MAHUBIRI YA NABII HEBRON KUPITIA TELEVISION NA REDIO: ZITAMBUE IBADA ZINAZOMCHUKIZA
MUNGU
·
IBADA ZA SANAMU
·
IBADA ZA WAFU
BABA yangu na MUNGU wangu asante kwa ajili ya
muda huu na libariki jina lako na litukuza asante kwa ajili ya Wasikilizaji
mahali popote wanakusiliza maana wanakusikiliza wewe wala hawanisikilizi mimi.
Eeee MUNGU naomba ukamfungue. Natuma Malaika wako kwa nguvu na Mamlaka na upanga ulionipa wafunguliwe fahamu zao na
akili zao wapate kujua wewe ni BWANA na huu ujumbe wa siku ya leo ukaingie
ndani ya fahamu zao na na akili zao na hitaji kuongea na Mwanadamu kamili
sihitaji kuongea na mapepo, mapepo yote yatoke ndani maroho ya dini yatoke yote
ndani ya kila mmoja katika jina la YESU KRISTO WA NAZARETI.
BABA yangu ninakurudishia sifa na Heshima na
Utukufu, Asante kwa Malaika wako walioshuka mahali hapa. Sifa na Utukufu nakurudishia
wewe. AMEN
Ndugu msikilizaji mahali popote ulipo Nchi
yeyote, Bara lolote, Kijiji Chochote, Mkoa wowote.
Leo hii nina mambo baadhi ya kuyazungumza.
Jambo la kwanza nitazungumzia kuhusu Sanamu,
Ibada za Wafu na mengineo ambayo nitaendelea leo kukuelekeza siyo mimi nakueleza
ni YESU mwenyewe anayekuhitaji wewe, Wewe kazi yako ni kusikiliza na kubadilika
tuu, mambo yameharibika Ulimwengu umetekwa na Shetani, kweli imeondoka, uongo
tuu wa shetani, Na YESU anahuzunika sana, lakini sikiliza siku ya leo
naulifanyie kazi, hakika hautakuwa kama ulivyokuwa.
Nitaanza kuhusu SANAMU: Ningependa nikueleze
kidogo maana ya Sanamu ni nini?
SANAMU ni kitu chochote kisicho na uhai, ni kitu
kilichotengenezwa na mwanadamu na hakina uhai wala hakipumui wala kuongea.
Naomba usikilize tena!
SANAMU ni kitu chochote kilichotengenezwa na
mwanadamu hakipumui wala hakiongei wala hakina uhai.
BWANA YESU ASIFIWE……………..
Tutasoma Neno la MUNGU KUMBUKUMBU LA TORATI 5:
8-9 Neno la MUNGU lina sema Usijifanyie Sanamu ya kuchonga mfano wa kitu chochote
kilicho juu mbinguni au kilicho Duniani au kilicho majini chini ya Nchi
usivisujudie wala kuvitumikia kwa kuwa mimi BWANA MUNGU wako, ni MUNGU mwenye
wivu nawapatiliza wana uovu wa baba zao hata kizazi cha tatu na cha nne
wanichukiao
BWANA YESU ASIFIWE………………
Ndugu msikilizaji napenda nikueleze kidogo asili
ya sanamu imetoka kwa shetani ili kukuangamiza wewe usimwabudu MUNGU aliye hai,
maana Sanamu yenyewe haipumui kwanza, mungu huyo unayemwabudu inamaana hana pumzi
ni mfuu, kama nilivyokwisha kukueleza kwamba ni kitu chochote kilichoumbwa na
MUNGU na mwanadamu ukakiabudu.
Ukisoma katika KUMBUKUMBU LA TORATI 5: 8 – 9 inaelezea
vizuri sana huu ni mpango wa shetani. Na asili ya kuwafanya watu waabudu sanamu
ilitokea kwa Lucifa yaani shetani tokea vizazi na vizazi na baadae shetani
kuwateka wanadamu ndipo MUNGU akamtuma MUSA ulimwenguni kuja kuwaokoa Wana wa Israeli
kwa Farao ili awatoe kifungoni na alipokuwa amewatoa kifungoni ni huyu huyu Musa
alienda mlimani kuongea na MUNGU, MUSA akakawia kule, na ndipo MUNGU akamwambia
rudi nenda ukaangalie watu wako wanashingo ngumu yaani hawaamini hawaelewi
wametekwa na shetani, na hata MUNGU wa kweli hawamtaki.
BWANA YESU ASIFIWE…………
Watu wanaoabudu sanamu mnafananishwa na wale
wana Waisraeli pale jangwani, wenye shingo ngumu hawataki kumsikiliza MUNGU
aliyekweli, aliye waumba anafanana na sura yao.
Muache baadae MUSA ukiendelea kusoma, MUSA
akakuta wametengeneza sanamu mfano wa ndama ndio wanamuabudu eti ndio mungu
huyu.
Ooooooh!! Leo yamerudi!
