MAELEZO YA
YOUTUBE: Nabii Hebron amtaja Baba yake wa kiroho aliyemzaa na kumbariki ni Moses
Kulola.
MUNGU WA IBRAHIM, MUNGU WA ISAKA, MUNGU WA YAKOBO anawapenda
wote, anahitaji watu wamrudie. Kisa kikubwa cha yeye kuniita katika utumishi ni
kwa ajili kanisa limemuacha, imebakia ni pesa tu. Na nilipita katika mambo
mengi mpaka nimefika hapa kama nilipo, mpaka nikaweza kufanya kazi ya MUNGU,
lakini haya yote alikuja kunieleza MUNGU alikuwa kwamba ananipitisha,
alinificha kama Musa alivyomficha kwa Farao na mimi nilikaa kwa Farao, yaani
watumishi ambao hawakuwa baba zangu wa kiroho, lakini pasipo wao kujua. Walinipiga
sana, waliniumiza, walinikatisha tamaa lakini MUNGU alikuwa pamoja na mimi.
Na uzuri kila walilokuwa wanakifanya MUNGU alikuwa
ananijulisha na niliendelea kumtii. Lakini ilipofika 2009 mwezi wa nne,
aliniambia niondoke katika kanisa nilipokuwa nasali kwa mara ya mwisho japo
nilisali katika makanisa mengi, lakini kokote nilikokuwa ninasali nilikuwa
ninashangaa kwa nini watumishi walikuwa wananichukia na waumini wananipenda, na
sababu kubwa ya kuchukiwa ni sababu nilikuwa nawaombea, wanafunguliwa pale
ambapo watumishi wanashindwa mimi nikiwa bado ni kondoo. Mimi nilifikiri
wangenipenda na kuniombea, lakini walinipiga na kunipiga wakaniita kila majina,
lakini sikupungukiwa na chochote MUNGU alikuwa pamoja nami.
Mwaka huo wa 2009 katika kanisa niliokuwa nasali jumapili moja
wapo YESU alishuka katika kanisa ile akasema na mimi peke yangu, pembeni yangu
alikuwa muumini wa kanisa hilo ambaye anaitwa Charles, BWANA akaniambia
nisikuone tena katika kanisa hili ondoka, mimi sipo. Nilijiuliza, lakini nikatii,
nilivyokuwa njiani nikamwambia Charles, YESU ameniambia nisirudi katika kanisa
hili tena, nikajiuliza lakini hayo mengine sikumfunulia, nikaondoka. Baada ya
wiki kama tatu akaja Malaika Gabriel, akaniambia, pale umeambiwa usirudi tena,
hata sisi Malaika tumewekewa X tusikanyage ni kanisa lote kwa jina hilo ambalo
silitaji, akaniambia MUNGU ameshaondoka, sasa ondoka, tutakuongoza, tupo na
wewe serikali yote ya mbinguni.
Sikuenda kanisa nilizuiliwa nikakaa, nilizuiliwa kama miaka
miwili, siendi popote, nafanya kazi yangu ya utalii ninaenda ninarudi, ninaenda
ninarudi, sina makao wala sina baba wa kiroho wa kimwili. Na akaniambia hakuna baba yako wa kiroho
Nikajiuliza sana sasa huko nilipokuwa ninasali ni nini? Lakini
alinificha kwa kuwa hata angenieleza nisingemuelewa. Unajua hata mtoto jinsi
anavyokuwa unazidi kumfundisha taratibu taratibu. Basi nikamtii yale alikuwa
ameniambia ambayo siwezi kuyaeleza hapa, BWANA YESU ASIFIWE. Nikaendelea,
nikaja nikaanzisha huduma kama alivyoniambia ambayo akanipa jina liitwe YESU NI
BWANA NA MWOKOZI WA MATAIFA YOTE.
Akaniambia wewe kabla ya kuumbwa misingi wala kuingia kwenye
tumbo la mama yako, tulikupa utumishi toka mbinguni, sasa tumekupitisha katika
tumbo la mama yako tu ili kwamba uzaliwe kazi iende. Kama vile mimi nilivyokuja
nikazaliwa hapa, wewe siyo mtumishi wa hapa duniani, hata mafundisho
utakayofundisha ni ya juu, kwa sababu alikuwa anajua muda wake ukifika
atanitumia, na ndio muda ndio huu sasa.
Nikaendelea, nikaendelea na kazi ya MUNGU kama ilivyo sasa
hivi ili kumuona MUNGU zaidi na zaidi, ikafika 9.11.2011 akaniambia sasa Hebron
nakuonyesha baba yako wa kiroho nikashtuka, nikaogopa, ni yupi tena wakati
ameshaniambia hayupo. Akanimabia baba yako wa kiroho amekuwa akiomba kwa muda
wa miaka mitatu, na mimi nimemuahidi kwamba ninakutengeneza na wakati wake
ukifika nitakupeleka, nenda kamuone nami nikachukua hatua, nilivyokwenda alikuwa
anajua sura ila jina alikuwa halijui, na MUNGU alimuambia mwisho wako wa kulia
akamuambia mbariki, akanibariki. Baba yangu wa kiroho aliniambia ni Moses
Kulola ndio alikuzaa, na YESU akasema naye tukiwa pamoja naye na mtoto wake
anaitwa Willy.
