Pages

Wednesday, April 1, 2015

JINSI PASAKA YA KUZIMU INAVYOSHEREKEWA.
PASAKA YA KUZIMU IPO HIVI…

Kama nilivyokwisha kuelezea kuhusu pasaka ya mbinguni ilivyo na inavyosherekewa mbinguni pamoja na wanadamu waliomfuata YESU wa ukweli. Hivyo hivyo na kuzimu pia wanaye yesu wao wa uongo na kila wakati wa pasaka wanasherekea hivyo hivyo na wanaungana na wakristo wa uongo waliopo hapa ulimwenguni katika ulimwengu wa roho ili waweze kuwaangamiza na kuwafungia watu wasije wakaenda mbinguni bali wakifa waende huko huko katika makao ya yesu wa uongo.

Hapa duniani hakuna mtu anapenda awe ni mkristo wa shetani na watu wanajua bila kuokoka hauendi mbinguni. Sasa shetani na yeye aliliona hili akamleta na yeye yesu wa uongo katika dunia hii akaanzisha njia zake ambazo ni za uongo hazipo katika biblia ili aweze kuwapata wakristo hata wale wateule wasiende mbinguni wakae, wazubae, wakifikiri wataenda mbinguni kwa akili zao kumbe laah, shetani anajua nini alichokifanya. Nawaeleza jamani, shetani ni mbaya, tena hata usitake uione sura yake. Mimi Hebron nimemwona simpendi kwa kweli, wala usitamani kumwona hata siku moja, unaweza ukawa kichaa kama neema ya MUNGU haipo na wewe. Ni lijitu linatisha na lina roho mbaya.

Mimi nilipelekwa na YESU mwenyewe hadi alipo na akaniambia huyu ndiye adui wa wandamu wote, sasa nimekupa mamlaka upindue kazi zake na ufalme wake katika ulimwengu wote. Uwaeleze watu kweli yangu, uniandalie kanisa la mwisho, muda wangu wa kurudi umekaribia na huyu amewashikilia 98% ya watu wote katika ulimwengu wote ikiwemo na watumishi walionisaliti, sasa huyu ndiye baba yao anayewapa nguvu ya kuujenga ufalme wake shetani na mpinga kristo. Habari hizi zaidi soma katika kitabu cha JINSI NABII HEBRON ALIVYOITIKISA KUZIMU.

Sasa katika pasaka ya kuzimu wakristo baadhi yao  hawaelewi na natumaini wangependa kujua ikiwa ni pamoja hata na watu wasiomjua YESU ili wamjue wapone roho zao.

ILI KUJUA MKRISTO UNASHEREKEAGA PASAKA YA KUZIMU SOMA YAFUATAYO:

·        Ukiwa umebatizwa kwa ubatizo ambao haujatoka mbinguni yaani wa Yohana uelewe wewe ni mkristo wa uongo japo haupendi au haujui. Uwe umebatizwa kwa maji ya kisima, kubatizwa kwa jina la mchungaji hata kama ni maji mengi.

·        Ukiwa ni mkristo halafu unasali katika madhabahu inayoabudu sanamu.

·        Haujaokoka na unapinga wokovu, japo unajiita ni mkristo wewe ni mpinga kristo. Ukristo huo siyo wa mbinguni bali ni wa yule wa uongo.

·        Kubatiza watoto wadogo.

·        Kuabudu wanadamu na kuwaomba wakuombee badala ya ROHO MTAKATIFU, ndiye msaidizi tuliyopewa atuombee yeye tu.

·        Kuombea wafu (ibada za wafu), kuchaji riba kanisa kama ni benki.

·        Kuabudu katika kanisa lolote linalochangisha watu pesa, partners.

·        Kuabudu msalaba na mengineyo yaliyo kinyume na mpango wa MUNGU.

·        Kuongozwa na watumishi wachawi, freemason, illuminati, walioasi, waliojiita, wanyang’anyi, watoza ushuru, kudai malipo ndio upate huduma ya kiroho.

Yapo mengi ila kupitia haya yatakufunulia na mengi zaidi na utapona sababu wengi  wanaonaga wapo sawa lakini kumbe wanapotezwa kwa sababu ya mapokeo ambayo hayapo hata katika biblia, yaliletwa ili kuwavuruga wakristo wawe wakristo wa kuzimu wasiende mbinguni na wanaposhiriki pasaka wakiwa katika hali hii ambayo nimetolea mfano mchache ina maana unayo mambo ambayo siyo ya YESU WA NAZARETI, na kupitia hayo matendo basi hiyo inakujulisha katika ulimwengu wa roho wewe hayo uliyonayo hayajatoka mbinguni basi shetani anakumiliki bila upinzani wowote.

Sasa nawasihi mataifa yote mrejeeni YESU najua hata wapo watumishi wanaompenda YESU ila hawakuyajua haya ya ukweli waliotekwa na shetani. Neema ya YESU ipo sasa wewe rejea na ukatengwe nao, toka huko mahali pa jinsi hiyo, wewe unaona kabisa pako kinyume na YESU wa kweli sasa unafanya nini tena? Usiangalie utukufu wa wanadamu, watakutenga, wao hawana mbingu ya kukupeleka zaidi usipotoka huko sasa na MUNGU na yeye atakukataa na ardhi itakusubiri kwa hamu kukula nyama yako utakapokufa na pia moto wa jehanamu.

Madhara ya kusherekea sherehe ya pasaka ya kuzimu unakuwa unazidi kujiunganisha na kuzimu kwa yesu wa uongo na kukufungia usiende mbinguni na kuzubaishwa ujione utaenda mbinguni ukiwa hapa duniani kumbe katika ulimwengu wa roho wewe unakuwa ni mfuasi wa yesu wa uongo, na hata alama zake unazo katika mwili na katika roho. Mfano katika mwili; angalia ubatizo ulionao na kiroho angalia unapoabudu; je YESU wa kweli anafuatwa au ni masanamu, michango tu na ufisadi. Zaidi soma kitabu cha Nabii Hebron cha UBATIZO WA KWELI KWA ULIMWENGU WOTE.

Sema BWANA YESU naomba unisamehe, nimeujua ukweli, nakukiri sasa wewe ndiwe BWANA NA MWOKOZI wa maisha yangu. Uniandike jina langu katika kitabu cha uzima wako mbinguni. Najitoa kwenye pasaka za kuzimu nilizoshiriki kwa kujua au kutokujua sizitaki tena. Nilijiona ni mkristo safi kumbe  nimetekwaga. Nakushukuru YESU kwa ufunuo uliompa Nabii Hebron kutufunulia siri hizi na sasa nipo huru. Amen.


NABII HEBRON.