NINI MAANA YA PASAKA NA EASTER DAY?
(Easter ni mungu mke)
SHALOM, BWANA
YESU ASIFIWE, tutasoma neno la MUNGU, kutoka katika kitabu cha KUTOKA 12:11-14 neno la MUNGU linasema;
11
Tena mtamla hivi; mtakula mmefungwa viuno vyenu, mmevaa viatu vyenu miguuni, na
fimbo zenu mikononi mwenu; nanyi mtamla kwa haraka ; ni Pasaka ya BWANA . 12 Maana nitapita kati ya nchi ya
Misri usiku huo, nami nitawapiga wazaliwa wa kwanza wote katika nchi ya Misri, wa mwanadamu na wa
mnyama; nami nitafanya hukumu juu ya miungu yote ya Misri; Mimi ndimi BWANA. 13
Na ile damu itakuwa ishara kwenu katika zile nyumba mtakazokuwamo; nami nitakapoiona ile damu, nitapita juu yenu,
lisiwapate pigo lolote likawaharibu nitakapoipiga nchi ya Misri. 14
Na siku hii itakuwa ukumbusho kwenu, nanyi mtaifanya iwe sikukuu kwa BWANA;
mtaifanya iwe sikukuu katika vizazi vyenu vyote, kwa amri ya milele.
Leo
tutajifunza habari ya Pasaka si habari ngeni na wengi tunaijua Pasaka, lakini
nataka tujifunze kuhusu Pasaka, je! Pasaka ina faida gani na Pasaka ni nini?
Pia tunasoma
neno la MUNGU, kutoka katika kitabu cha MAMBO
YA WALAWI 23:7-8. 7 Siku ya kwanza mtakuwa na kusanyiko takatifu
msifanye yoyote ya utumishi. 8 Lakini mtasongeza sadaka kwa BWANA
kwa njia ya moto siku saba; siku ya saba ni kusanyiko takatifu; msifanye kazi
yoyote ya utumishi.
BWANA YESU
ASIFIWE, maana wako wengine wanasema Jumamosi ni Pasaka lakini Biblia inasema
siku ya saba, hii inatukumbusha kwamba Pasaka kuna sadaka yake, na ile siku ya
saba pia. Lakini lengo kubwa hapa nataka tujifunze kuhusu pasaka na Pasaka ni
nini? Maana MUNGU aliponiita aliniambia
nataka ukarejeshe ulimwengu kama ninavyotaka mimi maana umeharibika kwa asilimia
kubwa sana.
Neno Pasaka limetoka kwenye neno la kiingereza PASS OVER
yaani MUNGU alipita juu ya wana wa Israeli; kuanzia alipokuwa kule jangwani na waliponywa kupitia damu ya wanyama ambapo
walichinja wakaweka kwenye milango kwa hiyo MALAIKA WA BWANA alipopiga usiku
aliondoa mauti kwa wana wa Israeli, wale
ambao walikuwa hawajaweka walikufa, hiyo ndiyo Pasaka ya kwanza.
Biblia inasema muifanye kila mwaka vizazi na
vizazi kwa hiyo na YESU alipozaliwa aliikuta kwa hiyo na yeye alikula Pasaka kwa
miaka 32 YESU alikula Pasaka hiyohiyo, lakini Pasaka ya mwisho ambayo MUNGU
ametupa ni BWANA YESU, baada ya BWANA YESU kuja tukawa hatumwagi damu za
wanyama tena, wala kuchinja na kuweka juu ya milango kwasababu DAMU YA YESU ilimwagika
na kumaliza kila kitu ikatuondolea
mauti, alikufa, akazikwa, akafufuka tumekuwa na ushindi yaani kuwa hata tukifa
tutafufuka.
BWANA YESU ASIFIWE, lakini nataka nikuulize
hivi wewe huwa unasherekea Pasaka au Easter? Sasa leo tutamchambua easter vizuri,
sidhani kwamba ulipokuwa ukisoma Biblia ulishakuta mahali umeambiwa usheherekee
easter? Tafuta kwenye Biblia ya kiarabu, ya kijerumani, ya kiingereza hakuna
kusheherekea kitu kinaitwa easter ni PASS OVER yaani Pasaka kwa Kiswahili.
