JE
UNAJUA BAADHI YA WATEULE WAMESHAPIGWA NAMBA YA MPINGA KRISTO AMBAYO NI NAMBA 666
KUPITIA MAJIRA YA SAA?
UFUNUO 13:18
Shalom watu wa MUNGU
wa mataifa yote walio wateule wa kwenda mbinguni na wale wote ambao hawajajua
habari za YESU wa Nazareti, nikimaanisha ambao hawajaokoka. Hiki ndicho kipindi
cha neema, bado kitambo kidogo tu Mwana wa pekee atarudi kuja kuwanyakua wale
ambao wamekubali kuishi maisha Matakatifu na siyo ya dhambi. Ufunuo 13:18 “18Hapa
ndipo penye hekima. Yeye aliye na akili, na aihesabu hesabu ya mnyama huyo;
maana ni hesabu ya kibinadamu. Na hesabu yake ni mia
sita, sitini na sita”.
Na katika mwaka huu
wote ambao nawaandikia mimi Nabii Hebron, watu wote wa dunia yote ili
mjielewe na muweze kupona na kuikataa hii namba 666 ambayo imeletwa kwa njia ya
kubadilisha majira ya saa. Mnamo mwaka 2009, nikuwa katika kazi aliyonipa BWANA
kwa muda, ili aniandae kwenda kumtumikia, pasipo mimi kujua, mpaka pale
alipokuja kunijulisha, ndipo baada ya mwaka nilianza kuongea na malaika
Gabriel, nikiwa jiji la Arusha wakati natokea Sanawari kupitia barabara ya
AICC (Arusha) kuelekea mjini, nilipofika eneo la ofisi ya Mkuu wa Mkoa,
pale kwenye mzunguko (round about), nilishikwa
na butwaa na sikuweza kumweleza mtu yeyote yule mpaka leo hii ndio
nawaeleza, mengine bado muda wake wa kuyasema, wakati huo nilikimbiwa na
kukataliwa hata na baadhi ya watu katika familia yangu, marafiki na ndugu wa
karibu. Maisha yalikuwa yameharibiwa na wachawi, kazi zangu zote ziliharibiwa,
yamkini walitaka nife kimwili lakini ikashindikana, wachawi walitaka kunitoa
kafara na mambo mengine mengi mabaya waliyokuwa wamenipangia hayakuwezekana. Baadhi
ya hao walikuwa wakijiita watumishi wa MUNGU kumbe walikuwa ni watumishi wa
shetani. MUNGU alinitenga nao kwa sababu MUNGU alikuwa na kusudi na mimi, na
mengi MUNGU alikuwa ananieleza lakini sikuweza kumjibu mtu kitu, na wakati hayo
yalipokuwa yakitokea sikuwa na mbele wala nyuma. Nilikuwa nimehifadhiwa kwa mtu
ambaye MUNGU ndiye aliyemwandaa, lakini pia hata yeye pamoja na familia yake hawakulijua
hilo, ila MUNGU ambariki sana na tayari alishabarikiwa pamoja na familia yake.
Sasa siku hiyo, majira
ya saa yangu ya mkononi yalionyesha 2:30pm (two thirty), yaani saa nane na nusu
mchana, lakini cha ajabu Malaika Gabriel aliniambia majira halisi na kwa namba
au tarakimu za kiswahili na akaniambia atakuja kuongea na mimi wakati mwingine,
tena kwa muda wa masaa ya Afrika Mashariki lakini sikumwelewa, na siku nyingine
nikiwa na watalii wa kijerumani katika eneo la Ngorongoro kuelekea Lake Natron
alisema na mimi na huyo alikuwa ni Malaika mwingine Mikael, akasema, tupo na
wewe Hebron katika safari hii tokea muda fulani, kwa majira ya nchi yako, na
safari hiyo ilikuwa ina ugumu kwa sababu shetani alijua kuwa
nitakuwa nani hapo baadae, hivyo alitaka nianguke na gari wakati
nikipita katika mlima Natron, mlima huo mrefu sana, wenye kona
nyingi wakati ukitokea Lobo kupitia Loliondo kuelekea ziwa Natron na kisha
unafika katika mji wa Natron, lakini nilifika chini salama na
nilimaliza safari na wageni wangu salama.
