A. JE UNAJUA MINARA YA BABELI BADO INAJENGWA
KATIKA MAKANISA YA LEO?
B. JE UNAJUA KUWA MINARA INAYOJENGWA KATIKA
MAKANISA NI SATELLITE ZA SHETANI?
C. NINI MAANA YA MNARA WA BABELI?
MWANZO 11:4-9
“4 Wakasema,
haya, na tujijengee mji, na mnara, na kilele chake kifike mbinguni, tujifanyie
jina; ili tusipate kutawanyika usoni pa nchi yote. 5 BWANA akashuka
ili auone mji na mnara waliokuwa wakiujenga wanadamu. 6 BWANA
akasema, Tazama, watu hawa ni taifa moja, na lugha yao ni moja; na haya ndiyo
wanayoanza kuyafanya, wala sasa hawatazuiliwa neno wanalokusudia kulifanya. 7
Haya, na tushuke huko, tuwachafulie usemi wao ili wasisikilizane maneno wao kwa
wao. 8 Basi, BWANA akawatawanya kutoka huko waende usoni pa nchi
yote; wakaacha kuujenga ule mji. 9 Kwa sababu hiyo jina lake
likaitwa Babeli; maana hapo ndipo BWANA alipoichafua lugha ya dunia yote; na
kutoka huko BWANA akawatawanya waende usoni pa nchi yote.”
BWANA YESU WA NAZARETI ASIFIWE enyi watu wote wa mataifa
yote, YESU anawapenda sana pia na mwenyezi MUNGU anawapenda na hataki mpotee na
kama mlipotea sasa mumrejee yeye sababu injili katika ulimwengu huu
imebadilishwa inachanganywa na uongo kupitia watumishi waliomsaliti YESU WA
NAZARETI wakajiunga na illuminati na freemason pamoja na mitandao ya joka kuu
ambaye ndiye baba yake lusifa. Hapo mwanzo baada ya gharika kuu shetani
aliwaingilia wanadamu katika fahamu zao walipokuwa katika nchi ya Shinari,
katika mji wa babeli wanadamu wakajenga mnara mrefu ili wamfikie MUNGU alipo na
muone, na jambo hili halikuwa ni mpango wa MUNGU bali ni mpango wa shetani ili
wanadamu na wao waangushwe chini kama yeye. Joka kuu alipojiinua mbinguni
(Isaya 14: 12-13) na yeye akatupwa chini na MUNGU. MUNGU hapendezwi kabisa na
wanadamu kufanya kinyume cha mapenzi yake.
Sasa nitaelezea kuhusu minara ya kawaida na minara ya kipepo
ili watu muelewe na mpone katika ulimwengu wote. Nitaelezea mfano wa minara ya
simu kama mahali hakuna minara ya simu fulani hata ukiwa na simu yako haupati
network na hauwezi kupata mawasiliano, katika mnara ambao ulijengwa babeli
lengo la shetani alitaka ufike mbinguni ili apate mawasiliano ya mbinguni na
pia wanadamu watupwe chini kama yeye sababu watakuwa wanakosea MUNGU. MUNGU
akasema hapana akawachafulia lugha sababu zamani watu walikuwa wanaongea lugha
moja wote, sasa ili wasielewane MUNGU akawachafulia lugha hivyo kila mtu
hakuelewana na mwenzake hivyo kazi ikagoma hapo. Na zaidi kupitia kujenga mnara
wa babeli hapo ndipo lugha tofauti zilianza na ndio sababu hata leo hii lugha ni
nyingi sana na makabila yote yana lugha tofauti tofauti asili yake ni pale
kizazi cha Nuhu baada ya gharika walipotawanyika wakaingiwa na shetani baadhi
yao wakajenga mnara wa babeli na MUNGU hakupendezwa na ujenzi huo.
MINARA
YA KIPEPO IKOJE?
