Pages

Wednesday, December 10, 2014

NINI MAANA YA BOXING DAY 26.12 KILA MWAKA!

Boxing day tafsiri yake kwa Kiswahili ni siku ya wapiganaji yaani watu wanaopigana, na pia ina maana kwa Kiswahili ni siku ya wabeba maboksi. Ila hapa watoto wa MUNGU ninaelezea katika ile siku ya 26.12 kila mwaka ambayo inaitwa boxing day eti wanaiita ndiyo siku ya kupewa zawadi za Krismasi. Mimi nawaeleza jamani ulimwengu ulishatekwa na shetani na wanadamu hawaelewi hata maana ya boxing day kuwa ni siku ya wagombanaji au wapiganaji, au wanabeba maboksi, lakini wao wameiita ni siku ya kupeana zawadi za maboksi ya Krismasi. Watoto wa MUNGU nataka muelewe YESU hachezewi na hastaili kuchezewa hata kidogo.

YESU alipozaliwa wale mamajusi walivyokwenda kumuona siku hiyo hiyo waliongozwa na nyota na walifika siku hiyo hiyo na siyo siku ya pili, walimpelekea zawadi wakaondoka. Sasa shetani akaja akaipindua ile siku ya Krismasi ndiyo siku ya kupeana zawadi, akawakamata fahamu miaka mingi akashirikiana na watumishi waliomuasi YESU miaka mingi wakaipindua ile siku ya Krismasi ya kupeana zawadi maana ndivyo ilivyo stahili, shetani akaiita 26.12 ni boxing day. Sasa nimeshakuelezea maana ya boxing day kama unayo akili timamu utaelewa vizuri kabisa haya ninayokuelezea. Na wanadamu walipoikubali na ikapitishwa hata katika kalenda ikajulikana rasmi na watu wakaitii. Sasa shetani anachokifanya ile siku ya boxing day anakuja kupanda magomvi katika mioyo ya kila mtu ambaye atampa mtu zawadi na kumuambia happy boxing day.

Jambo lingine inaitwa boxing day sababu siku hiyo ni siku ambayo kuzimu inakuja kuiba kila kitu cha mtu ambaye atatoa zawadi kwa mtu na kuziita boxing day, kinachofanyika hapo wewe mwanadamu utanyang’anywa kila kitu katika ulimwengu wa roho ambavyo ulibarikiwa navyo katika siku ya Krismasi katika ulimwengu wa roho na utabakia boksi tupu ndiyo maana inaitwa boxing day siku hiyo. Hivyo YESU alivyonijulisha hayo anataka baraka zenu zisiibiwe tena na kufilisiwa na shetani katika siku hiyo. Usishiriki ili usinyang’anywe vitu vyako ubakie boksi. Boxing day ni siku ya shetani na serikali yake kuja kuiba vitu vya watu katika ulimwengu wa roho, na ili usiibiwe ukitoa zawadi hata siku moja zawadi yako usiitoe boxind day, hata leo hii ukisema hivyo unaibiwa baraka zako katika ulimwengu wa roho. Haya tungeyajua miaka mingi sana ila YESU WA NAZARETI alikosa wa kumfunulia haya na kuwaeleza watu wote wa mataifa ili wapone. Na wewe uwatumie na wengine katika nchi zao na YESU atakubariki, na shetani hiyo siku anayowaibiaga watu vitu ateketee na ashindwe katika jina la YESU WA NAZARETI. Na mimi Nabii Hebron nawatakia mpeane zawadi na msiite tena ni siku ya boxing day mkafilisiwa na shetani. Ukweli uwaweke huru na mkae katika utakatifu siku zote ili akija YESU akupate.


NABII HEBRON.