Pages

Thursday, December 11, 2014

UBATIZO  WA KWELI NA UNABII KUHUSU TANZANIA MPYA.

Karibu sana ndugu msomaji katika kipindi cha Mtume na Nabii Hebron wa kanisa la YESU NI BWANA NA MWOKOZI WA MATAIFA YOTE.
Kwanza nitaanza kwa kukuombea, “ Baba katika jina la YESU, asante kwa ajili ya watazamaji na watoto hawa zaidi tu ya kutokuwa watazamaji ni watoto wako tu MUNGU uliowaumba wewe. Baba ninawakomboa nakuwasafisha na kuwatakasa, ninavunja nguvu zote, za uharibifu maeneo yote , ninakomboa  akili zao fahamu zao, nawatenga na roho zote za uovu kwa jina la YESU KRISTO wa Nazareti, ninabakiza nguvu zako tu, ndani yao zile ambazo tu ni mapenzi yako. Ninafungua, masikio fahamu  na akili zao kwa damu ya YESU KRISTO wa Nazarethi. Asante Baba nina kukabithi  ninakurudishia wewe mwenyewe  watoto wako, sifa na utukufu. Asante Baba kwa muda na wakati huu unapokwenda kusema na watoto wako. Amen!

Ndugu msomaji MUNGU akubariki sana. Siku ya leo  nitakwenda kuzungumzia somo la Ubatizo. Sawa sawa na YESU alivyoniita toka mwaka 2010, na mambo aliyo kwisha kuniagiza, kuyaeleza  na kuwafungua watoto wake na shetani asiwapate. Kwa sababu hii yote anawapenda. Lakini leo nitaelezea jambo moja kuhusu  Ubatizo na pia nitaelezea kuhusu mambo yanayokwenda kutokea katika nchi ya Tanzania ambayo MUNGU  ameichagua ni nchi yake teule Takatifu ambayo ameiita EDENI.


Wengine watajiuliza ni kwa nini Ameiita EDENI?  Ni yeye ndiye ameiumba. Mtayaona hayo na yeye ndiye amepanga. BWANA YESU ASIFIWE..!
Aa.. nitaelezea  kuhusu ubatizo, MUNGU ule aliouanzisha lakini umekwenda  kuachwa na kama umeachwa ukaenda tofauti ina maana watu hawajabatizwa. Ndugu msikilizaji na mwana wa MUNGU kila mmoja, anaijua katiba ya MUNGU ni hii BIBLIA. Hii ndiyo mwongozo wako, yeye mwenyewe ndiye ameipitisha kwa ajili yako wewe, na wengine wote ambao hawaangalii, BWANA YESU asifiwe,!
Nitaeleza  kuhusu ubatizo.  Ubatizo ni kiapo  kilichopo kati ya Mtu na MUNGU. Na jambo la ubatizo lilianzishwa na MUNGU baada ya anguko la Adam na Hawa katika bustani ya EDENI. MUNGU alichokifanya  aliitroduce Ubatizo na akamtuma Yohana  kuwasafisha, Bwana YESU asifiwe! Akamtumia Yohana wakabatizwa kwa maji mengi yanayotembea mtoni  kijito cha utakaso.


Na kupitia hivyo hivyo akamtuma mwanawe YESU wa Nazarethi ambaye ndiye mwana wake wa pekee aje aonyeshe njia namna gani sisi tutakavyo  batizwa ili kwamba tuwe tumeokolewa na  kusafishwa kama yeye. Na alipo kwisha maliza kazi yake, alirudi juu mbinguni lakini suala hili MUNGU alilolianzisha kuhusu  ubatizo,  limewekwa pembeni  98%. Na leo ninakuwmbia wote ambao wamekwenda kinyume na  mpango wa MUNGU na hata katika Biblia ,wote hamjabatizwa na MUNGU hawajui, na  amesema hamtaenda mbinguni. Iwe ni watumishi, na hata kama ni watumishi nyie siyo watumishi wake maana kama ni watumishi wake mngefundisha yale yale aliyoyafundisha YESU ambaye ndie njia ya uzima na kweli, kwa hiyo watu wanafuata uongo wenu, wanaacha kufuata kweli namtahukumiwa bila kuokoka upya na kubatizwa. Bwana YESU asifiwe!