Minara ya kipepo ni minara yote ambayo inajengwa katika
makanisa au kanisa lolote lile, uelewe madhabahi hiyo inayo satellite ya kuzimu
na ipo kinyume na MUNGU haijalishi wanalitaja jina la YESU au MUNGU. Nilipokuwa
nikiomba na kuongozwa na Malaika Mikaeli katika kubomoa mawasiliano ya shetani
alivyoyaweka kati yake yeye na wanadamu kiukweli mimi kama Hebron nilishtuka
sana sababu sikuelewaga maana yake hadi pale Malaika mkuu wa vita Mikaeli
aliponijulisha kazi ya hiyo minara kwa kiundani zaidi ila nitaelezea kwa ufupi sababu
ni somo refu ila ufuatilie zaidi katika website yangu www.prophethebron.org na uingie katika
blog nitaendelea kuelezea kwa wakati nyingine. Akaniambia Hebron, hii minara
yote unayoiona katika makanisa yote katika ulimwengu wote hizo ni satellite za
shetani kufanya mawasiliano na hizo madhabahu kupitia majini na mapepo. Akaniambia
kama ulivyokwisha fundisha ni jinsi gani kanisa la YESU WA NAZARETI liwe au
jinsi ulivyoliona kanisa la mbinguni lilivyo na ukaonyeshwa kanisa la kuzimu
lilivyo, je Hebron hauoni tofauti? Nilishtuka fahamu zangu sababu kila kitu
kumbe MUNGU anachokuonyesha lazima anayomaana ili kukusaidia katika picha ya
kanisa la mbinguni analosali YESU WA NAZARETI, halina msalaba, halina mnara,
halina kisima cha kubatizia watu.
Ila kanisa la yesu wa kuzimu niliona lina misalaba, lina
minara, lina kisima cha kubatizia watu
ndani ya kanisa na dini mbali mbali na aina za ubatizo pamoja na masanamu
pamoja na mengineyo. Akanieleza Mikaeli hii minara yote unayoiona inaungana na
minara yote iliyopo katika kanisa la kuzimu na kwa kupitia hiyo minara majini
yanajua hapo ni mahali pao na huja kuziteka roho za wanadamu pasipo wao kujua
au kwa lugha nyepesi ili uelewe hiyo minara inasimama badala ya mnara wa babeli
katika ulimwengu wa roho ili kuwafanya wale wanaoabudu katika kanisa hilo wawe
chukizo kwa MUNGU na pia watupwe katika shimo la moto wasiende mbinguni.
Jambo lingine ni alama ya kanisa la mpinga kristo haijalishi
linaitwa kanisa la MUNGU hii ni kuwapiga watu upofu na siri hii wanaijua
waanzilishi wa hizo dini na hata wao wote wapo kuzimu wanateseka na wanasubiri
moto wa jehanamu. Hivyo watu wote wa mataifa yote mpate kufunguka akili na
kuelewa, shetani alicheza na fahamu za watu na kuwapiga upofu, sasa amenituma
YESU WA NAZARETI niwaeleze ukweli watu wote, wewe utakayetii utapona na wewe
utakayepuuzia haya ile siku ya hukumu damu yako hautamlilia MUNGU katika mikono
yake sababu umeujua ukweli na umeupinga, heri ya hao watakaotii na kujitenga na
sehemu za ibada yoyote yenye minara.
Na zaidi wapo watumishi waliotokea katika kanisa la kuzimu
kabisa na wengine waliitwa wamtumikie YESU aliwaita ila baadaye wakamsaliti
YESU wakaenda kumtii yesu wa kuzimu akawa ndiyo baba yao kabisa. Moja ya
masharti wanavyo pewa pesa ni lazima wajenge minara katika makanisa yao hata
katika nyumba zao au mahali popote ambapo anajua huwa anakaaga au kulala usiku
au mchana. Ukiona hivyo unaelewa hao ni wachawi kabisa na ni watumishi wa
kanisa la shetani na ndiyo ni wawakilishi wake hapa ulimwenguni na hata watu
wanaosali katika kanisa hilo haijaishi wanajiita ni wakristo, waelewe wapo
katika kanisa la shetani 100%. Ila wanapigwa upofu, sasa amenituma YESU
niwafunulie siri hizi ili mfunguke ndivyo shetani alivyoliteka kanisa. Na pia
ujiulize kwa nini watumishi wanajenga minara katika nyumba zao? Je wanahitaji
mawasiliano gani? Jibu unalo. Mtumishi wa YESU WA NAZARETI wa kweli yeye
haitaji mnara wowote, anaye ROHO MTAKATIFU ndiyo direction yake. Ila watumishi
wa kipepo ni lazima awe na minara, sasa wale waliofaulu vizuri katika kazi ya
shetani sababu wanaenda kwa grade tofauti, na wengine minara hii inakuwa ni midogo
kama vile mita moja tu unaona kitu linajengwa kidogo kama becon au nguzo uelewe
huyo ni mchawi, na hiyo ni satellite yake ya mawasiliano na shetani na majini
yanakuja kusema na yeye na kumsaidia kufanya kazi za muendelezo wa lengo la
kanisa la shetani ili kuwateka watu wengi zaidi.
