Pages

Wednesday, January 7, 2015

JE UNAJUA NI JINSI GANI MAKANISA YALIVYOJIINGIZA KWA MIUNGU NA KUJITENGA NA MUNGU WA KWELI?

WAGALATIA 1: 15-16
15 Lakini MUNGU, aliyenitenga tangu tumboni mwa mama yangu, akaniita kwa neema yake. 16 alipoona vema kumdhihirisha mwanawe ndani yangu, ili niwahubiri Mataifa habari zake; mara sikufanya shauri na watu wenye mwili na damu.”

BWANA YESU ASIFIWE, YESU WA NAZARETI, mataifa mlioumbwa na MUNGU aliyeumba mbingu na nchi MUNGU anawapenda sana ili msiangamie na hata mlioangamia tayari endapo utayasikiliza maneno haya nikuelezayo Nabii Hebron na wewe utapona. Alichonituma MUNGU ni kuharibu ufalme wa shetani katika ulimwengu wote na kubomoa ufalme wa miungu yote ya kila aina katika dunia hii na hata iliyopo kuzimu na kazi hiyo imeshaanza. MUNGU anataka aabudiwe yeye peke yake wala siyo kupitia vitu alivyoviumba yeye mfano hata jua, mwezi, nyota, miti, wanyama, hata vya kazi ya mikono ya wanadamu kama vile vinyago au sanamu.

Nitaelezea kwa ufupi na naamini utaelewa na utapona na utakuwa huru. Shetani pamoja na miungu yake wamejiingiza katika makanisa mengi katika ulimwengu wote na kumfanya MUNGU wa kweli asionekane katika makanisa na wakabakia miungu tu 98% ya makanisa yote katika dunia ni makanisa ya miungu ndiyo inayoyaongoza pamoja na waumini wake, na hata waumini hawaelewi ni ki vipi wanaabudu miungu na bado wanajiita ni wakristo au kanisa ni la kikristo na wanasoma biblia na kila jumapili wanaenda kanisani. Walifikiri wanaenda kumuabudu MUNGU wa kweli na kumbe wamepigwa upofu kimwili na kiroho na kumbe wanaabudu miungu na kufanyika kuwa rafiki wa miungu na kuwa adui wa MUNGU wa kweli. Nawafunulia haya mimi Nabii Hebron sababu hata mimi katika maisha yangu nilipotezwa kwa kufundishwa uongo nikajiona ni mkristo safi namfurahisha MUNGU, ila aliponiita nikamtumikie 2010 hapo ndipo nilijiona nilikuwa ninanuka harufu mbaya mbele za MUNGU, sababu sikuujua ukweli na akaniambia mimi ndiye niliye kuumba wewe na hata mifupa ya nyama katika mwili wako ni mimi ndiye niliyeipa nguvu ikue na ukuwe mpaka ulipofikia hapa. Nimekuumba kwa kusudi langu peke yake na nilijua ikifika muda wake nitakutumia ila wewe hauna tofauti na Musa nilivyomuita nikamficha hata alipowekwa katika mto  ule ni mimi MUNGU ndiye niliyoifanya hiyo njia kumhifadhi mpaka wakati ulifika akawatoa wana wa Israeli na wewe ndiye Musa wa sasa uwapeleke watu Kaanani kwa jinsi nilivyokuelekeza.

Katika makanisa ya sasa pamoja na watumishi wengi wao siyo watumishi wa MUNGU bali ni watumishi wa miungu na watu wameshindwa kuwatofautisha watumishi wa MUNGU wa kweli na wa miungu sababu wote wanajiita ni watumishi wa MUNGU. Kila jambo unaloliona mtumishi analifanya lipime katika neno la MUNGU, je anafuata kweli au uongo, ki vipi? Nitakueleza na utaelewa.

