Pages

Monday, January 5, 2015

JE UNAJUA KUWA KITABU CHA SHETANI CHA KUANDIKA MAJINA YA WATU KINAITWA RADO?!

BWANA YESU ASIFIWE watu wote wa mataifa yote na YESU anawaoenda, amenituma niwaletee habari zake za mbinguni na kuwatetea na kuwatoa katika mateso ya shetani wale aliowafunga wote. Ilikuwa ni siku ya kumpinga joka kuu na utatu wake kuzimu, niliingia na YESU WA NAZARETI pamoja na Malaika mkuu Mikaeli, tukafika katika ofisi hiyo headquarters ya joka kuu na nikaonyeshwa jinsi alivyowatesa na kuupindua ulimwengu na watu wakawa wameandikwa katika kitabu chake, ni kitabu kikubwa sana Malaika Mikaeli akalichukua na ndani yake niliyaona majina ya watu mabilioni walio hai na hata waliokufa ambao tayari ni watu wake.

Niliposoma niliogopa sana, niliona ulimwengu karibia wote wapo, hata sikuweza kusoma nikamaliza. Akaniambia BWANA YESU WA NAZARETI Hebron hii ndiyo kazi ya shetani aliyoifanya akishirikiana na watumishi waliomsaliti kukijaza majina ya watoto wa MUNGU kuwapeleka jehanamu. Nikakifunga kitabu nikamaliza kukisoma, YESU akaongea na mimi kwa sauti ya ukali, akaniambia uwaeleze watu ukweli wasije wakaenda jehanamu ila ukimueleza mtu akadharau damu yake haitamlilia MUNGU katika mikono yake, wewe ndiye Nabii wa mwisho, uimalizie kazi yangu na jinsi tutakavyokuelekeza, sababu kazi hii siyo wewe Hebron uifanyaye ni MUNGU ndani yako, wewe ni chombo na ni mjumbe wa MUNGU katika hicho kitabu cha majina ya watu walioandikwa kwenda jehanamu.

Kwa ufupi niliona majina ya wachungaji wanaobatiza watu kwa ubatizo wa maji ya kikombe, majina ya watumishi wachawi na illuminati pastors, freemason pastors na wanamziki illuminati, freemason, watu maarufu sana wakiwemo marais waliopo hai na waliokufa, viongozi wa dini na madhehebu pamoja na waumini wao. Wachawi, walevi, waongo, watumishi wanaofanya mazingaumbwe, watumishi wanaojiita wao ni mungu wa majeshi, wanaojiita wao ni YESU, wote wanaoabudu misalaba, makanisa yanayofanya biashara yenye mabenki, SACCOS, watu wanaoendaga casino, wanaochezaga miziki ya dunia (disco), wanaoabudu watoto wa MUNGU na kuwafanya wao ndio MUNGU, na watu ambao hawajaokoka majina yao yalikuwepo katika hicho kitabu kinachoitwa RADO.

Nitaelezea kwa ufupi, baadaye baada ya kuzinduka ufahamu nikafundishwa na YESU tena akaniambia zaidi, hata wanadamu hawaelewi maana yake sasa uwaeleze sababu wengi hawajui ila na wengine wanaijua RADO hicho kitabu wao walishafika katika hiyo ofisi ya shetani hivyo hao manabii ni lazima wavae vitu vya jina hilo, akaniambia Hebron wewe ndiye mtumishi wa kwanza kukupeleka huko na kukuonyesha haya na wala sitapeleka mwingine sababu utaimalizia kazi ya kuharibu ufalme wa shetani kama nilivyotaka mimi na BABA yangu mbinguni. Sasa unapovaa kitu chenye jina RADO ujielewe katika ulimwengu wa roho wewe umejiweka katika kitabu cha shetani na mwili wako na maisha yako anaye yeye. Niliogopa sana kukuta kitabu cha shetani anachoandikia majina watu kimeandikwa RADO.

Nawasihi mataifa yote muokoke ili majina yenu yatoke katika kitabu hicho; sema BWANA YESU naomba unisamehe dhambi zangu zote, uniandike jina langu katika kitabu chako kilichoandikwa uzima na milele, ulitoe katika kitabu chake kilichoandikwa rado, uniongoze BWANA YESU. Amen.

Nakufunika kwa damu ya YESU WA NAZARETI aliye hai.


NABII HEBRON.