Ndugu msikilizaji na Mwana wa MUNGU tena
unafanana na yeye unapumua kama yeye! Embu funguka ufahamu wako akili zako umjue MUNGU wa
kweli na usiwe kama wale wana wa Israeli pale jangwani , walivyo muuzi MUNGU,
Soma neno la MUNGU linaeleza wazi wazi ya kwamba msiabudu sanamu na kuifanya
mungu wako utaangamia.
Soma KUTOKA 32 : 35 MUNGU hakuwa mjinga kukuambia wewe,
kukuumba wewe kwa mfano wake, amekuumba
ili umjue yeye peke yake, wala usiabudu hata kitu alichokuumba yeye, iwe kwenye
nchi, majini hata angani, hata Malaika wake hata Watakatifu walioko mbinguni
hao ni yeye amewaumba ni viumbe vyake vyote wanategemea msaada kutoka kwake,
kwa taarifa kamili ameniambia YESU na mimi sibadilishi mnaofanya hivyo mmepotea,
nilipokuwa ulimwenguni, YESU na MUNGU alivyoniambia niliwahaidi nitawatumia
msaidizi ambayeni ROHO MTAKATIFU ndiyo yupo kwa ajili ya kukuombea wewe sasa
nikuulize swali, ndugu msikilizaji?
YESU alituachia msaidizi huyu. Msaidizi
atakayekuongoza ili ufike mahali alipo YESU, yaani yeye, Je? YESU alisema hawa Watakatifu wawe wasaidizi
na ndio watakuombea na kukuongoza ufike mahali alipo yeye jibu ni hapana. Hapo
tayari umeabudu Sanamu na unapotea funguka ufahamu wako, hata kwenye kitabu cha
UFUNUO 22: 19 – 20 Ole wake atayeongeza
maneno ya unabii wa kitabu hiki, Nikuulize Swali ndugu msikilizaji Je? Hawa Watakatifu
wapi kwenye biblia wameandikwa au tumeambiwa hao watuombee??
Tafuta hakika asilimia mia moja (100%) hautaona
kuanzia mwanzo mpaka mwisho, sasa na kufungua ufahamu huu ni mchomeko wa
Shetani ili wewe upotee, uangamie na huu ni mchomeko kamili ni sawa sawa na Wanawaisreli walivyokuwa
jangwani, MUSA alivyoondoka kwenda kuomba shetani akawaingizia mchomeko
wakatengeneza sanamu kumfanya mungu , Sasa nikuulize wewe , wewe umerudi
kuabudu sanamu huyo sanamuinapumua, kama MUSA mwana wa MUNGU Mtumishi wa MUNGU
alizivunjavunja akaziboma kwani leo hii zimerudishwa tena, Kataa funguka
muabudu MUNGU aliye kweli.
BWANA YESU ASIFIWE……….
Kitu tofauti na hicho na MUNGU aliyeumba
Ulimwengu, huyu MUNGU wa IBRAHIM, MUNGU wa ISAKA na MUNGU wa YAKOBO usiabudu utahukumiwa. Soma
KUTOKA 32:33-35 Na BWANA atamfuta jina lake katika kitabu cha uzima mtu anayeabudu
sanamu,
Narudia soma KUTOKA 32:33-35 Mtu yeyote
anayeabudu Sanamu BWANA atamfuta jina lake katika kitabu cha uzima. Inamaana
kama sasa hivi unamuabudu bado sanamu tayari jina lako halipo ila uamue tayari
jina lako halipo ila uamue utoke huko ndiyo jina lako litafutwa. Sawa sawa na
wana wa Israeli Musa alivyovunja ili sanamu ndiyo wakaondoka wakapona kinyume
na hapo wangeangamia.
Musa akasema walio pamoja na mimi MUNGU wangu
wanifuate wale walimfuata MUNGU aliye hai MUNGU wa MUSA wakapona na ile sanamu
ikabomolewa, inamaana wangebaki kwa yule mungu sanamu wangekufa.
Oooooh!!! MUNGU tusaidie hivi ndivyo mwana wa
MUNGU injili ilivyobadilishwa, imekuwa tofauti kabisa na YESU alivyoagiza ndiyo
maana watu wanaangamia hamna majibu hata Mbinguni hawaendi.
BWANA YESU ASIFIWE………..
Oooooh!! MUNGU atusaidie yawezekana wewe
unampenda MUNGU ila umerithi sasa yakatae ili upone maana ni machukizo kwake.
Ndugu msikilizaji soma katika kitabu cha
KUMBUKUMBU LA TORATI 5: 8 – 9 MUNGU amekataa usichonge na kujifanyia sanamu na
kitu chochote Duniani hata kilicho chini ya Bahari usikiabudu na hii ni moja ya
amri aliyompa Musa kwa ajili ya Wanadamu wote na wewe sasa hii umeshavunja hii
amri ukisoma katika kitabu cha YEREMIA 17: 5 , 7 Amelaaniwa amtegemeaye Mwanadamu Amebarikiwa
amtegemeaye MUNGU, Inamaana umwabudu yeye tuu.
