Pages

Saturday, December 6, 2014

MAELEZO YA YOUTUBE: UJUMBE WA KILA  MTU KWA ULIMWENGU WOTE.

Ndugu msomaji nakusalimu katika jina la YESU KRISTO WA NAZARETI, mwokozi wa mataifa yote ninakuletea ujumbe ambao YESU ameniambia niupeleke katika ulimwengu mzima. Japo nitasema kidogo tu. Aliponitoa katika kazi yangu nilikuwa nikiifanya ya utalii aliniambia kwamba waambie wanadamu wote wamrudie yeye YESU mambo yameshaharibika. Sasa hivi watumishi wamekuwa wachawi, kazi aliyowatuma wameikataa na watu wengi wanaangamia na yeye YESU anawapenda na sio kwamba hawapendi, tatizo ni watumishi wamemkataa, wengi wamekuwa wachawi wameingia freemason 98% ya watumishi wote katika ulimwengu mzima sio wa kwake wala hawapo na yeye wameshakuachana naye kwa sababu aliwaonya wamekataa.


BWANA YESU ASIFIWE!!

Akaniambia mambo mengi sana lakini nitakuambia kiasi mengine utaingia katika website www.prophethebron.org. Utaingia kwenye blog utasoma vitabu vyote vile, ni YESU ameniagiza niueleze ulimwengu mzima. Amenituma niukomboe ulimwengu mzima na watu wote wamjue yeye na kazi hii ataifanya yeye na hakuna atayezuia maana kanisa sasa hivi limetekwa na shetani, kweli haipo.
Kazi yake yaani kwa jina lake kazi yake kanisa limekuwa ni mahali pa kukusanyia pesa tu, watumishi ni waongo, wamekuwa ni wazinzi, wamekuwa niwauza madawa ya kulevya. Akaniambia, “Hebron” mtumishi akiuza madawa ya kulevya, ina maana ni mimi ninatukanwa na kila mtumishi ambaye  MUNGU anamtumia ina maana YESU yupo ndani yake. Sasa kama anauza madawa ya kulevya huyo sio mtumishi wake .


Ameniambia niwaambie watu wote, mbatizwe ubatizo wa maji mengi aliobatizwa yeye. Huo ubatizo mwingine  sio wa kwake kabisa, na kila ambaye amebatizwa ubatizo mwingine tofauti na huo hataenda mbinguni na hata hao wanaobatiza sio watumishi wake. Maana yeye hakuwafundisha wanafunzi wake hayo, hata kitabu cha Biblia haupo. Kwa hiyo mnapoteza muda na ninawaeleza wazi, iwe ni askofu, iwe ni mchungaji, iwe una cheo gani chochote,  kama umebatizwa na maji hayo wewe sio mkristo kwa sababu Kristo hakubatizwa hivyo na tafuta katika biblia imeandikwa , “Ole wake aongezaye maneno ya kitabu cha unabii huu”.  Sasa  haya yanatokea wapi? Mnamuabudu MUNGU msiye mjua. MUNGU mnatakiwa mumfuate kwenye biblia. BWANA YESU ASIFIWE!!


Nataka nieleze pia kuhusu ubarikio, wote wanaobarikiwa wakiwa watu wazima sio mpango wake, tafuta kwenye biblia ambayo ndiyo katiba yake, sasa mnafanya kazi gani, hii ni kazi ya matakataka isiyo na mbele kabisa wala  MUNGU hapendezwi nao. Na watu mnatakiwa muelewe msikilize, haya ni mapokeo yaliyoletwa kutoka Ulaya baada ya wale watumishi waliomkataa MUNGU, wakabadilisha wakiingiliwa na shetani kwa hiyo sasa hiyo ni kazi ya mpinga kristo. Imeandikwa msiabudu sanamu. Lakini kanisani mnamtaja YESU halafu bado mnashika masanamu. Je! Ndugu wasomaji YESU anashirikiana na sanamu? Jibu ni hapana! Sasa njia ielewe , hawa wamekwisha kupotea na mimi nakuambia ukweli na nitaendelea kusema kweli na kufichua kila uovu, maana yeye ndiye yupo ndani yangu wala sio  ukaniona ni Hebron, mimi nilikuwa sijui kusoma biblia, amenitoa kwenye kazi ya kuendesha  watalii niliyokuwa nafanya Serengeti kama nilivyo  akanibadilisha na ndiyo nakueleza ujumbe, maana wamemkataa amewaonya wamekuwa freemason, wachawi kupindukia. 