Nitasoma katika kitabu cha Mathayo 3:13-17, Neno la MUNGU linasema hivi wakati huo YESU, akaja toka Galilaya kwenda Yordani kwa Yohana ili abatizwe, Lakini Yohana alitaka kumzuia akisema, mimi ninahitaji kubatizwa na wewe  nawe waja kwangu,  YESU akajibu akamwambia , kubali hivi sasa kwa kuwa  ndivyo itupasavyo kuitimiza haki yote. Basi akamkubali, naye YESU alipokwisha kubatizwa mara akapanda  kutoka majini, natazama mbingu zikamfunikia akamwona Roho wa MUNGU akishuka kama huwa  akija juu yake, natazama sauti kutoka mbinguni ikasema , huyu ndiye mwana wangu mpendwa ninayependezwa naye. Bwana YESU asifiwe. Ndugu msikilizaji wa Neno la MUNGU, njia sahihi aliyo onyesha ni YESU, na MUNGU alimtumia Yohana kuanzisha hiyo njia. Lakini Yohana alijua huyu ni mkubwa kuliko hata akatii Mungu aliyopanga.
BWANA YESU asifiwe, YESU na yeye akabatizwa akaingia kwenye maji akabatizwa baada ya kubatizwa ROHO MTAKATIFU akashuka juu yake akashuhudia “Huyu ndiye mwanangu mpendwa “ BWANA YESU asifiwe. Sasa jambo ambalo MUNGU alikwisha kulianzisha sasa hivi ni tofauti na imeandikwa katika  kitabu cha Ufunuo ya kuwa atakaye ongeza maneno ya kitabu cha unabii huu sehemu yake haipo kabisa, BWANA YESUasifiwe.


Kwanza kabisa  nitaeleza maana ya kubatiza. Kubatiza  ina maana ya kuzamisha. Lakini sasa  siku hizi imekuwa ni tofauti haijalishi unabatiza kwa jina la BABA , la MWANA  na la ROHO MTAKATIFU, hiyo  yote ni fake lazima kuingia katika maji yanayotembea ya Mtoni kama Yordani, ubatizwe kwa jina la BABA na la MWANA  na la ROHO MTAKATIFU. Bwana YESU asifiwe.
Sasa  hii imekuwa ni tofauti , katika mithali 13: 1 Mwana mwenye hekima husikiliza  mahusia  ya baba  yake, lakini Yule anayemdharau  hukataa kusikiliza mahusia ya Baba yake, na  wanadamu wamekataa kusikiliza mahusia ya MUNGU wamemdharau, kwa nini hambatizwi? Kama Neno la MUNGU linavyosema? Mmejitengenezea njia zenu na hizo njia sio za kwenu ni mmepotea acheni mambo ya wamissionary wamepotea wamekuja kupoteza watu, injili Ulaya hakuna imekufa. Wote ambao hamjabatizwa ubatizo wa maji mengi, hamjabatizwa na YESU ameniambia wote, wote ni kazi bure! BWANA YESU ASIFIWE!


Ukisoma katika kitabu cha Yohana 3: 5-7, Asiyebatizwa hatakwenda mbinguni, sasa nakuuliza wewe  hujazamishwa katika maji, halafu unasema ni mkristo, halafu unasema unaenda mbinguni, Yohana 3: 5-7 inasema hivi? Asiye zaliwa kwa maji haendi. Na wewe wewe hujaenda, YESU ndiye njia ya uzima nay a kweli, lakini njia hiyo wewe pia hujaifuata, umefuata uongo. BWANA YESU asifiwe,  watu wengine wanasema ubatizo ni imani yako,  wanabatiza watoto wakiwa wadogo, nikuulize swali, wewe mtoto mdogo ulikuwa na imani? Tazama YESU alipo batizwa  wakati anaenda kubatizwa  hakuwa na msimamizi hata mmoja, sasa  nyie  wanadamu hata na nyie watumishi wa huyu msimamizi  mwanamke na mwanaume  wametoka wapi? Tafuta katika Biblia kama MUNGU alianzisha hivyo? hakuna! Mmepotea  mrudi mkabatizwe kwenye maji, ni AMRI  na kiapo kinyume cha hapo huendi mbinguni.  Katiba  ya MUNGU umeshaivunja wala wewe  sio mkristo, Bwana YESU asifiwe. YESU amechukia  kabisa, mambo yameharibika,  huku ndiko  kutekwa na shetani. Kila aliyebatizwa ubatizo wa kumwagiwa maji kichwani ametekwa na shetani na ile siyo ubatizo ni ndiyo namba   ya 666, watu wanafikiri kwamba itakuja jina limeandikwa  kwenye paji la uso 666, inakuja katika roho, ndiyo hii 666 lazima ukabatizwe, kinyume na hapo YESU akija mbinguni hauendi.
Hajalishi kwamba mnamtaja YESU, BWANA YESU asifiwe! Hayo ameniambia na mimi sipunguzi ninawaeleza. 