A.    Watumishi wa miungu.
Hawa ni watumishi wachungaji, wainjilisti, manabii, mitume, waalimu vile vile ila wewe cha kukusaidia ili umuelewe yupo katika upande gani chunguza haya kwa watumishi wa miungu na bado wanalitaja jina la YESU na kumbe tayari ni watoto wa shetani au waajiriwa wa shetani na ndiyo sababu wanaziendeleza kazi ya baba yao.
·        Ukikuta mtumishi hajabatizwa kwa ubatizo wa maji mengi ambao upo katika biblia umetoka kwa MUNGU wa mbinguni, uelewe yeye yupo upande wa miungu na ndiyo sababu amebatizwa kwa ubatizo wa maji ya kichwa tu au kisima, au kubatizwa kwa jina la mchungaji, watumishi wa aina hii wote wawaeleze wapo chini ya miungu.

·        Watumishi wanaonyang’anya watu mali zao kwa kusema au kutumia jina la YESU hao ni majambazi na ni wanyang’anyi, na kazi ya unyang’anyi ni ya miungu bali MUNGU yeye hubariki.

·        Anayezini na kondoo au waumini, mlevi, anafanya mazingaumbwe anachangisha watu pesa kanisani katika kanisa na waumini wanatii waelewe hapo sipo mahali MUNGU wa kweli yupo, bali ni makao ya miungu, MUNGU amekataa mahali pake ni mahali pa sala tu na kumuabudu yeye na kumsifu, ila kwa miungu mambo hayo yanaruhusiwa na miungu, inawatendea watu miujiza ya kipepo sasa uelewe jinsi miungu ilivyojiingiza kwa njia ya makanisa, na makanisa mengi yanajengwa kwa pesa za miungu na maagano ya shetani. Nilikwisha wafundisha kuwa yupo yesu wa uongo na sasa nawajulisha pia yapo mungu wa uongo na yeye ndiye joka kuu, ila yeye anayo makundi mengi mengi ya miungu kwa jinsi alivyoiumba ili kuwapotosha wanadamu na kuwafarakanisha na MUNGU wa mbinguni ndio wanadamu wasiwe watoto wa MUNGU wawe watoto wa miungu na kuwa adui wa MUNGU aliyeumba mbingu na nchi.

·        Watumishi wote wenye kofia za kuvaa wakiwa wanahubiri, hiyo ni alama ya miungu sababu imeandikwa mwanaume anapohubiri kanisani asivae kofia sababu kichwa chake ni mahali ambapo MUNGU anapitishia utukufu wake, ila miungu wamejiingiza katika kanisa na watumishi wameikubali. Kukubali ni kule kuyatii mambo ambayo MUNGU ameyakataa halafu wanayatenda na hata kuyafanya ndiye uniform zao, hizo ni uniform za miungu.

·        Wagalatia 1: 6-8

6 Nastaajabu kwa kuwa mnamwacha upesi hivi yeye aliyewaita katika neema ya Kristo, na kugeuka injili ya namna nyingine. 7 wala si nyingine; lakini wapo watu wawataabishao na kutaka kuigeuza injili ya Kristo. 8 lakini ijapokuwa sisi au malaika wa mbinguni atawahubiri ninyi injili yoyote isipokuwa hiyo tuliyowahubiri na alaaniwe.”
Neno la MUNGU linaonyesha wazi wazi, unapoigeukia injili ya tofauti na biblia au kuchanganya na uongo tayari umelaaniwa, hii ni sababu MUNGU tayari yeye ameshalaani miungu yote na mambo yake na miungu ikafanya ujanja ikawateka watumishi na wengine siyo kutekwa wamejipeleka kwa miungu ili iwasaidie katika kazi za utumishi wao wa kutafuta pesa na kuharibu maisha ya wanadamu wa mataifa yote kwa kuwapoteza kwa kuwafundisha uongo, na uongo unapouamini au kuupokea hivyo ndivyo unakuwa na wewe unaongozwa na miungu.


·        Kila dini ni pando la miungu, dini zilikuwepo kabla ya YESU kuja na dini ilimkataa YESU WA NAZARETI kwa kusema ameleta elimu gani, elimu ambayo siyo ya wanadamu bali ni elimu ya mbinguni, hata wakati wa kuhukumiwa na baadaye ndiyo walimuua, hata wale mitume wa YESU waliuliwa na viongozi wa dini. Sasa cha ajabu ujiulize sasa kama dini ina muakilisha MUNGU wa kweli kwa nini impinge YESU WA NAZARETI? YESU alileta wokovu peke yake kupitia jina lake na damu yake iliyomuagika msalabani. Mbinguni hakuna dini mimi nimefika wala hakuna mahali pa dini ila pako mahali pa wokovu peke yake na atakayeokoka na kuishi maisha matakatifu ndiye atakaye kwenda, huo ndio ukweli, usipoteze muda usije ukajuta leo uokoke. Baada ya dini na viongozi wake kumuua YESU wakabadilisha makanisa yao wakayaita ni ya kikristo tu na watu katika makanisa wakaamini wao ni wakristo na Kristo alianzisha dini, kumbe ni uongo wao siyo wakristo bali ni upofu wa mbinu za miungu.