BWANA YESU asifiwe! Katika Afrika watumishi wameoza. Msitishwe na habari sijui nabii nani hakuna! Wameamua jina hilo wanafanya uchawi, nchi zimeharibika, wananchi wameharibika kwa sababu manabii  ni watapeli, manabii ni waongo, manabii wapo kwa pesa tuu, hao ni manabii wa MUNGU? Hao sio manabii wa MUNGU. Lakini YESU ameniambia mwisho wake umefika.  Kuzimu nimeshabomoa na wanaenda kuporomoka na watakamatwa, wala hakuna chochote ambacho kitakachosalia. YESU peke yake  ndiye  anawaadhibu na kazi hiyo imekwisha anza na ameanzia Tanzania, walizoea. Imeanza Tanzania na hakuna atakayeweza kunistopisha,  MUNGU hastopishwi, ajaribu! “Ataondoka”.


Mambo mengine aliyoniambia YESU ni wizi wa sadaka. Sadaka ya kweli ni fungu la kumi na shukurani, hizo za ujenzi nyingine zote ni za uongo, na pia ameniambia niwaambie ya kuwa yeye siyo omba omba,  MUNGU yeye ni tajiri hao wanao omba omba, hao wote hajawita. Maana kama mtumishi ameitwa , anamwandalia njia usidanganyike na habari ya jina la YESU, jina langu watu wanalitumia vibaya kwa sababu wanajua jina langu lina thamani ndiyo wanatafutia pesa, na nyie mnahangaika , mkiteseka mkilia lakini hamna chochote, lakini mwisho umefika.
BWANA YESU asifiwe !!!


Jambo lingine aliloniambia kuna watu wengine wanajiita MUNGU wa majeshi, na wengine YESU, Embu nikuulize ndugu msomaji, wao walizaliwa na Maria? Wao walikufa na kufufuka? Akili kichwani. Nchii imeharibika sababu, ya hawa watumishi ambao wamemuasi MUNGU, kwa hiyo MUNGU anazidi kupiga nchi. Wamebaki kulaumu viongozi hawafanyi kazi, viongozi wanatenda vibaya, wao ndiyo source, waache kuwalaumu viongozi.
Lakini MUNGU ameshawanyanyua viongozi na Tanzania  ndio EDEN. BWANA YESU ASIFIWE !!


Jambo lingine aliloniambia,  nitazungumza kwa kifupi  ili nijaribu kuyapanga, maana mengine yote utayapata katika kitabu changu cha JINSI KANISA LILIVYOTEKWA NA SHETANI.


BWANA YESU ASIFIWE!! Jambo lingine aliloniambia, habari ya kuandika majina sadaka, yeye amesema utoapo kushoto wala kulia isijue sasa hawa watumishi wanaandika majina ya ujenzi ya matofali wanatoa hadi vyeti vya congratulation, na wengine wanawaambia watu waandike majina yao kwenye bahasha, email address, poastal address, street, hawa wote siyo watumishi hawa ndio wale wanyang’anyi YESU alisema watapitia mlango wa nyuma. Mlango wa nyuma ina maana, ni maneno inayotoka nje ya biblia ambayo ni hayo sasa, kwa hiyo hao ni wanyang’anyi. Je ! Biblia inasema hivyo?  Jibu sivyo amenituma niwaambie, watumishi sasa hivi wananyang’anya mpaka waumini wake zao. Sio watumishi wake hao, amenituma niwaeleze watumishi wa sasa hivi wanauza madawa ya kulevya, amenituma niwaeleze watumishi ukiingia katika mtandao wa freemason, majina yote unayoyakuta ni kweli, maana lazima atoe damu, lazima uvue nguo  uchi  uingie kwenye hicho chama cha freemason  ili jina lake liweze kuingia huko.
Kwa hiyo sasa? YESU anafanya kazi na freemason? ! Lazima ufunguke. Lakini njia zake sio njia zetu, yeye mwenyewe anajua anachokifanya. Na kazi hii ameshaianza na serikali ya Mbinguni. BWANA YESU ASIFIWE!  Hakuna cha dunia nzima, kila mahali pameharibika. 

