Pages

Thursday, December 11, 2014

NINI MAANA YA CHRISTMAS CARD?
JE UNAJUA KADI ZA KRISMASI NI MPANGO WA SHETANI?
SOMA HAPA….

Nawasalimu watu wote wa mataifa yote, ambayo yeye YESU wa mataifa yote ndiye atakayewaokoa wanadamu ili wamrejee MUNGU kwa kupitia yeye peke yake. Ni miaka mingi shetani aliifanya dunia kama anavyotaka na kuipindua pindua na kuwakosesha wanadamu wapotee wamfuate yeye hata wale wasiompenda shetani wakatekwa pasipo kujua na yapo mambo mengi aliyoyabuni shetani na serikali yake na yakaletwa hapa ulimwenguni na wanadamu wakayaona ni mazuri kwa macho ila katika roho ni hatari sana. Hata mimi sikuyajua mpaka pale YESU aliponitokea, akanijulisha hayo, na YESU aliniambia, nawapenda watoto wa MUNGU, nilikosa wakumueleza na kuufichua uovu wa shetani ambao amewatekea wanadamu na wengi hawajui watumishi waliomsaliti na kama nilisalitiwa ina maana tayari wamekuwa katika umoja wa adui hivyo habari zangu haziwezi kwenda mbele. Ila sasa uwaeleze watu wote ukweli atakayesikia na kuifanyia kazi atapona, atakayekaza shingo ataangamia.

Mimi mwenyewe kama Hebron mara nyingine kwa jinsi nilivyooneshwa ulimwengu ulivyopotea natamanigi hata niondoke katika uso wa nchi, ila siku moja nilipokuwa nikiwaza tu, nikasikia sauti ya MUNGU kwa ukali, ni maneno gani hayo unayoyawaza? Akaniambia, hautaondoka katika uso wa nchi mpaka pale atakapokuja mwanangu kulinyakua kanisa lake, akaniambia, nimekuchagua wewe uikomboe dunia na watu watoke kwa shetani, watoto wangu wamepotezwa na adui na wanajiona wapo sawa. Nitautumia mwili wako kama chombo changu, utukufu wa kanisa la mwisho ni mkuu kuliko wa kwanza, na ndio unatimia na itakuwa kama vile kipindi cha Sodoma na Gomora. Wengi waliambiwa watubu wakacheka na baadaye waliungua kwa moto. Na itakuwa kama vile kipindi cha Nuhu, walimcheka Nuhu amechanganyikiwa na kwako ndivyo itakavyokuwa, mimi ndiye ninayesema na wewe peleka habari zangu. Na mimi Hebron nakuletea wewe na wewe uwatumie na wenigne na siri hii ulimwengu wote hawaijui zaidi ya vyama vya illuminati na freemason kuhusu kadi za Krismasi zinazotumika hapa ulimwenguni, asili yake ni wapi na ni nani aliyezibuni hizi kadi za Krismasi na malengo yao ni nini?

Ukisoma katika kitabu cha Mathayo 2:9-11
9 Nao waliposikia maneno ya mfalme, walishika njia; na tazama, ile nyota waliyoiona mashariki ikawatangulia, hata ikaenda ikasimama juu ya mahali alipokuwapo mtoto. 10 Nao walipoiona ile nyota, walifurahi furaha kubwa mno. 11 Wakaingia nyumbani, wakamuona mtoto pamoja na Mariamu mamaye, wakaanguka wakamsujudia; nao walipokwisha kufungua hazina zao, wakamtolea tunu; dhahabu na uvumba na manemane.”

Utaona YESU alipozaliwa mamajusi walimpelekea zawadi, hazina walizozifunga, vitu vya thamani dhahabu na vinginevyo. YESU hakupelekewa kadi alipelekewa kitu halisi, kadi haina kitu chochote. Kadi siyo soda, siyo dhahabu, siyo zawadi, zawadi siyo maneno, zawadi ni kitu halisi. Nikuulize swali je kadi hayo maneno unayoyasoma ni kitu halisi? Jibu siyo. Watu wengi walipigwa upofu, hata mimi Hebron nilikuwa sijui haya na nilipojua nilishtuka nikayahifadhi mpaka muda wake umefika niwajulishe maana ya kadi ya Krismasi. Asili ya MUNGU au mpango wa MUNGU katika siku ya Krismasi, ni siku ya kumpa MUNGU zawadi na ni siku ya watu kupeana zawadi halisi na kufurahi. Lakini imekuwa ni kinyume, shetani akaipindua akabuni kitu kinaitwa kadi za Krismasi na zikaletwa hapa ulimwenguni.