BWANA YESU asifiwe!Hivi nikuulize, YESU alionyesha njia  akiwa mtoto mdogo anaenda kubarikiwa Mariamu na Yusuphu walimsindikiza mtoto wao kubarikiwa. Sasa siku hizi mapepo na mashetani yakaliteka kanisa, mwanaume na mwanamke wakati  mtoto anapelekwa kubarikiwa , ikageuzwa kibao ndio anabatizwa. Sasa anabatizwa wapi?  BWANA YESU asifiwe!  Wengi hamjabatizwa na ninawaeleza ukweli, na siyo wakristo na wala hamuendi mbinguni iwe ni askofu, uwe sijui wa dini gani NO!! Tena  mtachomwa kwa sababu  mmeharibu, Neno la MUNGU  ukisoma katika kitabu cha Wagalatia 1: 6 injili aliyoianzisha MUNGU imebadilishwa, imepindishwa , imewekwa uongo, huu ndio uongo ninaowaambia ndugu watazamaji na kama ukislkiliza injili ya uongo na wewe umekuwa muongo, umepotea. Mnatembea mnaona mnaenda mbinguni,  hakuna  mbingu, muulize huyo anayekubatiza wapi kuna ubatizo  wa maji ya  kikombe?  Tafuta  hakuna. ! Muulize wapi imeandikwa mtoto mdogo ana imani ya ubatizo? Kwa nini YESU alionyesha njia? Akiwa mtoto mdogo yeye  ndivyo inatakiwa . Yohana 14: 6 , Yeye ndiye njia ya uzima na kweli. Sasa uzima upi na kweli ipi unaifuata? Hamjabatizwa mnapoteza muda mtachomwa, mtaangamia. Badilika hii ni Dunia nzima.


Ninawaambia ukweli, na wengine wameanzisha mtindo mwingine, hii kuchafua wanatumia nguvu za kichawi, watumishi, anakubatiza kwa  hivyo hivyo kwa maji mengi anakubatiza kwa jina la BABA na la MWANA  na la ROHO MTAKATIFU halafu anakuwekea na la Hebron hapo au la kwake.  Haipo hiyo kitu? Sasa wewe unaweka agano na mwanadamu ndio maana mmeshikwa, pesa zote mnapeleka kwa mtumishi hata mpaka unashangaa unachanganyikiwa, wanajua siri wanayofanya. Waulize!  Kama ni mahakama ya ya kibinadamu  wanatakiwa washitakiwe kabisa , kwa nini wanabatiza watu kinyume na MUNGU?  BWANA  YESU asifiwe,  ninawaeleza siri hii, Roho zenu zina kufa  mkabatizwe upya!!. Yeyote hujabatizwa kama YESU wewe siyo mkristo. Fuata njia za YESU alibatizwaje, BWANA YESU asifiwe,  Ninacho kitabu hapa ambacho nimekielezea UBATIZO WA KWELI usome katika internate utaujua ukweli hapa. Na hiki kitabu hakuna wa kukupinga dunia nzima, hata wewe unayebatiza kwa maji ya kikombe ukisoma hiki kitabu utajiona ni sifurihujui kitu,. BWANA YESU ASIFIWE, .


Na jambo lingine ni  UBARIKIO WA KWELI  KWA WATU WOTE  soma hiki kitabu hakuna mtu mzima kubarikiwa, ni mapepo hayo mnafanya, Bwana YESU asifiwe, lakini msijali mambo yameharibika shetani amelikamata kanisa,analivuruga vuruga kiapo YESU alichofanya kwamba ni yeye na wanadamu sasa kimeingiliwa. YESU hana watu, ana watu majina tu, wewe unaambiwa msimamizi wako ni Roho Mtakatifu, anakaa mwanamke anakaa mwanaume, mwanaume huku amelewa pombe yake, mwanamke huku ni mchawi wanakusimamia nini wewe? Roho Mtakatifu atashuka wapi? Nafasi ya MUNGU imechukuliwa halafu kumwagiwa maji sio ubatizo!! Ila ni alama ya chapa 666 na wanaofanya kazi hiyo ni wachapa 666.  Na  ninawaeleza kazi zote za shetani zimeshavurunjwa vunjwa, YESU anarudi anahitaji watu wake sasa.


Aliponitoa kwenye kazi ya utalii amenitoa, “ najua hujui chochote, mimi nitasema ndani yako maana nimewatuma wamenikataa, wamenisaliti.”  Watumishi wamependa pesa, wizi, ufreemason. Ni pesa kunyang’anya mali za watu tuu. Hawataki kusema kweli yangu, na nyie ndio maana mnapotea, sio kwamba  nawachukia nawapenda mataifa yote lakini yupo wapi wakuwaambia kweli? Mimi ni kweli mngeangalia Neno langu ambalo ni kweli, nyie mnaambiwa uongo ambaye siye mimi, uongo ni shetani lakini hatajwi shetani. BWANA YESU asifiwe.
Niwaulize ndugu watazamaji tafuta kwenye kitabu cha Biblia, Hakuna ubatizo wa kikombe!, sasa umetoka wapi? Wanakuambia ukifa utaenda mbinguni. Kwani yeye hajui watoto wadogo wapoje? Watoto wadogo hawana dhambi wametoka mbinguni wakikaa mpaka wakifika wakati wao wakiwa wakubwa ndipo waamue na imani yao kwamba nimeamua kubatizwa, watu  wanakubatiza kwa jina la MUSA, JOHN, sijui YOHANA, kwa jina la HEBRON mnaokubali mmeangamizwa, lazima maji mengi tena  yanayotembea hivi, churuuuuu…na  ya kisima pia fake!  BWANA YESUasifiwe. Ndivyo jinsi mambo yalivyoharibika. BWANA YESU asifiwe, Katika ubatizo YESU wakati anaenda kubatizwa, hakutoa ada ya kubatizwa, hivi ada zimetoka wapi? Katika kanisa hutakiwi kulipa ada yeyote, kanisa siyo secondary wa chuo. Nikuulize ndugu mtazamaji hiyo sadaka unavyotoa unapewaga receipt, kuna mtu anakudai? Sasa haya yametoka wapi? Ni biashara umedanganywa umeliwa wala mbinguni hamna 98% dunia nzima mambo yameharibika. Ninasema hivi!! Ni bora hata wamissionary wasingekujaga, maana ukisoma Biblia inasema kweli, wakatudanganya, wakatueleza ujinga , wengine wakasikiliza wengine wanaujua ukweli kabisa lakini hawataki kuusema.. ni wakati wa kila mtu kumjua MUNGU na kubadilika, mbinguni bila wokovu hakuna.  YESU  hana tabaka, ni wokovu peke yake. BWANA YESU asifiwe, na ndio maana  ile siku ya mwisho ndie yeye amechaguliwa kuja kuwakomboa wana wa MUNGU.


