MAHUBIRI YA NABII HEBRON KUPITIA YOUTUBE:
VIONGOZI VIPOFU.
MUNGU
anakupenda,
Usiogope!
Nitaanza kuomba: BABA katika jina la YESU
nawaombea watoto wako wote, ninafungua fahamu zao, nakomboa mioyo yao,
macho yao ya rohoni ninayafungua, kwa jina la YESU KRISTO wa Nazareti naondoa
mapando yote kwa nguvu na malaka uliyonipa, naachilia upanga na moto
nabomoa kila namna ya uchawi na upinzani,
kwenye anga, kwenye ardhi na kila nyumba ambapo wananiangalia sasa hivi
naachilia moto ukaondoe kila aina ya uchawi na kila mateso kwa jina la YESU KRISTO wa Nazareti, BABA asante kwa ajili ya
neno lako na ujumbe ulilonituma siku ya leo niwapelekee watoto wako, maana
umeniambia unarudi na sasa nitengeneze kanisa lako, BABA nakurudishia sifa,
heshima na Utukufu, Amen.
Watoto
wa MUNGU na wanadamu wote mlioumbwa na MUNGU ninakwenda kufundisha somo kuhusu
viongozi vipofu na mengineyo mengi yatakayo fululiza hii yote ni kukufungua wewe maana viongozi vipofu ndio
wanaofanya watu wasiende mbinguni japo wewe mwenyewe unapenda kwenda mbinguni
lakini anayekupeleka mbinguni humjui ni wa kweli au wa uongo.
BWANA YESU ASIFIWE,
Nimewaona wengi kuzimu, wanateseka, wanalia,
wanajuta walikuwa wakiishi makanisani wakijiona wao ni wakristo safi, kumbe si
safi na kumbe walikuwa wamewekewa mapando ya shetani, na YESU anaangalia Neno
lake alitimize basi, sio robo robo au nusu.
BWANA
YESU ASIFIWE
Utafungua
kitabu chako cha Neno la MUNGU, Biblia takatifu, Mathayo: (15:8-9 ) mstari wa nane na wa tisa “Watu hawa huniheshimu kwa midomo; ila mioyo yao iko mbali nami, Nao waniabudu bure, wakifundisha mafundisho yaliyo
maagizo ya wanadamu,” nitaruka
mstari wa Kumi na tatu mpaka wa kumi na nne (Mathayo15: 13-14)….:”Akajibu, akasema, kila pando
asilolipanda BABA yangu wa Mbinguni litang’olewa, Waacheni: hao ni viongozi vipofu
wa vipofu. Na kipofu akimuongoza kipofu mwenzake, watatumbukia shimoni wote
wawili.”
Hii
ni habari ya makanisa kwa sababu yamebadilika, utafungua kitabu chako tena
katika kitabu cha Yohana 15:7 Neno
la MUNGU linasema hivi ….”ninyi mkikaa
ndani yangu, na maneno yangu yakikaa ndani yenu, ombeni mtakalo lote nanyi
mtatendewa”
BWANA
YESU asifiwe, watoto wa MUNGU kila mtu anampenda MUNGU, lakini wapo ambao wanampenda
shetani na shetani amepiga upofu kanisa, kupitia watumishi wake wanasema uongo
wanafundisha uongo, mafundisho ya wanadamu, YESU anasema wanasema hivi wananipenda
kwa midomo, wanafundisha mafundisho ya wanadamu, wewe ni mwanadamu, Mwanadamu umeumbwa
na MUNGU, wewe umekuja duniani ukiwa tupu haya mafundisho umeyatoa wapi? MUNGU
anataka watu wafundishwe mafundisho yake peke yake, Wala sio mafundisho ya mtu
wa aina yoyote.
BWANA
YESU ASIFIWE,
Mnaelewa
watoto wa MUNGU, sasa viongozi vipofu ni watumishi ambao wanafundisha kinyume na
Biblia, nitakueleza kivipi? Kwa kifupi tu, YESU amenituma niyang’oe mapando ya
shetani, ili Neno lake liingie ndani yako ili wewe upate kupona unapokaza
shingo na kukataa hilo pando litakupeleka na wewe kule kule shimoni.
Kuna
vipofu wa aina mbili wako vipofu kiroho na kimwili – Nitaelezea upofu wa
kimwili, wa kimwili utaona mtu anapapasapapasa hivi na sasa wa kiroho ni
mtumishi ambaye anafundisha vitu ambavyo havijui wala havioni wala havijatoka
kwa YESU.
Wanafundisha
mafundisho ya kumtaja BWANA YESU, BWANA YESU, BWANA YESU! BWANA YESU asifiwe
lakini ndani yao mmmhhhhhhh!. Nami nimekutana naye, nimekaa naye nimeongea naye
amenituma niwaeleze mrejee katika neno lake yeye anakuja, atachukua wale ambao
hawana mapando ya shetani, mwenye mapando yake, Hayo mapando watu wasifikiri
yanapandwa kama mgomba au mahindi hapana, yanapandwa katika moyo wako kwa namna
ya maneno ya shetani.
