Pages

Wednesday, December 10, 2014

JINSI YESU ALIVYOJARIBIWA NA SHETANI JANGWANI, IMETOKEA NA KUTIMIA KWA NABII HEBRON KUJARIBIWA NA JOKA KUU.

BWANA YESU WA NAZARETI ASIFIWE. Katika tendo la kukubali kumtumikia YESU na kuifanya kazi yake kwa ajili ya kuukomboa ulimwengu na kumuandalia watoto wake ili atakapokuja anawachukua wale tu ambao watakubali na kuyatii yale aliyonieleza na wayafuate kama serikali ya mbinguni ilivyopanga. Sikutegemea katika maisha yangu, nije nikawa mtumishi na sikujua hata kama MUNGU ameniwazia jambo hili ile baadaye aliniambia nilikuumba kwa ajili ya kazi rasmi ya kuukomboa ulimwengu na kuikamilisha kazi yangu ila nilikuficha adui asikujue kuwa wewe ni nani kama vile nilivyomficha Musa mpaka wakati wa kumtumia ulipofika nikamtumia na wewe Hebron ilikuwa ni hivyo hivyo mpaka wakati ulipofika nimeanza kukutumia mimi mwenyewe nakuongoza na kukupa maelekezo ya safari ya nchi ya Ahadi katika roho ili kuwaongoza sababu mimi MUNGU ninayeijua njia ya kuja kwangu na hakuna aijuaye.

Mwanadamu yeyote asiyekusikiliza atapotea na kuangamia. Hata kipindi cha Musa wale wana wa Israeli ambao hawakumsikiliza Musa waliangamia jangwani na ndivyo ilivyo kwako. Niliogopa na kushtuka sababu sikuzoeaga kusikia maneno mazito kama haya. Akanifundisha mengi na kumuangamiza joka kuu na mengine ni yangu kama mimi. Akanikabidhi kwa malaika mkuu Mikaeli na Malaika Gabriel na hata Musa ambaye aliwaongoza wana wa Israeli na Eliya, Baba wa mataifa Ibrahimu, wazee 24 wote nimewaona na kuongea nao, sababu MUNGU anapenda. Jamani hapa ulimwenguni ni pabaya, mbinguni ni pazuri sana hapaelezeki ila jitahidi uokoke na uishi maisha matakatifu siku zote, siku moja ya mwisho utafika.

Nawashangaa wanadamu wanaipenda dunia ni sababu hawajui waendako, mimi napajua nawaeleza. Sasa naelezea yaliyonikuta 9.12.2014 kwa mara ya kwanza nilikutana na joka kuu kama vile YESU alivyokutana naye jangwani akamjaribu YESU.
Mathayo 4:7-9
7 YESU akamwambia, tena imeandikwa, usimjaribu BWANA MUNGU wako. 8 kisha ibilisi akamchukua mpaka mlima mrefu mno, akamwonyesha milki zote za ulimwengu, na fahari yake, 9 akamwambia, haya yote nitakupa, ukianguka kunisujudia.”

Na mimi Joka Kuu akaniambia umenitesa sana na kila siku unaharibu ufalme wangu na kunipiga basi sasa Hebron ninaomba uwe rafiki yangu tushirikiane na mimi na nitaamuru kaskazini na kusini ilete vyote na nitaamuru vyote nilivyonavyo nikupe wewe sasa hivi. Nilimuangalia joka kuu, nikamuambia rudia unachosema, akasema hivyo hivyo. Nilimjibu mali zako sitaki, kwanza hauna chochote, mimi ninavyo vya BABA yangu wa mbinguni, akanisihi tena nikamchapa kofi, akaniambia hata miguu yako iwe rafiki yangu, nikamkemea, sina uhusiano na shetani, akalia kwa uchungu joka kuu baada ya mimi kumjibu na kumkatalia ahadi zake, baada ghafla akatoweka. Nikabakia nimeshikwa na mshangao hii ni nini? Kwa nini aje aniambie maneno hayo, nikakumbuka na YESU alivyokuwa jangwani baada ya shetani kushindwa kwa njia zote sasa akamfuatia jangwani na bado YESU alimshinda, na kusudi la MUNGU lilitimia tu, nikapata tafsiri, nikapata tafsiri alivyoniletea YESU muda huo akaniambia na wewe ameshakufuatilia kwa njia zote alikushindwa, sababu upo na mimi na akakujaribu kama alivyonijaribu mimi na wewe ulisimama imara, umeshinda vile vile na hii ni dalili umeshinda na ndio sababu Amelia. Na wengine niliowaita walikataa kunisikiliza wakampa joka kuu masikio yao badala ya kunipa mimi YESU hivyo akawateka. Mimi YESU nilimsikiliza BABA yangu siku zote na ndio sababu hakuniweza na wewe unanisikiliza mimi tu na ndiyo sababu hatakuweza.

Watoto wa MUNGU shikeni sana ninayowafundisha sababu unapoyasikia hata jaribu liweje likija utakuwa unalo neno la kusema au njia ya kushinda. Katika maisha yangu nimejaribiwa mengi ila hili la kuambiwa uwe rafiki yangu nitakupa vitu vyote vya dunia hii. Nikuulize swali je ungepona au ungeangamia na muda huo huo ilikuwa itimie vyote upewe na joka kuu, je ungeshinda? Namshukuru MUNGU sana kwa kuniwezesha na kuniimarisha nikamjua yeye ni nani na kutokuangalia vitu kama YESU alivyoangalia vya MUNGU tu na mimi imewezekana.

Tamaa ni mbaya watumishi wametekwa hapo, idadi kubwa sana ya wale aliowaita YESU, tazama hata Yuda aliangalia vitu akatekwa na shetani na wasihi msitamani vya shetani, mbinguni vipo vingi kwa ajili yako, hivi ni vya muda mchache tu na ni shida na utaingia jehanamu na yeye. Makanisa yanapenda misaada hayajui misaada inatoka wapi. Wengi walipopokea misaada na mashirika mbali mbali yakajiingiza katika kanisa wao wakafikiri ni upendo wa KIMUNGU kumbe ni joka kuu  anawaletea pesa na miradi na walipoipokea tu tayari anawakamata sababu si wamepokea vyake, wengi mmepokea pasipo kujua na wengine wanajua. Zaidi soma makala yangu na website www.prophethebron.org.

Sema BWANA YESU naomba unisamehe dhambi zangu, uniandike jina langu katika kitabu chako cha uzima wa milele. Unishike mkono nisipotee tena. Amen.


NABII HEBRON.