Pages

Sunday, November 19, 2017

JINSI YA KUMJUA MTUMISHI ANAYEONGOZWA NA MIUNGU YA KIKRISTO
BWANA YESU ASIFIWE! Hapa naongelea mtumishi ambaye anaongozwa au kutumikia au ameitwa na miungu ya kikristo au yule ambaye aliitwa na KRISTO halafu akarudi nyuma. Huyu mtumishi ambaye aliitwa na KRISTO na baadaye akarudi nyuma huwa anachukuliwa na miungu ya kikristo na ndipo miungu hiyo huanza kumwongoza kufanya kazi za injili kwa njia ya miungu ya kikristo, wapo wengine wanajijua kabisa kwamba wao si watumishi wa YESU, na wapo wengine wanatekwa na miungu kwa kufuata mapokeo ya kurithi elimu ya wanadamu. Kama unaongozwa na mtumishi wa jinsi hii na wewe muumini unakuwa mfuasi wa miungu ya kikristo, kwa sababu jinsi alivyo kuhani na ndivyo alivyo muumini kiroho.

WANAOONGOZWA NA MIUNGU YA KIKRISTO HUFANYA YAFUATAYO:
§  Kuwaombea watu kwa kuwatoza pesa, wanakuwa na ma-partner ambao anawachagua yeye ili kuendeleza hiyo huduma akitumia jina la YESU. Atawabatiza watu kwa ubatizo ambao sio kama aliobatizwa YESU. Watabatiza ubatizo wa kisima, ubatizo wa kikombe, kulipindua Neno, kubarikia watu wazima badala ya kubarikia wakiwa watoto wadogo kama YESU alivyobarikiwa. Huchanganya mafundisho ya uongo na ukweli, huwaeleza waumini waandike sadaka zao majina, kiwango walichotoa, anwani (address) au barua pepe (email address) na huwapa waumini stakabadhi (receipts) wanapotoa sadaka. Hufuata watu nyumbani au ofisini kukusanya sadaka ambazo waliwalazimisha waumini watoe. Wengine hukopa benki na kuwalazimisha waumini walipe mikopo hiyo wakati MUNGU yeye anasema usije toza mtu RIBA. Kanisa linapoenda benki kukopa hiyo inakuwa ni miungu ya kikristo ndio inaenda kukopa kwa sababu yenyewe ni maskini, haina fedha wala dhahabu, bali YESU wa mbinguni Yeye anavyo vyote hivyo na kazi zake anazifungulia njia mwenyewe na wala si kwa njia ya madeni na kukopa.

§  Katika nyumba za ibada hufanyika harambee, katika nyumba za ibada huzikwa viongozi wao. Kwa njia hiyo watu wanakuwa wanaenda kusali kaburini kwa sababu kaburi lipo ndani ya hekalu. Hata kibinadamu kaburini ni mahali panapotisha, wapo mapepo au maroho ya giza. Hata YESU mwenyewe hakuzikwa kanisani alizikwa mbali na hekalu, sasa iweje leo mtu anazikwa kanisani? Jibu ndio hilo, miungu ya kikristo inafanya kazi yake ya injili ya miungu ya kikristo. Injili ya kikristo ikiwa inampinga MUNGU katika kweli yake, mfano imeandikwa usimpe mtu kilevi na hapo hapo utaona pombe inabarikiwa, tena bila aibu anatajwa Bwana YESU, sasa uelewe wakati huo ni yesu wa miungu ndiye anayekuja kulewa kwa sababu yeye ulevi na uovu ni mambo yake anayotaka wanadamu wayafuate.

§  Watumishi wanakuwa ni wachawi au wanachama wa freemason kabisa na hata katika matendo yao, ndiyo sababu hata baadhi yao huvaa misalaba ili waonekane ni wafuasi wa YESU wa mbinguni. Cha ajabu utaona mtu fulani amejiunga na freemason lakini amevaa msalaba, yamkini ni mchezaji au mwanamziki, wala usishangae huyo anakuwa amepewa hivyo vitu na miungu ya kikristo na hapo anakua anaitambalisha. Baadhi ya makanisa yanakuwa na bendera zake, wamezibuni, ila siri anaijua kiongozi na zile bendera, ni lazima aziweke zipepee kwa sababu kila moja inaashiria mfalme aliyepewa kwa ajili ya kulitawala hilo kanisa ili lipoteze watu na yeye afaidike. Huomba watu waliokufa wawaombee ikiwemo hata kuwataja wanafunzi wa YESU kwa majina yao, huabudu sanamu na mengine mengi, ila endelea kusoma makala haya utajifunza mengi na utakuwa huru kwa jina la YESU.

§  Hutoa makafara na kuwapinga wale watumishi ambao wameitwa na MUNGU ambao husema kweli kama ilivyo. Wanao umoja katika ulimwengu wa roho, hawa watumishi wa miungu ya kikristo hata kama hawajuani kimwili kiroho wanakua pamoja kabisa wakiwa na waganga, wachawi, majini na mapepo, hao wote ni roho za ufalme mwingine.

Jina la YESU limekuwa likitukanwa na watu kwa muda mrefu kwa sababu ya watumishi wanaoongozwa na miungu ya kikristo, wanafanya kinyume na YESU aliyoyaagiza, wanasababisha watu wanakwazika hata hawamtaki YESU. Mie nawaeleza hao ni wa miungu ya kikristo. Inawezekana wewe huipendi ila ulikuwa huelewi, sasa unaelewa, achana nayo hiyo miungu ya kikristo na mkimbilie YESU wa mbinguni na Yeye atakuponya utakuwa salama.

NABII HEBRON.