JE UNAJUA KUWA
KIBIBLIA AU KWA MUNGU MWANANDOA YEYOTE ANAPOKUWA AMEZAA NA MTU MWINGINE AKIWA
KATIKA NDOA TAYARI AMEIVUNJA NDOA YAKE?
TALAKA YA
KIKRISTO IPO HIVI…
BWANA YESU ASIFIWE, Nawasalimu watu wote wa mataifa yote na
wanandoa na wasio wana ndoa. Ujumbe huu utawasaidia kuzitunza ndoa zenu
zisivunjike na hata ambao bado hawajafikia katika ndoa mkifikia wakati huo
mjitunze ili kusudi aliloliunganisha MUNGU kwa wanandoa kisivunjwe na shetani.
Watu wengi wanafikiri ndoa hazivunjiki zilizounganishwa na MUNGU. Nataka uelewe
shetani yupo kwa ajili ya kuvunja au kuharibu kusudi la MUNGU katika ndoa, na
jinsi anavyotumia huwa analeta roho ya kutokuwa waaminifu kwa wanandoa pale
wanapoanza kuruhusu miili yao iingiliwe na watu tofauti na mwili uliokuwa mmoja
yaani mume na mke.
Ukisoma katika kitabu cha Mathayo 5: 31-32
“31 Imenenwa pia, mtu akimwacha mkewe, na ampe
hati ya talaka; 32 lakini mimi nawaambia, kila mtu amwachaye mkewe,
isipokuwa kwa habari ya uasherati,
amfanya kuwa mzinzi; na mtu akimwoa yule aliyeachwa, azini.”
Utaona maneno ya YESU anayoongelea kuhusu talaka, na neno
linasisitizwa siyo kwa kosa lingine unaruhusu kumwacha mke wako au mume wako,
ni endapo atazini na wewe ukipata uhakika kama ukivumilia . Katika kipengele hiki mimi Hebron nimekuwa nikipigiwa
simu na maswali mengi kuhusu ndoa na wengi wamepata majibu yao na wamepona, na
sasa wanafurahia maisha yao na wanaziona baraka za MUNGU na hata ambao walikuwa
na mpango wa kuzini nje ya ndoa wamepona kwa sababu wameujua ukweli.
Lengo la ujumbe huu, nia yangu; msome ili shetani asiweze
kuja kuzivunja ndoa zenu kwa sababu ndoa inapokuwa na uzima shetani hapendi na
siku zote shetani hapendi mapenzi ya MUNGU yatimie katika ndoa na yeye alibuni
mbinu zake za kuvunja vifungu vya mistari katika biblia; mfano Mathayo 5:32;
“32 lakini mimi nawaambia, kila mtu amwachaye
mkewe, isipokuwa kwa habari ya
uasherati, amfanya kuwa mzinzi; na mtu akimwoa yule aliyeachwa, azini.” Hapa
utaona wazi wazi YESU mwenyewe anasema ni kwa habari ya uasherati tu ndio ndoa inavunjika
na siyo makosa mengine. Sasa hapa inahusisha jinsia zote mbili awe ni mwanaume
amezaa akiwa ndani ya ndoa tayari yeye kaivunja ndoa yake na yeye ni mzinzi,
ndivyo biblia inavyosema kupitia maneno aliyoyasema YESU. Na ikiwa ni mwanamke na yeye yupo katika ndoa
halafu akazaa na mwanaume tofauti na mume wake, hapo tayari ameshaivunja ndoa
yake, na endapo katika hizo jinsia mbili yeye ambaye hajasababisha au ni
mwaminifu yeye hata akioa au kuolewa tena endapo atapata amani mbele za MUNGU
yeye siyo mzinzi na milango yake ya kuolewa au kuoa MUNGU atamfungulia kwa
sababu analiangalia neno lake; amtetee yule ambaye ni mwaminifu katika ndoa.
Point ya pili Mathayo 19: 3-11
“ 3 Basi Mafarisayo wakamwendea, wakamjaribu,
wakimwambia, Je! Ni halali mtu kumwacha mkewe kwa kila sababu? 4
Akakjibu, akawaambia, hamkusoma ya kwamba yeye aliyewaumba mwanzo, aliwaumba
mtu mume na mtu mke, 5 akasema, kwa sababu hiyo, mtu atamwacha babaye na mamaye, ataambatana
na mkewe; na hao wawili watakuwa mwili mmoja? 6 hata wamekuwa si
wawili tena, bali mwili mmoja. Basi aliowaunganisha MUNGU, mwanadamu
asiwatenganishe. 7 wakamwambia, jinsi gani basi, Musa aliamuru kumpa
hati ya talaka, na kumwacha? 8 akawaambia, Musa, kwa sababu ya ugumu
wa mioyo yenu, aliwapa ruhusa kuwaacha wake zenu; lakini tangu mwanzo haikuwa
hivi. 9 Nami nawaambia ninyi, kila mtu atakayemwacha mkewe,
isipokuwa ni kwa sababu ya uasherati, akaoa mwingine, azini; naye amwoaye yule
aliyeachwa azini. 10 Wanafunzi wake wakamwambia, mambo ya mtu na
mkewe yakiwa hivyo, haifai kuoa. 11 lakini yeye akawaambia, si wote
wawezao kulipokea neno hili, ila wale waliojaliwa.