Maneno
ya shetani hautaambiwa ni maneno ya shetani, yanachanganywa makanisani mfano mwepesi kabisa ubatizo wa
kikombe, ubatizo wa kikombe ni maneno ya shetani, YESU alisema fuateni njia
zangu ambaye yeye ndiye kweli alionyesha mfano sasa huu ubatizo wa kikombe umetoka
wapi? Kubatiza mtoto mdogo na kumbariki mtu mzima ! Hii kupindishwapindishwa
yote ni maneno ya shetani na kila ambaye yuko hivyo haendi mbinguni labda
abadilishwe,aokoke, abatizwe na aishi maisha matakatifu na atoke huko, na
atoke huko ndio atakwenda, ninawaambia niliyoyaona na sitaacha kuwaeleza na
kila nikikaa nakasikia mzigo, kwanini
husemi ujumbe wangu, kwanini husemi ujumbe wangu,
Mimi
ninavyokuwaambia hapa maneno haya sio mpaka maombi, haya umeshafunguka, nawaeleza
watu wote mkabatizwe,ubatizo wa maji mengi muishi maisha matakatifu na neno
lake MUNGU siku zote, milele siorobo, robo au nusu nusu.
BWANA
YESU ASIFIWE!
Jambo
lingine imeandikwa utoapo sadaka yako mtu yeyote asijue sasa unaandika jina,
unapewa risiti na hayo yote yakishajulikana ni mapando ya shetani, na MUNGU
hachukui na sadaka zote hizo mmetupa.
BWANA YESU ASIFIWE!
Nitakuja
kuelezea mfano mwingine, nataka muelewe habari ya viongozi vipofu, kama vile
dereva alivyo, asiyejua anaenda wapi,anaenda kuwatumbukiza watu shimoni huko na
ndivyo ilivyo watumishi sasa hivi vipofu wanawapeleka watu shimoni huko.
Nimewaona.
BWANA YESU ASIFIWE!
Nimewaona
ni roho, zamani ilikuwa kimwili sasa hivi ni katika roho. Kulitokea
mfano mmoja hapa Tanzania habari ya vikombe wakasema mtumishi ameoteshwa na
MUNGU, ameambiwa kwamba atachukua shilingi mia tano tu, wengine mia mbili, na
hizi zilifanyika na watumshi katika nchi nzima, sasa ninawaeleza kuwa ule
ulikuwa ni mtandao wa shetani, lakini kwa sababu viongozi walikuwa ni vipofu,
walitangulia na kusapoti, ukirudi kwenye Neno la MUNGU, limesema hivi nimekupa
bure toa bure iweje, huyo ni MUNGU aliandika Neno lake ambalo tunasoma katika
Biblia, sasa iweje huyu MUNGU abadilike aseme, toa shilingi mia tano tu? Je
MUNGU anaangalia shekeli yako? Je MUNGU ni hospitali?
BWANA
YESU ASIFIWE!
Sasa
uzidi kuelewa hao ni vipofu, na wote waliokwenda kule, walikwenda kupingwa
namba 666 na mpaka sasa hivi wanazo, waulize ni wapi MUNGU amesema kwamba
tukipewa cha kwake tutoe hela! Ndio upewe? imekuwa hospitali? Lakini watumishi
ndio wamekuwa wa kwanza kwenda huko, sasa nyie si watumishi wa MUNGU nyie ni vipofu
na hizo roho mlizokwenda kuzipoteza MUNGU atawadai zote mikononi mwenu
maana ni mafundisho ya wanadamu hayo.
Mafundisho
ya wanadamu kivipi? Mafundisho ya MUNGU unatoa bure, Ya mwanadamu leta pesa,
mafundisho ya wanadamu asili yake yanatoka kwa shetani.
Watu wote wanaokwenda kwa waganga si mnaambiwa
mlete pesa au kwa kitu fulani? eti MUNGU kasema! haaa hayo ni mafundisho ya
wanadamu, ambapo mungu Shetani, mungu aina ya shetani, shetani ndio hutapeli na
huchukua vitu vyenu.
BWANA
YESU ASIFIWE,
Sasa kanisa likajenga barabara na vyoo,
wakisema MUNGU ametenda katika nchi ya Tanzania! ninawaambia hivi yule ni “mchawi”
watu wote waliokwenda walipigwa namba ya
666, hataiona katika macho, inakuja katika roho, kingekuwa cha MUNGU mpaka leo
kingestawi kiko wapi? nikuulize ! Wangapi
mmekunywa na mpomnashida palepale na mnakufa?
BWANA
YESU ASIFIWE!
Haiwezekani
watu wanakwenda kumfuata YESU, ambapo eti kwenye kikombe ndio YESU huyo, alafu
wanafia njiani, wanakunywa na wanakufa, hapana mfunguke huo ni upofu.
BWANA
YESU ASIFIWE!
