Pages

Tuesday, December 16, 2014

JE UNAJUA KAZI YA FATHER CHRISTMAS KUZIMU?

Kama nilivyokuisha elezea katika makala za Nabii Hebron kuhusu father Christmas au Santa Claus, kuwa baada ya Santa Claus au Saint Nicholas kufa yeye hakuenda mbinguni yupo kuzimu na kuzimu anazo kazi alizopewa ikiwemo ni kueneza injili ya mpinga kristo pamoja na kuitawala ile siku ya Christmas watu waacha kumrudishia MUNGU utukufu mbinguni, wabakie na midoli ya mizimu ya Saint Nicholas na kuwafanya mataifa wawe maadui wa YESU kwa kushiriki kumuita yeye ndiye father Christmas, wakati hakuna anayestahili kuitwa father Christmas katika ulimwengu huu. Hapa jiulize tu, je huyu mdoli unayempamba na kumuita yeye ni father Christmas, je huo mdoli ndiye ahadi ya MUNGU kwa wanadamu? Au yeye huyo father Christmas yeye ndio mkombozi wa ulimwengu? Na kama siyo yeye, je umeshaona wapi mkombozi wa mahali popote haongei, hapumui, hali chakula, amening’inizwa kama maiti? Mpaka hapo enyi mataifa sasa mnapata picha kuwa mlidanganyika na kuingia katika kushiriki sanamu au ibada ya sanamu.

Unapoliweka ndani ya nyumba yako tu uelewe kwako panakuwa ni madhabahu ya masanamu, iwe ni kanisani, hotelini au popote pale, japo najua wengi hamuelewi na wengine hata wananishang’aa nasema nini. Huo ndio ukweli, amenituma YESU niwaeleze ukweli mataifa yote mpate kupona, mtakaosikia mtapona na hasira ya MUNGU, mtakao kaza shingo ile dhambi ya kuabudu sanamu ujue unaishiriki na wewe. Leo utubu na uepuke, usije ukawa adui wa MUNGU kama siku za nyuma, haya yangejulikana mara tu shetani alipo yabuni ila YESU aliniambia kila alipowanyanyua watumishi walikuwa wanafika mahali wanamsaliti na kumfuata shetani. Sasa amenituma kwa mataifa yote najua wengi hamjui na wewe watumie wengine ujumbe huu ili wapone. Hakuna ushirika wowote kati ya father Christmas na MUNGU bali upo ushirika na malango ya shetani kati ya father Christmas na shetani ili awateke wanadamu ambao ni watoto wa MUNGU. Na sasa haitawezekana katika jina la YESU WA NAZARETI, kwa wale ambao watatii maneno haya ambayo siyo yangu mimi Hebron mimi ni chombo tu cha kupeleka ujumbe wa MUNGU.

Kazi nyingine anaifanya father Christmas kule kuzimu ipo meli kubwa sana ambayo ukubwa wake ni kama 1,300,000 square kilomita. Meli hii inaendeshwa na nahodha anaitwa father Christmas ambaye ndiye mzimu wa Saint Nicholas, meli hii ilikuwa inapandwa na mtu mmoja tu ambaye alikuwa ni msaidizi wa joka kuu namba tatu katika ufalme wa shetani ambaye ni mwanadamu anaitwa Maxwell, kwa sasa anaitwa Isaya yupo katika kanisa la YESU NI BWANA NA MWOKOZI WA MATAIFA YOTE, nimemrudisha duniani kama alivyoniamuru YESU na kuubomoa ufalme wa shetani na serikali yake na bado naendelea na kazi hiyo sababu siyo siri wala sitaacha kumpiga joka kuu milele, aliwatesa watoto wa MUNGU na mataifa yote. Meli hiyo kazi yake ilikuwa kusurvey kazi za mpinga kristo na kuwaletea nguvu za kipepo ili makanisa ya uongo yashamiri kama ilivyo sasa 98% ya makanisa yote katika ulimwengu wote waliyaanza na mengine yameanzishwa na kuzimu kabisa 85% hayajaanzishwa na YESU hata kama wanalitaja jina la YESU, ni ya mpinga kristo hii asilimia 15% ni ya YESU katika hii 15% ya YESU 13% wamejiunga tena na shetani wakamsaliti YESU ikabakia 2% ulimwengu wote, ndiyo iliyobakia na YESU wa kweli.

Ni ajabu na inatisha nilipoangalia nchi mbali mbali nikiwa  na malaika Gabriel katika makanisa nchi nyingi sana hazikuwa ni kanisa la MUNGU wa kweli hata moja na katika nchi nyingine unakuta ni kimoja na bado limefifia hakuna nguvu za YESU, na sehemu nyingi makanisa yanaonekana ni giza tupu. Nikamuona na Maria Magdalena na yeye yule ambaye alikuwa na YESU alipokuwa hapa ulimwenguni. Yaani anampenda YESU sana na anampenda MUNGU sana, ukisoma katika habari zake ndivyo alivyo hata sasa katika bidii yake na MUNGU. Akaniambia, Hebron mwanangu ifanye kazi ya MUNGU kama ilivyo sasa. Sasa tunafurahi mbinguni sababu ilifika mahali hata Malaika walishindwa kuja katika makanisa sababu yamechafuka ila sasa malaika wanapanda na kushuka katika kanisa lako na tunashirikiana katika ibada zote na wewe, akanishika mkono na kunieleza hayo, na mengine ambayo ni yangu peke yake kwa ajili ya utukufu wa MUNGU.

Meli hii ndiyo iliyosmabaza roho za kuzimu kwa ulimwengu wote na aliyetumika ni mwanadamu aliyetekwa na shetani aliyeitwa Maxwell aliendeshwa na nahodha father Christmas, na meli hiyo ilikuwa na rangi saba na kila moja ilikuwa ina maana yake. Soma katika makala ya kadi ya Krismasi nimezielezea, ni kusambaza uharibifu. Meli niliilipua nikiwa na Malaika Mikaeli na ilipokuwa inakuja duniani walikuwa na wenyeji wao ambao mmoja ni nabii maarufu kutoka Afrika Magharibi na wengine wawili ni marais wastaafu katika moja ya bara la magharibi, na kupitia hao watu wote walipewa nguvu za kipepo, pamoja na nguvu za vyama vya illuminati na freemason, ila sasa njia hizo alinituma YESU nimezibomoa. Sasa ni wakati wa YESU WA NAZARETI kutawala ulimwengu wote, na MUNGU anawataka watoto wake ikiwemo na wewe umrejee.

Sema BWANA YESU naomba unisamehe dhambi zangu zote. Siabudu sanamu tena wala kupamba father Christmas, nisamehe sikujua au nilikua, uniandike jina langu katika kitabu chako cha uzima wa milele. Amen.

Zaidi ingia katika website ya www.prophethebron.org usome yapo mengi yatakufungua na hautadanganyika tena na shetani wala watumishi wa uongo na wanyang’anyi wa mali za watoto wa MUNGU. KARIBU Arusha, Tanzania katika kanisa la YESU NI BWANA NA MWOKOZI WA MATAIFA YOTE, utaombewa na kufunguliwa na utamjua YESU wa kweli. Ubarikiwe!


NABII HEBRON.