Pages

Thursday, May 11, 2017


JE MAANA YA EASTER NI PASAKA?

SHALOM, Maana ya Easter siyo Pasaka na Pasaka haiitwi Easter, bali neno Easter linatumika kulifanya jina hili lionekane ndio Pasaka katika sherehe ya kufufuka na  siku ya kufufuka kwake BWANA YESU, neno hili lina maanisha mungu wa kike wa kijerumani, ambaye alipewa hiyo nafasi miaka mingi na watumishi ambao walikuwa chini ya wafalme wa kijerumani ambao waliongozwa na huyo mungu mke ambaye aliitwa Ostren (yaani Mashariki) na baadaye ikaendelea katika dunia yote kwa lugha ya kiingereza akaitwa Easter wakatupiga upofu kuondoa “N” mbele sababu watu wangegundua ni Mashariki na Mashariki siyo Pasaka.

Hivyo usiseme unasherekea Easter tena,  unaposema unakuwa umemsherekea huyo mungu wa kike na siyo YESU, na ukitaka kusherekea Pasaka ya YESU wa kweli sema nasherekea Pasaka, na kwa kiingereza sema happy Passover.

Nashangaa sana,  mimi nilishafanya kazi ya utalii na nilishawabeba Waisraeli wengi sana tena hata katika kipindi cha Pasaka nilipokuwa nipo nao katika safari za utalii (adventure) kama kiongozi wao, sikusikia wakisema happy Easter walikuwa wananiambia happy Passover, sasa cha ajabu, huko kuliko anzia asili ya Pasaka  wao bado wanakiri Pasaka,  lakini huko ambapo siyo chimbuko alikotokea YESU wameghushi (wamefoji) kutupoteza mataifa tuabudu huyu mungu wa kike,

Huu ni mwisho wa shetani kughushi (kufoji) vitu vya MUNGU, zaidi soma blog hii prophethebron.blogspot.com  nimeelezea zaidi kuhusu Pasaka ni nini na Easter ni nini?

NABII HEBRON