Biblia
inasema msiabudu sanamu, kanisani watu wanaabudu sanamu, ni maneno ya wanadamu
ni upofu, MUNGU sio mbao! Wala MUNGU sio sanamu! wala YESU sio sanamu, amekwisha
kusema katika kitabu chake, lakini watu wanachukua maneno ya shetani ndio wanayoyatumia, kuabudu
sanamu ni maneno ya shetani, ninawaambia ukweli ukubali au ukatae, mimi
nakuambia YESU anarudi.
BWANA YESU ASIFIWE!
Mmezoea
kuambiwa YESU anarudi! YESU anarudi! Hamuoni , sasa ahaaa! sasa ninayowaambia
yanatimia yote nikiwa hai hivi hivi na maisha yangu, na hata atakapokuja
nitamwona.
BWANA
YESU ASIFIWE!
Na
atashukia nchi ya Tanzania, ninawaeleza mjirekebishe msije mkawa, kama YESU
kule Galilaya alipozaliwa watu wakamdharau, lakini huko sehemu nyingine
wakamkimbilia, na ndivyo ilivyo isije ikawa kwa Tanzania. Mataifa mengine wasije
wakakimbilia wakapona nyie msije mkazubaa. Ninawapenda Watanzania, ninawapenda
Wakenya nina wapenda watu wote wa Dunia nzima, wa Afrika Mashariki ni wakati wa
kuokoka, bila kuokoka, kuishi maisha matakatifu na kubatizwa ubatizo wa maji
mengi, ni bure.
BWANA YESU ASIFIWE!
Siku
ya Pasaka amekuja akaniambia, “BWANA YESU”, “Hebron”! Nimekutuma kwa mataifa
yote, waeleze wabatizwe ubatizo niliobatizwa mimi, waishi maisha matakatifu,yanayonipendeza
mimi,.
BWANA
YESU ASIFIWE!
Kinyume na hapo! Mhhhhh! Kwa hiyo kama wewe
mpaka sasa hivi haujaokoka, ujue wewe una pando la shetani, ni mkristo lakini eti
upo kanisani, hujaokoka, wewe ni pando la shetani YESU hakuja kupanda mapando
ya shetani, mapando ya shetani yameletwa na dini na ndiyo yapo kanisani.Makanisa
yamekuwa kama makampuni,
BWANA
YESU asifiwe,
Sasa
hivi , ni habari ya pesa tu, habari ya Michango, kunyang’anya watu pesa zao na
mali zao, nami nawaeleza maana mnafikiri
kwamba mtabarikiwa, mnaibiwa hao ni “wezi,”
BWANA YESU asifiwe,
Ninakuambia
hivi hao ni wezi, kama MUNGU amemwita mtumishi, hatumi kwenda
kunyang’anya watu pesa, nyumba yake sasa hivi imekuwa ni pango la kunyang’anyia
wana wa MUNGU pesa, nyumba yake sasa hivi sio nyumba ya sala tena, imekuwa ni
nyumba ya biashara, walaki, elfu kumi, harambee, matangazo ya kwaya, m’baki,
hiiiii! wewe ukishasikia kanisani matumizi,
taarifa, ina maana mnaosomewa nyiie ni kampuni, kama mna hisa hapo.
BWANA
YESU asifiwe,
Ni
wakati wakubadilika BWANA YESU asifiwe na kishtuka, na kumrejea MUNGU ninawasihi,
bila toba, hakuna kwenda mbinguni, toba takatifu.
Wengine
wameongozwa sala za toba ni bure, wengine wamesema nimekata shauri, ameomkoka
lakini yupo huko huko, kwenye ubatizo wa kikombe na sanamu eti amekata shauri,
hakuna kukata shauri ni kuokoka. Hilo neno kukata shauri ni mchomeko wa
shetani.
BWANA YESU asifiwe,
Ili
wewe uwe mfuasi wa YESU uongozwe na mtumishi ambaye si kipofu, anayemjua MUNGU,
ameitwa nayeye, na anaeleza kweli, Ukileta Biblia na sasa hivi uwaulize
watumishi wote wanachofundisha hawana majibu. Sasa wewe umeumbwa kuja kuwekewa
mambo ambayo siyo katiba ya MUNGU? Katika nchi katiba mtu ukivunja unashtakiwa
na katiba katika ulimwengu wa roho ni biblia amesema usiongeze maneno yeyote
katika kitabu changu wala kupunguza kuongeza ubatizo wa kikombe? Tayari
umeondolewa mahali pema pa uzima ule, nami nawaambia rejea maana wale
watangulizi waliwadanganya na walikuwa mapando ya shetani, waasisi wa hizi dini
nao wako chini kuzimu wanateseka.
BWANA
YESU asifiwe,
Kibinadamu
ukimuuliza hawa waasisi wameanzisha haya madhehebu, yamekuwa makubwa dunia
nzima, hivi hili neno la “ubatizo wa kikombe” ndio YESU amewatuma? Mbona yeye
hakubatizwa kama sisi? kwanini sisi tumebatizwa hivi? Ina maana wamewapiga
upofu, mpotezwe na nyie.