Na zaidi ukiona wanajiita ni watumishi halafu wanaenda
kufanya ibada katika minara uelewe siyo ibada wanapoenda katika minara hiyo na
wengine hutoa sadaka na hata kuyawekea mataji, anapoenda pae anaenda kupewa
nguvu za shetani na kupewa cheo kingine na kuwapeleka au kuwatoa waumini wake
kafara au sadaka kwa shetani.
Na njia rahisi ya kujua hii minara ya babeli au satellite za
shetani ukikuta myingine inawekewa kengele ya kupigwa kanisani, na nyingine ni
katika juu ya paa utaona ncha kali kama msumari imetoboza juu peke yake. Na nyingine
inakuwa juu ya misalaba ncha tofauti na nyingine wanaweka ncha katika kitu
mfano wa mwezi, na nyingine ni bendera kabisa zinakuwa makanisani na ipo
milingoti kabisa. Hayo yote ni satellite za shetani, mambo haya watumishi
wanajua siri hizo na lengo lao ni kuuangamiza ulimwengu wote.
Minara nyingine ya shetani ni mikuki, fimbo zinazobebwa
makanisani na watumishi viongozi, hizo ni satellite za shetani ili kuwaongoza
watu waende kuzimu na kuwachunga wasitoke katika zizi hilo la shetani, japo
kimwili linaitwa ni kanisa kwa kuwapiga watu upofu, sasa mataifa yote fungukeni
ufahamu katika jina la YESU WA NAZARETI aliye hai.
Kama mtumishi unampenda MUNGU kweli na umehsajua ukweli ili
upone utubu na uondoke hapo hata wewe muumini. Mshukuru YESU aliyenifunulia
haya natumaini mamilioni ya watu mmepona sasa na hautadanganyika.
NOTE:
Kila kitu ambacho unaliona lipo tofauti na biblia linajengwa
au kuwekwa katika kanisa uelewe hapo pana satellite za kupeleka watu kuzimu na
siyo mbinguni, haijalishi wanatenda miujiza, wanapiga vinanda na miziki mizuri
na mengineyo. Zaidi chunguza katika nchi yako utaiona ni nyingi na katika nchi
nyingine ipo wazi wazi kabisa, hiyo ndiyo minara ya babeli ambayo ni satellite
za shetani ambazo anawawekea wanadamu ili waangushwa chini katika shimo la
moto, na kila mtu ambaye yupo katika kanisa lenye minara ajielewe tayari na
yeye yupo kuzimu roho yake na nafsi yake. Sasa utubu, sasa utolewe kuzimu na
nafsi yako irejee na utoke hapo usishiriki tena.
Sema BWANA YESU WA NAZARETI, naomba unisamehe nimetenda
dhambi nimejenga mnara wa babeli kwa kujua au kutokujua naomba unisamehe na
mengine yote, uandike jina langu katika kitabu chako cha uzima wa milele. Uniongoze
wewe peke yako nisipotee tena. Amen.
Nakufunika kwa damu ya YESU WA NAZARETI na nateketeza minara
yote ya shetani na kuharibu mawasiliano yao yote duniani, angani na
kuzimu. Naibomoa kwa moto wa mbinguni iwe majivu na YESU nakuomba uwafungue
mataifa yote wakurejee sababu unarudi sasa. Nakuomba uwaponye wengi zaidi na
wakurejee wewe. Amen.
Zaidi endelea kusoma masomo katika makala ya Nabii Hebron
Kisamo utaelewa mengi na utafunguka hautapotezwa tena katika jina la YESU WA
NAZARETI.
NABII HEBRON.