Ili uwe mkristo ni lazima upokee kila alichokileta yaani wokovu. Sasa hizi dini zinasema ni za kikristo embu waulize mbona hawaokoki? Wala kumkiri YESU na kuacha uovu na kutenda matakatifu? Jibu hawana. Nawaeleza mataifa yote YESU atakuja kumchukua aliyeokoka kikweli na hata kuja kuchukua dini za kikristo sababu yeye hakuanzisha dini yeye alileta wokovu, hizi dini ni za miungu na ndiyo sababu zinaendeleza injili zake kama elimu ya shule za duniani na siyo elimu ya shule ya mbinguni na kuwafanya wanadamu wamekuwa chini ya miungu ya dunia hii badala ya kuwa chini ya MUNGU aliyewaumba. MUNGU anapendezwa na wokovu mtakatifu peke yake wala siyo dini. Asili ya dini ni miungu kama vile mila zote hizi ni dini, matambiko na hili ni pando la miungu na katika sehemu nyingi, nchi nyingi kupitia hawa viongozi nchi zao zimekosa amani sababu ni miungu inawatawala na nchi imetawaliwa na miungu kupitia watumishi wa jinsi hiyo.

·        Makanisa yenye misalaba, hiyo ni sanamu na kama ni sanamu basi hapo ni mahali pa miungu, hata vazi la mtumishi likichorwa msalaba ile wakiwa ni wa miungu (soma Wagalatia 3:1-3), watu wamepotea sababu ya viongozi vipofu na upofu umeshika mizizi katika dunia yote hata watu wanakata tamaa kama vile hakuna MUNGU tena bali wamebakia waganga, wachawi na shetani. Nawaeleza MUNGU yupo na anakaa na hao wanaomtii ila wasipomtii ni miungu inakaa na waumini wakafanyika kuwa kanisa la miungu. Sasa ufunguke macho ya rohoni na mwilini. Zaidi endelea kusoma makala ya Nabii Hebron na uingie katika website yangu www.prophethebron.org utajifunza mengi na utapona, hautakuwa kama mtu asiye na akili ya kumjua MUNGU wake.

·        Kila Nabii anayejiita mfano yeye ndiye MUNGU , au yeye ndiye mungu mweupe, au mungu mweusi, au yeye ni YESU, au yeye ni Malaika Gabriel au Mikaeli, au yeye ni Maria na wengineo. Hao wote ni mashetani ndiyo yapo ndani yao yanafanya kazi, na miungu inawavurugia na wanakubali iwatumikishe na hata makanisa yao na waumini wao wanakuwa wote tayari ni mali ya miungu ya dunia hii, wafunguke ufahamu watoke wakajitenge nao, dunia imeharibika kiasi ambacho mtu anajiita yeye ni MUNGU au anajifananisha na YESU na watu wakamuamini, wakati MUNGU hafananishwi na chochote kile, na MUNGU siyo mwanadamu, wala MUNGU haoi, wala MUNGU hazai. Sasa jiulize huyu anajiita yeye ni MUNGU aonyeshe nchi yake aliyoiumba au watu aliowaumba, jibu hana, hawa ni vipofu walioteuliwa na shetani ili kuwapofusha watu wabakie kwa miungu. Sasa ikatae na usishiriki, hata sadaka unazozitoa uelewe unazitoa kwa miungu siku zote za maisha yako. Na hata miujiza wanapoitenda ni miujiza ya miungu au mapepo au mazingaumbwe.

