Pages

Saturday, November 11, 2017

MAMBO MANNE YA KUJIULIZA KABLA YA KWENDA KANISANI AU KWENYE MAOMBEZI YEYOTE.

BWANA YESU ASIFIWE! Mambo haya ni kwa ajili ya usalama wako wa kiroho, sasa hivi ulimwengu umebadilika, unaweza ukafikiria utaupata msaada wa MUNGU katika kanisa unaloenda au katika maombezi na badala yake unakutana na shetani ndiye umeenda kumwona yeye.

1.     Angalia huyo mtumishi je ni MUNGU ndiye yupo nae au huyo ni mganga anayetumia biblia akijipa cheo cha uchungaji au mwinjilisti akitumia nguvu za giza, watu wengi wanakataa mambo ya ushirikina wameamua kumrudia MUNGU lakini hata sehemu baadhi wanazosikia jina la YESU likitajwa wakienda wanamkuta pastor ni mganga wa kienyeji nikimaanisha amejenga kanisa kwa nguvu za uchawi, na anasaidiwa na nguvu za uchawi yeye anaishi kwa maagano, wapo wanaotoa sadaka za damu kwa shetani na wachawi.

2.     Ikiwa unaenda kukutana na MUNGU hautachajiwa pesa yeyote na utapokea uponyaji wako na ukiwa unaenda kwa mganga ni lazima utachajiwa pesa, hata za kuonana na mtumishi uongee na yeye na mengineyo yasiyompendeza MUNGU asiyoyataka utafanyika kama vile mganga afanyavyo masharti masharti MUNGU yeye njia zake ni salama.

3.     Jambo la tatu unaenda kulishwa chakula cha kiroho kilicho salama au sicho salama. Chakula cha roho kilicho salama kwa roho ya watu ni neno la kweli ambalo halijachanganywa na uongo. Mfano wengine ni kweli mnafundishwa lakini hakuna kuokoka au umebatizwa ubatizo wa uongo wa kikombe, wa kisima, jina la mchungaji, zote hizo hata kama hapo ya kweli bado uelewe unalishwa chakula cha kiroho cha shetani sababu kiapo cha agano la mtu na MUNGU ni ubatizo uliootoka mbinguni kama alivyobatizwa YESU na ndio huo upo kwenye biblia. Ufunuo 22:18-19 inaonyesha wazi hauna sehemu yako mbinguni, sasa umeshajua ukweli ni bora uitafute nafasi yako sasa ya mbinguni ubatizwe kwa  maji mengi (Soma kitabu cha ubatizo wa kweli kwa ulimwengu wote kilichoandikwa na Nabii Hebron), na jambo ambalo YESU analiangalia ili uwe umetimiza haja yake uende na yeye ni uokoke umkiri yeye, na siyo uwe mkristo lakini hautaki kuokoka iwe ni mtumishi au muumini kama haujaokoka na kubatizwa kama YESU bado haujawa mwanafunzi wake bali ni mwanafunzi feki; yeye hana feki huo ni mchomeko wa shetani kukupotezea muda na kukupumbaza ili uje uchomwe moto na yeye. Yapo na mengineyo, usome kitabu Mkristo usikubali kuwa mpumbavu lipo katika blog.

4.     Jambo la nne je utakutana na chakula cha kiroho salama, ikiwa mchungaji mwenyewe anaye MUNGU anafundisha kweli na hachanganyi na uongo, hakuna michango siyo sokoni, watu wote ni sawa, hakuna kulipia kanisa madeni ya benki, kuwasoma majina waliotoa pesa nyingi hayo yasiwepo, ubatizo uwe kama wa YESU ulivyo na siyo mwingine, roho mtakatifu atawale au YESU mwenyewe ndio kiongozi wa kanisa hilo hapo utakuwa upo salama. Hivyo wengi wakienda hukutana na kuwekewa appointment na waganga wanaotumia biblia wakifikiri wana nguvu za YESU, madhara yake yule pepo aliyopo ndani yake huiba vitu vyako na kukufanya kuteseka na ndio sababu wewe chunguza watu wengi wanapoenda kwenye maombezi huchoka maisha yao kimwili na kiroho, sababu hawajaenda kukutana na YESU bali wanakutana na mganga wa kienyeji, na wachungaji wengi sana ni wateja maarufu na waganga wa kienyeji, kama unabisha tafuta mganga  wa kienyeji atakueleza. Watu wanakuwa wanaongozwa na waganga na jinsi alivyo kuhani wa kondoo hufanana nao kiroho. Ukiyajua hayo baadhi yatakusaidia na utafunguka kabisa, sababu hizo ni kamba za kiroho.


NABII HEBRON.