Pages

Wednesday, April 1, 2015

JINSI PASAKA YA MBINGUNI INAVYOSHEREKEWA.

Nawasalimu watu wote wa mataifa yote kwa jina la YESU WA NAZARETI aliye hai na sasa yupo mbinguni. Katika kipengele hiki nitaelezea kuhusu pasaka inayosherekewa mbinguni pamoja na wakristo wa kweli ilivyo kwa sababu wakristo na watu mbali mbali husherekea siku hii pasipo kujua inawapasaje washerekee ili wawe wanasherekea pasaka ya mbinguni. Ninasema hivyo kwa sababu nataka uelewe pia yupo yesu wa uongo, na kama yupo hivyo na yeye alivikopi vitu vya YESU wa kweli katika njia yake ili kuhakikisha anawapiga upofu watu kama alivyowapiga baadhi yao badala ya kusherekea pasaka ya mbinguni wakajikuta wanasherekea pasaka ya kuzimu.

Pasaka ni ukombozi ambao kwanza kabisa asili yake ilianza pale MUNGU alipowatoa wana wa Israeli kwa Farao na alipomaliza kuwatoa aliwaagiza wawe wanafanya siku kuu ya pasaka kila mwaka katika vizazi vyote na ndivyo ilivyo; hata na YESU na yeye akaikuta pasaka na akaisherekea (Mahayo 12:1-3) inaelezea hii ndiyo pasaka ya kwanza na pasaka ya pili ni ile ya kifo cha BWANA YESU WA NAZARETI ambaye yeye alikufa kwa ajili ya watu wote, siyo kwa ajili ya wakristo tu ili wapate kukombolewa kama alivyoahidi MUNGU, hiyo ndiyo sababu wakristo husherekea siku kuu ya pasaka kila mwaka kwa kumtukuza MUNGU kwa ajili ya ukombozi wake.

Ili ushiriki pasaka ya YESU WA NAZARETI aliye mbinguni yakupasa ufwate matakwa yake kama yalivyo mapenzi ya MUNGU na endapo utakuwa kinyume tu na YESU  basi uelewe pasaka hiyo itakuwa ni ya yesu wa kuzimu sababu hata na wao kuzimu huwa wanasherekea hivyo hivyo na wale wanadamu wanaofuata ya yesu wa uongo. Ili ushiriki pasaka ya mbinguni ni lazima uwe umeokoka na umebatizwa kwa ubatizo wa maji mengi katika mto; maji yanayotembea, wala siyo maji ya kisima kazi ya mikono ya wanadamu na uishi maisha matakatifu.

Mimi pia Nabii Hebron kabla ya kufunuliwa na YESU kuhusu pasaka ya kuwa ipo ya mbinguni na ya kuzimu niliogopa sana na jinsi alivyonifundisha, nilijiona miaka mingi nilikuwa ni mkristo wa uongo na nilishiriki kusherekea hizo pasaka pasipo kujua; nilizaliwa katika dini ya wazazi wangu, nikabatizwa ubatizo usiotokea mbinguni wa maji ya kikombe. Ubatizo huo ulininyima haki ya kuwa mkristo wa kweli kwa miaka mingi mpaka pale nilipobatizwa kwa maji mengi ndipo nikawa mkristo wa kweli na ndipo nilianza kusherekea pasaka na mbinguni.

Nataka uelewe shetani ni mpumbavu, akawaona watu wanaokoka ila akawateka tena katika huo ubatizo wa kikombe kwa baadhi ya watumishi waliomsaliti YESU wakageuza tena katika ubatizo wa maji mengi wakawabatiza watu kwa majina yao. Nawaeleza uliyebatizwa hivyo wewe haujakamilika, huo ni ubatizo wa Yohana wa kuzimu, na wengine wamebatizwa ubatizo wa kisima, hata hapo ukristo wako unayomashtaka mbele za MUNGU na shetani anacho kitu cha kukushtaki kwa sababu hayo maji hayatembei ni kama josho la kuogeshea mifugo.

Faida ya kushiriki pasaka ya mbinguni; kwanza unamfurahisha MUNGU, unazidi kuinuliwa. Madhara ya pasaka ya kuzimu, unazidi kuangamia kiroho na kimwili na kujiunganisha utakapokufa uende huko huko alipo yesu wa uongo kwa sababu umeyafuata mafundisho ya uongo, hayajatoka mbinguni.

Sema BWANA YESU naomba unisamehe dhambi zangu zote. Uniandike jina langu katika kitabu chako cha uzima wa milele. Sitaki tena kushiriki pasaka ya kuzimu, nimeujua ukweli nakushukuru YESU. Amen.

Zaidi ingia katika website ya www.prophethebron.org, ingia katika link ya blog na YouTube utafunuliwa zaidi.


NABII HEBRON.