Pages

Wednesday, November 15, 2017

Mungu REHEMA
(Hili ni pepo)

Mungu Rehema ni aina ya miungu, yeye hukaa na kuishi katika makanisa ambayo yanaongozwa na miungu ya kikristo. Mahali ambapo hapana kweli ya MUNGU au mahali ambapo NENO la MUNGU limechanganywa na uongo ila Biblia husomwa kama kawaida kabisa. 

Kazi ya huyu mungu rehema ni kupumbaza watu pale wanapoomba toba na msamaha, ambapo watu huamini wamesamehewa dhambi zao. Cha ajabu utakuta mtu ni mkristo, hataki kuokoka bali anataka asamehewe dhambi zake, halafu huyo huyo ambaye hajaokoka anaomba asamehewe dhambi zake na anaamini kabisa amesamehewa na MUNGU, wakati hajasamehewa dhambi yeyote ile.  Biblia inasema TUBU na UOKOKE hapo ndipo utasamehewa dhambi zako, yaani uache uovu. Siyo kujiita mkristo wa uongo, nikimaanisha haujasamehewa dhambi, bado unakua ni mkristo mwenye dhambi, unakua unapumbazwa na huyo mungu rehema, cha ajabu utasikia mtu huyo huyo anaenda kanisani anasema naenda kupunguza dhambi wakati hajaokoka, sasa anazipunguzia wapi? 

Mtu huyo anakuwa amepumbazwa na huyo mungu aina ya rehema ya kishetani, asiyetaka mtu aokoke kwa sababu anajua akiokoka na kutubu hatampata tena. Hivyo, mkristo au mtu yeyote, kwa imani yeyote ile, ili usamehewe dhambi zako ni mpaka uokoke. MUNGU hafanyi kazi ya ujinga, eti watu hawataki kuokoka halafu wanataka wasamehewe dhambi zao, wakati MUNGU ameshatuwekea namna ya kutubu na kusamehewa dhambi kupitia YESU, ni lazima uokoke, umkiri ndipo utasamehewa.

Watu wengi wanakufa bila kuokoka, nataka muelewe kwamba hao wanasubiri hukumu, na hata wewe ambaye unamkataa YESU sasa, halafu unadanganywa ukifa utaombewa ili upokelewe, nakueleza hapo unadanganywa, wakati wako ni sasa, tubu ukiwa hai na ukiwa na akili zako timamu, siyo ukiwa mzoga au maiti. MUNGU ni wa watu wenye uhai na siyo MUNGU wa watu waliokufa au maiti. Maiti haiongei. Yakupasa ukiwa una uhai, unaongea na una akili ya kutubu, utubu sasa na uokoke na kuacha dhambi kabisa. Jitenge na huyu mungu rehema, anawapumbaza watu wengi na makanisa mengi na watumishi wengi katika dunia yote, ila sasa awaachie. 

YESU amenituma niwaeleze na kuwafundisha mataifa KWELI YAKE ili waokoke, usirudi tena kwa huyo mungu rehema, atakuangamiza kiroho. Huyu ni aina ya miungu anayevuvia fahamu za wanadamu ili wazubae na wasitubu ili atakapokuja YESU kulinyakua kanisa awakute bado wakristo wapo katika milki ya shetani na ni mali ya shetani, shetani anakuwa anao uhalali kabisa na watu hao. Sasa ili umnyime shetani uhalali wa maisha yako na nafsi yako, tubu na uokoke. Ukiwa haujatubu na haujaokoka unakuwa ni mali ya shetani kabisa, kwa kujua au kutokujua. UKWELI umeujua sasa.

NABII HEBRON