Utasema
mimi siendi kuzimu, wapi wewe! Kama haujabatizwa, nakuambia maji mengi mpaka
sasa hivi jina lako liko kuzimu, ukubali! ukatae, habari ndio hiyo unapobisha,
ile siku utajuta nakuambia, utanikumbuka.Na wapo wengine wana batiza watu feki
feki tu, wamejiita na wanatumia uchawi, wamejaa Tanzania, wamejaa Kenya,
wamejaa Uganda wamejaa Rwanda, naongea habari ya Afrika Mashariki Ole wao,
Wataumwa magonjwa yasiyotibika, wako watakaopata magonjwa ya aibu kwa ajili ya kuwatesa wana wa MUNGU, umaridadi
wa shetani siku zote aliokutumia mwisho.
BWANA
YESU ASIFIWE
Lakini
amenituma nikueleze habari njema, ubatizo ule wa kikombe umeletwa na hao
waasisi wa dini ili kuwapiga watu alama za shetani, ndio maana ukizaliwa tu unawahiwa mapema ili YESU
asikupate utakapofika katika umri wako YESU alisema utakapokuwa na ufahamu wako
mwenyewe, kama yeye ndio ubatizwe kama yeye sasa shetani anakuwahi ukizaliwa tu
Kap! Anakupiga chapa yake unaishi maisha mabaya mpaka watu wanalalamika,
wanalaani kwanini wamezaa watoto, shida ipo wapi, tayari wewe sio wa YESU, huna
Baraka zile toka ukiwa mtoto mdogo kwa hiyo utashangaa watoto ni walevi,
majambazi, ni majangili, haya yote ni kwa sababu ya ubatizo wa kikombe
umepingwa pando la shetani, usijali kwa jina la Baba na Mwana na la Roho Mtakatifu, alafu na kikombe.
MUNGU anaangalia Neno lake, haliendani na Neno lake hayo unayoyafanya, hivi
nikuulize kuna mtu waanayetakiwa kuheshimiwa kama MUNGU?hakuna ! sasa kwanini
Neno lake aliloandika mnaweka dosari dosari , tiki, vema mstari hapa
mnabadilisha badilisha ina maana MUNGU hana akili, enyi wanadamu nani
aliyewaloga? Wazungu hamna kitu wameleta utapeli katika makanisa. Makanisa huku
yakasimamisha mizizi kuendesha utapeli hata wao sasa hivi ulaya hawaendi
makanisani kabisa wameshtuka, wengine wameona ni utapeli tu lakini wameshtuka lakini
watakuja kupona Tanzania ninawasihi rejeeni kwa YESU okokeni,
BWANA YESU ASIFIWE!
Ni
wakati wa mapando ya shetani kuyakataa hautaambiwa ni pando la shetani , ahaaaa
Maneno unayofundishwa wewe mda wote unatembea hapa na msalaba. Msalaba ndio
YESU? YESU anatakiwa akae moyoni,
BWANA
YESU ASIFIWE,
Lakini
haya yote ni mafundisho ya uongo yakachanganywa na uchawi, na miujiza ya kipepo
kama hii ya kufufua misukule YESU alipokuwa akifufua misukule alionyesha maiti
hii hapa na akafufua,wewe unaambiwa yule njoo njoo njoo njoo haya ni mazingaumbwe hao ni mashetani.
BWANA
YESU ASIFIWE
Yako
ndani yao ili kuvuna roho, unaweza ukaambiwa ni kanisa la uponyaji, la miujiza
la ufufuo, au la kinabii au la kitume, hii imewadanganya watu. Chunguza matendo
yao ndio utawajua, kivipi
wanayoyafundisha? Lakini ole wao hao ndio maadui wa YESU.
BWANA
YESU ASIFIWE!
Wengine
wamekuwa ni wachawi wananyang’anya mali za watoto wa MUNGU, MUNGU amewaumba
ninyi wanadamu amewapa vitu vyenu mmefilisika mnabaki kumlaumu MUNGU mbona
MUNGU ninakutolea sana mbona naishiwa? Ninakuambia hivi amechukua shetani wala
usimlaumu MUNGU nenda mwambie akupe mali yako aaache kukuchezea kabisa
BWANA YESU ASIFIWE
Haya
makanisa yote yenye Mabenki ni ya shetani nawaeleza YESU alipokuwa hapa
ulimwenguni alisema hivi usichukue fedha wala riba sasa kanisa linakuwa lina
riba ayaaa hilo ni pando la shetani.
Ninawaeleza matawajuaje? Chunguza matendo yao , Ni wakati
wa kufunguka na kuelewa BWANA YESU ASIFIWE
Msitishwe
na habari za miujiza ila sasa hivi ile miujiza
hawana nguvu, YESU anawashughulikia wanakijua kwenye ulimwengu waroho .
BWANA
YESU ASIFIWE!