Watakatifu wote hawa walikuja
ulimwenguni ni mwanadamu hawa siyo MUNGU wakati YESU ananielezaujumbe huu
pembeni yake nilmuona Ibrahim BABA yetu wa Mataifa ambao sisi ni kizazi chake
ni mmoja wa wazee 24 na pembeni yake mama yake
YESU akihuzunika sana na kuumia moyo wake akichukia yeye kuuabudiwa,
YESU akaniambia nafikiri unaona hata mama yangu analia, na kwanini YESU
alinionyesha ilikuwa ni katika shule anayonifundisha ili nijue cha kueleza
maana mimi haya yote ni yeye ananifundisha mimi Sifundishwi na mwanadamu,
Yanatoka juu anakuletea wewe. Ni jambo la kuhuzunisha soma jinsi mpango wa
MUNGU ulivyobadilishwa, hata amri zake kuzarauliwa tena wazi wazi aacheni moto
unawasubiri wafanyao hivyo aacheni mtaangamia,hii ni janja ya shetani ndani ya
kanisa ili msimuone YESU.
YESU siyo mnafiki na mahali ambapo amri za MUNGU
hazifuatwi haijalishi jina lake linatajwa hapo, ni kupoteza muda maombi hayo
hayaendi mbinguni ni machukizo ameniambia YESU na mimi sipunguzi neno lolote
nampenda na kumheshimu, wala siogopi
wala sipunguzi alivyofanya yeye na mimi ndivyo nafanya hivyo hivyo.
Nilivyoelezwa na MUNGU sibadilishi, Funguka upone nikuulize swali
je? kama umeshajua sanamu haina uhai na
unaabudu je? Itakujibu? Na je Majibu
utakayojibiwa yatakuwa ni ya ni MUNGU aliye hai au Mungu mfuu, jibu ni mungu
mfuu, mungu mfuu ni shetani.
Ukiangalia Wana wa israeli pale jangwani baada
ya Musa kuja kupasua ile sanamu wakashutuka wakaona kabisa ni mungu mfuu hii
sanamu, MUSA akasema walio na mimi wanifuate wasio na mimi wakae pembeni, sasa
na wewe umefanyika kwamba unayeabudu sanamu hauko na MUNGU wa Musa,uko na mungu
mfuu, uko na mungu shetani wakakimbia na wewe kimbia ili upone.
BWANA YESU ASIFIWE………
Mpango wa MUNGU kitu chochote kisiabudiwe na
kufanywa Mungu ukishiriki wewe ni mali ya mfuu na huendi mbinguni na chanzo cha
kuabudu sanamu ndani na nje ya kanisa ni baada ya wale Mitume wa YESU kuondoka
wengine wakakengeuka na kumkufuru ROHO MTAKATIFU.
Narudia chanzo cha kuabudu sanamu ni kumkufuru
ROHO MTAKATIFU na hiyo dhambi haisameheki,
tafadhali wacha ujumbe huu ni kwa ulimwengu wote wanofanya hivyo ujue
umepotea na hauna YESU na panapofanya Ibada kama hizi YESU ameniambia sipo,
Hayupo hapo na kama YESU hayupo, shetani ndiyo yupo ndiyo amekaa hapo funguka,
utaona Musa mwenyewe alivyovunja ile sanamu ile ya ndama na zaidi hata mama
yake YESU na wazee 24 hawataki waabudiwe na wanachukia sana na zaidi wanafanya
hivyo hamsikilizwi maana kama MUNGU ameshakataa hata pia katika kitabu cha
Muongozo wa Safari ya Mbinguni yaani BIBLIA imekataa na haya ya kuabudu sanamu
YESU amekataa sasa ni kwanini mnajilazimisha kuabudu kataa wewe soma katika
kitabu cha UFUNUO 22: 18-20 aliyeyaleta haya hukumu inamuhusu na amemkufuru
ROHO MTAKATIFU, Tafuta kitabu chote hautaona, Mrudie YESU na umuabudu yeye
ndiye Mfalme wa Wafalme, Bwana wa Mabwana.
BWANA YESU ASIFIWE……
Jambo
la pili nitanzungumzia juu ya Ibada za Wafuu.
IBADA ZA WAFUU : YESU hazitaki hayo ni mapokeo
ya shetani ni ibada ambazo zinaushirikiano kati ya wewe na mizimu, mizimu ni
roho za watu waliokufa walivyokuwa hapa ulimwenguni hawakuokoka au kuishi
maisha Matakatifu, sasa wakifa hawa huenda kwa baba yao kuzimu maana kuzimu ni
mahali ambapo shetani anakaa, Ndiyo maana wanaitwa mizimu, ukienda Mbinguni
unaitwa Mtakatifu na wanaokufa katika Utakatifu wanaenda Paradiso. Wanapumzika
wanasubiria ule mwisho, siku hizi watu husema peponi YESU ameniambia sio sawa
peponi ni nyumbani kwa mapepo.
