Pages

Monday, January 1, 2018

UNABII WA NCHI YA TANZANIA NA DUNIA ITAKAVYOKUWA 2018

BWANA YESU ASIFIWE, Mfalme wa wafalme, Mwana wa pekee wa MUNGU aliye hai. Napenda kuwajulisha watu wote wa mataifa yote yale niliyoelezwa na MUNGU kwa mwaka 2018 kuhusu nchi ya Tanzania katika baadhi ya maeneo ambayo niliyoruhusiwa kuyasema na mengine ni ya kwangu. Napenda mtambue kuwa MUNGU ameiandaa Tanzania kama ndiyo nchi yake ambayo hata ile siku ya mwisho mwanae atashukia katika anga la Tanzania katika unyakuo, na pia ndiyo Edeni ya sasa.

Ukirejea katika makala ya blog ya Nabii Hebron kupitia tovuti (websitewww.prophethebron.or.tz kuanzia mwaka 2014 na 2015, kuhusu unabii alionieleza MUNGU umetimia, kuanzia kumpata rais huyu wa sasa ambaye MUNGU alimficha na hakujulikana wala kutazamiwa, kuhusu shirika la ndege kuinuliwa, kuhusu bandari, kuhusu mgodi wa Tanzanite kurejeshwa kutoka AFGEM na kupewa watanzania, kuhusu uchumi kuinuliwa juu, kuhusu usalama wa jeshi la nchi kuwa bora na mengine mengi aidha uliyasoma au utayasoma na yametokea. Na mwaka huu 2018 yapo mambo mengi ambayo MUNGU atafanya njia kwa kuwatumia watu wake waaminifu.


1.     UCHUMI WA TANZANIA

·        Uchumi wa nchi ya Tanzania MUNGU ataunyanyua mpaka utakuwa ni uchumi namba moja katika bara la Afrika, myaonapo hayo mtukuzeni MUNGU na yeye tayari yupo kazini.

·        Kuna wizi mkubwa sana ambao haujawahi kufichuliwa aidha na watanzania au serikali tokea nchi hii ipate uhuru, ni mali ya Tanzania iliyofichwa na baadhi ya watu, wengine wapo hapa Tanzania na wengine wapo nje ya nchi hii, ni vitu vyenye thamani ya pesa nyingi ya ajabu. MUNGU atawafichua.

·        Pesa nyingi za nchi zilizoibiwa zitarejeshwa.

·        Kuhusu viwanja vya ndege nilishaeleza 2013/2014, bado kasi itaendelea zaidi wala hakuna atakayeweza kuzuia au kukwamisha, jicho la MUNGU lipo hapo.

·        Kuhusu madini ya Tanzanite: Madini ya Tanzanite yatapotea katika nchi za nje na hivyo watakuja wenyewe kununua hapa nchini.


2.     MUUNGANO WA TANZANIA

Tanzania itabakia kuitwa Tanzania tu milele yote. Mimi Hebron tokea MUNGU aniite na nimfahamu, nilipokuwa naongea naye hajawahi kuniambia omba kwa ajili ya Tanganyika au nimekuita unitumikie katika nchi ya Tanganyika. Nilishasema muungano hautavunjika kamwe, hiyo ni sauti ya MUNGU na ni mpango wa MUNGU, na katika upande wa Zanzibar patatokea soko kama lile la Dubai au China, nilishaelezea, hii yote ni MUNGU anatengeneza nchi yake iwe Eden kwa ajili ya utukufu wake. Upo usemi usemao, watu ni sauti ya MUNGU, mimi napenda kuwaeleza, siyo kila usemi au sauti za watu ni sauti za MUNGU, sauti nyingine ni sauti za shetani.

Kama wewe ni msoma Biblia mzuri, YESU alipokuwa anasulubishwa katika nchi ya uyahudi zaidi ya miaka 2018 iliyopita je wale watu waliokuwa wanasema asulubishwe tena ni wengi je zile sauti zilikuwa ni za MUNGU au sauti za shetani? Jibu ni kwamba zile zilikua ni sauti za shetani. Hata hapa Tanzania sauti hizo za shetani zitaendelea kusikika ila hazitafanya kitu, sababu shetani yeye hapendi mpango wa MUNGU utimie Tanzania, ila utaona, itatimia tu.