Malaika Mikaeli alikuwa
amevaa saa yake iliyokuwa mkononi haisemi uongo, au kwa
lugha nyingine tulifundishwa shuleni eti saba ndio saa moja (7am), na moja ndio
saa saba (1pm) na alikuwa akionyesha majira lakini cha ajabu alikuwa hataki kabisa
kuangalia saa yangu, nilidhani kuwa labda kwa vile ilikuwa ya bei rahisi au
haifai, kwa maana ya kwake ilikuwa ni ya gharama, la hasha, kumbe ni
kwa sababu saa yangu ilikuwa ikisoma majira tofauti na ya Mbinguni.
Malaika Mikaeli alipokuwa
akija alikuwa anapewa muda wa kuongea na mimi, muda aliopewa na MUNGU, na
alipokuwa akianza kuongea na mimi alikuwa akiangalia muda na dakika kila mara,
na zilipokuwa zimebakia dakika chache alikuwa ananiaga, kuwa muda wake
ulikuwa umekwisha, lakini akili yangu ilikuwa ni ya kijinga, nilikuwa
naonyeshwa na kufundishwa kuhusu majira ya saa lakini sikuelewa. Ilipofika wakati
wake nilimwona YESU akija kwenye gari la wageni nililokuwa naendesha, na
alikuwa ananiambia vua saa yako, halafu ndio anaanza kuongea na mimi, hata kwa
masaa mawili, nikiwa naendesha gari kwenye mapori ya wanyama na ilipofika
mwaka 2010, akaniambia kuanzia sasa saa yako isome kwa namba za Kiswahili kama
ilivyo saa moja ni saa moja, saa mbili ni saa mbili na saa tatu ni saa tatu.
YESU akaniambia,
Hebron hivyo ndivyo adui alivyouteka ulimwengu na kuweka uongo na kufanya hata
mtu ambaye ananipenda asije akafika mbinguni, ili mradi tu awe nakizuizi, kwa
sababu MUNGU yeye ni wa haki na siku ile ya mwisho, shetani anamshitaki kila
mtu kuwa hao siyo watu wako sababu wanatembea na namba 666, katika majira yao. Sasa mimi nawaeleza mataifa yote
mfanye marekebisho katika saa zenu, iwe za nyumbani, ofisini, katika gari
na za mikononi.
Wewe ambaye hupendi
namba hii 666, unakuwa umeweka majira ya uongo, kama nitakavyoelezea hapa chini,
utaona mwenyewe, utafanya mahesabu utakuta kila saa ni namba 6 badala ya saa ya
kweli na zaidi hata ukisoma kwa lugha ya kingereza namba 1 ni one
na sio seven, na namba 2 ni two na sio 8. Shetani ni mjinga
sana, na je umesha jiuliza ni kwa nini saa
saba inakuwa one o’clock, au saa sita
kuitwa 12 o’clock? Jibu ndio hilo alilolileta shetani ili kila
anayebadili au kuandika saa yake hivyo anakuwa anaishi na kutembea na namba 666 pasipo yeye kujua ila wengine
ni kwa kujua.
Nitaeleza kwa kifupi
ila kwa ufasaha namna namba hii 666 ilivyotengenezwa na jinsi ilivyofuatwa na
dunia yote.