Nikuulize swali wewe msikilizaji, kwa nini tunasema
toka pepo? Shindwa pepo, umelaaniwa pepo, hata Kiswahili unashindwa kukielewa
hii ni technique amekamata shetani alivyokamata kanisa hata kinywa, anaenda
peponi inamaana umemwambia mtu anaenda kwa mapepo, ni Paradiso tuu hicho ni
Kiswahili kimebadilishwa, nafikiri mnaelewa mapepo, huu usemi sio sahihi ni
kuulize je unapenda kwenda kwa mapepo au unapenda kwenda Paradiso, maana kinywa
kinywa kinakiri unaenda wapi, Jibu hapana Watu wameshikwa ufahamu wa kujua
wanatamka nini. Ibada za wafuu huo ni mpango wa shetani ili wewe usitengeneze
maisha yako au ushirikiano wako wewe na MUNGU ukijua kwamba ukifa utaombewa na
kwambia inakula kwako.
Soma kitabu cha MUHUBIRI 9: 4-9 Nitaanza
MUHUBIRI 9 : 5 – 9 Kwasababu walio hai wanajua ya kwamba hawatakufa wafu
hawajui neno lolote maana hawana ijara tena maana kumbukumbu lao limesahaulika.
BWANA YESU ASIFIWE……..
Ukishakufa tu yamekwisha sasa unaombewa nini,
Acha kudanganywa na zaidi hata soma katika kitabu cha WAEBRANIA 9: 27 Neno la
MUNGU linasema ukisha kata kauli baasi.
WAEBRANIA 9 : 27 Na kama vile watu wanawekewa
kufa mara moja na baada ya kufa hukumu sasa nikuulize Ibada ni za nini hizi,
wewe unaacha kutengeneza unasubiri utafanyiwa, funguka hizo ni Ibada za vipofu
tuu, kama imeandikwa ukikata roho ni hukumu hizo Ibada za wafu ni za nini tena
unapoteza muda usidanganyike hizo Ibada kila unaposhiriki wale wafu
wanakunajisi na wewe, uwe kampani moja mkamwabudu shetani.
Funguka usishiriki ni Ibada sawa nakuabudu sanamu , kufanya
matambiko kushiriki uchafu, nikuulize swali je? YESU ndiye ametufundisha haya?
Hapana; kama hapana imetoka wapi? Imetoka kwa yule muovu, YESU ameniambia hata
kaburi lake lisiabudiwe limetengenezwa na mwanadamu tena limechongwa na yeye
akaenda kuwekwa tu na yeye hayupo hapo yupo mbinguni ndipo makao yake kiakili
kibinadamu tunajua YESU ameenda kutengeneza makao na amesema hivi hapa siyo
kwenu, makao yenu yako mbinguni, sasa kwanini usimuabudu aliyoko Mbinguni,
unaabudu vitu vilivyokuwa hapa.
Kaniambia hapa ulimwenguni kwenye Mabara yote
Baadhi ya Watumishi wamejenga makaburi na kuyaita kaburi langu na kuliita ni
Makaburi ya Watumishi walio maliza kazi ya hapa Duniani yaani ni wale Mitume
wale wa kwanza, mwingine kaburi la Paulo, mwingine la Isaya , mwingine Daudi,
mwingine Yoshua, na mengine mengi, kaniambia ooooh Namuona YESU mbele yangu anavyohuzunika
jinsi ulivyopotea ulimwengu. Akaniambia hawa sasa hata waliokufa 99% Watumishi
Wa sasa hivi 99% hawajaenda Mbinguni wapo kuzimu hawajapokelewa wanasubiria
hukumu huu ni ukweli asilimia 100% siyo kufikiria kuwa utumishi ndio tiketi ya
kwenda Mbinguni utakatifu na kufuata aliyoagiza MUNGU, kama hukufuata na
ukaabudu vinginevyo mfano sanamu utaenda kwa mwasisi wa sanamu mwasisi wa
sanamu ni shetani ambaye ameazisha kazi hiyo maana anaouhalali na wewe
unamwabudu MUNGU aliye hai MUNGU aliye hai hana uhalali na wewe maana
haujamwabudu yeye na umemkana na yeye anakukana waziwazi.
Badilika mrudie YESU
wa kweli usidanganyike maana Wana wa MUNGU ukiambiwa hapa ni nyumbani mwa
mtakatifu yeyote hapa duniani makao yao yapo mbinguni nakwambia, na ukikuta
kunakaburi ukaambiwa, na ukaambiwa hapa ni Goligota au lamba udongo,au sujudia
au lala hapo juu, piga magoti msujudie mungu piga kichwa chini usikubali, YESU
ameniambia huu ni usanii kwanza kiafya tuu, kulamba udongo utapata minyoo
magonjwa na ni uchafu.