Sio
kama anashindwa kuwaangamiza anawaangalia tu,anawachekecha anawachekea,
msifikiri YESU ni mpole, YESU ni mkali, hatari mngekuwa mmetumwa nay eye au
mnajua na yeye au mnamjua yeye msinge
fanya upuuzi huo kama ni ubabe ni YESU, aliingia hekaluni walikuwepo mamia
lakini aliwafukuza wote sasa wewe unafikiri YESU ni mpole ole wenu mnaoendelea
na mambo hayo wacheni nawaeleza utafika wakati msioujua mtakumbuka maneno haya
msifikiri ni sauti ya Hebron ni sauti ya
MUNGU inasema, rejea kwa YESU achana na mambo ya dini pokea wokovu, utakatifu,
ubatizo wa maji mengi basi hicho ndio YESU alichokileta YESU hajaleta madhehebu
hajaleta dini yaani yalikuwepo tu yeye ndiye mzabibu wa kweli akazaa tawi lake
sasa YESU tawi lake ni wokovu, utakatifu na maji mengi basi. Lakini leo ni
madhehebu yako hata milioni mia moja dunia nzima YESU, hakuleta madhehebu.
Madhehebu ni Elimu ya wanadamu na
Yalikuwepo na kwa sababu yalikuwepo sio aliyaanzisha, MUNGU na ndio maana alimtuma YESU. YESU mwenyewe
alipokuja wanampinga, wanamkataa na alikuwa anawaambia enyi vipofu , enyi
vipofu, enyi vipofu rejeeni, rejeeni
acheni na mimi leo hii nawaambia enyi vipofu, enyi vipofu acheni rejeeni kwa
YESU, acheni kupokea mafundisho ya kipepo
BWANA
YESU ASIFIWE
Mmefunga
sana ni kazi bure navyowaambia jicho la MUNGU linawaangalia mtamjibuje BWANA YESU, YESU, anarudi na anarudi na
anashukia Tanzania anayedharau , dharau lakini utakumbuka maneno haya. Mimi
sidaiwi roho yako BWANA YESU amesikia nimekueleza fanya uamuzi mwenyewe acha uchawi,
acha ushirikina, acha ulevi. Wachawi wote hapa duniani tayari wao ni wa kuzimu tu,
hata kama una hirizi wewe ujue huendi mbinguni jina lako liko kuzimu, una
mipando ya shetani wewe tayari huendi mbinguni
BWANA
YESU ASIFIWE
Cha
kufanya haraka ni wewe uokoke leo hii hapa uachane na hayo na BWANA
atakurehemu, lakini wako ambao wametengeneza
mambo ya uchawi hao wameshagombana na MUNGU hayo mimi hayanihusu wata
pambana na yeye, maana hata mimi siwezi kufanya lolote ni yeye yuko ndani
yangu, ni kama chombo tu nikueleze BWANA YESU ASIFIWE.
Toka
mwaka 2010 aliponituma kwenye kazi yake nikaianza mwaka 2011 nilikutana na vita
vingi sana lakini aliniambia hakuna hata limoja ambalo litafanikiwa juu yako
nami nimeyaona na bado nayaona zaidi maadui wanaangamia nakuteketea mimi
nasonga mbele watu wanazidi kumjua YESU,ndio kitu mimi ninachotaka na kulala
usingizi wangu,
BWANA
YESU ASIFIWE
Msiogope
watoto wa MUNGU mlizoea kuambiwa uchawi mnalongwalogwa, usiogope wewe
nitakapakuombea, ole wake anayekuloga namfyeka, haijalishi uko wapi , sijui
wapi ninapoomba utafuatwa,
BWANA
YESU ASIFIWE
Na
ninaona kila kitu rejeeni kwa YESU msitoe tena pesa makanisani za michango,
hayo ni mapango ya biashara mahali alipo YESU yeye ambaye anakaa ndani ya
Mchungaji au mtumishi YESU hasemi leta hela, leta leta hela, ahaaaaaa! Yeye ni
Neno lake, ukitaka utatoa mwenyewe, mchango ! mchango ! Mchango! Mpaka Tanzania
imeingia kwenye laana. Michangio !
michango ! michango makanisani !
Mmebaki kulaumu nchi na kulaumu viongozi sasa kama viongozi wa kanisa
wenyewe vipofu watawaombeaje viongozi wa nchi? Unakuta ni hao hao viongozi
vipofu , utakuta huyu yuko kwenye chama hiki, huyu yuko chama hiki, ni
mwanachama kabisa na anakadi sahihi kabisa, mtumishi aliyeitwa ma MUNGU
hutakiwi kuwa na chama chochote kile.Unatakiwa uwaombee vyama vyote.
BWANA
YESU ASIFIWE!
