Pages

Tuesday, November 7, 2017

JE MUNGU ANAPOKEA SADAKA ZA KUDAIWA KWA KUFUATWA MPAKA NYUMBANI NA KUKUSANYWA NA WAZEE WA KANISA?

BWANA YESU ASIFIWE, Watu wote wa mataifa yote mnaompenda YESU na kulitetea Neno lake na Jina lake. Hapa ninaongelea  sadaka ambazo hazitolewi kanisani na badala yake uongozi wa kanisa unakuwa na orodha ya majina ya waumini wake wanaofuatiliwa mtaa kwa mtaa au mji kwa mji. Ukisoma katika Mathayo 6:4, inaelezea jinsi ya kumtolea MUNGU sadaka, SADAKA iwe ni siri yako wewe na MUNGU na wala asijue mtu mwingine kuwa umemtolea nini MUNGU ibada yako.

Jambo la kwanza, hao wanaotumwa katika nyumba za waumini kuchukua sadaka kwa lazima kwa kutishiwa usipotoa hiyo fedha siku unapopata tatizo kanisa halitahusika na wewe, nataka mfunguke akili na ufahamu wenu, ndiyo maana hata Timotheo akasema ni nani aliyewaloga nyie Waebrania hata mdanganyike na mkasahau Neno linavyosema. Nikuulize swali, je sadaka hutolewa kanisani au nyumbani kwako? Jibu ni kanisani na je ni wapi Katiba ya MUNGU inaruhusu kuandika majina ya waumini na baadae akishalipa kuandika kiasi alichopangiwa na binadamu? Nasema huyo siyo MUNGU bali ni binadamu. Swali linguine, jiulize wewe unamtolea MUNGU sadaka au unamtolea binadamu? Kwa sababu mwanadamu anaweka kumbukumbu (records) zako za mapato yako ili siku ukifariki ndio ile pesa uliyolipa kwake huyo mungu binadamu na watu wake waje wakuzike.

Nilipokuwa naongea na YESU nilisikia sauti Yake akihuzunika sana juu ya wizi na unyang’anyi huu. Watu wanafikiri wanamtolea YESU, kumbe ni mapepo ya kamari, haijalishi limetjwa Jina lake. akaniambia hao ni wanyang’anyi na hao wote iwe ni wazee wa kanisa, mwinjilisti, askofu, nabii na wengineo wote, sehemu yao ni katika ziwa  la moto na huo ndio ukweli na mie sipunguzi wala siongezi.
Ujumbe huu ni wa kwako wewe popote ulipo, YESU akaniambia, “wanajipangia pesa zao na kuwapangia waumini jinsi ya kuwalipia madeni yao”, akaniambia, “waeleze mimi sipo kabisa katika madhabahu hizo, haijalishi wanalitaja Jina langu, nilishasema watakuja na watatumia Jina langu na nyie ni mashahidi mnayaona ni wizi wa kitalaam kupitia shetani tena zaidi wanawafuata watu majumbani kwao nyakati za saa 11 alfajiri, kabla hawajafungua milango wao wapo nje na msalaba wa mti wakiutumia kana kwamba ni YESU wakati ni mbao tu tena ya Cyprus, na watu huogopa na kutoa pesa wakielezwa ni YESU”.

Amenituma niwaeleze, YESU hajawatuma na wala hatakaa awatume, tazama hata Mathayo alikuwa mtoza ushuru, akamwambia “acha nifuate mimi ukanitumikie” sasa hamuoni ni ajabu baadhi ya makanisa ya leo yamejengwa na pepo Mathayo, yanatumia jina la YESU kuwaibia watu pesa na mali zao na wengine kwa njia ya kuchezesha kamari makanisani. YESU hachezi kamari kabisa.