BWANA YESU ASIFIIWE lakini kuna mahali shetani alifanya mambo yake, lakini sasa
nataka Pasaka irejee kama vile MUNGU alivyotaka na anavyotaka iwe katika Dunia
nzima, haya mambo ya easter kuanzia leo hayatakuwepo tena.
Lakini
nataka nikufundishe, na uelewe kuwa unaabudu kitu usichokijua sio ESTA, kuna ESTA
ya kiingereza, na kuna easter, sasa nikuulize kuwa ni sehemu ipi katika Biblia
imeandikwa kila mwaka mtakuwa mnakumbuka easter? Wasomi wa Biblia ya kiingereza
kasomeni, haijaandikwa hivyo.
BWANA YESU
ASIFIWE nilikuwa nimekaa na MUNGU nikasikia ananiambia Hebron easter vipi? Hivi
easter ni nini? Sasa akishaniambia hivyo najua ni wakati muafaka wa mimi
kuwaeleza jinsi ambavyo MUNGU anataka iwe, kama hajaniambia sizungumzi, aniuliza je! mimi ni easter? YESU akaniambia Hebron
hivi easter ni nini? Nami nikamuuliza kwa nini? akaniambia ni wakati wake sasa
wa kuwafundisha ulimwengu, kwamba mimi siyo easter mimi ni Pasaka,
nitakutafsiria kwa kiingereza, mpaka easter ilivyokuja na ikatolewa Pasaka.
Tunadanganyana
hapa na makanisani wanasema happy easter badala ya heri ya Pasaka, ni jinsi ulimwengu ulivyopotea muda mrefu ziko Pasaka
za kweli, ziko pasaka za kipagani, na ziko
za kimiungu.
Pasaka ya
kwanza ni ile ya wana wa Israeli walivyokuwa jangwani, Pasaka ya pili ni ile ya
BWANA YESU mwenyewe, sasa kwanini Pasaka isiitwe PASSOVER? wazungu wakabadilisha na kuiita
easter? Soma Biblia ya kiingereza je kuna kitu inaitwa easter? Wala Pasaka
haiitwi jina lingine easter hakuna. BWANA YESU ASIFIWE lakini nitakufundisha
kidogo , na pia unaposoma Biblia haijasema tuabudu easter jamani uliza hata
wazungu inaitwa ni PASSOVER sasa kama MUNGU ameleta PASSOVER yaani Pasaka sisi
tunaleta easter nani kichaa hapa? Biblia inasema wanadamu wameangamia kwa
kukosa maarifa je? nani kaileta hii easter?
Je sisi tumeletewa
easter au tumeletewa Pasaka? Sisi tumeletewa Pasaka, sasa kwanini huwa tunasema happy easter? Uthamani wa neno Pasaka
ulifichwa na shetani ndipo tukaletewa easter. BWANA YESU ASIFIWE sidhani kama mnanielewa; lakini bado nataka tuichambue
easter vizuri nataka uelewe, unajua mimi napenda mtu aelewe, maana jambo hili lina
madhara makubwa sana , hata mimi Hebron nimeikuta, sikujua na mimi nilikuwa
nasema happy easter kumbe nimepokea na kushiriki pasaka ya kipagani, Waisraeli
wenyewe ni wajanja hawajakubali kusema happy easter, wamesema Pasaka tu BWANA
YESU ASIFIWE, YESU hajakuta inaitwa
easter, amekuta inaitwa Pasaka tu MITUME WA YESU hawajawahi kusema easter
wamesema Pasaka tu lakini akaja
anayeitwa mungu wa kughushi. (kufoji), na kuifanya Easter itapakae dunia nzima.