Majina ya namba 666,
saa 1 inaitwa 7 na ukitoa 7-1=6
Mfano:
|
Saa
|
Inaitwa
|
Ukitoa
|
|
1
|
7
|
7-1=6
|
|
2
|
8
|
8-2=6
|
|
3
|
9
|
9-3=6
|
|
4
|
10
|
10-4=6
|
|
5
|
11
|
11-5=6
|
|
6
|
12
|
12-6=6
|
|
7
|
13
|
13-7=6
|
|
8
|
14
|
14-8=6
|
|
9
|
15
|
15-9=6
|
|
10
|
16
|
16-10=6
|
|
11
|
17
|
17-11=6
|
|
12
|
18
|
18-12=6
|
|
13
|
19
|
19-13=6
|
|
14
|
20
|
20-14=6
|
|
15
|
21
|
21-15=6
|
|
16
|
22
|
22-16=6
|
|
17
|
23
|
23-17=6
|
|
18
|
24
|
24-18=6
|
Mpaka hapo watu wote wa dunia hakuna anayeweza
kubisha kuwa hiyo si namba 666, na cha ajabu hebu jiulize, siku moja ina masaa
mangapi? Jibu ni masaa 24, utakuta ni masaa 18 (18 hours) na siyo masaa 24 (24
hours) sasa anza kuhesabu kuanzia 7 mpaka 24, utakuta ni masaa 18 na sio
24, hivyo basi utakuwa unafuata majira hayo ya uelewe na wewe hata siku
yako inashikiliwa na 666.
Nilimshukuru YESU kwa kunifunulia siri
hii, japo ziko nyingi za namba 666 na zaidi waulize Warumi walinunua saa zenye
namba za kirumi zinazosoma I ni saa 1, II ni saa 2, III ni saa 3, IV ni saa 4, n.k.
kwa nini unadanganywa kirahisi? Wapo Wasomi wa mahesabu kwa nini wasifundishe
ukweli? Wamefungwa fahamu na kuongozwa na roho, hiyo. Hata mimi Hebron
nilifuata huo uongo, ni cha ajabu hata makanisani utaona
baadhi wanaandika majira ya uongo, mfano Ibada inaanza 02:30-20:00
hrs, yaani ibada inaanza saa nane na nusu mchana, mpaka saa mbili
kamili usiku, wakati huo ni uongo, ibada zipo katika uongo na kufanya MUNGU na
ROHO MTAKATIFU asionekane katika ibada hizo kwa sababu kibao
chenyewe cha ratiba za ibada kinaonyesha majira ya 666. Kwenye maofisi na hata
kwenye sehemu za biashara, angalia saa utakuta inaishi
na namba 666, yaani inaishia na mpinga kristo. Unaweza ukajiona
kweli wewe haumpendi mpinga kristo, lakini mbona unaishi naye, unatembea naye na
mpaka ukikata roho unatembea na majira ya 666, hicho kinakuwa ni kibali kamili
cha kuchukuliwa na ufalme wa giza.
Zaidi fuatilia katika website: www.prophethebron.org; pia ingia katika link ya YouTube na Blog utajifunza mengi na yatakusaidia kufika
mbinguni siku moja.
Karibu kwa YESU umfungulie moyo
wako. Sema, Bwana YESU, naomba unisaheme dhambi zangu zote, uandike jina langu
katika kitabu chako cha uzima wa milele, uniondolee namba 666, sitaki kutembea
nayo, nashukuru nimejua ukweli na sasa nachukua hatua kufuata majira ya kweli
yanayofuatwa na Mbinguni, sitaki majira ya kuzimu tena. Amen.
Angalizo: Kwa maana nyingine haya majira ya uongo ndio majira
yanayotumika kuzimu, na unapoyafuata unakuwa upo katika majira ya kuzimu au kwa
maana nyingine unakuwa umefuata majira ya freemason, au kuishi na
majira ya freemason aidha kwa kujua au kutokujua. Huo unakuwa ni
mlango wao wa kukuibia vitu vyako, kwa sababu wana uhalali huo wa majira yao
ambayo ni ya uongo, ambayo umeyakubali yakuongoze badala ya kukubali majira ya
kweli ya mbinguni.
NABII HEBRON