UNABII KATIKA
NCHI YA TANZANIA 2015.
Nawasalimu kwa jina la YESU WA NAZARETI aliye hai na kwa
jina lingine anaitwa Nabii Issa, yeye ambaye atakuja kulinyakua kanisa lake na
pia atakuja katika wakati wa kiama. Yeye ndiye aliyenituma nikafanye kazi yake
na akaniambia katika nchi uliyotokea MUNGU alikuisha iandaa ndiyo Edeni yake ya
sasa ila nitaiinua mimi mwenyewe YESU (Nabii Issa) kwa utukufu wa MUNGU
mbinguni. Tokea mwaka 2012 April kama nilivyoelezea katika vipindi vya redio,
television, na hata katika makala ya Nabii Hebron mengi mmeyaona na yametokea,
nilisema uchawi haufanyi kazi tena katika nchi ya Tanzania, na katika meneo
yote na mmeona. Walioiibia nchi wakatumia na uchawi ili wasijulikane wamejulikana,
nilisema mawaziri wazembe, waizi na wasio waaminifu watafukuzwa na wengine
wataacha wenyewe na mmeyaona, zaidi usome makala ya Nabii Hebron 2012, 2013
kuhusu nchi ya Tanzania utayaona yametimia, nilieleza mengi ila yasome tena na
na uangalie tarehe yaliyotokea, unabii wa Nabii Hebron kuhusu nchi umetimia
kuanzia kiuchumi, amani na mengineyo imetimia kuhusu viongozi wa nchi
kunyanyuliwa yaani Rais Jakaya Kikwete katika Umoja wa Mataifa, viwanja vya ndege,
mbuga za wanyama na mengineyo mengi kama nilivyoelezea huko nyuma.
Haya yote ni MUNGU kayafanya ili kuiinua nchi yake kama
Edeni ya pili ambaye hata sasa yeye yupo Tanzania na ndio sababu Tanzania haitakaa
ivamiwe na nchi yeyote ile na tokea niwaeleze haijatokea nchi ya Tanzania
kuvamiwa kivita na haita tokea, huo ndio ukweli japo wapo maadui wa nchi hii
waliopo nje ya nchi na hata ndani ya nchi hawatafanikiwa lolote wakafanye kazi
nyingine watafanikiwa ila siyo kuigusa nchi hii, hata kama ni nchi matajiri
kiasi gani hawataweza na wameshashindwa tokea 2012. Hayo mengine ni yangu mimi
mwenyewe kama nilivyoelezwa na MUNGU. Katika mwaka 2015 yapo mambo mengi ambayo
MUNGU atayafanya yeye peke yake na lazima yatatimia kabla ya 2015 kuisha na
hata sasa tayari ameanza mengine:-
A. UCHUMI
Uchumi utapanda na kuvunja historia tokea nchi ipate uhuru. Uchumi
utakuwa zaidi katika viwanda, mbuga za wanyama, madini, viwanja vya ndege na Watanzania
wataongezeka kununua ndege zao binafsi za usafirishaji.
Katika kilimo 2015 mvua zitanyeesha nyingi na kwa wakati na
ardhi itazaa zaidi sababu ardhi imerejeshwa uthamani wake ulioibiwa na joka kuu
pamoja na baadhi ya wakoloni na wawekezaji ambao waliwekezaga katika nchi hii
wakiwa wana nia ya kuifilisi tu na siyo mema. Mashamba ya serikali yatafufuka
na viwanda vilivyokufaga na yale niliyotabiri 2012, 2013 yataendelea kuwa juu
na kukua zaidi. Haya yote ni MUNGU ndiye aliyeamua wala hakuna wa kuzuia tayari
imeshakuwa na MUNGU ameniambia Hebron nitayafanya haya yote na mengineyo.
B. BUNGE
Kama nilivyokuisha sema bunge la Tanzania linabadilishwa na
MUNGU kalishika yeye peke yake. Mliona bunge lilivyobadilika wakijali maswala
ya nchi hii, na kufichua uovu na mengineyo. 2015 watafanya zaidi na yapo mambo
mengi ambayo MUNGU atawafungulia wabunge wayajue tena kwa wepesi na yatafichuka
peupe peupe, ikiwemo rushwa, mikataba mibovu, uwizi wa pesa za nchi katika
manispaa na wizara mbali mbali. Wabunge watakuwa wakali sana katika kusimamia
maswala ya sheria za nchi hii tofauti na 2014, MUNGU ameshayaandaa hayo na
mengineyo ambayo sijaruhusiwa niyaseme.
C. UNABII
KUHUSU RAIS WA TANZANIA 2015.
Kama nilivyoelezea 2012, 2013, 2014 kuhusu Rais wa Tanzania
2015, tayari MUNGU amekuisha muandaa mwaka huu na uchaguzi nawaeleza rais
hatatoka kwa waganga wa kienyeji au kwa
kuiba kura au kwa kuwanunua watu kwa pesa. Wengi wanaotamani cheo hicho watatoa
pesa na kuwahonga watu ili wawachague wakianzia katika vyama vya siasa na
katika makundi makundi, haya yote MUNGU kasha yaona. Nawaeleza, muache, mtajuta
kwa jinsi mambo yatakavyogeuka. Watu walizoea wanajipangia wenyewe, mwaka 2015
MUNGU atamweka rais peke yake kupitia Watanzania ambao ni watoto wa MUNGU
aliyewaumba yeye, hawatalogeka, siku ya uchaguzi atawabadilisha wapige kura kwa
yule ambaye MUNGU anamtaka na nataka muelewe Watanzania siku zote kusudi la
MUNGU halizuiliki kabisa na ndivyo itakavyokuwa maajabu 2015. Itakuwa hivyo
hivyo pamoja na Zanzibar pia.
D. UCHAGUZI
WA UBUNGE.
Wabunge wapya wataingia katika bunge na wapo ambao
ikikaribia kipindi cha uchaguzi watakosa kupewa nafasi na vyama vyao. Wengi watahamia
katika vyama tofauti tofauti na baadhi yao 70% watashinda ubunge, wapo mawaziri
watakaopoteza ubunge kabisa na hii itafanyika pia kwa madiwani, madiwani wengi
watakuwa ni wapya. Na pia mpaka sasa wapo wabunge ambao tayari nawaona
wameshapita katika uchaguzi wa ubunge na ushindi ila wakati wake wa kuyasema
haya sijaambiwa, haya alinijulisha MUNGU wakati nikiombea nchi kwa jinsi
nilivyomuomba yeye anionyeshe ila akanionya usiyaseme hayo na mimi ninayatii
maneno ya BABA yangu wa mbinguni.
NOTE:
Watakaotumia uchawi hawatashinda kiti chochote, MUNGU
hapendi uchawi kabisa. Yeye atasimamia uchaguzi mwenyewe na mtaona waliotumia
uchawi watakavyoaibika baadhi yao. Na pia wengine watashindwa kutokana na hali ya
wananchi kutokumpigia kura pasipo yeye kushiriki uchawi katika hali ya kawaida
tu.
MUNGU IBARIKI TANZANIA, UZIDI KUIINUA KATIKA JINA LA YESU WA
NAZARETI. AMEN.
NABII HEBRON.