Katika karne ya nane, kasisi mmoja
akaibadilisha maana zamani ulikuwa ukiletewa Injili ya mahali Fulani, kuna
wafalme nao wana miungu yao, sasa yuko
mungu anaitwa mungu easter yuko huko ujerumani . Kwa hiyo ile siku ya Pasaka yuko
mungu wa kijerumani anaitwa mungu mke, mungu wa kike alikuwa anaabudiwa na
wafalme huko ujerumani zamani BWANA YESU ASIFIWE.
Mnanielewa jamani kwa hiyo walipokuwa
wakianziasha jambo jipya lazima lipitie kwake, BWANA YESU ASIFIWE kwa hiyo
wakaiba Pasaka wakaiita easter, sasa easter ina maana ya Mashariki kwa
kijerumani ostern BWANA YESU ASIFIWE, hii easter shetani
bado akaichezea chezea ina maana ni Mashariki sasa ikaongezwa “r” pale
wakaondoa “n” ingekuwa “n” ingeitwa easten watu wangeshituka kuwa mbona ni
Mashariki. BWANA YESU ASIFIWE sasa nikuulize jamani MUNGU alizunguka Mashariki
au alizunguka juu? Unaona wanadamu wanavyoangamia, unaona sasa kwahiyo miaka na miaka hata mataifa ya Ulaya
na wenyewe ile sherehe ikaanza kubadilika easter sasa mnaelewa? tukapigwa uvuvio wa kutupumbaza kama na mimi pia
nilivyopigwa na uvuvio huo nikaamini easter ndio Pasaka na nimesoma na
nimeelewa kama na wewe ulivyosoma, ukisoma Biblia, ukichambua unakuta kabisa
MUNGU hakuleta easter alisema Pasaka.
Pasaka kwa
kiigiriki ina maana yake, kwa kiebrania ina maana yake kwa kichaga ina maana
yake kwa Kiswahili inaitwa Pasaka kwa kiingereza inaitwa PASSOVER sasa mimi
nashangaa tunaabudu Mashariki nini wewe unasema furaha ya Mashariki? Unaona
tulivyovurugwa? Matokeo yake sasa unaposema happy easter, au unasheherekea
easter unaungana na mungu wa kipagani, Je! Wewe hujaabudu mungu wa kipagani? pale
unaposema kwa kinywa tu unakuwa umeshiriki,
sasa utajiuliza mbona makanisani wanasema happy easter? Hivyo ndivyo kanisa
lilivyotekwa na shetani katika maeneo mengi, linafanya mambo lisilo yajua ndio
maana unaambiwa kwenye Biblia Utukufu wa mwisho ni mkubwa kuliko wa kwanza .
MUNGU amenituma kuyafichua yote, utashindwa kwenda Mbinguni ,utashindwa
kusheherekea Pasaka kwa kusema happy easter hata Kanisani kwangu sitaki kusikia hicho kitu.
Sasa Pasaka
hii watu wengi wamekula ya kipagani, ni mungu mke wamemsherekea, wewe mwanamke
unamuabudu na huyu mungu mke mpaka sasa
hivi kwa wazungu wanavyomsheherekea wanatumiaga sungura maana sungura wanaamini
ni mnyama anayezaa sana kipindi cha mwezi wa 3 na mwezi wa 4 BWANA YESU ASIFIWE
halafu wanachukua na mayai wanachora msalaba, kwa hiyo sasa wanawapa watu
zawadi huku wakiamini kabisa yale mayai ukipewa utapata miujiza na baraka ndipo
ikaanza enzi ya miungu mpaka sasa hivi Ulaya wakati wa Pasaka wanatoa sungura
na mayai je! nikuulize YESU alileta sungura na mayai? kwanza sungura ni mnyama ambaye kiroho
anatafsiriwa muongomuongo, mjanjamjanja BWANA YESU ASIFIWE sasa huyu easter akasambaa kila mahali,
unakuta mtu ana master au ni doctor amesomea Biblia na yeye bado anasema happy easter
na yeye amevurugwa na shetani na akili imepumbazwa muulize kama MUNGU alileta
easter? Hatakuwa na jibu sasa huyu
shetani mmbea anakaa pemben ianakushtaki kwa MUNGU, anasema siunaona
wanamuabudu easter huku likicheka
hehehee! Huku akisema hawa ni wangu, sasa ndivyo ilivyo kipindi cha Pasaka watu
wengi utasikia wakisema happy easter,
Makanisani
happy Easter, mapastor happy easter yaani mnakuwa mmesema furaha ya yule mungu
mke wa kipagani, jambo hili ni matokeo ya kuwa wakati wa pasaka watu hawafufuliwi kiroho, sasa kwa kusema
neno easter watu hawainuliwi kiroho, wala hawasongi mbele, yule mungu wa
kipagani anawamaliza kwa sababu anao mlango,(uhalali nao) sasa wewe nyumbani
kwako pambo happy easter kwanini usichukue pambo la heri ya Pasaka?
