Pages

Friday, January 9, 2015

ILLUMINATI NI NINI?

Illuminati ni chama cha joka kuu ambacho lilianzishwa katika mwaka wa 1000 ila lilijulikana mwaka 1700 hapa ulimwenguni. Aliponiita YESU nikaifanye kazi yake ya kuupindua ulimwengu umrudie MUNGU akaniambia Hebron ninayokueleza kuupindua ulimwengu ina maana tayari upo ufalme uliojengwa na lengo lake ni kuwazuia watu wasiende mbinguni. Sasa Hebron nimekupa mamlaka kwa jinsi ya tofauti kwa ajili ya kuharibu ufalme wa shetani alioijenga hapa ulimwenguni na akashirikiana na watumishi hata niliowaita mimi wakanisaliti, badala ya kuendeleza kazi yangu na kujenga ufalme wangu baadhi yao niliyowainua hata kwa kiwango cha kimataifa na wengine hata siwajui wamechipuka na kuungana na shetani wakaupindua ulimwengu.

Sasa Hebron nakutuma na mimi YESU akanipa maelekezo na nilifanya na bado naendelea jinsi aniongozavyo yeye. Akaniambia, adui mkubwa wa MUNGU pamoja na mimi ni hicho chama cha illuminati sababu ndicho chama cha joka kuu alichokianzisha mwaka wa 1000. Lengo ni kuupindua ulimwengu hicho chama hicho ndicho lengo lake, maneno hayo alinieleza YESU, ila nitaelezea kwa ufupi ila endelea kusoma makala ya Nabii Hebron Kisamo nitaendelea kuelezea kila mara sababu ni somo refu sana. Chama hiko ndicho chama chenye pesa kuliko chama cha freemason. Illuminati ni chama cha joka kuu na freemason hiki ni chama cha lusifa amekianzisha yeye chama hiki lilianzishwa na mtu anaitwa Adan. Hichi ndicho chama ambacho kilitaka kuanzisha mtandao wa mashoga hapa ulimwenguni kupitisha katika ncho mbali mbali na baadhi ya nchi wamekataa huu mpango wa shetani na mimi nawaeleza endeleeni kuwapinga na mumkatae, mnapoyakubali mjue mmemkubali joka kuu na mnapokataa muelewe mmemkataa joka kuu.

Ni ajabu sana hapa ulimwenguni yapo makanisa yanayoruhusu ushoga tena wanafungisha ndoa, hayo makanisa yanayofanya hivyo kazi yake ni kuupindua mpango wa MUNGU na kujenga wa shetani, uyakimbie ili upone. Aliponituma YESU kwenda kuzimu kumtoa aliyemsaidizi namba tatu katika ufalme wa shetani ambaye alikuwa ni mwanadamu na ni mtanzania nilishangaa sana kukuta yeye ndiye aliyekuwa mwenyekiti wa chama hicho cha illuminati na ndiye aliyemiliki hata account zote za pesa zao alikuwa anaitwa Maxwell sasa anaitwa Isaya ameokoka. Yeye alihusika kusimamia kitengo hicho pia ila hapa duniani kimwili anaonekana ni mtoto ila nilipoenda kuzimu alikuwa ni mtu mkubwa sana ambaye ukubwa wake ni kama mlima mrefu, alikuwa ana mikono nane ana macho matatu na anayo radio call katika kichwa chake, hawa ndio walioanzisha ushoga na chama cha mashoga ambacho ni mtandao (MWUNWM)- Mashoga Wa Ulimwengu Na Wake za Majini, hicho ndicho kirefu chake na mtu huyo kule kuzimu anaitwa P.BW 16 ndiye kiongozi wa mashoga, hivyo mtu yeyote aliye shoga yeye ni mke wa majini. Sasa ni ajabu nchi zimekubali wananchi wake wawe wake za majini na baadhi makanisa yana thubutu hata kufungisha watu ndoa za jinsia moja ili kuwageuza wanadamu wawe wake za majini. Hivi ndivyo hiki chama lilivyoshughulika katika kuupindua ulimwengu, sasa ni mwisho kila mtu aelewe na alikatae kama anampenda MUNGU ila kama anampenda joka kuu atabakia nacho na baba yake atakuwa ni shetani milele na hata sasa wale waliopo katika chama hicho hao baba yao ni shetani na mungu wao ni joka kuu.