Akamuambia, wewe mwenyewe umebaki wako wapi wenzako walikuwa
na wewe? Wameniacha umebakia mwenyewe, hata uliowazaa baadhi yao wamekuwa
wachawi, tazama hata na mguu wako huu, wakati huo alikuwa anaumwa na mguu, ni
mmoja wa watoto wake ambaye amemzaa kiroho ndio alikuwa amemwekea kile kilema
atembee na fimbo, ili amtoe kafara lakini ikashindikana, wanadamu wanabadilika.
Akamuambia hautalia tena, basi ilikuwa furaha na mimi wakati
huo wa kumjua baba yangu wa kiroho. Alinifurahia sana, aliniombea, japo sasa
hivi ni marehemu, lakini pia nilimuona mbinguni, tayari amepumzika kabisa wala
msilie, kwa hiyo nina amani maanake nililia, sijawahi kupendwa na baba wa
kiroho, walikuwa wananipenda kwa sababu ya pesa yangu.
Wengine sasa hivi baada ya mimi kuinuliwa wanasema mimi ni
mtoto wao wa kiroho NO! siyo,
nilipitishwa huko kama mzururaji, baba yangu yuko mbinguni, ametulia, na sasa
hivi ni YESU peke yake ndio ananilea, wala sihitaji mwanadamu yeyote kunilea
kiroho, nalelewa na BABA yangu tu. Nilipigwa na watumishi niliangamizwa, na
nyie watumishi mnaona mnashindwa kukua au kondoo makanisani mnaagamizwa na
watumishi ujue huyo ni baba yako wa kiroho wa kambo. Ni bora baba wa kambo wa
kimwili au mama wa kambo wa kimwili anahuruma kuliko baba wa kiroho, anakuua
kabisa, anakumaliza kila kitu kwa sababu ya wivu, BWANA YESU ASIFIWE.
Basi ndio ikawa ni furaha yangu toka wakati huo mpaka sasa
kwa hiyo nikawa namshukuru MUNGU sana. Na mimi ninawaeleza, muendelee
kumwangalia MUNGU, mambo yameharibika, na cha ajabu 14.6.2010 nilipelekwa
mbinguni, cha ajabu nilivyopelekwa mbinguni, nilionyeshwa katika watumishi wa
Tanzania nilionyeshwa Kulola peke yake, Moses Kulola ndio yuko mbinguni, lakini
sikuelewa kwa nini maana yake, akaniambia Hebron huyu ndio amenifurahisha moyo
wangu, na huyu ndio alianzisha injili Tanzania, lakini sasa hivi injili imekufa
amebaki mwenyewe. Akanionyesha majina mengine yote sikuyaona ya watumishi wakubwa
hapa Tanzania, kabisa kabisa hakuna hata mmoja hata na madhehebu hakuna hakuna,
na hii ninawaambia ukweli na kama yeye hayupo ina maana hamna kitu chochote 98%
shetani ameshikilia.
Akamuambia katika Afrika BWANA YESU tukiwa na Moses Kulola
wakati huo bado yuko hai, katika Afrika amebakia yeye peke yake, sasa hebu
jiulize ndugu msomaji, kuna watumishi wangapi? Halafu anaambiwa amebaki Moses
Kulola, halafu ameondoka, ni nini kipo? Manabii ni waongo, wauza madawa ya
kulevya, waizi, wana mazingaumbwe, kweli imeondoka ni uovu mtupu. Ninachowasihi,
mnaotaka kupona muokoke kikamilifu tena muishi maisha matakatifu yakumpendeza
MUNGU na kama ni kazi ya MUNGU fanya ya kumpendeza MUNGU na siyo kunyang’anya
nyang’anya watu hela na siyo kubatiza watu kwa maji ya kikombe huendi, kubariki
watu wazima huendi. Hata kuchukua pesa za watu makanisani, mnamfanya MUNGU
anakuwa nyang’anya nyang’anya, lakini wakati umefika sasa ulimwengu lazima
ubadilike na hii anaifanya MUNGU mwenyewe wala hakuna atakayemsaidia, wala
haitaji nchi yeyote wala nini, huo ndio ukweli, kama unaweza shindana na Eliya
au unaweza shindana na Musa, shindana naye, hao ndio wamepewa kazi sasa ya
kuangalia BWANA YESU ASIFIWE.