Fahamu kwanza kuwa hii easter ilianzia wapi, ni kwa jamaa zetu weupe lakini watapona BWANA
YESU ASIFIWE hakuna anayeweza kukataa jambo hili ninalokuambia ndio maana shetani anatamanigi
nife mimi “Sitakufa” nitawaambia ukweli tu, kwahiyo sasa kuanzia leo mwisho kusema happy easter, utasema
ninafunga mfungo ili ninyanyuke utanyanyuka kweli? BWANA YESU ASIFIWE .
MUNGU
alimleta Mwanae ili kwamba tukapate kupona lakini unakuta hii pasaka ibada zinafanyika
sehemu mbalimbali baadhi, maisha ya watu hayana mabadiliko kwa hiyo kipindi cha
Pasaka ni kipindi cha watu kunyanyuliwa
kila mwaka kiwango kingine na kingine kama ni mtumishi kiwango kingine na
kingine lakini yuko easter, Mimi sitaki kusikia kwenye Kanisa langu mtu anasema happy easter. Sasa kwanini
wapagani wakawa na mungu mke anaitwa easter?
Zamani walikuwa wanaangalia jua linachomoza Mashariki linaenda Magharibi
kwa hiyo wakawa wanaona Mashariki ndiko kunakoanzia mambo mazuri BWANA YESU
ASIFIWE kuna shida imani zimekufa, zimekuwa za kipagani, ukija kwenye amri ya
MUNGU inasema usiabudu miungu na wewe unasema huabudu miungu je? Hii happy
easter je? Message zako za happy easter utachorewa na vinyumba , utachorewa na
keki imeandikwa happy easter sasa heri
nyie mnaojua Kiswahili tunasema Pasaka maana huku kwetu haijachakachuliwa sana,
sasa ibada zote za kizungu ni happy easter utasikia wakisema today is easter
day! Haleluya! anakuambia hawasemi PASSOVER today wanasema ooh receive the bless
of easter utachukuwa baraka na kipagani mpaka ukome, sasa tazama ni mataifa
mangapi wanasema happy easter?