Hapa utaona Mafarisayo walimuuliza YESU kwa kumtega na yeye
aliyajua hayo, akawaeleza je hamkusoma tokea mwanzo MUNGU aliwaumba mume na
mke, na sababu hiyo wataambatana pamoja na watakuwa ni mwili mmoja? Mafarisayo wakamuuliza
tena swali lingine, basi ni jinsi gani Musa aliruhusu kumpa hati ya talaka na
kumwacha? YESU akawajibu, Musa aliyaruhusu hayo ni sababu ya ugumu wa mioyo
yenu, ila haikuwa hivyo tangu mwanzo. Hapa utaona YESU anafunua siri hata ambayo Musa alikuwa na yeye hajafunuliwa, ila
YESU hapa ameifunua hiyo siri kuwa tokea mwanzo haikuwa hivi. Verse 8 ; utaona
YESU anasema wanakuwa ni wawili tena hapa ni baada ya kufunga ndoa, hivyo
aliowaunganisha MUNGU wawe mwili mmoja mwanadamu asiwatenganishe.
Hapa MUNGU anaonya mtu asiwatenganishe; alitoa onyo hili
sababu MUNGU anaona mbali kuwa ni mtu ndiye atakaye tumika na shetani tu ili
kuitenganisha hiyo ndoa na ikawa tena siyo mwili mmoja, sababu mwili wa
wanandoa unaunganishwa na miili miwili, ya kiume na ya kike. Verse 9 YESU akasema
9 Nami nawaambia ninyi, kila mtu atakayemwacha mkewe, isipokuwa ni
kwa sababu ya uasherati, akaoa mwingine, azini; naye amwoaye yule aliyeachwa
azini.” BWANA YESU ASIFIWE, katika
mstari huu wa 9 nataka muelewe sababu kuna watu wametekwa au kufanyiwa matendo
mabaya katika ndoa kwa jinsi nitakavyoelezea utapata picha na ikifika mtu mmoja
wapo iwe ni mwanandoa wa kike au kiume yeye baada ya either mwenzake akiwa
katika ndoa yeye akazaa na mwanamke nje ya ndoa au mwanamke akatoka nje ya ndoa
akaenda akazaa na mwanaume mwingine na hadi matunda ya uzinzi wakayaona. Yeye hata
akiamua kuoa au kuolewa, yeye aliyekuwa mkamilifu yeye anaruhusiwa kabisa na
yeye hataitwa mzinzi.
Soma biblia inasema wazi na adhabu ya mwanandoa anapoingia
katika ndoa halafu akafanya uasherati tu yeye hana cha kumtetea mbele za MUNGU,
na neno halibadiliki kwa sababu ndivyo ilivyo elezwa na adhabu yake iwe ni
mwanaume au mwanamke. Katika siku zako zote za maisha yako iwe utaoa au kuolewa
utakuwa siku zote wewe unazini tu na hata aliyekuoa au kukuoa, hivyo katika
paji lako la uso unabakia na alama hiyo ya jina la mzinzi, kwa sababu mshahara
wa dhambi hiyo ndiyo hiyo. Wewe soma utaelewa, verse 11 YESU akawaambia “11
lakini yeye akawaambia, si wote wawezao kulipokea neno hili, ila wale
waliojaliwa.”
Hapa YESU alijua kuwa unapojua mmoja wapo katika ndoa siyo
mwaminifu hata imefikia hatua iwe ni mume au mke yupo katika ndoa halafu
akaenda kuzaa na mtu mwingine, tendo hili ni libaya na la aibu sana na ni la
kumkasirisha MUNGU sana kwa sababu mwanandoa ambaye yeye amejaribu kutokuwa mwaminifu na akawa adui wa MUNGU
akazini akiwa katika ndoa, akazaa nje ya ndoa tayari yeye ni adui wa YESU, na
pia ni adui wa jamii ambayo yeye alioa au aliolewa na ni adui kati yake na
mwana ndoa mwenzake; yaani amemdharau. Ila MUNGU na yeye anayo neema yake kwa
wanandoa waminifu wanaotendewa mabaya endapo atataka kuoa au kuolewa yeye
anaruhusiwa; talaka atoe na anaruhusiwa kuoa hata atakaye muoa au kuolewa yeye
ataitwa mwanandoa safi mfano; mume bora kutoka kwa BWANA au mke bora kutoka kwa
BWANA.