Dini  nyingine  wanamuita Nabii Issa. Sasa wewe kama hujakuwa kwenye chama chake unategemea nini? Hivi mnamuona MUNGU ni mpuuzi ana waangalia,  laity ungepata kuisikia sauti yake usingefanya upuuzi. Mimi mwenyewe hata biblia nilikuwa siijui. Utiisho wake naogopa, sitaki kabisa lazima niwaambie ukweli. Ananiambia tarehe hii nenda kawaambie hivi, hata sasa usifikiri ni Hebron  ni MUNGU anakuambia; ile  mwisho zitapita computer na video zako utasema kwamba hujasikia na umeona. Mnabaki kudanganywa ukifa hauendi mbinguni. Utaenda mbingu gani wewe hujabatizwa? Soma Yohana 3:5-7 hakuna kitu waulize wamesoma digrii  na madigrii , digrii gani matakataka mnafundishwa? Hii ni kazi ya wamissionary bora wangebaki huko huko .


BWANA YESU asifiwe! Na huko ndiko wameharibika sasa watakuja Tanzania kuponea hapa. Hili ndilo Taifa MUNGU amelichagua kama ni EDENI amekwisha kulikomboa ni nchi yake. Tanzania bwana hakuna nchi itayoivamia Tanzania tena. Nimewaambia mimi MUNGU ndiye kaniambia hakuna nchi itakayo ivamia yeyote. Ila huko ndani wale ambao hawana MUNGU wataendelea kutandikwa tuu kwa namna yake.  BWANA YESU ASIFIWE. Kwa sababu MUNGU hawezi kuangalia kama  hamumtaki lakini mnanitaja wa nini? Yeye atawapa njia gani? BWANA YESU asifiwe, ni wakati wa mabadiliko lazima ubatizwe na wakati wa kubatizwa  usikubali kubatizwa na Nabii wa uongo, usikubali kubatizwa na mchungaji ambaye hajabatizwa na maji mengi na yeye  hajabatizwa! Wala sio mwanafunzi wa YESU. 

Tazama wale mitume wa YESU  ndio walofundishwa kazi hii? Jibu  siyo. Walimuua Petro  halafu ndio wakaanzisha mambo yao sasa nakuambia Petro wa leo Nabii hebron, nakuambia mimi hakuna kitakacho nisimamisha , Bwana YESU asifiwe, kama hili jiwe hili, mimi sisikii kitu. Bwana YESU asifiwe, YESU amelijenga kanisa , nakuambia ukweli ubadilike,  mnaua wananchi , mnaua mataifa, watumishi mnawapa sumu, kitu gani? Hata nyie viongozi na wasomi kaangalieni Biblia hii tafuta kama kweli wanampenda MUNGU, kama kweli hawamchukii  huyu MUNGU tafuta kwa nini hawafuati Neno lake, wanatafuta ya huko? Je! Wewe mwanadamu umeumbwa  ili uwekewe ya huko au ya hapa!


