Pages

Saturday, January 17, 2015





















JE UNAJUA KUWA IBADA YA NJIA YA MSALABA NI NJIA YA KWENDA JEHANAMU?

Kama nilivyokuisha kufundisha katika blog yangu kuhusu msalaba ni nini na nikaelezea kuwa hakuna msalaba mtakatifu katika ulimwengu wote wala haipaswi kuitwa msalaba mtakatifu sababu ni MUNGU peke yake ndiye anayestahili kuitwa mtakatifu, yeye hatendi dhambi. Msalaba ulitumika kuwaulia watu walio laaniwa katika kipindi hicho cha zamani. Nataka uelewe pia hata msalaba aliosulubiwa nao YESU kipindi hicho, msalaba huo huo ulishasulubia wengine kabla yake, ilipokuwa inatumika ilikuwa ilikuwa inahifadhiwa tena hadi itokee mtu ahukumiwe kifo tena. Ukisoma katika kitabu cha Yohana 14: 6 inasema hivi, YESU akawaambia mimi ndimi njia na kweli na uzima. Mtu haji kwa BABA ila kwa njia ya mimi. Nataka muelewe enyi watu wote wa mataifa yote mnaompenda MUNGU na hamtaki mumkosee MUNGU kwa kutokujua japo wapo wanaojua kabisa wanafanya makusudi ili kuwapoteza watu na kuwapeleka jehanamu.

Ili uende mbinguni njia ya kukupeleka ni YESU peke yake na njia hii ni katika roho na tena ni mpaka uokoke na uishi katika maisha matakatifu na kulifuata neno la MUNGU kama lilivyoandikwa katika biblia wala kulibadilisha au kulichanganya na uongo. Katika ulimwengu huu inashangaza sana shetani analitawala kanisa katika sehemu mbali mbali kwa kuanzisha ibada za njia ya msalaba. Sasa nikuulize wewe msomaji tafuta katika biblia hautaona tumeambiwa tufuate njia ya msalaba ili kutupeleka mbinguni, hakuna. Na kama hakuna basi hayo ni mafundisho ya jehanamu ambayo uliyafuata unakuwa na wewe unaifuata njia ya Jehanamu. Na pia nataka uelewe kila unaposhiriki ibada ya njia ya msalaba ina maana na wewe katika ulimwengu wa roho una beba msalaba ukahukumiwe kwenda jehanamu, na hata unapovaa msalaba shingoni ina maana wewe upo tayari kuhukumiwa na shetani na YESU alibeba ili tusisulubishwe tena.

Sasa nawauliza mataifa je yale mateso aliyosulubiwa YESU ni ya bure? Sasa kama siyo ya bure je hamuoni kuwa huku ni kumkufuru MUNGU? Na kama ni kumkufuru MUNGU basi malipo yake ni jehanamu. Na zaidi watu wakapotezwa kabisa haikutosha njia ya msalaba tu, bali wakaamua kutengeneza mwili wa bwana na wakauwekea alama ya msalaba hata mimi Hebron nilisha ila sana pasipokujua, ila nilipojua ukweli nilitubu na nikaponywa na YESU. Sasa unapokula huo mwili wenye msalaba ujijue nafsi yako imekula hukumu na katika ulimwengu wa roho mapepo ya kiyahudi yanakuhukumu bila kipingamizi na utakapokufa unaenda jehanamu.

Sasa mfunguke, amenituma YESU WA NAZARETI niwaeleze ukweli na wewe utakayeupokea utakuwa huru. Na pia hata unasali pale unapoweka alama ya msalaba kwa kulitaja jina la baba na mwana na roho mtakatifu uelewe ni njia ya kumdharau MUNGU na kumfanya yeye ni msalaba wakati MUNGU hafananishwi na chochote. Sasa fikiria ni mara ngapi umemuuzi MUNGU kwa kumfananisha na msalaba au ni mara ngapi umeifuata njia ya jehanamu? Na hata ukaletwa katika nyumba yako. Ikatae kuanzia sasa na ujitenge ili usije ukachomwa moto siku ile ya mwisho na wote wanaoendelea na njia hizo bila kutubu na kutoka katika madhabahu za jinsi hiyo hawatapona na tena waokoke.

Sema BWANA YESU naomba unisamehe dhambi zangu zote. Uniandike katika kitabu cha uzima wa milele na unitoe miguu yangu katika njia ya Jehanamu na niifuate njia yako ya mbinguni ambayo ndiye wewe YESU na siyo kingine. Amen.


NABII HEBRON.