JE
NI KWA NINI UNAPOACHA UOVU BAADHI YA WATU WANAKUDHARAU?
Napenda kuwatia moyo watu wote mnaompenda
YESU na mmeamua kuokoka, songa mbele katika utakatifu na kukaa katika sheria
zake MUNGU. Hili si jambo geni, naishangaa dunia hii pamoja na watu wake na wewe
pia msomaji wa Blog hii ya Nabii Hebron
nadhani unashangaa. Tukianzia kwa kuhani wetu mkuu YESU, yeye alichukiwa na
wale ambao walikuwa hawataki mazuri bali wanapenda uovu udumu katika maisha yao
na akapendwa na watu waliopenda mema. Sasa hivi kanisa lina matabaka mengi ila
nitaongelea matabaka matatu:
1.
Wapo wanaofurahi mtu anapoacha uovu akaokoka;
2.
Lipo kanisa ambalo linafurahia uovu halitaki
watu waache dhambi na wampokee YESU linapenda watu waendelee na matendo maovu,
hili siyo kanisa lenye kumpenda YESU ni kanisa lenye mfumo wa mpinga kristo.
3.
Lipo kanisa ambalo halitaki watumishi waseme
kweli ya Neno la MUNGU kama lilivyo na ukisema ukweli wanakuchukia kwa sababu
ndani yao ipo hiyo roho ya muovu na siyo Roho Mtakatifu katika mioyo yao,
limtokalo mtu ndilo lililomjaa mtu katika moyo wake ikiwemo mafundisho ya uongo,
ujue roho wa uongo ndie amejaa ndani yake.
Sasa cha kujiuliza ndugu msomaji na mtoto
wa MUNGU, kwa nini unapoamua kuacha uovu, badala ya jamii ya kikristo kufurahia,
wanaanza kukusema, watakudharau, na hata mara nyingine kukutemea mate kwa sababu
umekataa uovu. Nataka uelewe kwamba ipo roho ya uovu ndani ya hao wanaokuchukia
kwa sababu umekata mawasiliano na ushirika na hizo roho, hivyo wewe siyo
mwenzao na hizo roho zinaona moto na Roho Mtakatifu ndani yako, wewe usisubiri
kutiwa moyo na dunia, BWANA YESU atakukumbatia ile siku ya mwisho na kuvikwa
taji lako kwa jina lako endapo utashinda uovu. Tambua siyo kwa kuokoka tu ndio
kwenda mbinguni, uokoke na matendo yako yawe mema.
Wapo walioacha uzinzi, ulevi, umalaya;
utaona marafiki wanawasema vibaya, sasa ninachotaka kuuliza, je mbele za watu
wote ni bora kutenda mema au mabaya? Sasa mtu unapoamua kwenda kwa MUNGU mbona
watu wengi wanawacheka? Je mbona mtu akiwa mchawi, mlevi, mzinzi na mengineyo anaonekana
anafaa sana na baadhi ya watu. Hii inaonyesha kuwa idadi kubwa ya watu ipo kwa
shetani, kuanzia kanisa mpaka kwa watu. Baadhi yao wapo upande wa shetani na hawapendi
utakatifu kabisa. Hata katika baadhi ya makanisa ukiokoka wanakutenga, wala usishangae
ni lazima wakutenge kwa sababu wapo katika njia ya uovu ambayo wewe umeikataa
katika imani, umeitaka njia takatifu, hivyo hiyo roho haiwezi kukutaka kwa sababu
umekuwa ni moto katika roho na siyo giza.
Nawatia moyo muokoke msiogope kuchukiwa,
mbele yako yapo maisha mazuri ya milele na ya kifalme na hao wanaong’ang’ania
uovu na kusema eti uovu ni mtindo (fashion).
Unapotenda uovu na kumkataa YESU, na yeye atakukataa, wakati ni sasa, okoka.
Sema, BWANA YESU, naomba unisamehe dhambi
zangu zote, ulifute jina langu kwenye kitabu cha hukumu na kuliandika katika
kitabu chako cha uzima wa milele, mimi sitaki tena maisha ya uovu, nisaidie
niweze kuishi maisha matakatifu yanayokupendeza wewe na ule mwisho nivikwe taji
la milele, Amen.
Wanaokucheka ipo siku watalia na kusaga meno
katika moto wa milele, wewe tengeneza maisha yako sasa.
NABII
HEBRON.