BWANA YESU asifiwe, soma katika kitabu cha Ufunuo 22: 18-19 “ na mtu yeyote akiondoa lolote katika maneno ya unabii  wa kitabu hiki  MUNGU atamuondolea sehemu yake katika ule mti wa uzima na katika ule mji mtakatifu ambao habari zake zimeandikwa katika kitabu hiki. Sasa kuna nafasi ya kubadilika hii ndiyo nafasi ya kumrudia MUNGU, kinyume na hapo No! haijalishi ulibatizwa Yordani wapi? Wengine wanabatizwa kwenye maji mengi mnadanganywa tuu, kwanza muangalie anayekubatiza kama ana MUNGU kweli, utamjuaje? Chunguza matendo yake ukikuta habari ya pesa tu hamna kitu, michango kanisani hukuna kitu, ndio kazi kanis la sasa hivi iliyobakia na MUNGU hahusiki nalo. Na ameniambia YESU  waambie Hebron, wamepotea. Mimi siangalii pesa zao, mimi sijatuma wakachangishe harambee, mimi sijatuma wakawe na mapartiner na kutafuta watu wenye pesa kuwaambia ndio wasapoti huduma zangu, mimi najisapoti peke yangu. Mimi sijawatuma watumishi wakatume namba za account kwenye TV na  kwenye M-Pesa kuomba pesa za kuwezesha, mimi sijawatuma hao ni wezi, Biblia inasema, usijisumbukie  utakula nini, utavaa nini, maua ninayanyeshea, je wewe mtumishi wangu kweli si bora zaidi? Mbona mimi siombi? Nikukuambia nimekutuma,nimekutuma inatosha. Hicho ni kibali mambo yatanyooka. Sasa hivi ni uchawi, mnatishwa na majengo, sasa hivi siyo majengo ni  mapango, BWANA YESU asifiwe, mimi nimekaa hapa kwenye mawe nipo na  YESU, bwana. Haya  majengo bwana yamekuwa ni masoko, wizi mtupu! 

Hamna kitu. BWANA YESU asifiwe,  kawachunguze ndani yao ndiyo wauza madawa ya kulevya, ndio wanao walala wanawake zenu, na wanaume zenu, na watoto wenu, hawa hawa!! YESU anakaa ndani ya mtumishi na ina maana kama yupo ndani ya Mtumishi ina maana Mtumishi ni YESU anakaa ndani yake. YESU hazinigi jamani, hawa wana mambo yao, BWANA YESU asifiwe!


Inaudhi sana, inaumiza sana  lakini ole wao. Mimi ni Nabii bwana ninakuambia, ukubali ukatae usinione mtoto nipo hivi ninachokuambia hayo ndiyo  ya YESU NINAYOKUELEZA. Wote ninarudia mliomwagiwa maji hapa! Uwe mchungaji askofu sijui cheo gani hujabatizwa wala wewe sio mkristo, wewe sio mwanafunzi wake, wala huifuati kweli yake unafuata uongo wake, kitabu kinachoelezea kweli ni Katiba, ninacho kitabu cha UBATIZO WA KWELI kisome. Hakuna kitu, sasa badilika. Badilika utubu utubu! Wako wengine wana kiburi. YESU akaniambia wanajifanya awana shingo ngumu, mimi ninawaangalia, ninawaangalia, ninawaangalia lakini!? Ole wenu. Mtakavyobaniwa, hamtaamini. Uchawi sasa hivi hakuna tena, hakuna tena ni ajabu katika nchi ya Tanzania mwaka 2010 nilipelekwa mbinguni. Jina la Mtumishi lilikuwa la MOSES KULOLA tu!! Hao wakubwa, sasa ameondoka kuna nani? Uchawi mtupu! Wote hao watumishi wenye  mali kubwa, nyingi, matajiri wengine wanasema mimi nawaonea wivu, hakuna! Hizo mali ni za kunyang’anya watu na uchawi na mazingaumbwa. BWANA YESU asifiwe, wote wenye mabenki hayo hata wanasoma Biblia na mifungo yote ni fake nawaambia watoto wa MUNGU. BWANA YESU asifiwe.


Nitaelezea mambo yanayokwenda kutokea Tanzania. Nitaelezea katika uchumi kwanza MUNGU ameirejesha Tanzania. Ndege zitajaa nchini Tanzania, watalii watajaa Tanzania, ni nchi ijipange na miundo yake. MUNGU anawarejeshea na uthamani wa Tanzania uliibiwa, na hawa hawa wageni. BWANA YESU asifiwe. Viwanja vya ndege vimeinuliwa mtaona mabadiliko makubwa sana. Na jambo lingine katika bandari ya Dar es Salaam, ndiyo bandary sasa hivi kwenye ulimwengu war oho namba moja katika Afrika Mashariki. Mtasona mabadiliko pale, meli nyingi zitakuja ipo siri iliyofanyika pale na hawa watawala wa zamani lakini MUNGU amekwisha kuibomoa.


Jambo lingine ni kuhusu Zanzibar, Zanzibar! Ooh Namshukuru MUNGU sana, kwa kuifungua Zanzibar. Zanzibar itakuwa,  haaa..!! sijui nikuelezeje, nitaelezea kwa kidogo. Ni kiini cha soko watu wengi wanakimbia Dubai, wanakimbia China, sasa wataanza kwenda Zanzibar. Wengine watasema itakuaje, ndugu mtazamaji, embu nikuulize, hapo zamani Zanzibar ilikuwa nini? Si ndio ilikuwa sako la watumwa. Sasa unafikiri ile connection kwa nini nchi zote zinzenda pale, ule uthamani wake uliibiwa ukapelekwa nchi ambayo siitaji. Sasa imerejeshwa, Zanzibar sio ya kawaida imenyanyuliwa.