Lakini
unakuta mtumishi anakadi ya chama Fulani huyo ni pepo, tayari anaubaguzi ndani
yake sio MUNGU huyo ni kipofu, muwafukuze muwatoe huko wanawaletea laana,
mtumishi wa MUNGU haruhusiwi kugombea kabisa uchaguzi wa aina yeyote,
haruhusiwi ndio maana wengine makanisani mnapiga debe mpigieni mtu Fulani,
tayari wewe una chuki sasa heeeee nyie si vipofu utabisha.
Vichwa
vyenu watoto wa MUNGU visiongozwe na wanadamu tena mwangalieni MUNGU, peke
yake, mzidi kufuatilia vipindi vyangu kila wakati, kwenye television, kwenye
radio kwenye you tube, website yangu,kila wakati na vipindi vyote katika redio
na vitabu vyote nilivyoandika, endelea kusoma utapona roho yako.
Ninamwamini
YESU mimi ni muuminina mshirika wa YESU
peke yake sina chama chochote cha kimwili hapa duniani zaidi ya BWANA
YESU, peke yake, huwezi kuwa na mabwana wawili leo una biashara alafu unakuja
kanisani ni kipofu.
Kazi
yangu ni kuombea kila mtu. BWANAYESU ASIFIWE, anayesikia asikie na anayekataa
akatae ile siku mtajuta na kulia na kusaga meno itakuwa ni siku ya kutisha.Na
isiyoelezeka hata waliokufa nakwambia watasimama wotw kupita mbele kwenye
mstari, kila mtu atalipwa sawasawa na matendo aliyoyafanya na wakati ule
utakuwa sio ule wakati wa kuongea na YESU na kumshauri mimi sikujui sikujui,
atakuambia sikujui, sikujui wewe ni mzinzi, ulivunja amri zangu kumi, sikujui
wewe ni mchawi, sikujui wewe ulikataa ubatizo wangu, nenda kule, nenda kule.
Neno la MUNGU halirudi bure ndio maana kuna jehanamu na kuna paradise sasa wewe
shetani ndio amewekewa jehanamu pamoja na wafuasi watakaomfuata. Mimi nawaomba
nawasihi rejeeni maana ninaona huruma kwa jinsi nilivyoona mateso, watu
wanavyoteseka huko kwanzia sasa hivi, na wengi walipewa mapando ya kristo wa
uongo wako na masanamu, walidanganyw watawaombea mwaka kwa mwaka, ninawaambia
wote wako kule for you information dunia nzima, hakuna cha cheo gani au elimu
gani kila kitu ni upeezi mbele za MUNGU.
BWANA
YESU ASIFIWE
Ni
wakati wa kumrejea YESU nawasihi atapita
Malaika Mikaeli na BWANA YESU, maana yeye ndiye Malaika mkuu, sijui
niwaelezeje, ninawaomba muweze kuelewa ndani ya mioyo yenu na mioyo yenu
ifunguke maana haifai hata , mengine kinywa changu kinafungwa, mdomo nisiseme
maana siwezi nikuzungumza, mdomo
unafunga nisiseme hili hapana , bado wakati, bado wakato wake, linawekwa kaa la
moto nyamaza lakini ninachowaomba mumrejee BWANA YESU muokoke acheni mambo ya
dunia unapoipenda dunia wewe ni wa kuzimu na unapopenda ya mbinguni wewe ni wa
Mbinguni hapa ni pa kupita tu, ingekuwa ni mahali pa kuishi miaka yote
ungekaa pote basi. Hapa duniani hakuna
kitu kama ni magari mazuri yako mbinguni, kama ni majumba mazuri yako mbinguni,
kama ni kila kitu kiko Mbinguni hizi ni takataka watoto wa MUNGU.
Mali
mlizonazo, vyeo mlivyonavyo ni takataka mbele za MUNGU. Vyeo viko huko, hivi
ulishawahi kufikiri kama watu wanajiona hapa duniani wana waliumbwa na MUNGU
wana maisha mazuri eee wanajisikiaaa sasa hebu rejesha akili yako tu je yeye aliyewaumba wanadamu akawapa na uwezo wa
kutengeneza maisha yao mkayaona mazuri
yeye atakuwa anaishije? Yeye atakuwa anaishije? Hayo yamefichwa ninawasihi na
ndio maana hii miili ile siku ya mwisho kwa sababu tumetenda dhambi, utavalishwa
miili mingine tazama ELIYA peke yake ndio alipaa pamoja na HENOKO na BWANA YESU,
sababu miili yao ilikuwa mitakatifu hawakutenda dhambi hii miili itavurugwa
yote upewe miili mingine lakini wewe uwe jina lako tayari lipo kwa BWANA YESU,
BWANA
YESU ASIFIWE
Ninachowaeleza
kitabu cha BWANA YESU hakina majina kabisa, hakina yaa ni machache sana utakuta
katika Tanzania labda 4,000,000wanasema wameokoka nakuambia hivii wako
15,000 au 12, 000 nakuambia hivi hata
wewe uliyeokoka jichunguze njia zako, jichunguze maisha yako. Nahitaji na
wengine muokoke nitakapo kuongoza sala ya toba nikupe tiketi ya kweli maana
mimi si kipofu maana kama uneongozwa sala ya toba na kipofu ni connection yake
ni ya kipofu, BWANA YESU ASIFIWE, kama umeongozwa na mtumishi mchawi, mzinzi,
anayenyang’anya mpaka waumini wake, alafu anakuja kuuambia haleluya. Haleluya
BWANA anasema, mchawi !