Nataka muelewe ya kwamba, siyo watumishi wote ni wa YESU, haijalishi hata wakisema amewaita wengi, wao ni waongo na ni mawakala (agents) wa shetani ila MUNGU ameshawazimisha, na wale wa MUNGU wa kweli wataendelea kudumu na hawataporomoka. Wapo walioitwa hapo mwanzoni lakini baadaye wakamkataa YESU, wakajiunga na miungu na freemason.

3.     KUHUSU NGOs

Baadhi za NGOs (taasisi zisizo za kiserikali) zilizopo hapa Tanzania siyo za mpango wa kunufaisha watanzania bali zimefunguliwa na baadhi ya watanzania kwa ajili ya kujifaidisha kwa kutumia watanzania, zitafungwa.

4.     KUHUSU WATUMISHI WASIO WAAMINIFU

Watumishi ambao watakuwa wezi na wengine wasio waaminifu au kujipatia nafasi hizo kwa njia ya nguvu za giza watashangaa wanaachishwa kazi tu, kwa sababu MUNGU anataka aitengeneze nchi, na yeye hafanyi kazi na mchawi, kwa sababu mchawi yupo katika ufalme mwingine, labda mtu huyo atubu na aache.

5.     KUHUSU WANACHAMA WA FREEMASON

Wanachama wa freemason, katika mwaka 2018, japo siyo rahisi kujulikana na wengi ni watu matajiri na maarufu, wengi watakufa, ku paralyze na wasiamke tena, hili litafanyika katika dunia.

6.     KUHUSU UMOJA WA MATAIFA

Katika Umoja wa Mataifa kutakuwa na mpasuko mkubwa katika yale mataifa kiongozi, na baadhi ya nchi zitavunja uhusiano na nchi nyingine, na pia maafa makubwa zaidi yatatokea katika dunia ambayo haijawahi kutokea, yatakuwa ni ya aina yake ajuavyo MUNGU, mimi naleta taarifa tu.

7.     MBUGA YA LOLIONDO

Mbuga ya Loliondo itarudishwa katika mikono ya nchi ya Tanzania.

8.     KUHUSU WANAO ITAKIA TANZANIA MABAYA

Wapo ambao wanaitakia nchi ya Tanzania mabaya, MUNGU atawazimisha kama mshumaa. Nikimaanisha kwanza wale wanao watakia mabaya viongozi, watu aliowaweka MUNGU, hao ni watumishi wake, ikiwemo kiongozi wa nchi hii. Asifanyiwe mabaya, mtapigwa na MUNGU, na wapo wengine tayari wameshapigwa na MUNGU japo hawaelewi. Yeye ameteuliwa na MUNGU, ni mtu wa MUNGU, anaongozwa na MUNGU ili aijenge nchi hii kwa utukufu wa MUNGU, haijalishi anajijua au halijui hilo.



9.     KUHUSU UCHAGUZI WOWOTE

Hapa namaanisha kuanzia hata chaguzi za ubalozi wa mtaa, katika sector binafsi, serikalini, katika vyama vya siasa hata vyama vya mpira, vyama vya wafanya kazi, wakulima, na wengineo. Alichoniambia MUNGU, “sipendi wizi wa kura, Mimi ni MUNGU mwenye haki natenda haki. Waeleze wasiibe kura kwa mtu yeyote ili apate nafasi ya uongozi kwa ajili ya kuwaongoza watanzania. Mimi MUNGU nitamnyima amani mtu huyo atakayeiba kura au kununua ushindi, hata pata amani katika maisha yake, pili mauti itamfuata ili aondoke nimweke mtu aliyepata kwa uhalali, ili niweze kumtumia kuongoza watanzania”. Yatakapomtokea mtu asishangae na msione ni mzaha ndivyo ilivyo na haibadiliki.

ANGALIZO:
Yapo mengi ila nitayatoa wakati atakaponiruhusu MUNGU mwenyewe kwa wakati wake na sehemu husika.

MUNGU IBARIKI TANZANIA.


NABII HEBRON.