Na katika Serikali ya Zanzibar kule kuna mawaziri wataanza kufukuzwa, muda sio mrefu na mafisadi. Nilikwisha kueleza kuhusu Tanzania na mmeona wanavyofukuzwa nab ado wataendelea kufukuzwa. Ni YESU  mwenyewe anafanya na anatumia watu hivyo hivyo. Usalama wa Taifa na Jeshi la Tanzania limeinuliwa juu sana. Sio lakuchezea tena, siyo la kudharau maana MUNGU ndiye amewashika na anawapenda. BWANA YESU asifiwe. Bunge la Tanzania mtaendelea kuona mabadiliko sana, katika vyama vya siasa, yeyote anayekwenda kinyume na mapenzi ya nchi hii au anania mbaya kuhusu nchi hii atakuwa anatolewa tu , anatolewa tu, anakataliwa hata afanyaje hata alogeje, Jambo lingine katika uchaguzi mwaka 2015 katika nchi ya Tanzania, watu wengi watalia wagombea, wabunge  wengi watalia na mawaziri, hawatakubaliwa, kwanza na vyama na wananchi. Wote wanaoenda vibaya na atakaye tumia uchawi hatapata urais. Hayo mengine nitayasema kwa wakati wake. Watu walizoea kuwa na kikundi hiki  nitapanga watu wangu, oohoo..!!  pangeni tu, hao watu ni wa MUNGU, atawageuza mwenyewe watakula hela zenu, wanaishia wewe mrudie MUNGU, muombe MUNGU lakini MUNGU mpaka sasa hivi anamjua rais wa Tanzania ni nani. Kwa muda wake na wakati wake, lakini hayo hajaniruhusu kuyataja mpaka muda wake na wakati wake. Akili za wanadamu mara Yule mara Yule nawaambia itakuwa ni kilio kwa Rais atakayetolewa. Siyo huyo mnaemtazamia au hao, nimekwisha kuwaeleza, BWANA YESU asifiwe, mmeshamuonaga MUNGU, wewe!! Ni wa kuchezea kujipangia tu, hii ni bustani yake ameamua yeye. Wala mimi hakuna atakaye niua, nakueleza ukweli, amenitoa mimi ni  mtanzania halisi,  BWANA YESU asifiwe. Na  amenipenda hivi hivi, kwenye nchi yake hivi hivi na mimi ninaipenda nchi yangu.  Walioiba pesa za Tanzania, huko Ulaya zitarejeshwa, haina muda! Hata mfanyaje zitarejeshwa kwenye akaunti za Serikali. Hiyo ndiye YESU atakaeifanya wala sio mwanadamu, wala hakuna wa kuzuia. BWANA YESU asifiwe.


Jambo lingine ndugu watazamaji, hii habari ya masadaka kanisani. Hizo sio sadaka, sadaka ya kweli ni fungu la kumi na shukurani. Hizo nyingine zote ni uongo. Soma kwenye biblia hakuna sadaka ya matofali, ya ujenzi, ya uinjilisti, ya uchungaji ya mtume, hakuna.! Ni hao wanaiba hizo pesa nawambia hao ni waizi maana MUNGU ameniambia mimi sikuwatuma hivyo na ole wake, anaye watesa wana wa MUNGU. Watu wengi wamekuwa wanalalamika na kulia ya kwamba MUNGU mbona hatubarikiwi, MUNGU tunafilisika, tumetoa mpaka mafungu ya kumi tumechanganyikiwa mambo hayaendi.
Nikuambie??  Hazijaenda kwake, ni kwa jamaa.. na wajamaa wanaenda kuuzia madawa ya kulevya umewapa wajamaa wamepeleka nyumba ndigo, unawapa wajamaa wanaenda kunywea pombe, unategemea MUNGU atakubariki? BWANA YESU asifwe.
Jambo lingine habari ya kuabudu masanamu, ndugu watazamaji hivi niwaulize, MUNGU ni sanamu? MUNGU ni msalaba? Kwa nini mnaabudu misalaba? YESU yupo zake mbinguni amestarehe, ameonyesha njia mumwabudu yeye katika moyo, hata kama umeweka nyumbani kwako hiyo ni laana.