Msidanganyike, ikishasikia habari ya partner usitoe, mimi
nakuambia ohhhhh ! wewe nenda ukale hizo pesa upate afya ukitaka kumtolea MUNGU
uamue na uangalie pia, ukishaoma mtumishi anamapando ya shetani kimbia ninakuambia kuna watu wana
miaka ishirini (20) sadaka yao haijawahi kwenda kwa MUNGU hata moja, lakini kila jumapili yuko kanisani
wanatoa unajua unapotoa sadaka unatakiwa uwe kichwa sio mkia kutokana na ahadi
za MUNGU, ukisoma katika Malaki inasema utakuwa kichwa wala sio mkia . heeeeh !
hebu jiangalie, msikubali kuwa vitega uchumi vya watumishi ndivyo wakristo
wamefanya na YESUameniambia watoto wake wamefanywa kama wafanyakazi wa
watumishi, watafute wawaletee, basi wawanyang’anye na wanawawekea mapando yao,
mapando yao, ehe !
Mtumishi:
Unataka kuniona ehee leta elfu hamsini, leta laki, MUNGU amesema toa mara nne
ni uongo, MUNGU anaangali Neno moyo wako tu MUNGU sio wa ubaguzi,
BWANA
YESU ASIFIWE
Na
wote ambao wanabatiza ubatizo wa kikombe hao ni viongozi vipofu soma katika biblia haupo wanaabu sanamu ni
vipofu sasa vipofu wamewakamata vipofu wamekuwa wengi sana nami ninawafungua
huo upofu utoke mrudi kwenye neon la MUNGU “Biblia” ambacho ni kitabu
kitakatifu alafu muone, vitabu viko vingi sana, kitabu cha kweli bwana ni
biblia tu, katika ukristo, sijui cha nani na nani vyote ni vya uongo, hichi
ndicho kilichohakikishwa hivyo vingine
vimetoka wapi? Msicheze na elimu ya MUNGU, msiongozwe maisha yenu kwa
theologia.
Mwanzoni nilipoanza huduma nilikuwa na mtumishi mmoja rafiki yangu, lakini nilishangaa
sana akaanza kunifundisha mambo ya kipofu unajua katika maombi bwana wakati
unapoomba pale ukiona wamama wengi yaani lazima ukizema kuna mama anaumwa tumbo
hapa lazima ztatokea ehheee nilishtuka sana, alafu ukisema kuumwa kichwa lazima
ukisema utakuta mtu anaumwa kichwa tu ,
ehee ukisema BWANA ameniambia kuna mtu anaumwa kichwa ehe! Wanaona kweli
kumbe ni fix, mhhh nilimsikiliza.
Siku
nyingine akaniambia Hebon tafuta wamama sitini, kila mwezi wakupe laki moja, kwa
mwezi una milioni sita, haujauchinja maisha yako, mimi nilizidi kushangaa tena
kumbe ndivyo mnavyodanganywa, watoto wa MUNGU na mmedanganywa dunia nzima,
BWANA
YESU ASIFIWE,
Jambo
lingine nalopenda kuwaeleza hi habari ya
stika, hizi stika zinatoka nch za Afrika Magharibi, watu wanaweka kwenye magari
halafu zina saini, unanunua pesa nyingi, nawaeleza kuwa zile stika ni hirizi,
nawaeleza kuwa zina nguvu amayo unapokaa nayo wewe nyumbani kwako au kwenye
gari kuna nguvu, aliyoivuvia pale ya
kipepo, kwa hiyo maisha yako na Baraka zako zinanda kwake zote anakucontrol na
wengi sana wamekwenda ndio shida imewazidi ujiulize unakwenda kwenye msaada wa
MUNGU eti shida ndio inazidi?
Uelewe hivyo, kuna watu wanastika ambazo zina
mikono hivi, unaambiwa kaa nazo sema MUNGU ananilinda, haya hizo ni hirizi,
ukazitupe au uzichome au kitambaa unaambiwa chukua elfu kumi au elfu tano YESU
hakai kwenye vitambaa choma tupa nimekuambia hizo ni hirizi yeye anakucontrol
anakuunganisha na yeye kipepo ili akuchune, hawa sio wachungaji wa MUNGU ni
wachungaji wa kipepo na ninayowaambia wengine watakufa mda sio mrefu, haya
nimewaambia!