Pili Maana yake kulamba udongo makaburini
unapolamba huo udongo nafsi yako unajipatanisha na mauti iliyo juu ya ilo kaburi.
Tatu unaanza kuporomoka maisha yako ya kiroho na
kimwili na mwisho wake na wewe ni wakuzimu
Nikuulize swali, Wapi YESU aliagiza hivyo yeye
ndiye njia ya uzima na kweli soma katika kitabu cha YOHONA 14:6
Sasa ndiye mwasisi amesema tufanye hayo, Jibu hapana unakuwa umeabudu
sanamu.
BWANA YESU ASIFIWE ……………………
Jambo lingine hili ni sugu kiasi ambacho
inafanyika kwakumpinga YESU ndani ya Kanisa jambo hili ameniambia ni kuhusu
sadaka ya mavuno, ameniambia niwaeleze
watoto wangu hiyo sadaka siitaki na sizipokei kwa maana, hata nilivyokuwa
ulimwenguni, moja wapo ya mambo niliyoyakataa ni hiyo sadaka ya mavuno kwa
jinsi ilivyoletwa kwenye nyumba ya Baba yangu pia ikafanya nyumba yangu siyo
nyumba ya sala tena imekuwa Soko ukisoma katika kitabu MARKO 11: 15-18 inaelezea vizuri YESU aliingia
Hekaluni bakakuta nyumba ya Baba yake imekuwa Soko, akanimbia mwanangu na kufunulia zaidi
nilikuta hivi hivi, sasa mimi siyapendi, waeleze watoto wangu, wafunguke maana
wananipenda.
Funguka ndugu msilikilizaji nakuelezea vizuri uelewe
maana ya sadaka ya mavuno au mazao hii sadaka ya fungu la kumi kutokana na kile
ulichokipata, ndicho ukitoe katika mazao yako. Sasa hii wewe uza kwanza mfano
umepata magunia 10 ilo limoja liuze ile hela weka kwenye bahasha ndio ukapeleke
kanisani ni gunia moja tu uza uweke kwa bahasha, akijua mtu tu tayari hapo ni
sanamu .
Pili unapoleta hayo mazao kila mtu anajua
umemtolea nini, Matokeo yake siyo siri tena haupati thawabu ya MUNGU unapata thawabu
ya wanadamu. Jambo lingine unavyoleta hiyo unamfungulia shetani nafasi ya
kurudisha yale aliyoyakataa YESU yasifanyike ndani ya nyumba ya sala mazao hayo
utashangaa baada ya Ibada kanisa linakuwa soko au mnada , Elfu , Elfu ishirini,
mia, laki sasa halijakuwa soko jibu limekuwa soko, sasa ndugu msikilizaji Embu
soma kitabu cha MARKO 11 : 15- 18 inaeleza jinsi YESU alivyowakuta wakiuza
ndani ya Kanisa alikasirika akatibua kila kitu maana hayo hayafai na sio mahali
pake, siku hizi hayo mambo yamerudishwa, na aliyerudisha ni shetani.
Nikuulize
swali je mnada unaruhusiwa ndani ya kanisa au YESU anapenda biashara ifanyike
ndani ya nyumba ya sala au je kazi yake kanisa ni kunadi vitu jibu ni hapana,
usishiriki tena ndugu msikilizaji, unatakiwa utoe uuze uweke kwenye bahasha
ufunge isionekane na mtu yeyote, Madhara yake sasa kwako wewe unayeshiriki
unakuwa unashiriki kuchafua nyumba yake ya MUNGU unakuwa haubarikiwi, maana
kila mtu anajua siri yako. Neno la MUNGU linasema kushoto wala kulia isijue,
unavyobebana na magunia yako, watu wote siwanaona ni siri tena hiyo inakula
kwako.
Jambo la tatu Baraka zako zinanadiwa watu
wanapanda bei zaidi ya watatu nahao wanakuwa wameshiriki, mnagawana unabakia
hauna unafilisika unabakia hauna Mkono wa MUNGU
haupo juu ya mazao yako, Nikuulize swali je MUNGU yeye hajui kwamba wewe
umetolea ilo gaunia moja na anajua thamani yake lakini huyo huyo kwanini watu
wengine waende kuuongezea thamani huyu MUNGU aliye kupa hayo magunia kumi
anajua thamani yake na Baraka zake ziko katika gunia lako limoja katika fungu
la kumi haya mengine yametoka wapi kuja kuharibu Baraka zako huo ni mchomeko wa
shetani ili kuuondoa Baraka zako kuongezea na baraka za shetani usikubali, Baraka zako za fungu la kumi
kushirikiana na watu wengine kataaaa.
BWANA YESU ASIFIWE……………….