Vizazi vingi vikashiriki kuwa na kadi za Krismasi na kutumiana zoezi hili   mpaka sasa nafikiri katika ulimwengu huu 90% ya watu wote tayari wameshapokeaga kadi za Krismasi au hata kutumiana wao kwa wao. Ila ufurahi kwa sababu ujinga wa shetani alioutumia sasa naufichua wazi na kueleza kila kitu na lengo lao. Waliipindua siku ya Krismasi ndiyo siku ya kupeana zawadi ambayo ndiyo 25.12 kila mwaka, wakaifanya iwe 26.12 wakaiita boxing day. Nikuulize swali, je siku alipopelekewa YESU zawadi ilikuwa ni siku ya pili ya kuzaliwa kwake? Jibu, ni siku ile ile walioona nyota usiku na wakaifuata na hawakwenda mikono mitupu. Sasa shetani akaipindua ili kuivuruga Krismasi, ile siku ya Krismasi wanatakiwa wampelekee YESU zawadi, akabadilisha wampelekee kadi, na ile siku ya kumpelekea YESU zawadi ambayo ni siku aliyozaliwa ikabadilishwa jina boxing day. Je ushawahi kujiuliza kwa nini iitwe boxing day 26.12? majibu utayapata sasa, na je umeshajiuliza siku zote kwa nini imeitwa boxing day? Na swali lingine hivi ikiitwa boxing day ina maana pia katika maboksi ni empty, hiyo ni empty day. Hii yote ni ili kuvuruga watu wasipate Baraka za YESU na wamkosee MUNGU kama ilivyo watu wengi hawaelewi ila sasa uelewe ukweli ndio huo, hakuna kadi ya Krismasi.

Madhara ya hizi kadi, kila unapoitumia tayari wewe unakuwa umewatumia kuzimu kadi yao na unasherekea na yesu wa kuzimu sababu na yeye sherehe yake huanza 23.12-27.12 kila mwaka.

Na pia unazikosa Baraka za kweli za Krismasi za mbinguni pasipo wewe kujua. Nilipoingia kuzimu niliyaona na niliyajua hayo na kitendo hiki cha kutengeneza Kadi kilikuwa chini ya Maxwell ambaye alikuwa ni mtu wa tatu katika ufalme wa shetani na aliyeficha siri zake zote, ila YESU alinituma nimemtoa na sasa ni mwanadamu wa kawaida anaitwa Isaya. Unapoitumia hiyo Kadi tu hata ukimuandikia mtu uelewe ulikuwa unamtumia joka kuu, lusifa na Maxwell na watu wengi wamemtumia ikiwemo hata mimi Hebron pasipokujua. Yaani kile kitendo cha kuvinunua tu tayari umeungana na kuzimu au kuitamani tu. Na katika hiyo kadi ya Krismasi zipo rangi saba ambazo nitazielezea katika makala nyingine zinamaanisha nini ila kwa ufupi zinawekewa nguvu za roho za uongo au mpinga kristo azidi kusambaa huku duniani hata kwako wewe unayetumiaga kadi hiyo. Ila sasa uelewe.

Na pia wakabuni njia ya haraka zaidi, wakatumia internet wakaweka kadi ya Krismasi ili watu washiriki kwa haraka wawapate wengi kabla ya YESU kurudi, shetani awe amewateka wengi. Ila ashukuriwe MUNGU anayetupenda. Nataka uelewe haya mambo mawili. MUNGU yeye hutoa zawadi kamili inayoonekana siyo zawadi ya maneno matupu. Ila mpango wa shetani yeye anatumia kadi na watu hawaelewi. Tazama hata enzi za kina Ibrahim watu walipeana zawadi na siyo Kadi, jiulize hizi kadi sasa zimetokea wapi? Je ndio ufunuo wa MUNGU? Jibu,umelipata. Ila sasa mkitii mtakula mema ya nchi na kuyatapika ya  shetani. Ni ajabu sana hata katika makanisa utakuta mtu au mkristo amenunua kadi kadi ya Krismasi ameiandika special for JESUS (yaani kadi ya YESU tu). Amemuandikia YESU nakueleza ukiandika hivyo unakuwa umemuandikia yesu wa uongo wakati wewe haupendi.

Nimekurudisha katika formula ya MUNGU yeye hatumii kadi ni kitu halisi. Ila shetani ili amuunganishe wanadamu na Krismasi ya kuzimu akabuni kadi na zimekubalika hapa ulimwenguni na zaidi shetani na serikali yake wanafurahia sana na kushangilia pale mtu akiwa nayo au kumtumia mtu wanafurahia kazi yao inakubalika na wanadamu, na mpango wa MUNGU umepuuziwa. Sasa swali je wewe unataka mzigo wa kadi za shetani au zawadi tu? Na katika zile kadi za Krismasi kuna vitu vimewekwa na vyote vinavyo maana yake nitawaelezea maana yake.