BWANA YESU asifiwe!  Kumeoza msitishwe na miujiza, imekuwa ni mazingaumbwe MUNGU hajawaita, wanatafuta pesa tu. Hata wanao omba omba kwenye TV, siyo yeye amewaita maana kama amewaita ameniambia yeye, angetengeneza njia lakini   hiyo siyo njia wanawaibia pesa ni wizi, wanawaibia viongozi wa serikali ni wizi, mawaziri, watoto kila kitu. Ameniambia  ndiyo wanaoongoza kutoa  makafara  kuua watoto wa MUNGU. BWANA YESU ASIFIWE!


Ameniambia niwaeleze msidanganyike na kuimba kwa muda mrefu makanisani na kutembea na   hata kubeba misalaba, yeye hakai kwenye mbao, yeye yupo Mbinguni. Imeandikwa mwabudu MUNGU katika roho nyie mnakwenda wapi. Ameniambia niwaeleze, mtu akifa,  kama hajatengeneza maisha yake baasi. Mnadanganyika na hizi ibada za wafu ni uongo.


Amenituma niwaeleze ukweli, amenituma niwaeleze ya kuwa yeye anawapenda, mnaodanganyika msidanganyike tena hata unavyoisikia sauti hii unafunguliwa. Na uendelee zaidi kusoma vitabu katika website  www.prophethebron.org utazidi kufunguka, na shida yeyote inayonayokusumbua imeshindikana dunia nzima , wewe njo!  Maombi ni bure, unafunguliwa  bure, mmepewa bure  toa bure, hayo  mengine yote ni ya wizi. Akaniambia kwa sauti ya uchungu sana. Hebron, kwa nini wanatumia jina langu na hawanitaki? Akaniambia , midomoni mwao wana nitaja BWANA , BWANA, lakini ndani yao ni mbwa mwitu, ni walevi, akaniambia , mimi YESU sifanyi biashara, mimi YESU nimekwisha waeleza msichukue riba, sasa makanisa leo hii ndiyo yana mabenki. Mabenki ni kwa ajili ya waumini na serikali, ya Kaisari mpe ya Kaisari hayo hayanihusu mimi!! BWANA YESU ASIFIWE. Na mengineyo mengi utaendelea kufuatilia katika vipindi vyangu vya redio, makala na vitabu  utafunguka.


Mwezi uliopita  siku moja katika nchi ya Tanzania  katika watu wote walio kufa, watu kumi na nane tu ndio walikuwa wameenda paradiso na kuanzia mwaka 1949-12th December 2013  hakuna kiongozi yeyote  iwe mfalme iwe rais ambaye ameenda paradiso, ndugu wasikilizaji  kama  ni viongozi wanaombewa  ni marais lakini bado hawaendi. MUNGU yupo kwenye haki,  hukaa kwenye haki, tengeneza maisha yako. Mnadang’anywa na hao ni wapinga Kristo ninakueleza ukweli kama hutaki shauri yako. Hujui  leo upo au kesho kutwa mwisho umefika. BWANA YESU ASIFIWE!! 

Ila nakutia moyo, mtafute BWANA YESU wa kweli, maana makristo wa uongo  wamezidi ndio wamejaa  kila mahali 98% dunia nzima. Ni makristo wa uongo. Na kama wewe umeshiriki hayo mafunzo na wewe pia ni mkristo wa uongo, hata mimi nilibatizwa ubatizo wa maji ya kikombe ile ni chapa 666 lakini wewe huwezi kuijua kama ile ni chapa 666 inakuja katika  roho maana kila mtu angejua angekimbia, makanisa sasa hivi yamekuwa ni Makaini, yana  roho ya laana tuu, hayatendi vyema, yamekwenda kinyume. BWANA YESU ASIFIWE! Uokoke umkamate YESU katika roho na kweli. Hata makanisa ya wokovu yameoza!! Ya dini yameoza! YESU hakuleta dini, YESU hana dini, dini yake ni Wokovu.


