BAADHI YA NDOA ZA
WANADAMU ZIMEUNGANA NA
SODOMA NA GOMORA
Shalom! Karibu tena
katika mafundisho ya ndoa takatifu ili uachane na ndoa ya uchafu au ndoa inayomchukiza
Mwenyezi MUNGU aliyekuumba wewe binadamu.
Nitawaeleza kuhusu
ndoa inayomkasirisha Mwenyezi MUNGU kutoka katika kiti chake cha Ufalme. Ukisoma
katika kitabu cha Mwanzo 14 mpaka Mwanzo 20; utasoma kuhusu habari ya
Lutu alivyotolewa Sodoma ili asichomwe moto kwa sababu yeye hakufanya huo
uchafu au uzinzi wa mitindo ya wanyama (Style
za X). Ukisoma katika kitabu cha Waebrania
13:4 na 1Wakorintho 7:4-5, yapo
maelezo ya ndoa na maonyo kwa sababu MUNGU alijua kuwa shetani bado anafuatilia
ndoa ili zisiwe za MUNGU bali yeye shetani ndio azitawale.
Nitaelezea kwa kifupi
yatakusaidia na utaelewa na wewe unayetaka kupona utapona ila hata sasa nasikia
katika roho baadhi yao wanaumia roho kwa sababu wanapenda kuingiliana kama
mbwa, au kuku au kinyume na maumbile hiyo ndio furaha yao, ikiwa ina maana kuwa
pepo Sodoma na Gomora ndilo limejaa katika ufahamu wao na ili waache ni mpaka
hilo pepo liondoke na lisipoondoka hawataweza kuacha kukutana kimwili kwa mitindo
(style) hiyo ya wanyama na
usipoacha hautaenda mbinguni; sehemu yako itakua ni Jehanam, kila
unavyoendeleza na hizo style za X,
ndivyo unavyozidi kujiunganisha katika safari ya kwenda kuchomwa moto kwa sababu
umemkubali mnefili.
Nashangaa na hata wewe pia ushangae, ni ajabu ukienda katika semina ya ndoa au
kabla wanandoa hawajaoana wanaingizwa katika ofisi ya Mchungaji, watapewa
mafunzo ya mitindo ya kuingiliana katika tendo la ndoa kwa njia ya Kisodoma
badala ya kufundishwa yale anayoyataka MUNGU, sasa hapo unakua umepewa yale ya
shetani na unapoyafuata basi ndoa yako au hizo ndoa zinakuwa ni chukizo
mbele za MUNGU. Mfano, eti utaambiwa muwe na mitindo (style) nyingi ili msichokane au
mwenzako atakuona wewe ni mshamba, haujui mapenzi, (wakati hayo sio mapenzi
bali ni kifo).
Nitaeleza baadhi kwa
ufupi:
·
Kunyonyana mate ni dhambi;
·
Kutumia ulimi kunyonya viungo vya kiume au vya
viungo vya kike ni Sodoma. Mdomo kazi yake ni kumsifu MUNGU na kula, madhara
yake utapokea laana ya kuwa kibogoyo na meno yatang’oka mapema na uthamani wa
kinywa chako kuibiwa na shetani. Ulimi hutumiwa na wanyama kama mbuzi, ng’ombe,
nyani sasa wewe kwa nini uwe kama mnyama?;
·
Mitindo ya chuma mchicha, mbuzi kagoma,
kukutana kama jogoo anayempanda mtetea, mwanamume kulala chini halafu mwanamke
anamlalia juu ili kutenda tendo la ndoa;
·
Kunyonya viungo vya siri mpaka mbegu zitoke na
zaidi zinamezwa kama chakula, mbegu hizo zinatakiwa ziende mahali pake na siyo
kwenye kinywa cha mtu, kwa njia hiyo elewa umerudia matapishi ya Sodoma na
Gomora na kukufanya uje uchomwe moto katika siku ile ya hukumu, hivyo ni bora
uache kabisa sasa hivi na utubu;
·
Na zaidi utaweza kukuta watu wa jinsia moja
wanaoana, mfano mwanaume kwa mwanaume au mwanamke kwa mwanamke na
wanafunga ndoa na wanaishi kwa kusudi la kuwa mwili mmoja kwa njia za shetani.
Wakristo kama wanampenda MUNGU wafunguke, dunia yote wasikubali kuongozwa na mchungaji
shoga, awe wa kike au wa kiume, yeye tayari ameshakuwa mtaji wa Jehanamu na
anapokuongoza kiroho na wewe unanajisika katika roho, alipo yeye anayekuongoza
na wewe utamfuata huko huko. Jinsi alivyo kuhani ndivyo alivyo muumini. Je!
utapenda kuitwa muumini wa shoga?;
·
Kuzini na wanyama;
·
Kufanya punyeto;
·
Kuzini na roboti au sanamu za ngono (artificial sex organs) au sanamu.
Angalizo:
Yapo mengi kwa kupitia haya mafundisho yatakusaidia na utapona kabisa ila
yakupasa kutubu. Sema, BWANA YESU naomba unisamehe, dhambi zangu zote
ikiwamo hii ya Sodoma na Gomora, nakataa mimi siyo mtaji wa Jehanamu, naivunja
ndoa ya Sodoma katika ulimwengu wa roho na mwili. Amen.
NABII
HEBRON.