Pages

Saturday, January 17, 2015

UNABII WA NABII HEBRON UMETIMIA KUHUSU TANZANIA.

Nawasalimu kwa jina la YESU WA NAZARETI aliye hai au kwa jina lingine anaitwa Nabii Issa. Aliponiita aliniambia atabadilisha Tanzania na nchi hii ndiyo Eden ya sasa nilikuisha elezea katika makala ya Nabii Hebron, usome niliyoyatabiri kuhusu nchi ya Tanzania 2012, 2013, utaona yametimia kwa macho ya damu na nyama.

1.     Nilielezea elimu ya Tanzania itakuwa bure bila malipo kuanzia primary school, secondary school na vya serikali, sasa imeshaanza Zanzibar. Rais katangaza katika sherehe ya miaka 51 ya Mapinduzi elimu ya primary na secondary ni bure upande wa Zanzibar na huku bara itakuwa hivyo hivyo, muda siyo mrefu itatangazwa.


2.     Nilielezea kuhusu mgodi wa Tanzanite 2012 utarudishwa kwa nchi na kwa Watanzania na sasa imetokea, migodi ya Tanzanite upo katika mikono ya serikali na wananchi.


3.     Nilielezea mawaziri watatolewa na bado watatolewa tena wale wote watakaoenda kinyume, ni MUNGU ndiye anafanya kazi hiyo ili kuinua nchi yake.

4.     Nilielezea uchumi utainuliwa, mafuta yatatokea, ndege zitaongezeka na viwanja kuinuliwa na mengine mengi na mnayaona sasa, na bado yatatokea. MUNGU ameachilia kibali nchi hii ainyanyue, aitengeneze kama Edeni.


5.     Na kuanzia 2015, wapo wawekezaji ambao waliwekeza katika nchi hii ila lengo lao ni kuifilisi nchi na wengine wameiibia nchi na wana nchi wake. Hao wataondoka wenyewe mambo yao hayataenda tena. Watakuja wawekezaji wema na Watanzania wenyewe sasa watakuwa ni wawekezaji katika vitu mbali mbali ndani ya nchi yao. Na huu mwaka 2015 mikataba yote isiyo na faida itafutwa ikiwemo ya makampuni ya mafuta upande wa Zanzibar na pia Bara. Haya yote ni mwenyezi MUNGU ndiye ayafanyae na amekwisha nieleza na maneno yake ni kweli na ndivyo ilivyo.

NABII HEBRON.