ALIYEKUWA
KIONGOZI MKUU WA ILLUMINATI KUZIMU NA DUNIANI AKAMATWA NA YESU WA NAZARETI.
BWANA YESU WA NAZARETI ASIFIWE, Tarehe hii ya leo 14.12.2014
nimeamua kuujulisha ulimwengu wote msiogope tena sababu YESU WA NAZARETI
aliyeniita mimi Nabii Hebron kuipindua ulimwengu tokea 2010 nikifanya kazi hiyo
na tarehe 2.6.2014 nilienda na YESU na serikali yake mbinguni mpaka kuzimu na
kumtoa kiongozi mkuu wa chama cha illuminati ambaye yeye ndiye aliyepewa uwezo
na mamlaka ya kuupindua ulimwengu ili umuasi MUNGU na lusifa atukuzwe, ilikuwa
ni vita vikubwa sana. Joka kuu alimteka Maxwell akiwa na jini Sandra la kike
siku ambayo wazazi wake waliitunga mimba pasipo hata wazazi wake kujua, mtoto
akazaliwa duniani jini halafu yeye binadamu wa asili wakamchukua, wakamfundisha
mambo mengi hata ikafika muda joka kuu akamchagua ndiye kiongozi namba tatu
katika ufalme wake akampa siri zote na mafaili yote na utawala wa ulimwengu
wote na nguvu zake ambazo sasa nimeziteketeza, na sasa yupo katika kanisa la
YESU NI BWANA NA MWOKOZI WA MATAIFA YOTE, ameokoka anamtukuza YESU WA NAZARETI.
Aliponiita YESU nikaukomboe ulimwengu na niupindue ufalme wa
shetani sikuelewa muda ule ila siku nilivyoendelea kuifanya kazi yake na yeye
ndivyo alivyoniongoza na kunifunulia mengi. Huyu Maxwell (Isaya) yeye ndiye
aliyewaongoza Illuminati watu wote waliopo katika ulimwengu huu, wakiwemo wahubiri,
viongozi mbali mbali wa nchi, dini, miziki, mabenki na kila utajiri wa shetani.
Na hata sasa hawa illuminati member hawana amani sababu tegemeo lao halipo tena
na lengo la kuibadilisha dunia iwe (new world order) haitawezekana tena. Yaani waliifanya
dunia yote imtukuze shetani badala ya
kumtuuza MUNGU kwa kupitia miziki, uchawi, wahubiri wa uongo, na hata
sasa ukiangalia katika google search; illuminati pastors, bishops, preachers,
utawaona na ndiyo wahubiri wakubwa katika ulimwengu huu.
Sasa injili wanayoihubiri muelewe ni mpinga kristo na kazi
yao ni kuwamiliki wanadamu wamgeuke MUNGU na wamtukuze shetani, hiyo ndiyo kazi
yake, ila sasa mwisho umefika nawatangazia katika jina la YESU WA NAZARETI
aliye hai na ambaye alikufa akafufuka na baada ya kusalitiwa na watumishi
wakamgeukia lusifa ndio dunia ikaingizwa katika mkumbo huu, hivyo unapowaona
watu wa jinsi hii uelewe ni shetani ameivaa hiyo miili yao na ni nusu mtu na ni
jini iwe ni yeyote yule ni wakati wa kupona sasa wala siwaogopi kabisa, hao ni
maadui wa MUNGU, na huyu Mazwell nahodha wake wa meli ni father chritmas ambaye
watu huwaweka katika nyumba zao na makanisani na zaidi hata kimwili wewe fuatilia utaona katika
mambo zao ipo picha ya father Christmas pia, sasa imetokea wapi? Uelewe na wewe
unapokuwa na huyo mdoli au katika kadi au nguo zake ujijue unaunganika na illuminati kuupindua ufalme wa
MUNGU na umbaji wa MUNGU katika ulimwengu wa roho.