Na MUNGU akaniambia Hebron, mimi nimeumba watu wote, mimi sijaanzisha dini, watu wote mimi ndiye nimewaumba ni wangu wanirudie mimi  kupitia mwanangu YESU KRISTO wa Nazareti ambaye ndiye njia ya uzima na kweli na hata ule mwisho utakapofika yeye ndiye atakayekuja. Dini nyingine wanamwita Nabii Issa, sasa kama wewe hujakuwa mwanachama wake unategemea nani akuchukue?


BWANA YESU ASIFIWE!, unataka kwenda mbinguni ingia kwenye chama cha YESU, okoka mshike yeye, siku akija atachukua wale walio wa kwake. Nimekueleza, yakae ndani yako. Lengo kubwa  alilonipa BWANA YESU katika kazi yake ni kuupindua ulimwengu utoke kwa shetani umrudie yeye. Na masomo aliyonifundisha na yale ninayokufundisha utayakuta katika vitabu vyangu na CD na katika KANISA LA YESU NI BWANA NA MWOKOZI WA MATAIFA YOTE. Na yeye peke yake ndiye anayenifundisha . Mimi sihitaji kufundishwa na wanadamu ameniambia wameoza. Kwa sababu yale aliyowatuma wayafanye hawafanyi, mafundisho  makubwa ni pesa , kuwaibia watu mali zao. Kwa hiyo, unataka kwenda Mbinguni soma vitabu vya Nabii Hebron, utafunguka yapo matoleo mengi sana. BWANA YESU ASIFIWE! 

Ila wewe usiogope maana anakupenda, lakini  ukubali kwenda na yeye, ukiwa kinyume bye bye. Lakini watu wengi wamekuwa siyo kinyume, kwa sababu hawaelewi, wamefundishwa  uongo kama wewe umefundishwa ubatizo wa kikombe ni ubatizo wa MUNGU wakati ni wa uongo tayari wewe umeshamwabudu mungu wa uongo!, kama wewe umebarikiwa ukiwa mtu mzima badala ya kubarikiwa kama YESU. YESU alikwisha onyesha njia, sasa una cha kujitetea? Na cha kujiuliza hawa watumishi wametoka wapi? Ni wa kweli au wa uongo? Kama wanafundisha masomo ya uongo basi ni wa uongo. Usitishwe na sauti eti mtu ananena, hata mapepo yananena. Hayo nakueleza kwa ujasiri kabisa, wala sihitaji nguvu za  mwanadamu wa aina yeyote. BABA YANGU WA MBINGUNI NDIYE ANAYENIFUNDISHA  peke yake. Na mimi namuadhimisha.  Nasema kweli na nitaenda dunia nzima kwa wakati wake na muda wake. Na Tanzania ndio EDENI na majibu yameanza. Na Mataifa yatakuja Tanzania kufuata injili ya kweli.


BWANA YESU ASIFIWE, ni uovu, uovu, uovu, imebakia sasa hivi ni kuwalaumu wadamu ambao siyo watumishi, wanamakosa, wanamakosa, chanzo ni watumishi wameoza. Mwalimu akishaoza atafundisha uozo na uozo utapokelewa, wengi wamejichanja miili yao haifai, wengi wamejiita, wamejifanya kuifanya kazi ya MUNGU wanatumia jina lake wakaweka na uchawi huko, watu waone mapepo wanalia ng’angaa. Wanaiba nyota, mikutano imefanyika mingi sana lakini wanaokwenda kule ni kuibiwa nyota tu.. ndiyo malengo yao. BWANA YESU asifiwe! Mwisho umefika, na kazi hiyo nimeshaianza. Dunia nzima nimebomoa japo nipo Tanzania. Na nitapenya kila mahali, kila mtu anayetaka kumuona MUNGU ni wakati wa haki yake. Haijalishi una cheo gani au nini NO!! kwa MUNGU hakuna, wote ni sawa. Na ndiyo ninamrepresent MUNGU wa kweli, mambo ya uongo uongo bye bye.. shetani hana chake tena!

Asante sana, karibu uendelee  katika kusoma  makala na vitabu vya kanisani kwangu Arusha Moshono.
Utahudumiwa bure, uponyaji ni hapo hapo. MUNGU AWAINUE, MUNGU AWAOKOE, Muijue nuru na nuru iwaweke wazi,uongo muujue na uwakimbie.

NABII HEBRON.