JE INA MAANA GANI UNAPOTOA SADAKA KANISANI HALAFU KANISA LINAKUPA
RISITI ILI URUDISHIWE NA SERIKALI (GOVERNMENT).
BWANA YESU ASIFIWE, watu wote wa Nchi zote, siku chache zilizopita
nilikuwa nikiongea na YESU kuhusu jambo hili ambalo baadhi ya wakristo katika
nchi zao wamejiwekea mfumo ambao sio wa Mbinguni au wa kutokubarikiwa na MUNGU,
akaniambia huo sio mfumo wa BABA yake yaani MUNGU, na haijalishi kama jina la mtu limetajwa hapo hayo ni machukizo kwake makubwa
sana.
Kwa mtu asiyejua; ngoja nikuelezee, katika baadhi ya nchi wakristo wanapotoa sadaka zao mfano dola 10, atapewa risiti ya
kuonyesha kuwa ametoa dola kumi kwenye kanisa (Sadaka) hivyo huzitunza hizo
risiti mpaka mwisho wa mwaka kisha huzipeleka katika serikali husika, kisha
zitajumlishwa zote – kwa mfano jumla ya fedha ambazo umetoa zimefika dola 2000
au kiasi fulani ambacho umetoka kwa mwaka mzima, serikali husika huwa
inamrudishia mhusika fedha zake. (Yaani
sadaka ambazo umetoa kwa mwaka mzima kanisani).
Sasa nataka ujiulize, unapomtolea MUNGU si
unategemea kubarikiwa na MUNGU Mbinguni? Hivyo ndivyo ambavyo baadhi ya wakristo walivyopigwa
chini na shetani, sasa mtegemee serikali hizo ndizo ziwabariki au kwa lugha
nyingine hambarikiwi na MUNGU kwa sababu mnarudishiwa na Kaisari.Ndio sababu
mateso hayaishi na pia ni sababu ambayo imelifanya kanisa kuwa sehemu ya
kubadili fedha(Money exchange).
Nawaandikia na kuwatangazia kuwa habari hii
inamuudhi sana YESU, Malaika wote na Mbingu yote kwa sababu ya mfumo huo, na
mimi Hebron nawaeleza wala sipunguzi amesema “ Waeleze kuwa hawaniletei mimi
bali wanajiwekea akiba zao kwa Kaisari, ili wapewe baada ya muda, wengi
wanaomba wananiambia nizikumbuke sadaka zao waulize ni zipi ambazo wamenitolea
mimi? Waeleze Abel aliponitolea sadaka yake ilienda Mbinguni
kupitia moshi (Mwanzo 1:2-15)”.
Hata
kipindi chaYESU alipokuwa hapa ulimwenguni alikuwa akitoa sadaka lakini
hakuwa anapewa risiti ili baadae akadai kwa kaisari, hivyo basi mdaini kaisari baraka
na mengineyo kwa sababu mlimpa yeye.
Cha kustaajabu, hata wapo baadhi ya
waumishi wengine ambao wanalifahamu jambo hili kuwa sio sawa, na wamekataa kulisema ili watu wasipone na wasione
baraka zao na mengine yamefichwa ikiwa inamaana mmemshukuru shetani au wametekwa
fikra zao na shetani au wamekuwa vipofu. Na kupitia jambo hili hizi ni dalili
kuwa vipofu ni wengi wanaongoza watu na watu hawaoni njia, na tayari
wametumbukia katika mashimo, wapo baadhi ambao wanajua na wengine wanaiga
mifumo ya vipofu.
MUNGU anaheshimiwa na Mataifa yote, (TAHADHARI
(ONYO)) Huo mfumo uachwe mara moja na uachwe na mengineyo hivyo ndivyo ninavyoelezwa
mda huu ninahimizwa ujumbe huu. Utayesikia sikia hii ni dhambi kutoa sadaka halafu unaidai
serikali ikurdishie hapo umetoa kwenye serikali ya kaisari.
Note:
Na zaidi ibada bila sadaka siyo ibada kamili
hivyo basi kwa mfumo huo wa kutoa sadaka halafu mwisho wa mwaka unaenda kudai
ofisi za Serikali (Government) ili wakupe cheque ya marejesho ya fedha
ulizozitoa hapo hakuna ibada yeyoye ambayo anafanyiwa MUNGU wa Mbinguni bali
unakuwa unamfanyia kaisari ibada.
NABII HEBRON WILSON KISAMO.