Pages

Monday, March 30, 2015















JE UNAJUA MAANA YA MSALABA KUWEKEWA TAJI LA MIBA KANISANI NI KUWAVALISHA WAUMINI NA MATESO KATIKA MAISHA YAO?

Kama alivyonituma YESU kwa watu wote niwaeleze ukweli, utakayesikiliza utapona. Baada ya kanisa kutekwa na shetani akayaingiza mafundisho yake ambayo hata katika biblia haijatuagiza hivyo wala kufanya. Inapokuwa ni tofauti tu basi uelewe huyo ni shetani. Ila nitaelezea kwa ufupi kuhusu taji la miba ambalo watu huliweka kanisani wakati wa kipindi cha pasaka wakifikiri ni jambo zuri sababu hawaelewi, walipokea kwa njia ya mafunuo ya wamisionary kwa njia ya mpinga kristo. Wote tunajua kuwa YESU ndiye akiyewekewa taji la miba katika kichwa damu ikadondoka na alipata maumivu kwa ajili yetu. Alivalishwa yeye kwa ajili yetu.

Sasa katika ulimwengu wa roho, kila taji la miba unapowekwa katika msalaba na ni kanisani, kitendo hilo katika ulimwengu wa roho, kila muumini anachomwa na ule mwiba katika kichwa chake na madahara yake, maisha ya waumini hao roho ya mateso inakuwa inawafuatilia na kuwatesa sababu ya hilo taji linalowekwa katika msalaba. YESU alishamaliza pale msalabani, akauwawa katika msalaba uliokuwa unawaulia watu waliolaaniwa na sasa cha ajabu wakristo wengi wao hawaelewi jambo hili hata wakafanya alama ya msalaba ndio ukristo. Alama ya ukristo ni wokovu tu.

Nilipopelekwa mbinguni nilishangaa katika ofisi ya YESU sikuona msalaba wala taji la miba. Ila nilipopelekwa na YESU katika ofisi ya joka kuu nilikuta msalaba, taji la miba. Sasa funguka akili muujue ukweli; miba na msalaba iliyomuulia YESU ilitokea kwa shetani. Cha ajabu makanisa yanaweka product za shetani na hata kuzibusu baadhi yao. Hii haifai. Hatakuvaa msalaba shingoni, unapovaa katika ulimwengu wa roho unahukumiwa wewe na ndio sababu matatizo kwa wakristo hayaishi, hiyo ni sababu moja wapo mahali penye msalaba siyo patakatifu, wala hakuna msalaba mtakatifu ni sababu haijatokea mbinguni.

Msalaba ni mzigo wako wa hayo maovu uyatendayo, watu tafsiri wamekosea;  sasa wanabeba msalaba shingoni kimwili. Tupa usivae; mateso yatakuacha. Ingekuwa ni mtakatifu hakuna pepo lingekufwata, usingekuwa na matatizo lakini cha ajabu wengi wao wanaovaa ndiyo mashetani yanaishi ndani yao. Zaidi endelea kusoma vitabu vya Mtume na Nabii Hebron, ingia katika YouTube, blog, website www.prophethebron.org. watumie na wengine wapone utabarikiwa na YESU.

Sema BWANA YESU naomba unisamehe dhambi zangu zote, uniandike jina langu katika kitabu chako cha uzima wa milele. Najivua misalaba yote niliyoivaa na kuibusu sitaki tena sababu wewe haupo katika msalaba, umeshinda upo mbinguni na uliteswa ili mimi nisihukumiwe tena, na damu yako ikamwagika ili nipone. Asante kwa mafunuo yako uliyempa Nabii wako Hebron yameniponya. Amen.


NABII HEBRON.