Chama hiki lengo lake ni kuwafanya wanadamu watoke kwa MUNGU wa kweli na kuwapeleka kwa shetani na zaidi waliotumika wahubiri waliojenga na chama hicho wakawa ni makuhani wa shetani, halafu hapa duniani wanajifanya wanahubiri injili. YESU amenituma niwaeleze mataifa yote ili mpone sababu anawapenda.

Katika hii benki ya Illuminati ipo kuzimu ambapo katika ardhi ukitoka kuzimu unatokea katika nchi ya Bangladesh, ila sasa nimeshailipua.


PICHA YA LANGO LA CHAMA CHA ILLUMINATI KUZIMU

Katika picha ya lango la illuminati kuzimu, sasa utaona upo msalaba na unayo alama yake ya mnara juu ya ncha. Hii misalaba ililetwa na hawa illuminati ili kuwapoteza watu wakijua kuwa msalaba ndiyo YESU wakati YESU siyo msalaba, na ndiyo sababu ukiona wanachama wake utaona wanavaa misalaba shingoni. Embu wachunguze wanamiziki wale walio wanachama wake utaona wanayo misalaba na wengine kwenye pete, kama nilivyoeleza katika makala zangu embu endelea kusoma nimeelezea kuhusu misalaba na kuwa msalaba haupo katika kanisa la mbinguni ila upo katika kanisa la kuzimu, na ndio sababu wale watu waliookoka wakristo wa kweli hawaweki misalaba. Waliijua siri hii kupitia ROHO MTAKATIFU, mimi nimeyaona kuzimu na macho yangu na nimeyabomoa na amenieleza YESU niwaeleze, wewe unayetaka kupona utapona na wewe unaye kaza shingo damu yako haitamlilia MUNGU kwenye mikono yake wakati wa hukumu. Na makanisa ni mengi sana ya illuminati ambayo ni ya joka kuu.

HII NI PICHA YA KIKOMBE CHA KUWAPAKA MAFUTA WATUMISHI WANAOTUMIA NGUVU ZA GIZA NA MANABII WA UONGO ILI WAPANDISHWE VYEO
(NIMEKICHOMA HAKIPO TENA).

MAANA YA ALUMINATI

A= THE ADAN
L= LEARN TEAM
U= UNITED
M= MIRROW
I= IBRAHIM AND ADAN
N= NEW
A= AREA
T= TO
I= KILL THE HUMAN.
Hii ndiyo maana kwa kila herufi.

Sasa ukiangalia katika ulimwengu hata labda katika eneo lako wewe jichunguze utaona kuwa hiki chama kinaongozwa makanisa mengi na hata kuwafanya watoto wa MUNGU wanaompenda MUNGU na wasijue kuwa wameingizwa katika hichi chama kupitia makanisa na kutengwa na MUNGU pasipo wao kujua, enyi watu wa mataifa yote YESU WA NAZARETI anarudi kila unabii umetimia na amenieleza kila mara ninapoongea na yeye waeleze watu wamrejee waeleze ukweli ili wapone roho zao wengi wamepigwa upofu hawaelewi sasa uwajulishe Hebron na mimi YESU WA NAZARETI nawaangalia na Malaika wanachukua rekodi yao hao watakaochukua hatua sasa kutoka katika makanisa yaliyojiingiza huko na yaliyo wanachama wa illuminati, watajua waeleze kwa mifano wataelewa sababu hayaandikwi majina. Ila chunguza wewe mwanadamu utapona.

Sema BWANA YESU naomba unisamehe dhambi zangu zote, unitoe katika pango la illuminati uniokoe na uniandike jina langu katika kitabu chako cha uzima, ulitoe katika kitabu cha shetani. Uniongoze milele wewe peke yako, na siku ile ya mwisho naomba uninyakue nisishiriki mateso ya dhiki kuu. Amen.

Ubarikiwe, nawafunika kwa damu ya YESU KRISTO WA NAZARETI aliye hai na yupo mbinguni anayejiandaa sasa kuja kulinyakua kanisa lake.

NABII HEBRON.