Pages

Thursday, March 15, 2018


KILA MTU ANAYETAKA KWENDA MBINGUNI NI LAZIMA AOKOKE

BWANA YESU ASIFIWE, watu wote wa mataifa yote ambao mliumbwa kwa mapenzi ya MUNGU na kwa mapenzi yake ili siku moja mfike tena mbinguni mahali ambapo ndipo penye makao mazuri ya milele. Ili ufike mbinguni sharti ni moja tu UOKOKE na umpokee BWANA YESU, uishi maisha matakatifu na kufuata sheria zake na Neno kama lilivyo katika kweli na siyo lipunguzwe au kuongezwa mapokeo ya wanadamu au shetani.

YESU anapenda muelewe ukweli kwa sababu wengi mnampenda sana ila mpo katika njia ya upotevu mkifikiri mpo na yeye kumbe mpo na mpinga kristo au shetani. Anasema Yeye ndiye njia ya kweli, na Yeye ni wokovu na ili umpate yeye sharti uokoke kwanza ndio upate tiketi ya mbinguni, cha ajabu watu wengi hawana tiketi hiyo wanabakia kuwashangaa wenye tiketi ya mbinguni huku wakipumbazwa na wasiokoke na kudhani wataenda mbinguni wakati hawaendi. Sisi hapa duniani tuliookoka ni wapitaji, kwetu ni mbinguni bali kama haujaokoka, wewe umekuwa ni mkaaji wa hapa hapa, atakapokuja YESU kulinyakua kanisa mtabakia hapa hapa na shetani na mtachomwa moto. Hivyo basi nyakati hizi ni za hatari sana shetani anawazuia wanadamu wasikate tiketi za wokovu yaani wasiokoke na wengine waliookoka wanarudisha tiketi za mbinguni wanarudia tiketi za hapa hapa ulimwenguni na kuachwa na YESU.

Mara nyingi ninapoongea na YESU anakuwa na huzuni jinsi ulimwengu unavyopotezwa na mpinga kristo na watumishi wenye maagano na shetani ya kuwaangamiza watu wa MUNGU kwa kuwaweka katika njia ya uongo katika ulimwengu wa roho na mwili. Ndio sababu baadhi ya wakristo hawataki kuokoka kabisa au kwa lugha nyingine hawataki kwenda mbinguni pasipo kujua na wengine wakijua. Sasa mkristo bila wokovu bado unayo hasara, unakuwa bado haujaupata tiketi ya mbinguni, kwa sababu mwokozi YEYE alikuja kutuokoa kwa yule atakayependa, hakuja kusema tuwe wafuasi wake na tusiokoke, hapana. Hili linakupa picha ya kweli kwamba wakristo wengi zaidi hawajampokea YESU bali hao wanakua ni wakristo ambao hawataki kwenda mbinguni.

JINSI YA KUJIJUA HAUENDI MBINGUNI
1.     Haujaokoka mpaka sasa au uliokoka na ukauacha wokovu;

2.     Umeokoka ila matendo yako ni ya dhambi bado;

3.     Umeokoka halafu hautaki kubatizwa kwa maji mengi ya mtoni yanayotembea;

4.     Umeokoka lakini umebatizwa kwa jina la Mchungaji au umebatizwa kwa ubatizo wa maji ya kisima.
Na mengine mengi soma vitabu vya mafundisho ya Nabii Hebron na makala zaidi za YouTube, utajifunza mengi na utakuwa huru zaidi.

Angalizo:
Katika ule mwisho wa dunia, YESU ndiye Mtume na Nabii wa MUNGU pekee ambaye ndiye aliyechaguliwa kwa ajili ya kuwakomboa wanadamu wote kwa rangi zao na kwa sura zao, hata manabii wote waliopita hawakupewa kibali hicho cha kufanyika wokovu na kukupeleka mbinguni. Siku ile ataangalia aliyemkubali wakati huu na ndiye atakayemchukua aende katika makao aliyoyaandaa kwa ajili ya waliookoka tu na siyo kwa ajili ya watu ambao hawajaokoka. Dini nyingine wanamuita Nabii Issa.

YESU ameniambia niwaeleze anawapenda sana na ili mpone na Jehanamu sharti lazima kuokoka sasa hivi na siyo ile siku ya mwisho akija ndio watu waseme YESU nakuhitaji uniokoe, atakuambia sikujui sikujui na ndipo litatimia lile Neno “nitawaambia sikujui sikujui” soma Mathayo 7:22-24 na kuendelea. Sasa je na wewe ni mmoja wao? Jipime kwa ujumbe huu ndani ya moyo wako, ufanye maamuzi sasa na uokoke kikweli na siyo uwachukie wanaookoka. Tazama kipindi cha Nuhu akijenga Safina walimcheka. Na wewe uewacheka wangapi waliookoka? Tubu na uokoke, gharika inakuja itakuangamiza,. Usidanganyike na neno wanalosema hakuna wokovu hapa duniani ni mpaka ufe, hilo ni pepo lipo ndani ya mtu likipinga watu wasiende mbinguni, ukifa kama haujaokoka uelewe unayo tiketi ya jehanamu, na usidanganyike utaombewa toba uende, kumbuka unapewa muda ukiwa na uhai na akili timamu ili utengeneze na MUNGU, uokoke tu na siyo kingine.

MUNGU siyo MUNGU wa mizoga, haongei na mizoga. Mizoga inakuwa tayari inanuka, imeharibika haina uhai, na wala mtu hayupo tena katika ule mwili huu ni uongo mkatae kabisa. Maneno haya yananirudia sana, hivyo ni lazima niyaseme ili nipate amani ya MUNGU na wengi mtapona msiyoijua siri hii. YESU hana dini yeye ni wa watu wote, anawahitaji mumfuate YEYE umkiri kama BWANA na MWOKOZI wako kuanzia sasa. Si dini, wala dhehebu, wala utajiri, wala umaarufu, wala jeti au ndege haikupeleki mbinguni ila ni YESU tu. Basi sasa muelewe hakuna chochote wala binadamu yeyote au Nabii au Mtume aliyeteuliwa na MUNGU aliyekuumba wewe, ufanye wepesi utii ili usiangamie.

Sema, BWANA YESU naomba unisamehe dhambi zangu zote, uniokoe, uniandike jina langu kwenye kitabu chako cha uzima wa milele kuanzia sasa wewe ndiye Bwana na Mwokozi wangu, uniongoze milele. Amen.

NABII HEBRON.