BWANA YESU ASIFIWE! Vifo
vibaya sana sio mimi nimetamka hayo ni MUNGU, mtakayo yaona haya msishangae
wala kuogopa, mjue ni MUNGU, ni MUNGU, wala msilie mimi nimewaeleza maana MUNGU
anafanya kazi yake mwenyewe amewatuma wengi – walipopata pesa wakamkimbia
wakaamua kuifuata dunia, wengine, wanasema wanakula maisha sasa kwa YESU ndio
kuna maisha, hayo maisha wanaokula usifikiri ni chakula ahaa wameenda kwenye
kunywa pombe na uzinzi na wanawake, na kukataa kukaa katika utakatifu, na
kumfanya MUNGU aonekane maskini omba, omba, MUNGU sio maskini, MUNGU sio omba
omba, BWANA YESU ASIFIWE, na baadae hao
wengine wakaamua kwenda kwa huyo muovu awape nguvubaada ya YESU kwaaacha, kwa
hiyo wakaendelea, BWANA YESU ASIFIWE, maana wamekataa njia zake na kumchafua
BWANA YESU, ninawasihi mumrejee BWANA YESU muokoke
Mbinguni
hakuna kwenda kwa jina ni utakatifu peke yake, na wokovu na ubatizo wa maji
mengi, ameniambia waeleze dunia nzima. Kama wewe unajua haujabatizwa na maji
mengi, huendi mbinguni, huo ndio ukweli kama haujaokoka huendi na umeokoka,
vitu vyote vitatu na uishi maisha matakatifu.
Leo
mkristo ni mlevi, mzinzi, mvuta bangi na mshirikina muabudu sanamu, wewe unaenda
wapi wewe? Umnamjoke MUNGU wacha ujinga!
usidanganywe na upofu nimekufungua macho, Soma biblia usimrudie MUNGU kwa mazoea mazoea, MUNGU sio
mchezousimwone MUNGU mdogo wako, utakabana naye, utabenana naye, wakati Malaika
Gabriel anakuja kuchukua roho yeye anayejua inaenda wapi.
Matendo yako
uliyoishi nayo hapa ndio huko huko okoka, Narudia kila mlevi haendi mbinguni,
kila mchawi haendi, kila mwenye hirizi
haendi, wakati ni leo okoka, tubu na mubadilike na usidhirikiane hivyo vitu
tena maana hivyo ni vitu vya kuzimu, usizini na watumishi wanaokuzinisha, ondoka huo ni uchafu, pepo huyo mtumishi
anazini inamaana haiwezekani YESU hayuko ndani yake YESU angekuwa ndani yake
asingezini.
Mrejeeni
BWANA YESU, Mambo yameharibika lakini ninakuletea habari njema nitakuongoza
sala ya toba.
Sema
BWANA YESU naomba unisamehe dhambi zangu zote nilizozifanya Kwa kujua au
kutokujua namkataa shetani na kazi zake zote.
Ee
BWANA YESU , ninakureja wewe nishike mkono, niondoe kwenye mapando, niondolee
na roho yoyote inayonishikilia inayonifanya nisikufuate wewe, roho yako iingie
ndani yangu niongoze wewe unishike,
Mimi
ni mali yako hata huko huko nilipo mbali unilinde tembea na mimi, usiniache,
Amen
BABA
ninawaombea wagonjwa, ninawafungua kwa nguvu na mamlaka ya jina la YESU, nawaombea
usalama wataifa, nawainua, nawainua wanajeshi, nawainua maaskari,
nawawainua mawaziri namwinua raisi, Kwa
jina la YESU kwa damu ya YESU nawakomboa na kuwasafisha nawaombea neema ya
MUNGU ikajae ndani yao kwa damu ya YESU.
Nazidi
kuiinua Tanzania juu naondoa roho yoyote ya upofu katika nchi ya Tanzania
na hizi nchi nyingine zote kwa damu ya YESU kristo wa Nazareti
Mioyo
ya watu naifungua kweli yako MUNGU ikajae ndani yao kwa jina la YESU,
ninaifunika kwa damu ya YESU Kristo wa Nazareti mlioshikiliwa na shetani namnyang’anya,
mliokuwa kuzimu nawatoa nafsi zenu, nazirejesha kwa jina la YESU Kristo wa
Nazareti muwe sasa ni wa YESU nawakabidhi kwake MUNGU awabariki, MUNGU awainue,
msikubali tena kudanganywa na vipofu kuanzia sasa ninakuambia kwa nguzvu na
mamlaka ya jina la YESU uwe hai uwe mzima, usonge mbele usikubali tena kwenda
kanisani kumwabudu mtumishi kumpigia magoti na kumwomba yeye akujibu majibu
huyo ni pepo, maombi unatakiwa ujibiwe huko mbinguni ,
BWANA YESU ASIFIWE,
Usikubali
kubatizwa kwa jina la mtumishi, usikubali kutoa
huduma ya M- pesa, kanisani popote pale, ili upewe huduma hilo sio kanisa ni wizi, pesa zenu makae
nazo, mle mfurahie maisha yenu.
Nami
naendelea kuwaombea huko huko mlipo, tutaonana siku yeyote MUNGU akipenda kama
sio hapa duniani tutakutana Paradiso.AMEN
NABII
HEBRON