Ndugu Msikilizaji embu angalia Kanisa
lilivyotekwa na Shetani, mpaka mambo ya shetani, yanapewa kipao mbele na ya
YESU yanapuuzwa nakwambia 98% YESU hayupo ulimwenguni asilimia 2% tu. Amua
uingie upande wa YESU wa kweli, Kanisa limekuwa ni biashara kweli haipo,
Watumishi 45% ni washirikina kwa kiwango cha juu sana, sasa kweli utaponea wapi
mwangalie YESU.
BWANA YESU ASIFIWE………………………
Jambo lingine nitanzungumzia kuhusu madhabau
iliyokufa sababu katika kitabu cha TORATI 5: 8 utasoma mwenyewe muda hautoshi,
Madhabahu iliyokufa ni Madhabau ambayo haifuati taratibu za MUNGU na maelekezo
aliyoacha YESU chunguza madhabahu unayoabudu ukikuta haiko sawa na YESU mwasisi
wa Kanisa alivyopanga ikiwa kinyume ujue hiyo ni madhabahu mfuu ukikuta
inachangisha pesa hiyo ni mfuu, kwasababu MUNGU hataki ukikuta mnaandika majina
kwenye sadaka hiyo ni mfuu MUNGU hataki.
BWANA YESU ASIFIWE……………………
Nitaelezea kidogo maana ya Sadaka halafu
nitaendelea tena.
SADAKA ni Ibada yako kamili kati yako wewe na MUNGU
aliyekuumba unamtolea MUNGU ili sadaka yako inene kama ya Abel na ili sadaka
yako inene mbele ya MUNGU kwanza mtu asijue umetoa kiasi gani, ukisoma katika
injili ya MATHAYO 6 : 2-4 Inaelezea usishauriwe na mtu hata Mtumishi asijue
umetoa kiasi gani, Sadaka yako ya kweli ni fungu la kumi na shukrani, Sadaka za
michango hizo hazi muhusu MUNGU sadaka za kuahidi madeni Imani eti ukipata eti ulete na zote
hata Ukombozi siyo ya mpango wa
MUNGU, Hiyo ni ujanja wa shetani
ameliteka kanisa na kubadili mpango wa MUNGU na wewe usifanikiwe na
ushindwe kufanya hayo ambayo aliyaruhusu upate kushiriki dhambi.
BWANA YESU ASIFIWE……………………………………
Ukiambiwa toa mpaka ikuume usifanye hivyo
haipokelewi toa kwa furaha YESU hanyang’anyi pesa kama ilivyo makanisani siku hizi
huyo ni shetani na anayefanya hivyo ndani ya moyo wake Mtumishi huyo ana roho
ya kuasi na tamaa juu ya pesa ukifuatwa kudaiwa pesa nyumbani kwako eti mchango
kanisani labda pesa mfano wa kununua kitu mfano kinanda, gari, mabati msitoe.
YESU ameniambia mimi siyo omba omba na hana
shida kama nimpango wake ataleta watu watafanya tena kwa furaha ukitoa ndugu
msikilizaji haubarukiwi ni sawa sawa na kutupa jalalani wote mlikuwa mnafanya
hivyo mmetupa jalalani, Unashangaa Asubuhi saa 12 ni ngongoooo nataka hela ya
kununua mabati tunataka hela ya mbao. Kama hilo kanisa ni YESU amelileta
ataleta hela pale kanisani siyo kukufatafata huko mjue hayupo huko au unaambiwa
kinanda mchango, unafutwa asubuhi na mzee wa kanisa. Eeeh leta leta , hata
unayefanya hivyo hujui, Funguka usiende kukusanya ooooya una muudhi MUNGU,
ameniambia YESU niwaambie ulimwengu wote YESU anarudi Utukufu wake ni wa mwisho
ndio huu sasa umeaanza ni kweli tu mpaka aje na sasa hivi anaharibu uovu wote.
BWANA YESU ASIFIWE………………………….
Ukikuta madhabahu inachangisha au kukopa pesa
benki hapo hayupo nasema sadaka zenu zinapotea YESU halipi Riba. Leo oooh
mnalazimishwa kulipa riba, YESU kama yeye mwenyewe alishakataa huyo ni shetani
ameingia ndani ya kanisa mnalipa riba, hapo shetani amekunja nne anawachuna,
YESU hakopi wala kulipa Riba leo hii iweje kanisa likope benki siyo kanisa
likope benki siyo kanisa lake ameniambia hata kama jina lake linatajwa hayupo
ni machukizo, Soma katika kitabu cha MARKO 7 : 6 -7 Inaelezea vinzuri kabisa.
BWANA YESU ASIFIWE…………………….
Funguka ufahamu ndugu msikilizaji mahali popote,
madhabahu iliyokufa inakopa Benki hiyo ni mfuu ukikuta madhabau inatoa huduma
za kiroho mfano kukuombea unaambiwa utoe pesa hiyo ni mfuu madhabahu inafanya
kazi ya Biashara ni mfuu, madhabahu hauwezi kutumikia Mabwana wa wawili,
madhabahu ya YESU , YESU hakutumikia mabwana wa wawili, YESU na yeye mwanzoni
alikuwa fundi Seremara aliacha kamtumikia MUNGU peke yake, Sasa leo hii mwasisi
wa Kanisa amesema hawezi kuwatumikia mabwana wawili hizo biashara si mabwana
wengine hayupo hiyo ni mfuu.