Maxwell huyu lazima ujiulize kuzimu YESU alimtoa, na
akanituma na mimi pia, ni sababu bila yeye kutolewa shetani angeendelea
kutawala dunia sababu konection yake bado ilikuwepo ambaye ndiye Maxwell, na
sasa msishangae mkiona wanaporomoka au uchumi za nci ambazo zilitegemea pesa za
illuminati na mabenki yataporomoka sababu aliyetumika kuwasaidia na kuwapa pesa
sasa hayupo tena na wanajua kabisa. Utukufu wa kanisa la mwisho sasa umetimia
hata malango ya kuzimu hayawezi. Illuminati ni chama kikubwa kuliko vyote
ambavyo vipo katika ulimwengu huu ikifuatwa na freemason, hawa illuminati ni
wakubwa kiutajiri sana na ni maarufu sana, ila freemason wao hawana kiwango cha
utajiri au umaarufu mkubwa katika kila bara wapo marais wengi ambao hivyo vyeo
wamepewa na illuminati vya kuongoza nchi zao. Sasa ikiwa ni hivyo ingia katika
mtandao utajua nchi yako, rais wako, au ufalme au umalkia alipataje hicho cheo
na kama utakuta basi uelewe nchi inaongozwa na shetani na ufalme wake.
Mimi nawajua wote ila nakufunulia wewe mwana wa MUNGU
ufunguke uelewe jinsi dunia ilivyopinduliwa badala nchi ziongezwe na viongozi
walioteuliwa na MUNGU zinaongozwa na viongozi walioteuliwa na shetani. Swali kiongozi
akiwa wa shetani na nchi itakuwa chini ya nani?
Ukija kwenye wanamziki maarufu tena wanajiita hata kimwili
wao ni wanachama wa illuminati, inakupasa ukae mbali sababu ukicheza hata
miziki yake ujijue unamsifu shetani na weewe unaunganishwa katika ufalme wa
shetani pasipo kujua au kwa kujua, zaidi soma vitabu vya Nabii Hebron matoleo
yote na blog utaelewa zaidi, na pia sikiliza katika YouTube pitia www.prophethebron.org. Ulimwengu
ulitekwa na shetani, sasa YESU anarudi atautumia mwili wangu mpaka atakapokuja
kuukomboa ulimwengu na watoto wake na kuwaangamiza mapepo na wafuasi wa shetani
wote, walioshiriki kuwaangamiza wanadamu na kuwafanya ndio chakula chao cha
kuzimu. YESU ni mzuri na anatisha na hakuna kama yeye katika uliwmengu huu. Sasa
kazi imeanza na hao waliomsaliti wakajiingiza katika hivyo vyama wakaangamiza
watoto wa MUNGU hao wataonana na yeye.
Nawaeleza ukweli hamna njia tena huu ndiyo mwisho, na dunia
itayashuhudia hayo na viumbe vyote. Mnatumia
jina la YESU kufanyia biashara, uchawi, kubadilisha biblia, na wengine kujiita
ni MUNGU wa majeshi, mara YESU, wote hao ni waongo. Enyi watu wa mataifa 85% ya
makanisa yote asili yake yalianzishwa na mpinga kristo na yanastawi kila nchi,
ikabakia 15% ya YESU katika hii 15% bado 13% ikamgeukia shetani ikabakia 2%
mpaka aliponiita YESU ndiyo ipo na yeye all over the world. Angekuja YESU
angepata watu ila shetani angevuna wengi na akawatumia wanaojiita manabii,
mitume, waalimu, wachungaji, wainjilisti wakubwa na wadogo. Uwe makini, watu
wamechoka na makanisa sababu ya matendo ya uovu na kunyang’anywa mali zao.
Sasa ufunguke, useme BWANA YESU naomba unisamehe dhambi
zanngu. Uniokoe unitoe katika ufalme wa shetani uniandike katika kitabu chake
cha uzima wa milele. Shetani sikutaki na vitu vyako, YESU uniongoze katika
sehemu ambapo yupo mtumishi wako ambaye hajakuasi wewe na upo unaishi ndani
yake nisipotee tena. Amen.
NOTE:
Ili kuwaelewa kimwili hawa illuminati:
1.
Search kwa google sign zao, mavazi yao, kama ni
wafanya biashara search kama ni maaskofu, wachungaji na mengineo kwa vyeo vyao
na hata kwa majina yao. Kwa kiasi kikubwa majina yao yanaonekana na hao wadogo
yapo katika group la freemason na wengine ni wachawi.
2.
Huku duniani chama hiki cha illuminati
kilianzishwa na myahudi aliyeitwa kwa jina la Adamu Weishaupt 1.5.1776, na
alikuwa ni kiongozi wa kanisa, na lawyer na pia alikuwa anajifunza kuhusu elimu
ya majini, alijifunzia Misri na lengo lake ni kuifanya (New World Order).
NABII HEBRON.