Ila walioharibu ndoa zao kwa ajili ya uasherati iwe ni
mwanaume au mwanamke; hao siku zote za maisha yao iwe waolewe au waoe, kila
wanapokutana tendo lao la ndoa siyo takatifu bali itakuwa ni uzinzi tu, kuvunja
amri ya sita. Neema hiyo haipo tena kwao ndivyo neno lisemavyo, hivyo chunga
sana ndoa yako, usije ukafanya mchezo wa uasherati halafu ukasema utaoa au
utaolewa tena. Sawa utaoa au kuolewa lakini siku zote tendo lako la ndoa
itakuwa ni uzinifu na uasherati.
Jambo lingine kwa kuongezea, unaweza ukakuta wanandoa kati
yao mmoja wapo yeye alimpata mwenzake kwa kutumia nguvu za giza na hata
wakafanikiwa kufunga ndoa kanisani, ndoa hiyo inakuwa haijaunganishwa na MUNGU
kwa sababu mwanzilishi ni nguvu za giza na kwa sababu kanisa limepigwa upofu na
shetani unakuta watumishi wanafungisha ndoa kupitisha kazi za shetani. Ndoa za
jinsi hii hazidumu kabisa na bado
hazijaunganishwa na MUNGU na hazitakaa ziunganishwe na MUNGU, siku zote giza na
nuru vinatengana, hivyo ndivyo na alivyo katika ndoa. Wapo wengi ambao wanajua
historia ya ndoa zenu kama wewe ulifanya siri ukamteka mwenzako sababu
ulitamani vitu vyake au mafanikio yake, ukamloga, akakukubalia; uelewe hauna
ndoa mpaka sasa na unayo dhambi kubwa mbele za MUNGU kwa sababu umetumika
kuzuia mpango alioupanga MUNGU, mfano; J aolewe na X na wewe ukafanya J aolewe
na Y. Ikiwa ni hivyo maisha yenu ni shida na zaidi hautafanikiwa lolote sababu
siyo MUNGU kaunganisha ila limetumika jina la MUNGU kwa kumsingizia katika haya
makanisa ambayo tayari yamemsaliti YESU baadhi yao.
NOTE:
Watoto wa MUNGU mpaka hapo kwa somo la leo itawafungua wengi
na mtakuwa huru na nira zitawaachieni. Yeye MUNGU ndiye ajuaye mioyo ya
wanandoa na amenifunulia haya kama Nabii wake Hebron niwaeleze; utakaye yashika
hakika ndoa yako itapona na haitavunjika kwa jina la YESU. Wanandoa wengi
walizoea kutenda uasherati na kujitetea eti alichokiunganisha MUNGU
kisitenganishwe. Sasa umeelewa kumbe biblia inasema ukifanya uasherati na upo
katika ndoa siku zote hata ukiachwa au ukaenda kuoa wewe utakuwa unafanya
uzinzi tu hata na huyo aliyekuoa au kuolewa tena jambo ni mmoja na
umemwambukiza mwingine hiyo dhambi.
Wanaume wengi wapo katika ndoa na wana watoto wanazaa na wanawake
ambao hawajawaoa na bado wapo katika ndoa; hao tayari wamezivunja ndoa zao
wanaitwa waasherati na biblia ndivyo isemavyo. Na pia wapo wanawake wengi
katika nchi mbali mbali wapo katika ndoa na wanzaa na wanaume wengine na wapo
katika ndoa na hata kuzaa watoto wa nje na kuwasingizia kuwa ni watoto wa ndoa,
hiyo ni dhambi kubwa sana. Familia nyingi zina shida hii; ingekuwa kama
wanandoa wangekuwa wanacheki DNA utakuta watoto wengi watu wanasingiziwa na
siyo damu zao, hii ni dhambi. Unapokuwa umezaa nje ya ndoa, huyo mtoto anakuwa
siyo wa ahadi kutoka kwa BWANA, ni mtoto wa matunda ya uzinzi.
Nawaeleza YESU anazipenda ndoa zenu, mzitunze kwa usafi na
utakatifu. Wapo wengine wamezaa na wachungaji, maaskofu, mitume, manabii; hata
hao ukizaa nao usifikiri utabarikiwa, unakuwa umejilaani iwe ni mwanamke au
mwanaume na kufanyika wote ni waasherati na kujifungia baraka za maisha yako.
Zaidi fuatilia masomo katika vitabu vya Mtume na Nabii
Hebron, ingia katika website, ingia katika blog na YouTube, utajifunza mengi na
utapona. Karibu pia katika kanisa la YESU NI BWANA NA MWOKOZI WA MATAIFA YOTE. Ndoa
yako yenye shida na vifungo mbali mbali vitaombewa na utapona.
Sema BWANA YESU naomba unisamehe dhambi zangu katika maisha
yangu na katika ndoa uiponye. Uniandike jina langu katika kitabu chako cha
uzima wa milele. Niongoze nisirudi nyuma tena, naacha tabia chafu katika ndoa,
nitakuwa mwaminifu, YESU nisaidie. Amen.
NABII HEBRON.