·        Miungu ni masikini, ili huduma zake ziendelee ni lazima aombe ombe na kuchangisha sababu wanadamu ni matajiri kuliko miungu na makanisa mengi ni omba omba sababu hawana MUNGU wa kweli bali yana miungu. Au msingi wa kanisa ambalo ni mtumishi yeye anajua siri yake ametoa wapi hiyo huduma ya kipepo na ili huduma hiyo iendelee ni lazima michango, kunyang’anya watu vitu na kuwafilisi watoto wa MUNGU wakiona wamemtolea MUNGU wa kweli kumbe wametoa kwa miungu. Nawaeleza mnaitolea miungu.

·        MUNGU aliyeumba mbingu na nchi yeye ni tajiri, ila MUNGU amechafuliwa sana kwa kuonekana yeye ni omba omba, wakati ni makanisa ya miungu ndio wanaomba omba. Mwaka 2012 MUNGU alikuwa anaongea na mimi kwa uchungu sana na hasira, akanieleza Hebron, kwa nini hawa watumishi wananifanya mimi ni omba omba, na kuliabisha jina langu wakati mimi siyo MUNGU wao, wao wanao miungu ambao ndiyo baba zao. Akasema Ole wao moto upo tayari, na mimi leo nawaeleza mataifa yote manompenda MUNGU msishiriki tena hayo mambo ya miungu, tena na watumishi wa jinsi hiyo ni watumishi wa miungu pamoja na makanisa hayo mpate kuelewa, watumishi wanauza madawa ya kulevya, wenye benki hao ni watoza ushuru, MUNGU hatozi ushuru, kazi ya ushuru ni kazi ya Kaisari, ila kwa MUNGU hakuna mambo hayo kabisa, na kanisa linalojishughulisha na mambo ya Kaisari basi lijielewe tayari limeikaribisha miungu na hiyo ndio njia ya miungu ilivyokaribishwa katika makanisa 98% ya makanisa ya miungu katika ulimwengu, dunia hii wengi ni wachawi, wamejiita, na wengine waliitwa kweli na YESU lakini wamemsaliti, wametekwa na shetani, wamebakia kulitaja jina la YESU kwa mdomo ila ndani ya mioyo yao ni unafiki mtupu. Wanatafuta pesa na ndio sababu makanisa siku hizi mengi ni biashara tu, na kama ni biashara ni mahali a kuwaibia watu pesa zao na kuwafilisi sadaka zao na haifiki kwa MUNGU bali zinapelekwa kuzimu, pesa zao ndio hizo zinatumika kununulia pombe, kununulia mipira ya kondom, mitaji ya kufanyia biashara ya madawa ya kulevya na ufisadi.

NOTE:
Kwa uongozi wa kila nchi zote duniani, nchi na wananchi wanapotezwa na makanisa ya uongo ambayo wanawaangamiza wananchi wenu kwa kuwaingiza kwa miungu na kuzifanya nchi zilaaniwe kwa kupitia watumishi wasio waaminifu au wanaotumia jina la MUNGU kujifichia uovu wao na kumfanya shetani aharibu na apate njia ya kuangamiza nchi zenu. Mimi nawajua kwa macho ya nyama na damu, nawapa njia ya kuwaelewa matapeli na watumishi wa shetani kila serikali ikague simu ya kila mtumishi na msome meseji zao au email zao au mrekodi simu zao. Nawaeleza hata wadadisi watakapozisoma au kusikiliza hizo simu wanaweza wakachanganyikiwa sababu itaonekana mtu ambaye siyo mtumishi yeye kumbe ndiye karibu na MUNGU kuliko mtu anayeitwa mtumishi. Katika ulimwengu huu imebakia 2% tu hao ndio watumishi wa kweli wapo na MUNGU, hao 98% ni watumishi wa miungu. Je hawaoni sasa miungu imetawala makanisa na miungu imejenga makanisa yake na watu hawajui.

Sema BWANA YESU WA NAZARETI naomba unisamehe dhambi zangu, unitoe kwa miungu uniandike jina langu katika kitabu chako cha uzima wa milele. Nakushukuru YESU WA NAZARETI kwa kunifundisha na nimepona. Amen.

Na wewe uwatumie na wengine ujumbe huu ili wapone na utakuwa umemfurahisha MUNGU na umeichukia miungu kabisa.


NABII HEBRON.