Ukiangalia kwenye TV utaona kwenye matangazo I
wish you happy Easter jamani yaani huyu mungu wa kipagani tu ndio anatajwa,
mara utasikia karibu dinner ya Easter, kwanini usimwambie karibu Pasaka? Utamkapo neno hili kwa kujua au kutokujua ujue
tayari umemla huyo jamaa, mungu mke; sasa iweje dunia nzima shetani ameirubuni
hata watu wasielewe kwamba hiki hakifai? Sasa mnaelewa jamani tafuta kwenye Biblia
kama kuna easter ukiangalia kwenye dictionary watakuambia ni Pasaka. (watakuambia
easter day kwasababu hawajui) sasa ni lazima NENO LA MUNGU lisibadilishwe
lazima litajwe lilelile BWANA YESU ASIFIWE siyo tunaletewa maneno ya uongo
uongo halafu tunapokea haya hayajaanza leo yameanza miaka mingi utasikia wafalme
wanasema ninawatakia happy easter wananchi wangu, tusiendelee jamani kumuabudu
MUNGU kwa kisaniisanii au kikomedikomedi ndivyo watakavyokuja siku ile ya Pasaka
MALAIKA wanakuja kukutembelea, ili baraka zako zije kwako,
MUNGU haji
kwako MALAIKA hawatembelei maisha yako kwasababu
umemtaja easter hapo unakuwa umemfukuza MUNGU halafu unataka vitu vya MUNGU? ;
lazima ulimwengu ujue ukweki sasa, soma Biblia hakuna kitu kinaitwa easter hata
wale waanzilishi wa kule jangwani kina Musa hawakusema easter sasa imetoka
wapi? Ikaingizwa ndani ya watu ikasambazwa, ile siku sasa ya Pasaka wanaambiwa happy easter mimi Hebron nimetumwa
habari ya kueleza Pasaka, sasa easter ikasambazwa wakatumwa Wamissionary
wambeawambea na waongo wakasambaza wakapewa na pesa na magari kutusambazia
uongo ni wakati wa kuteketeza ndio maana na wewe umepotea kwasababu umepokea
uongo jua kwamba kuna Wamissionary wa uongo kuna washetani wakusambaza kazi za
ibilisi kama ilivyo lazima ziondoke, wakati MUNGU amemleta YESU kwa ajili yetu
Pasaka hakuileta ichezewe kupitia hili JINA LA BWANA YESU, BWANA YESU ASIFIWE .
Muulize
mtumishi yeyote maana ya easter, hatakuwa na jibu sasa ukiongozwa na kipofu
unaenda wapi? Shimoni ndio jinsi ambavyo dunia imeenda shimoni BWANA YESU ASIFI
Sasa nikuulize MUNGU alipita Mashariki
ili akuokoe? MUNGU si alipita juu sasa tunakwenda wapi? Imani yako inapotea,
unakaa kila mwaka unasema happy easter unapotea hata na yule anayetengeneza
kadi anaiga na yeye amepotea, mtaigaiga mpaka mapepo, YESU alienda kuzimu akanyanyuka sasa amekwenda
kwa ajili yako yaani ili kila mwaka vitu
vyako viwe vinashuka kwa ajili yako na kunyanyuliwa lakini unasema happy easter
baraka zako zinapita mpaka mwaka mwingine tena BWANA YESU ASIFIWE.
Shetani
akome amebadilisha vitu vingi sana yaani hata siku ya MWANA WA MUNGU kusulubiwa
msalabani ametolewa sadaka atubadilishie iitwe Mashariki? hakikisha kitu unachotamka unakijua sasa Pasaka
ikafichwa, lakini yupo MUNGU achunguzaye, endapo kuna shida ipo wapi? siku ile ya mwisho utasema mimi sikuabudu
miungu, ndipo li happy easter linatoka
na mkia wake, linakushitaki kuwa wewe kila mwaka unanitaja, Mara utasikia
kongamano la easter, semina maarufu ya easter sasa hapo lazima adhihirike huyo
mungu easter kwasababu mmeshamtaja , mimi namjua YESU aliyekufa ndio maana na
mimi nina Pasaka, unajua ukisema kweli
watu wananuna wenyewe wanune lakini shetani akome, watu wapone, unajua
ukishapenda uongo ina maana na wewe hautaki tena kwenda Mbinguni unataka kwenda jehanamu, sasa watu
wanamuabudu huyu mungu wa kipagani, mungu mwanamke wakati kuna MUNGU MWANAMUME
tunamuacha BABA YETU, tunaanza kwenda kwa miungu ya kike, BWANA YESU ASIFIWE
sasa nikuulize Pasaka ni nini na easter
ni nini? easter nimekufundisha kwamba ni mungu wa kipagani wa kike akaingizwa
kwenye Pasaka ili Pasaka iishe nguvu ili
watu wasiinuliwe, watu wasimuone MUNGU hii
nguvu ya kupumbaza itoke dunia nzima na itoke kama nyie mnavyosoma sasa
ni wakati wa kuikataa na lile pepo liondoke hata ninavyokuambia sasa hivi akili
yako inavyofunguka ina maana bado ilikuwa imepumbazwa na gundi ya shetani
usielewe yanawekwa mapepo ya ulinzi usijue siri hii sasa umejua, umefunga mifungo
mingi kwa miaka mingapi? siku arobaini? Je ni kwa MUNGU au kwa easter sasa ashukuriwe
MUNGU nimekujulisha ili ukifunga kitu kijibu. BWANA YESU ASIFIWE lakini tunaita
easter.
