana yupo njiani anarudi, kuwachukua wale walio wake, jitahidi usiwe na shitaka
, kabatizwe sasa.
Nabii
Hebron Kisamo.