Pages

Wednesday, January 31, 2018

UKIABUDU SANAMU UNAFANANA NA SANAMU

ZABURI 115: 4-8
Shalom, katika makala hii ya somo linalohusu sanamu, nitaelezea zaidi kwanini MUNGU anasema anayezitumainia anafanana nazo.
 Kwanza sanamu ni kitu kilichotengenezwa, hakiongei, hakisikii na kama hakisikii kwanini mnakiabudu kanisani? kwanini unakiamini kikusaidie? Kama nilivyokwisha kufundisha katika masomo ya nyuma yapo mengi,  niliyowaelezea kuhusu sanamu ya kuwa hakuna faida mtu atakayoipata ambaye anayeabudu sanamu bali atapata hasara na kuhukumiwa katika ile siku ya mwisho kama hatatubu sasa na kuacha na kuokoka.
 Ninalo swali  kwa wafuasi wa BWANA YESU wa Mataifa yote , hivi YYESU ni sanamu? Jibu yeye sio sanamu, au Mariam Mama yake YESU yeye ni sanamu? Jibu ni hapana na je! wewe unoyesoma makala hii, wewe ni sanamu au mtu? Cha kujiuliza katika nchi mbalimbali zipo sanamu za aina nyingi, je! umeshawahi kuona zikiongea au kurukia au zikinusa kwa pua au zikiangalia kwa macho yake? Jibu hazina lolote. Bali nyakati hizi shetani amebuni njia nyingi za kuwapoteza hata wateule ili wasiende mbinguni, kwa kuwapofusha imani zao wasijue kuwa YESU ni MUNGU na yupo hai  na kubadilisha imani na fikra kwa mafundisho ya uongo na baadhi ya wakristo wakamfanya YESU sanamu  na YESU akafananishwa au kufanywa sanamu au kwa Kiswahili kinyago hii ni dhambi kabisa ya kumtengeneza  YESU kama sanamu au kumfananisha kama sanamu, yeye ni MUNGU hafananishwi na chochote na zaidi anaitwa mwana wa pekee wa MUNGU hakuna kama yeye duniani na mbinguni hivyo basi kile kitendo cha kuchonga sanamu na kuiita YESU ni kufuru na pia tendo la kuiabudu na hata kuitolea sadaka hiyo sanamu au  kinyago hicho ni dhambi kubwa sababu kwa njia nyingine  tayari unakuwa umevunja amri ya MUNGU, usiabudu kitu chochote wala kukisujudia alichokiumba MUNGU, wala alishokitengeneza mwanadamu au shetani. Huu ni upofu ulioletwa na mpinga kristo ili kuwaangamiza watu sasa unapoiabudu sanamu unafanana nayo katika ulimwengu wa roho  na  hata kimwili  na kufanya usionekane na MUNGU  na zaidi ulishafanana na kinyago  au sanamu  kwa sababu Mbinguni wataenda wale wanaofanana  na MUNGU, kwa mfano wake ila aliyefanana na sanamu hatakwenda yeye ataenda kwa muasisi wa sanamu ambaye ni shetani.
 Hivyo nilipokuwa naelezwa na YESU habari hizi ili niwaeleze na kuwafundisha watu wote ili mpate kupona kwa wale ambao watahitaji kwenda mbinguni waachane na sanamu na kufanya ibada za sanamu, kwasababu hata wanaotumia sanamu katika ibada zao wanafana  na sanamu na  hazifanani na ibada za MUNGU Mtakatifu  hata kama jina lake linatajwa YESU alishasema wengi watapotezwa kwa kutumia jina lake na waongo au mpinga kristo yamkini wajijua au hawajijui.
Akawaonyesha ulimwengu wote ndio maana mnaona kuwa ni watu wachache waliookoka ndio wanafanana na MUNGU na watu wengi ambao  idadi yao kubwa hawafanani na MUNGU katika ulimwengu wa roho na sura zao zinakuwa sanamu.
 Hivyo akaniambia Hebron waeleze maana idadi kubwa hawajui madhara yake waeleze wanifuate mimi “YESU” na wanajiita kwa jina langu halafu hawaokoki, kila mtu anayenipenda aokoke, anipokee, niwe Mwokozi wake, mimi YESU ni Mwokoziz kila mtu anipendaye aupokee Wokovu wa kweli  na aishi katika utakatifu, akaniambia narudi kulichukua kanisa na kanisa ni watu sio dini au dhehebu, mimi ni wa watu wote, wakinipokea watafanana na mimi na wasiponipokea  hata nikija sitawachukua  sababu hawafanani na mimi. Akaniambia wengi hawajielewi na nimekutuma  usipunguze wala kuongeza neno langu  sema kwa  dunia yote waeleze wote wanirejee watubu. Na hata waliopo katika sanamu (madhabahu za sanamu/ Zenye sanamu)  wasibutu kwangu wakiwa huko (Kwenye sanamu) maana mimi sipo huko kabisa wala sifanani na sanamu wala msalaba.
Na zaidi  unapoiabudu au hata kubusu sanamu au kuufuata au kuweka msalaba kwako au hata kanisani, tayari huyo MUNGU aliyeumba vitu vyote anakuwa siyo MUNGU wako, kwa sababu tayari wewe unaabudu sanamu  na unaongozwa na mungu sanamu haijalishi kuwa unasoma biblia na unasheherekea krismas na pasaka au unatoa sadaka. Zote hizo unakuwa kwenye ufalme wa mungu sanamu  na kuwafanya watu kushikiliwa na mungu sanamu,  kwa kujua na kutokujua, na zaidi hata mafundisho ya mila,ibada ya wafu  zote hizo ni huwa chini ya miungu na siyo MUNGU, Tubu mrejee YESU, uokoke na wewe uweze  kufanana na YESU na siyo sanamu .


Imeandikwa na Nabii Hebron Wilson Kisamo.


USISAHAU KUSUBSCRIBE YOUTUBE CHANNEL
 YETU YA PROPHET HEBRON KWA KUBONYEZA LINK HII https://www.youtube.com/prophethebron?sub_confirmation=1 KUTAZAMA

 VIDEO ZAIDI