MUNGU si ametupa Pasaka? Sasa kama si
kuchanganyikiwa na kutaja vitu ambavyo vimeingizwa kimchomeko kwenye JINA LA
BWANA YESU, sasa haikutosha sasa hivi katika dunia hii bado kuna watu wana pasaka
zao wanachinja mbuzi, au kondoo zinachinjwa hivyohivyo, BWANA YESU ASIFIWE sasa MUNGU akatupa MWANA
KONDOO WAKE ndio maana mpaka leo husikii watu wanachinja kwa ajili ya Pasaka kwa
hiyo ibada za kuchinja zote zinazofanyika sasa hivi hizo zinakuwa ni makafara
si za YESU, YESU alishamaliza kila kitu MUNGU alituletea yeye na ndio maana
akasema hivi Pasaka nyingine nitakula nikiwa na nyie nitakaporudi, alikula na
wanafunzi wake maana ile siku walimla yeye na yeye YESU akala Pasaka na wanafunzi wake BWANA YESU ASIFIWE lakini ilikuwa bado ni mafunuo yamefichwa
msielewe
BWANA YESU ASIFIWE: MITUME wake wakala Pasaka kama wale walivyo
kula Pasaka na ndio wakatuambukiza dunia nzima kufuata Pasaka, wakaendelea kusema Pasaka NI YESU,
lakini haikutosha walivyoondoka na kufa wajamaa wengine wakaanza kubadilisha
easter, sasa amenituma kun’goa eastern na mengineyo, unajua shetani anafikirigi
MUNGU hana watu wake ambao amewaandaa watasema
kweli sasa ni wakati wakulipiga hili li mungu easter na kulibomoa katika JINA
LA YESU, ashukuliwe MWENYEZI MUNGU yeye ambaye ametupa neema ya kujua Neno lake
la kweli na jinsi ya kutufungulia tupate kuelewa.
Ukisoma 2WAKORITHO
4:2-4 2 Lakini tumekataa
mambo ya aibu yaliyositirika, wala hatuenendi kwa hila, wala kulichanganya Neno
la MUNGU na uongo; bali kwa kuidhihirisha iliyo kweli twajionyesha kuwa na
haki, dhamiri za watu zikitushuhudia mbele za MUNGU 3 Lakini ikiwa
injili yetu imesitirika, imesitirika kwa hao wanaopotea; 4 ambao
ndani yao mungu wa dunia hii amepofusha fikira zao wasioamini, isiwazukie nuru
ya injili ya utukufu wake Kristo aliye sura yake MUNGU.
Mnaona sasa
fikira zimepofushwa tufanywe watu wa dunia hii kupokea injili ambayo si mpango
wa MUNGU huku baadhi ya makanisa na
watumishi wametulia tu hawataki kuongea
maana wanakatazagwa na shetani wasiongee hivyo ndivyo shetani alivyolichezea
NENO LA MUNGU na kupiga upofu na kulizuia; haya ikaja tena ikikaribia Pasaka
watu wanaambiwa msile nyama eti mtakuwa mnamla YESU jamani nyie kuleni nyama
YESU YUKO MBINGUNI, BWANA YESU ASIFIWE siku ya Pasaka ni siku ya furaha
siyo kurudisha tena watu kwenye majonzi eti YESU anakata roho YESU YUKO
MBINGUNI.