Msalaba ulitumika kuulia watu toka zamani wenye laana, hakuna msalaba Mtakatifu, BWANA YESU asifiwe, ni kwa sababu kipindi kile ni kwamba mtu akifa lazima apitie kwenye jambo kama hilo kwenye msalaba. Ina maana ingekuwa ni kamba, watu wangechukua kamba takatifu? Na ole wao, mambo yameharibika. Tazama hata YESU alipo kuwa na wanafunzi wake, ujue mambo yameharibika ndugu watazamaji mnapewa sumu, YESU alitengeneza ile chapatti ambayo ndio ilikuwa mwili wake, twaeni mle hivi, sasa nikuulize ule mwili ulikuwa na alama ya msalaba? Wote mliokula msalaba mmemeza laana. Na wote wanaotembea na ile misalaba hivi ndani yao wanatembea na laana kwenye ulimwengu wa roho wamepelekwa golgota. Ndio maana mnakaa na misalaba mnapigwa na mapepo, mnabondwa! Nimewafunulia siri nanakuambia ndugu mtazamaji hata msalaba unavyowekwa pale kaburini si unadondoka unaliwa na mchwa, unaenda nao? Unaoza. Hata YESU alivyozikwa kwa nini hakuzikwa na msalaba? Eti msalaba ndio alama ya Mkristo? Msalaba ndiyo alama ya YESU? Hakuna. Rudini kwenye neno la MUNGU, tazama sasa watu walivyopotea, tazama watu walivyopotezwa, hivi mmeshajiuliza kwa nini makanisa watu waliookoka wajanja hawawekagi alama ya msalaba? Walikwisha jua sasa mpaka unawekwa kwenye hii inaitwa chakula ya nini wala sio chakula ya bwana, chakula ya hao, hivi unakula, unakula laana. Inaingia kwenye damu, kwenye mwili, una dunda nayo na wengine mnatembea na msalaba hapa, YESU alisema hivi, nimekwisha kubebea msalaba, Yule aliyekuja kubebamsalaba wa YESU si Simoni? Si alikuja akaubeba?
Ni kwa ajili yenu msibebe tena. Nani aliye waloga nyie wana wa MUNGU, mnabebeshwa misalaba vitu kama hivyo. BWANA YESU asifiwe. Zaidi upate kitabu cha MAFUNDISHO YA NABII HEBRON. Utafunguka ufahamu wako, upate kitabu cha MPINGA KRISTO,hii yote ni YESU amenieleza nikueleze wewe. Bwana YESU asifiwe.


Jambo lingine usome kitabu  MKRISTO USIKUBALI KUWA MPUMBAVU. Vipo kwenye Internate na kanisani kwangu. BWANA YESU asifiwe, MJUE YESU KRISTO WA UONGO, yupo wa uongo, sasa wengi wana wa uongo, wa msalaba wa uongo, michango wa uongo na wewe umekuwa muongo pasipo kupenda, basi pata tena kitabu kingine JINSI KANISA LINAVYOMUABUDU SHETANI. Lakini hawamtaji shetani Yapo mambo soma huku ndani. BWANA YESU asifiwe. JINSI KANISA LINAVYOMKUFURU ROHO MTAKATIFU, vyote hivi visome na vingine vingi na uendelee kufuatilia vipindi vya mtume na Nabii Hebron. BWANA YESU asifiwe, Haleluya!!  Lakini usiogope leo ni wakati wa wewe kumjua MUNGU na kuujua ukweli.  BWANA YESU asifiwe, BWANA YESU asifiwe, nakwenda kuombea wale ambao hawajaokoka.


Sema BWANA YESU, naomba unisamehe, dhambi zangu zote, nilizozifanya kwa kujua au kutokujua, uniandike jina langu kwenye kitabu chako cha uzima wa milele, BWANA YESU nimeteseka sana nimebebeshwa msalaba, nimedanganyika hata nimebatizwa ubatizo usio wa kwako na wewe ndie njia ya uzima, lakini angalia mambo yalivyoharibika, YESU niokoe. “BABA ninaomba uwaokoe,” majina yao ukayaandike kwenye kitabu chako cha uzima, uwalinde hukohuko. Baba ninakwenda kuombea wagonjwa ninawafungua walioibiwa nyota, ninazirejesha. Vyeo ninarejesha waliofukiwa maisha yao ninafukua maisha yenu, faraka kwenye ndoa naziondoa, kila aina ya kifungo nina kivunja, kwa jina la YESU KRISTO WA NAZARETI. Kaskazini, Kusini napiga mapepo, freemason nalipua, pepo la umasikini, nabomoa kwa jina la YESU. Ndoa za kipepo navunja kwa damu ya YESU KRISTO wa Nazareti. Ubaki wewe BWANA YESU peke yako, Bendera yako isimame na bendera za shetani nazivunja, nang’oa zote kwa jina la YESU KRISTO wa Nazareti, Baba, nina muinua rais wa Tanzania, mpe nguvu mpe hekima mlinde na wote wenye nia mbaya kwa jina la YESU mpe hekima akaongoze nchi vizur na mawaziri na serikali wakuu wa mikoa wote, mpaka idara ya chini wakafanye kazi vizuri uchumi ukaendelee kunyanyuka juu, wasitishwe  na hao wanaiba madini nafunga roho ya kuiba madiniya watanzania yabaki kwa watanzania na mikataba mibovu naifuta kwa damu ya YESU KRISTO wa nazareti. Mali hii MUNGU ulileta kwa ajili ya watanzania, na watanzania ndio wafaidike. Baba, tumekuwa na akili sasa, na hao wana akili MUNGU, sasa wamiliki, wape uwezo waongoze kwa jina la YESU KRISTO wa Nazareti. Asante MUNGU wa Ibrahimu, asante MUNGU wa Isaka katika jina la YESU KRISTO wa Nazareti.