A.    CARD YENYE PICHA YA NYOTA
Ile nyota inatumika sasa kuiba nyota yako na shetani anaichukua na ndio sababu watu wengi unakuta hata hawajalogwa na wachawi ila maisha ni magum na ni mabaya ni sababu nyota yako imeibiwa na shetani. Kwa njia ya ile card iliyopo Krismasi kadi na shetani anakucheka hauna ujanja. Hivyo ni lazima anyanganywe nyota za watoto wa MUNGU arejeshe mara moja.

B.    ALAMA YA MWEZI
Alama hizi zinatumika katika kadi za Krismasi, ina maana kupitia ule mwezi uliopo katika hiyo kadi kila mara maisha yako yanachomwa na huo mwezi kwa ncha yanatobolewa katika ulimwengu wa roho.

C.     CHRISTMAS LIGHT
Maana ya zile taa zinazowaka na kuzimika pale inapowaka inasababisha maisha yako kuwaka na kuzimika, hata wale wanaoenda disko zile taa za disko light kazi yake ni kuuzimisha maisha yako, iwe ni mahali popote unaona taa hiyo uelewe maana yake ndiyo hiyo ila watu wanaona ni urembo tu. Shetani yupo kazini.

D.    MIPIRA YA KUNING’INIZA KATIKA MTI WA CHRISTMAS TREE.
Ile mipira unakuwa ndio wewe uliyezihifadhi au kurembea na ile kamba ni mikuki wa kukuchoma maisha yako. Nataka muelewe jinsi shetani ni mbaya na hawapendi wanadamu, na sasa wewe uamuzi ni wako.

E.     VIBOKSI
Zile picha za viboksi unapokuwa navyo katika kadi ya Krismasi katika ulimwengu wa roho Baraka zako zinaibiwa zote na maisha yako yamebakia boksi yaani tupu na shetani anawanyanyulia bango ninao uhalali sababu wana vitu vyangu, kwanza hawa wanadamu hawakupendi, wakati kawateka fahamu, sasa shukuru sababu maisha yako na vitu vyako ulivyoibiwa nitakuombea uje kanisani nimnyang’anye shetani vyote uwe sawa sawa na usizitumie tena wala kuwatumia watu, ili usipatikane kwa njia hiyo na kama unazo zichome.

Hivi vitu vinavyoitwa Christmas tree, father Christmas, kadi za Krismasi na boxing day vyote vimetoka kuzimu vikaletwa ili wanadamu wamuuzi MUNGU na wapate kuwaibia watu maisha yao na baraka zao. Ninajua inauma sana lakini ukweli ndio huo. Ili Krismasi yako iwe nzuri usiweke hivyo vitu katika nyumba yako, hata  ofisini, hata hotelini, unakuwa kuzimu yote iko kwako sababu wanaona vitu vyao na hiyo ni njia.

Zaidi katika huo mtandao wa kadi kuzimu, bado hawakuishia hapo tu katika kadi za Krismasi, walitengeneza kadi za mapenzi, uchumba, marafiki, baba, dada, uncle, son na nyinginezo kwa majina yao. Mfano ukikuta kadi imeandikwa U&ME ina maana ni wewe na majini ya kuzimu japo wewe unamaanisha kimwili na huyo unayemtumia hiyo kadi, inakuwa ni kinyume sababu kadi zote ni zao, ili wampate binadamu wametumia njia hiyo.

Ukiwa na kadi imeandikwa darling- wewe unakuwa kwanza ni darling wa kuzimu na kisha wanazini na wewe katika nafsi yako muda huo huo pasipo wewe kujua.

Kadi iliyoandikwa fiancé- unakuwa tayari unakuwa mchumba wa jini lililohusika kubuni hiyo kadi na madhara yake uchumba unakuwa ni vuruguu, balaa na hata kuachana sababu yupo mwingine, mchumba ambaye yupo naye japo wewe haujui.