MBINGUNI hawajui
easter wanajua Pasaka sasa wewe unaabudu kitu ambacho kimetolewa kwenye midomo
ya watu? Ukisoma ufunuo 22:18-19 ole
wake aongezae maneno ya kitabu cha unabii huu, sasa neno easter limeongezwa
yaani kwa namna hiyo shetani anapata watu wengi siku ile ya mwisho.
Ukisoma NENO
LA MUNGU KATIKA KITABU CHA UFUNUO 12:9 Yule
joka akatupwa, yule mkubwa, nyoka wa zamani, aitwae Ibilisi na shetani
audanganyae ulimwengu wote; akatupwa hata nchi, na malaika zake wakatupwa
pamoja naye.
Yule joka
audanganyae ulimwengu ametupwa ameudanganya ulimwengu umeacha kusema heri ya Pasaka
unasema happy easter sasa mnaona BWANA
YESU ASIFIWE hii yote unapumbazwa ili usikutane na muujiza wako ili kwamba
usikutane na ile ahadi MWENYEZI MUNGU aliyoileta kwa ajili ya mtoto wake kwa
ajili yako wewe ukanyanyuliwe, sasa wamekuwepo baadhi ya watumishi ni wahuni wengine ni wachawi wanatumia NENO LA
MUNGU huku wanaenda kuzimu, mimi kuzimu nimefika na MBINGUNI nimefika
ninawaambia ninachokijua unayesikia sikia utakwenda kupona, BWANA YESU ASIFIWE ,shetani
huko kuzimu wao wanasheherekea easter
ndio maana unasikia kuna pasaka ya kuzimu hiyo ndiyo inaitwa easter.
MBINGUNI
wanasheherekea Pasaka wanakumbuka vile MUNGU alivyofanya wanampa BWANA YESU
hongera kwa kufanya kazi nzuri Haleluya sasa na huko kuzimu wanamwambia easter
ulifanya kazi nzuri tumeshawachukua wanadamu husikii wanasema happy easter,
sasa fikira zimeharibiwa shetani ameudanganya ulimwengu, lakini shetani ili afanye kazi na MUNGU ili
afanye kazi anamtumia mwanadamu anayemkubali ndio maana mtu anatumia JINA LA
YESU anatafuta pesa anakuambia BWANA
amesema lete laki utaponywa mimi namjua huyu MUNGU WA MBINGUNI yeye
hachukui pesa anakuponya bure, utasema umemuona nabii kumbe umemuona mchawi.
Ukisoma NENO
LA MUNGU kutoka katika kitabu cha 1WAKORINTHO
5:7-8 7 Basi jisafisheni mkatoe ile chachu ya kale, mpate kuwa donge
jipya, kama vile mlivyo hamkutiwa chachu. Kwa maana Pasaka wetu amekwisha kutolewa
kuwa sadaka, yaani Kristo 8 Basi na tuifanye karamu, si kwa chachu
ya kale, wala kwa chachu ya uovu na ubaya, bali kwa yasiyochachika, ndio weupe
wa moyo na kweli.
Sasa Pasaka
iliyochachika ndio unaitaka? easter ndio kuchakachua huko BWANA YESU ASIFIWE
imani zimeharibiwa, baraka zimeharibiwa yaani ni kama DAMU YA YESU imechacha
ndivyo maisha yalivyokuwa kwa wana wa Israel kule jangwani walikula mikate
michachu si ndio? lakini YESU yeye siyo
mchachu usifuate chachu ya zamani DAMU
YA BWANA YESU haijachacha ni fresh BWANA YESU ASIFIWE
Sema BWANA
YESU naomba unisamehe dhambi zangu zote nilizozifanya kwa kujua na kutokujua
ninamkataa shetani na mambo yake yote nakushukuru kwa siku ya leo nimejua
ukweli kuhusu Pasaka, na namna ya kutofautisha kati ya Pasaka na easter na
maana zake, simtaki tena mungu wa kike katika JINA LA YESU Amen.
NABII HEBRON