Sadaka inatakiwa itolewe kanisani kwa kuamua katika moyo wako mwenyewe, tena kwa kumtolea MUNGU kwa furaha, kwa sababu ile ni ibada kati yako wewe na MUNGU, ikiwa inafuatiliwa na watumishi au wazee wa kanisa katika nyumba zenu wakidai tumekuja kuchukua pesa ya BWANA wewe usiwape, tena uwaeleze kuwa unatoa kanisani, na ukristo wako wasiufanye kama mdaiwa sugu, kwa MUNGU hakuna mambo hayo, waeleze tafadhali ondokeni kwangu katika jina la YESU, waeleze sadaka yangu au pesa yangu siwapi kabisa. Kama nyie ni kaisari labda mnidai ankara (bill) ya maji nitalipa au ya umeme nitalipa au kodi ya nyumba uliyopanga hiyo lipa, kwa sababu yakupasa kulipa deni, ila kwa MUNGU ni tofauti.

MUNGU unamtolea kanisani kwa amani yako. YESU hakuwazii mabaya eti ukipata shida aone utapata msaada wapi, Yeye anatuwazia mema kila siku na Damu yake YESU inanena mema juu yetu. Sasa cha ajabu jiulize kama kanisa ni la YESU kwa nini wanakwambia “ngoja tuangalie akipata shida nani atamsaidia”, unachotakiwa hapo kujua ni kwamba hilo siyo kanisa la MUNGU ni kanisa jina tu, ni jengo la biashara na malengo yake ni ya kibinadamu kupitia siri zao za unyang’anyi.

Jinsi baadhi ya makanisa katika ulimwengu wote yalivyo acha njia ya MUNGU mpaka inakuwa ni aibu, kwa sababu makanisa mengi pia yameanzishwa na shetani ila yanatumia jina la YESU, na jinsi ya kuyajua ni kupitia matendo ya jinsi ya kuziendesha hizo huduma ikiwemo na hii ya kufanya makusanyo kwa kumwinda muumini nyumbani kwake asubuhi na mapema kabla hata hajaamka au siku za sikukuu (holidays), kwa sababu wanajua mtu amepumzika na watamkuta ili awape pesa.

MUNGU hapendezwi kabisa na hao wakusanyaji pesa, iwe ni mzee wa kanisa au yeyote yule, mbele za MUNGU au mbele za huyo muumini wewe ni mwizi kama vile kibaka anayevunja nyumba ila tofauti yako wewe unatumia kivuli cha jina la YESU kuiba na kunyang’anya kwa wepesi.

YESU ameniambia niwaeleze kuwa, pesa hizo mnaibiwa tu. Wapo waumini wanao omba na kumwambia MUNGU kumbuka sadaka zangu nilizotoa kwa kanisa lako asubuhi ulipowatuma watumishi wako nyumbani. Hao waliokuja asubuhi kwako na ukawapa sadaka, wote ni wezi tu na ukiona kanisa linakwambia ukipata tatizo hawatahusika kwa sababu umekataa kutoa mchango, uelewe kwamba hapo ni kwa mapepo, hata ukichukulia kibinadamu, mchango ni hiari yako na siyo kulazimishwa, tena hata huko duniani unatoa kwa uhuru wako lakini makanisani unalazimishwa kutoa kwa ubabe yaani ni lazima. Jiulizeni, je bado mpo Misri kwa Farao au mpo huru kwa YESU?

Mwenye akili na aelewe ujumbe huu. Msitoe sadaka zenu kwa wazururaji na wasumbufu wanaodai watu pesa. Wameleta mbinu za Kaisari za kukusanya mapato kwa kutumia jina la YESU. Kanisa siyo Kaisari, ya Kaisari mpe Kaisari na ya MUNGU mpe MUNGU. Watu wote msije mkafikiri mtapata baraka yeyote kwa MUNGU kwa kumtolea kwa njia hiyo, hizo zote mmetupa na mnaoendelea kutoa kwa njia hiyo bado mtakuwa mmetupa kwa shetani na kuangamia. Wajulishe na wengine.
MUNGU Awabariki!

NABII HEBRON.