Ndugu wasomaji MUNGU azidi kuwainua, MUNGU azidi kuwabariki, msidanganyike tena. Kanisa sasa hivi limetekwa na shetani ukisikia habari ya michango michango, hata harambee mnaokwenda kushiriki kusema harambee laki,elfu kumi, laki  wabaki mmelaaniwa, nyumba ya MUNGU ni nyumba ya  sala peke yake. Kama ni yak wake atafungua milango, itafanyika, sasa hao wanafanya hivyo wanatumia uchawi, Afrika imeoza, Ulaya imeoza, hawajui wanachokifanya asilimia mbili tu ndio imebaki na YESU, yamkini hata na wewe nakuambia hapo haupo na YESU, unafunga sana mpaka na vidonda matumbo yametoboka, utabaki unakemea unakemea nini wakati wewe mwenyewe umewekwa kwenye ngome ya shetani, hivi nikuulize wewe umepigwa chapa 666 hapa, ubatizo wa kumwagiwa hapa. Kwa jina la  Baba na la Mwana na la Roho Mtakatifu, yupo Baba wa kuzimu, yupo mwana wa kuzimu, yupo Roho mchafu wa kuzimu, lakini hatajwi maana mngekimbia waulize imetoka wapi?


Kataa..!! kabatizwe upya uwekewe kibali na YESU uwe shirika moja kati yake na wewe, ukatae kabisa katika jina la YESU.  Pia na katika vipindi vya redio mbali mbali, katika nchi nzima ambapo waneneza habari za YESU. Mliopo nchi zote mfunguke.

Soma katika makala ya Nabii Hebron, siyo ya kwangu ni YESU ameniambia nikuletee wewe, mimi  bwana sijaitwa kwenye kazi ya MUNGU, na baba yangu, na mama yangu na dhehebu ni peke yangu tulikuwa wawili na hakuna wa kusimama mbele yangu, kama yupo ajaribu, ni wakati wa watu wote kumjua MUNGU ni wakati wa kukaa vizuri. Usitishwe hizi biblia unasomewa mistari luka 10, hazifanyi kazi, zaidi ni watu wanamapepo ya utambuzi, majini, wachawi watupu, ndio wanaopaa usiku kama mwewe, ndio wanawanga sawa sawa.., nimekuwa nikiletewa simu nyingi watu wanalalamika mchungaji anamwambia mtu nipe laki tano, milioni, usipompa anakulaani, usitoe, MUNGU hawezi kumtuma kwako, halafu wewe mwenyewe huna hela, halafu nakuambia unipe hela, hivi nani amewaloga? Mmewekewa roho ya punda, sasa hivi ni bye, bye, mbatizwe ubatizo wa maji mengi ambao upo katika katiba ya MUNGU, mtu asije akakuambia ni imani yako, ukijisikia, soma kwenye Biblia. Ndiyo kubatizwa ni imani yako, wewe mtoto mchanga anaimani? Wametoa wapi hiyo akili ya kumuweka mwanaume na mwanamke  mchawi mlevi,biblia imepindishwa pindishwa ndio elimu ya uongo nanyi mnapokea uongo pasipo nyie kujua. Makanisa yamenuka yamekuwa ni mapango! Hakuna kitu , wizi mtupu! Na serikali ziwamulike ziwachunguze , hata mimi nichunguzwe wafuate biblia huu ubatizo huu ni wanaua wana wa MUNGU, hata nyie viongozi mmeuliwa, hao wamissionary wamepotea, waliwaua wanafunzi wa YESU ndio uongo sasa. YESU yale aliyofundisha kwa wanafunzi wake ndio amerejesha kwangu niwaeleze na unaposikiliza mimi ninakufungua,unafunguka. Shida yoyote inayokusumbua njoo katika kanisa la YESU NI BWANA NA MWOKOZI, bure unapona, hakuna habari ya pesa No!! nimekupa bure toa bure, hao wanakuambia habari ya hela waizi, waongo, kataa achana nao. BWANA YESU  asifiwe, wanasema wanaombea nchi, wapi?? Ndio nimekuta wameloga nchi ya Tanzania, viongozi hao wanajifanya kwenda kuwasalimia viongozi wa nchi, labda waziri fulani, tunakukaribisha, wanavyompa mkono tu hivi,wanamloga, nyan’ganya kila kitu, anakuwa taahira, kazi mimi nikuombea kufungua viongozi,unafungua, unafungua, hawa hawa na wewe unaweza ukawa kiongozi, hii kazi ya kanisa imeharibika. Mwangalie MUNGU mtegemee MUNGU, BWANA YESU asifiwe.
MUNGU akubariki, MUNGU akuinue, tutaonana tena muda mwingine wakati mwingine, siku kama hii ya leo. Wakati kama huu.. Haleluyaa.. ubarikiwe.




 NABII HEBRON.