Kazi ya Kanisa siyo kufanya biashara ukiona hauoni
majibu unakaa hapo miaka nenda rudi haukuwi kiroho wala kimwili wala kubadilika
ujue mfuu hilo, Ukiona ni mateso magonjwa na umaskini, ufakara tu ndio umekujaa
ujue kwamba ni mfuu ilo kanisa, huwezi kaa kwenye kanisa hai hayo matakataka
yabaki ndani yako ukiona nguvu za giza zinakutesa na hazikutoki unaenda hapo
kanisani na hayatoki miaka na miaka wewe unanyongwa na majini mapepo wachawi
wanatembea nyumbani kwako madukani kila mahali watoto, mambo hayaendi naunaenda
hapo kanisani ujue hapo unaposali ni mfuu.
BWANA YESU ASIFIWE……………….
Sasa napenda nikuulize kwa nini madhabahu
zinakufa sababu unakuta mtumishi hana muda na YESU.
Moja ni mzinzi, ni mlevi, au anatumia nguvu za
giza au anaifanya hiyo kazi kama ya mshahara, au amejiita mwenyewe na hata wengine wameitwa lakini wamebadilika kwahiyo akibadilika
tu madhabau inakufa au yupo kwa kusudi la pesa tu. Japo wengi ni washirikina
mahali hapo hautaona jibu na zaidi unapokuwa kwenye madhabahu mfuu tayari na
wewe hapa duniani unakuwa mfuu japo unatembea unakuwa box tu.
BWANA YESU ASIFIWE…………………
Hii ndiyo namna ndugu msikilizaji nazidi
kukufungua ujue jinsi kanisa lilivyotekwa ni pesa tu, limerudia tu, sasa hivi
wameacha kuyasema haya kweli na haya mengine yametoka kwa wanzilishi wa hizi
dini wakaleta huku kwetu tukayapokea na mahali pameandikwa Wa kwanza atakuwa wa
Mwisho na wa Mwisho atakuwa wa Kwanza, na hii injili ilianza kwa watu weupe
wakaijua ukweli wanaukataa sasa YESU amerudi anaufungua ukweli yeye mwenyewe,
Watumishi wamekataa kusema kweli japo YESU ameniambia wanakuchukia lakini
usijali mimi nimekushika kwa mkono, Mimi niko ndani yako nina hitaji watoto
wangu kwa gharama yeyote sasa nawafungua wanijue mimi njia zake si njia zetu,
Akili yake sio akili yako, akasema BWANA YESU akaniambia watu wakisikia habari
za YESU wanafurahi ninafurahi na mimi na wewe YESU anakufurahia lakini
umepotoshwa.
Funguka na hayaniliyokueleza siku ya leo
yakafanye kazi mimi sitoi hapa duniani ananichukuwa kaa andika ananifundisha na
mimi na kueleza yashikilie sana haya ndugu msikilizaji utapona usiabudu sanamu
tena unapoabudu sanamu mungu unaabudu mungu mfuu mwasisi wa sanamu ni shetani
ukiabudu shetani unamchukiza MUNGU hata ukisema sala ya Baba yetu hausikiwi
wala haziendi huko, zinaenda kwingine.
Funguka soma tu mwenyewe katika kitabu
cha Neno la MUNGU ambalo ndio mwasisi aliyeagiza yafuatwe na MUNGU mwenyewe
alivyowatuma Manabii wake akiwepo MUSA, YEREMIA,wote walitolewa juu wakiwa wanapewa
ili kuyafanya, anasema watumishi wanamtaja kwa midomo yao tuu kwamba wanampenda
lakini hawayatendi, ni waulize ndugu wasikilizaji hata wewe funguka je
anayaabudu sanamu huyo anampenda MUNGU? Anamuheshimu MUNGU, huyo kama
hamuheshimu kama angekuwa anamuheshimu MUNGU angefanya kama MUSA uvunjevunje
haya masanamu.
Ndugu msikilizaji funguka wachana na hayo mambo
mambo, ni machukizo na ni mabaya sana sana yanakunajisi wala Mbinguni huendi wala usibusu sanamu imetupasa
kumuomba MUNGU na kumuabudu katika roho.
Sasa mmerudi kimwili wewe unaabudu sanamu kwanza
haujarudi kimwili utamuona MUNGU humuoni MUNGU.
BWANA YESU ASIFIWE……………….
