Pages

Monday, May 8, 2017


MAOMBI YA MTUMISHI YA KUMLALIA MUUMINI AU MTU KIFUANI KWA NINI WANAYAFANYA?

 SHALOM (BWANA YESU ASIFIWE) Watu mnaompenda MUNGU na msiompenda MWENYEZI MUNGU mimi nawapenda wote ila sipendi hiyo roho ya shetani ndani ya watu itoke haraka. Napenda kufundisha na  kufichua hii siri ya maombezi ambayo inafanywa na baadhi ya watumishi  ambao bado wanatumia JINA LA YESU kumbe tayari wameshajiunga na uwakala wa shetani katika ngazi tofauti, wengine freemason, wengine ngazi ya uganga na uchawi, wengine katika ngazi ya mizimu na majini. Sasa watatumia JINA LA YESU na usishangae hata wanasoma neno, hata pambio wataimba mkijua kuwa ni MUNGU ametukuzwa Kumbe yeye ni wakala wa shetani au majini yamejaa ndani yake, na ili yamsaidie, yatamtie nguvu yamempa masharti baadhi na anapoyatimiza basi anaendelea kusaidiwa.

Yapo maombezi yakutia aibu kiasi fulani yanawafanya watu wengi kutokutetea habari za YESU sababu ya makwazo hayo na mengineyo, mimi nawaeleza haya siyo ya YESU hayo ni ya maagano na YESU hana maagano yoyote juu ya kichawi na ya giza au uchafu. Sasa kuhusu kufanyiwa maombi unaambiwa ulale chini mwanamke, halafu mtumishi analala katika kifua chako amekushika mkono kama vile watu wanavyozini na ameweka miguu yake katikati ya mwanamke halafu anafanya maombi akimuombea mtu, na mtu sababu ya shida ya kutaka kuombewa au kufunguliwa katika jambo fulani anaamini ndivyo ifanyikavyo; nawaeleza dunia yote hivyo siyo, hayo ni maombi ya uchawi, anakuzika, anakuwa juu ya maisha yako na baraka zako, majini yakimsaidia kuiba vtu vyako na zaidi maombi hayo hufanywa kwa siri. Sasa uwe na akili, kwanini asifanye katika nuru? Jibu giza hukumbia nuru. Unapofanyiwa hivyo ni lazima ufunguliwe upya; umengamizwa maisha yako tena umebaki mwenyewe.

Yapo maombi mengine watu wananyonywa viungo vya siri na wengine pastors baadhi wamewanyonya wanawake maziwa na wengine wamewanyonya waumini mate eti ndio wanawafanyia  deliverance na wengine wanafanyiwa deliverance kwa njia ya zinaa iwe wanaume au wanawake. Nawaeleza mmeangamizwa watu hao, kwa njia hiyo anachukua vitu vyako na baraka zako wewe unabakia kuchoka maisha yako.

Wapo wengine wamenyolewa au kukatwa kucha, hayo yote ni maombi ya kuwaangamiza kabisa, hivyo YESU anajua wengi wanamtafuta, mnampenda lakini wakati mwingine mnamtafuta shetani na siyo yeye. Yeye siyo mchafu.  Funguka akili msikubali maombi ya jinsi hiyo ikiwemo na maombi ya kufukia BIBLIA, watumishi wote wa jinsi hii huongozwa na nguvu za majini na uchawi wa kununua, hivyo unaweza ukafikiri ni kazi za MUNGU kumbe ni za majini zimejengwa katika maeneo mengi kiroho na kimwili.

NOTE:
Mambo haya yote hufanyika sababu wanatafuta pesa na wameamua kumchukia MUNGU kutoka katika mioyo yao na kumpenda shetani na kuamua kuziingiza sheria zake na kuzilinda na kuzisambaza zifanye uchafu. Nasema washindwe kila mahali kwa JINA LA YESU WA NAZARETI

NABII HEBRON