Jambo lingine pia katika kanisa nilikuwa nimepita, MUNGU
ambalo alinifukuza huko, akaniambia huyu sasa hivi yeye waumini ndio wanamuita
MUNGU, halafu sasa hivi anabatiza watu kwa jina lake. Mfano mimi nakubatiza kwa
jina la BABA, na la MWANA, na la ROHO MTAKATIFU halafu nakuwekea kwa jina la
Hebron, hivi, tafuta kwenye biblia ipo hiyo? Haipo. BWANA YESU ASIFIWE, kwa
hiyo mambo yameharibika, ni kuchunguza na kuwa waaminifu, kuangalia, kuwa
makini sana. Mashetani pia wanaamini YESU ni mwana wa MUNGU, sawa, ndio, hata
watu wanaamini kuna mwana wa MUNGU lakini hawana neno, watu wanahangaika na
Zaburi 23 zimekaa kichwani lakini mapepo yamejaa, mjiulize shida iko wapi?
Zaidi soma katika mafundisho ya vitabu vya Nabii Hebron
ambavyo MUNGU alinipa mimi, na mimi ninakueleza tena hayo ni madogo tu, kwa
sababu nikitoa makubwa zaidi, ufahamu wako unaweza pasuka. Sasa hivi watumishi
wanapaa kuliko mwewe au njiwa angani, usiku wanapaa, wa kweli ni wachache sana. Nchi
zimelaanika, haya makanisa yachunguzwe ni wauzaji wa madawa ya kulevya, yaani
kanisa linaingiza madawa ya kulevya halafu wanadamu wanavuta, inamaana YESU
ameingiza madawa ya kulevya.
Enyi wa Galatia imeandikwa, nani aliyewaloga? Enyi nchi zote
za dunia nzima, viongozi na serikali nani aliyewaloga? Nawafungua fahamu zenu
na MUNGU awainue maana anawapenda sana. Mfanye kazi yake vizuri, mlinde raia
wenu, watumishi sasa hivi ndio wanakuwa wanaharibu nchi zenu na siyo nchi zenu
ni za MUNGU. Ulikuja uchi utarudi uchi, ni wakati wa kutengeneza nchi, haujui
leo upo, kesho haupo, sasa hivi watumishi ni kujinadi kwenye TV namba za benki,
Mpesa, MWIZI! Kama MUNGU angemtuma yeye, angemuandalia njia, ameniambia yeye
siyo omba omba, na kwa nini wanaomba, ni kwa sababu hawajaitwa.
Mimi YESU aliponiita ameniambia Hebron nimekuita, ndio neno,
kwa hiyo kila kitu kitanyooka. Maharambee harambee harambee uwizi mtupu,
mnaibiwa, mnazidi kumchukiza MUNGU kwa hiyo mbadilike, mumrejee MUNGU na
muokoke, bila wokovu hakuna kwenda mbinguni. Kazi ya MUNGU wana wa MUNGU
imekuwa ni biashara sasa hivi, hakuna ukweli, hili jina kwa sababu ni la
thamani kila mtu analikimbilia.
Usitishwe na mtu ananena. Sasa hivi watumishi wanatoa watu huku
machuma, huku machungwa wanatoa huku mawe, hayo ni mazingaumbwe uwongo. Kila mtu
afunguke, BWANA YESU ASIFIWE, itafika mahali watu wanatoa watu maembe kichwani,
hivi mnaona mazingaumbwe haya? 98% kanisa limekwenda, na kanisa lililokwenda
haliko na YESU maana likiwa na YESU haliendi halitekwi. Na watumishi
wanachukiana sana. Ukisema ukweli tu unachukiwa, mimi sijali, hata BABA yangu
YESU alichukiwa lakini si alishinda. Mimi hata kukohoa sitakaa nikohoe, hata
hakuna atakayekaa mbele yangu, wameshasimama wengi, hata kunisemea kwa kiongozi
wa nchi mimi najua lakini imeruhusiwa mkachorwe huko uwovu wenu, BWANA YESU
ASIFIWE, na mengine mengi muendelee kusoma vitabu, msiogope, ninawaombea wote
kwa jinsia yote, sina ubaguzi, naombea nchi zenu zifunguliwe, na nchi ya Tanzania
imeshanyanyuliwa ni Edeni.
Habari ya kuloga loga viongozi hakuna tena kuzoea kuloga
viongozi na kuwalaumu. Ukishakuta serikali inalaumu viongozi hawaendi vizuri
kanisa linashida, wako wapi wawaombee? Sasa wenyewe wanamazingaumbwe, MUNGU
anasikiliza wana mazingaumbwe?
BWANA YESU ASIFIWE. MUNGU awainue, MUNGU awaokoe. Endelea kufuatilia
vipindi vya Mtume na Nabii Hebron, ninaachilia moto ubomoe kila nguvu
zinazokusumbua ndani yako kwa jina la YESU, kwa damu ya YESU. Amen!
NABII HEBRON.