Kila neno la jina la kadi uelewe unapoinunua au kutamani tu au kutumiwa au kutumia mtu uelewe ni wewe unakuwa wa huyo aliyopo kuzimu na anakuwa na uhalali kabisa, shetani alibuni siri hii akajua atawateka wengi na ndivyo ilivyo. Hebu jiulize zamani wazazi au mababu, mabibi hawakuwa na mambo ya kadi. Walikuwa wakimpenda mtu anachukua kalamu na karatasi halafu anaandika ujumbe wake na mambo yanakuwa mazuri wanaelewana. Sasa siku hizi watu wanapigwa upofu wanaenda kununua ujumbe labda kwa ajili ya mchumba halafu unamtumia mchumba. Nikuulize je wewe mchumba hayo maneno yametoka katika ufahamu wako na moyo wako? Jibu siyo, na je unamjua ni nani aliyeandika ujumbe huo, jibu haumjui. Sasa watoto wa MUNGU hamuoni mnadang’anywa tu mnapeana maneno ambayo unaandikiwa na madahara yake upendo haudumu, unaibiwa na mapepo sababu ulikosa akili yako ukatumia akili ya walioandika maneno ambayo haujui yana roho gani. Kama nilivyoelezea sasa mfunguke YESU anawapenda, mfunguke fahamu zenu mumcheni MUNGU na msiangamie tena enyi mataifa yote. YESU alitaka myajue miaka mingi lakini alisalitiwa na watumishi akakosa wakumfunulia haya. Na nyie mliofunguka msimsaliti YESU mkatumia vitu hivi.

Tazama hata makanisani siku ya Krismasi utakuta midoli ya father Christmas, miti, kadi za Krismasi na taa za kuzimu, maisha ya wanadamu. Zaidi endelea kusoma  makala nilivyoelezea kuhusu Krismasi ya Nabii Hebron utapata majibu yako hata kama haujaelewa utaelewa kabisa na utafunguka macho yako na usome masomo mengine na vitabu nilivyoviandika hakika utapona. Katika makanisa wanapoziweka vitu hivyo kuzimu yote inajumuika na waumini wote sababu ya hizo kadi na miti, midoli na watu wanaposherekea boxing day 26.12 badala ya 25.12 aliyozaliwa YESU siku hiyo kuzimu wanakuja kumuibia kila mtu ambaye atasema anatoa zawadi ni siku ya boksi day. Unaibiwa kila kitu unabakia mtupu. Ila kama ukimoa mtu zawadi usimuambie hii ni zawadi ya boxing day hapo utapona, ila ukiandika tena boxing day siku yeyote ile na wewe unakuwa unajiunganisha na siku ya kuibiwa vitu na shetani katika ulimwengu wa roho ndiyo inaitwa boxing day.

Mamilioni wanaibiwa baraka zao miaka nenda rudi sababu hawakuujua ukweli na makosa siyo yao wala siyo ya YESU, ni makosa ya watumishi aliowaita YESU wakamsaliti na YESU akakosa mjumbe wa kupeleka habari nyingi ambazo shetani aliwatengenezea wanadamu ili awateke. Krismasi hii usiweke mti, midoli ya father Christmas, wala kadi za Krismasi wala zile taa za Krismasi, utaona Krismasi njema na utabarikiwa na YESU na utamfurahisha MUNGU mbinguni na atakubariki. Ila ukiweka uelewe YESU unamfukuza kwako, na unamuuzi MUNGU na hautaona baraka zake, sasa funguka.

Sema BWANA YESU naomba unisamehe dhambi zangu ikiwemo na hii ya kutokujua au kujua nikashiriki katika kadi za krismasi, uchumba na nyinginezo. Nashukuru YESU kwa kunifunulia haya kupitia Nabii wako Hebron. Nisaidie, niongoze nisipotee tena, shetani sikutaki tena, father Christmas sikutaki, Christmas tree sikutaki, Kadi za Krismasi na taa zake na vitu vyote vya shetani mlivyovianzisha siwataki katika jina la YESU WA NAZARETI ALIYE HAI. Amen.

NOTE:
Kadi za Krismasi zilibuniwa kuzimu ili kuwateka wanadamu na sasa zinajaa kila mahali ili na wewe unapoitumia unashiriki Krismasi na kuzimu. Formula ya MUNGU ni kupeana zawadi halisi kutoka katika moyo. Sasa kadi hayo maneno tu siyo zawadi unayoiona kwa macho, pia hayo maneno siyo wewe unayeandika, haujui yalipotokea, ni bora umuandikie mtu kwa barua heri ya Krismasi au email kuliko kadi hizo, na hautakiwi hata ubuni kadi yako, jambo ni lile lile tu, unakuwa unarejea katika msingi wa kadi ule ule tu.

Nawatakia Krismasi njema isiyo na giza. Karibu katika kanisa la YESU NI BWANA NA MWOKOZI WA MATAIFA YOTE, uombewe na ufunguliwe mambo yaliyoshindikana na mengine na usogezwe kwa YESU.


NABII HEBRON.