Hii ndiyo shetani pia ameliteka kanisa na
kidonda sugu ni sadaka ukiambiwa sasa hivi hivi mwana wa MUNGU ndani ya nyumba
ya MUNGU wa laki laki simama, miatano
mchango usitoe hata unakuwa umeshiriki kufanya biashaya ndani ya nyumba ya
MUNGU , usitoe hata mafandraise ya michango ya majengo usishiriki ameniambia
hivyo YESU, yeye sio omba omba, Watumishi wamuombe yeye, yeye ataleta Sadaka
zote ulizokuwa umeahidi na kwambia usitoe na hizo naziri nazifute leo wala
usirudi huko unaibiwa haziendi kwa YESU, nazungumza kwa ujasiri sana na mimi
wala siogopi alivyotumwa Musa alivyotumwa Paulo, alivyotumwa Yeremia, Na YESU
mwenyewe alivyotumwa na BABA yake Mbinguni na mimi MUNGU nimeongea naye
ameniambia na wewe nenda kafanye kazi hii mimi siogopi.
Nakueleza ukweli
nitapita hivi hivi siku zote nchi zote nitamaliza, wako wengine wanaomba
niondoke Tanzania, Siondoki ng’oo ng’oo ukweli lazima ujulikane uchawi mwisho,
Kuzimu nimeshafunga tangu mwezi wa 4.2012 watu wamrudie MUNGU Jehanamu ipo ila
ya waovu, hawawezi kupona wote, Embu nikuulize asilimia 2% Ulimwengu mzima embu
angalia nyie mnaoenda makanisani mnaomba mnaomba halafu hiyo asilimia 2% haupo,
Jenga urafiki na YESU tu mwangalie YESU atakusaidia atakuongoza, badilika
badilika na leo mnakwenda kufunguliwa sana tupa ma sanamu huko, wala usiambiwe
MUNGU Fulani mpaka nisaidie.
Aaaah!, MUNGU hana mpaka wewe unamuwekea MUNGU mpaka
unaakili kwanza wewe. Unamuomba Mtakatifu Fulani nisaidie mbinguni
nisaidie,MUNGU alikwisha tuachia ROHO
MTAKATIFU ndiyo atuombee, jenga ushirika na ROHO MTAKATIFU basi.
BWANA YESU ASIFIWE………………………
Ndugu msikilizaji MUNGU akubariki sana.
Nitaenda kukuongoza sala ya Toba kwa wale
wanaopenda kuokoka na kuacha ma sanamu ni machukizo na usitoe tena mambo ya
sadaka ya mavuno usiende kufanya biashara utapigwa.
SEMA BWANA YESU….
Naomba Rehema naomba unisamehe hata nilipo abudu
sanamu na kurudia wewe, uandike jina langu kwenye kitabu chako cha uzima wa
milele, Na mkataa Shetani na kazi zake zote na Ibada zake zote, usiniache nishike
mkono niongoze mimi ni mali yako YESU, sio mali ya mwanadamu au ya dhehebu au
ya jengo nilitoka kwako nishike mkono hapa duniani uliponileta nikazaliwa
nimekutana na machafu haya nikanajisika ili nisirudi ulipo wewe. Ulikotoka
Mbinguni ukaja Duniani BWANA YESU, Ukashinda ukarudi kwa BABA na mimi
najikonect hivyo hivyo nishinde nirudi ulipo haya ma sanamu ma ibada mengine
matambiko sitaki tena niongoze mahali ulipo wewe YESU. AMEN
Nakuombea wenye magonjwa
na shida zingine.
BABA katika jina la YESU kwa nguvu na mamlaka
uliyonipa kufungua wana wako dunia nzima Bara lolote, mahali popote, mtu yeyote
anayesikiliza rangi yeyote maana ni rangi zako, wewe sio MUNGU wa ubaguzi,
maskini kwa matajiri wote BABA!! Ninatuma Malaika wakufungue na wale wanao ng’ang’ania
uchawi yawatese hayo mauchawi mpaka wakurudie, katika jina la YESU KRISTO WA
NAZARETI yule ambaye anajikonect na nguvu uliyonipa ili akatumie kwenda kuiba fedha
na kuchangisha watu hakika na kwambia haitakuwa wala haifanikiwi
BWANA YESU ASIFIWE…..
Ninabomoa nateketeza, nyota zenu mrudishiwe mapepo
ngome zote za shetani, malaika wa shetani lucifa kwenye anga la kwanza la pili,
Baharini angani, kaskazini mashariki dunia nzima mfee wote, mikutano yote ya
kipepo ninaharibu wala msiende katika jina la YESU KRISTO WA NAZARETI, msiende
mahali popote alipo shetani kwa nguvu na mamlaka ya Jina la YESU Asante MUNGU
wa IBRAHIM, Asante MUNGU wa ISAKA. Sifa na Utukufu na kurudishia wewe MUNGU
akubariki MUNGU akuinue MUNGU akutengeneze, mrudie yeye akushike mkono. MUNGU
wa IBRAHIM, MUNGU wa ISAKA.
Akulinde
akuongoze, jina la BWANA litembee na wewe, Malaika watembee na wewe, katika
Jina la YESU. AMEN!
NABII HEBRON.