Pages

Wednesday, December 10, 2014

MAANA YA YESU NI BWANA NA MWOKOZI WA MATAIFA YOTE!

Kila mwanadamu na watoto wa MUNGU nawasalimu kwa jina la YESU NI BWANA NA MWOKOZI WA MATAIFA YOTE. Neno hili siyo ligeni katika masikio ya watu katika ulimwengu wote. Aliponiita YESU aliniambia nimekuita ukaniandalie kanisa langu ambalo nikija nitakuja katika kanisa hilo katika ule mwisho yaani unyakuo. Hebron kanisa uliite hivi YESU NI BWANA NA MWOKOZI WA MATAIFA YOTE, na mimi nilifanya hivyo hivyo na imetokea sasa ninalo kanisa linaloitwa kwa jina hilo hilo. Kwa nini limeitwa hivyo na YESU peke yake? Ni sababu ni kanisa ambalo litaponya mataifa yote kupitia madhabahu hii ya YESU NI BWANA NA MWOKOZI WA MATAIFA YOTE na kuwapeleka mbinguni, hivyo siyo kwa ajili ya hapa Tanzania tu hapana, ni katika kila nchi MUNGU atawaokoa watu wake, atafanya yeye ajuavyo wala hakuna litakacho weza kuzuia kusudi la MUNGU.

Nilivyoanza huduma watu walinichukia, walinitukana, waliniona nimechanganyikiwa, nimepoteza mwelekeo, lakini mimi nilijua kusudi la MUNGU lazima litimie na matunda yanaonekana na itakuwa katika ulimwengu wote. Imeandikwa YESU atakuja kulichukua kanisa lake, ina maana litakuwa ni moja siyo mengi kama ilivyo, sababu 98% ni makanisa ya uongo, yalishatekwa na shetani, watumishi wamemsaliti YESU, wanatumia jina lake kutafuta pesa, kunyang’anya watu mali na kufanyia mambo mengine maovu na kufanya shetani atawale kwa kiwango kikubwa na kumfanya YESU awe na watu wachache, ikiwemo hata mtu yeyote anayejiita yeye ni mkristo lakini hajaokoka, ajijue yeye ni mkristo wa uongo. Sababu YESU alikuwa ameokoka na haina maana ukajidanganye wewe ni mkristo halafu haujaokoka. Ili uwe mkristo ni lazima uokoke kama yeye. Makanisa mengi yanajiita ni ya kikristo sehemu mbali mbali katika ulimwengu huu, hawajaokoka na wala hawana kitu kinaitwa wokovu.

Sasa kama hamna wokovu basi uelewe ni feki (ukristo wa uongo) ndio unaitwa hivyo sababu haujakamilika. Ila sasa uokoke ili uwe mkristo na uachane na ukristo wa uongo ili YESU awe BWANA NA MWOKOZI wako na nyie wote katika mataifa yote. Na zaidi YESU atawakusanya wale wote watakaomkubali katika madhabahu yake na atawapeleka mbinguni, sababu ndivyo ilivyo pangwa na MUNGU, hata biblia haijasema makanisa ya mwisho yatakuwa na nguvu za kushinda kuzimu, bali neno linasema ni kanisa la mwisho milango ya kuzimu haitaliweza. Sasa hapa uelewe, YESU atawakusanya mataifa yote hata sasa ameanza awakomboe yeye mwenyewe na awatoe kwa shetani. Alinituma kuibomoa kuzimu, nimemfunga joka kuu na msaidizi wake wa tatu katika ufalme wake alikuwa ni mwanadamu aliyeitwa Maxwell nimemtoa, sasa hivi yupo katika kanisa la YESU NI BWANA NA MWOKOZI WA MATAIFA YOTE anamfurahia YESU.

Zaidi visit YouTube ya Prophet Hebron na blog utapata na maelezo ya jinsi nilivyoitikisa kuzimu pia soma na vitabu. YESU NI BWANA NA MWOKOZI WA MATAIFA YOTE, ninamshukuru alivyonieleza Hebron muda wangu wa kurudi umeshafika wakati wowote, jiandae na uandae mataifa, na nyie mliopo mbali mnaposoma na kutubu huko huko unaongozwa katika kanisa la YESU NI BWANA NA MWOKOZI WA MATAIFA YOTE unawekwa na malaika katika listi ya waliomrudia MUNGU.

Sema BWANA YESU naomba unisamehe dhambi zangu, uniandike katika kitabu chako cha uzima wa milele. Uniongoze nisipotee nipo kwako sasa mimi ni mali yako YESU. Amen.

Zaidi karibu Tanzania katika kanisa lake YESU NI BWANA NA MWOKOZI WA MATAIFA  YOTE ili uwe moja wapo wa kondoo wa kanisa la mwisho. Ubarikiwe!


NABII HEBRON.