Pages

Wednesday, December 3, 2014

KWA NINI YESU ALISEMA WENGINE NI WANYANG’ANYI NA SIYO WATUMISHI WAKE?
INA MAANA GANI? WANYANG’ANYI NI NANI HAO?

BWANA YESU WA NAZARETI ASIFIWE. Karibu katika shule ya YESU akufundishe neno lake na akufungue ufahamu na macho na masikio ili umsikie yeye na umuelewe ili uzifuate njia zake. Nitaelezea katika kipengele kimoja kwa nini YESU alisema wengine ni wanyang’anyi na siyo watumishi wake? Soma katika kitabu cha Yohana 10: 1-2, 7-10
1YESU aliwaambia, Amin, amin, nawaambieni, yeye asiyeingia mlangoni katika zizi la kondoo, lakini akwea penginepo, huyo ni mwivi naye ni mnyang’anyi. 2 Aingiaye mlangoni ni mchungaji wa kondoo. 7 Basi YESU aliwaambia tena, Amin, amin, naawambieni, mimi ndimi mlango wa kondoo.  8 Wote walionitangulia ni wevi na wanyang’anyi lakini kondoo hawakuwasikia. 9 Mimi ndimi mlango; mtu akiingia kwa mimi, ataokoka, ataingia na kutoka naye atapata malisho. 10 Mwivi haji ila aibe na kuchinja na kuharibu; mimi nalikuja ili wawe na uzima, kisha wawe nao tele.”

Hapa watoto wa MUNGU wengi wamepigwa upofu hata kushindwa kulielewa neno la MUNGU na bado wakashindwa kutofautisha kati ya mnyang’anyi na mtumishi, YESU alimaanisha nini? Alimaanisha akijua kabisa mtumishi ni yeye mwenyewe anamuita na anaishi ndani yake na mnyang’anyi yeye haishi ndani yake, yeye ni mwizi. Lakini mfano huu umekuwa ni fumbo sababu hakuna mtumishi anayejiita mnyang’anyi sababu alijiita hivyo, hakuna mtu atakayemfuata sababu neno linasema kazi ya mnyang’anyi ni mwizi, kuiba, na sasa 98% ya wanaojiita watumishi katika ulimwengu wote ni wanyang’anyi na watu hawawaelewi na wanapigwa upofu na mtu kujiita mtumishi tu. Watu wakamuamini na kumbe ni kinyume. Katika kanisa ili umuelewe mtumishi ni nani chunguza matendo yake na ili umjue mnyang’anyi chunguza matendo yake, yale yote ayatendayo huyo anayejiita mtumishi ambayo ni mabaya; mfano kazi ya michango, harambee makanisani, kukusanya madeni, kutoa huduma kwa kuchaji pesa au hata ukitaka umuone lazima ulipe malipo ya kiingilio upate appointment, hao ndio wanaitwa wanyang’anyi, ila wanajificha kwa jina la mtumishi. Mpaka hapo natumanini sasa umepata picha kiasi fulani, kutofautisha mtumishi ni nani na mnyang’anyi ni nani?

Mtumishi siku zote yeye husema neno la MUNGU katika kweli na halibadiliki, hana kuficha ficha yeye injili yake ni kweli tupu ili mpone, sababu hiyo ndiyo sauti ya YESU, na injili ikiwa ni ya kuficha ficha ukweli, uelewe injili hiyo ni ya kutoka katika kitengo cha unyang’anyi; mfano halisi ili uelewe wanyang’anyi anaowataja YESU katika neno lake, ni nani hao na wakoje? Hawa wanyag’anyi ni watumishi wanaojiita wao ni watumishi wa YESU na kumbe siyo sababu ya kwanza wamemnyang’anya YESU neno lake lisitumike katika makanisa yao, jambo la kwanza wamemnyang’anya YESU ubatizo wa maji mengi ambao ndio uliotoka mbinguni wakautoa wakaweka wa maji ya kikombe, huu ni mfano wa kwanza hivyo hao ni wanyang’anyi na wala hawatampeleka mtu mbinguni ni sababu ya kwanza wao wenyewe hawaendi mbinguni sababu ni wezi na pia ni adui wa MUNGU.

Jambo lingine, wamelipindua neno la MUNGU ambaye ndiye BABA yake YESU, wanaruhusu kuabudu sanamu, kubatiza watoto wadogo, kubariki watu wazima, wanaongeza huduma 6 badala yya kuwa tano, huduma ya sita ni (Uaskofu).

Badala ya kumuabudu MUNGU, ROHO MTAKATIFU, na YESU peke yao wao wameongeza watoto ambao aliwaumba MUNGU na viumbe vyake ikiwemo hata jua, nyota, miti, makaburi na mengineyo.

Wanaitwa wanyang’anyi na YESU sababu wapo kwa ajili ya kutafuta pesa tu na kuifanya jina la YESU ni jina la kutafutia pesa tofauti na ilivyo katika biblia, mtumishi hapaswi kuhangaikia mambo hayo ya kuwachaji pesa waumini na kuwachangisha.

Ni wanyang’anyi sababu wengine wanabatiza watu kwa majina yao badala ya jina la YESU, hapa wanamnyang’anya YESU wewe ambae umebatizwa, badala ya kuwa ni wa YESU yeye hakupati tena sababu a huyo (hawa ndio wanyang’anyi ni wezi wanakuibia wewe mwenyewe, pia wanamuibia YESU, wanamuibia pia na MUNGU, ili akukose yeye aliyekuumba na kukupeleka katika ufalme wa shetani pasipo wewe kujua na wengine wanajijua kabisa tayari wao ni kizazi cha nyoka.

Makanisa yenye benki, SACCOS huu ni msingi wa wanyang’anyi sababu MUNGU hachaji riba. Sasa benki na SACCOS si zina chaji riba? Riba kwa kanisa likidai tayari ni kanisa la unyang’anyi au wanyang’anyi, kitu huitwa kwa jina la matendo yake.

Kuzimu, mtumishi au mnyang’anyi wale wanaozini wote ni wanyang’anyi na muwe makini, hawa ni wachawi, wanasimamia amri za shetani ziimarike katika dunia hii ndio sababu wanazini, wachawi, freemason, walevi, wanavaa kofia kanisani, wanadai mshahara na mengineyo mengi. Hao wote ndio wanyang’anyi YESU anaowaelezea, wameingilia kwa mlango wa nje yaani wa shetani na kuwapiga watu upofu hata sasa mamilioni ya watu katika ulimwengu wote wajijue hawaongozwi na watumishi wa MUNGU wa kweli bali wanaongozwa na wanyang’anyi au wezi kama ndio viongozi wao wa kiroho. Sasa ujipime na ujiulize kama unaongozwa na kiongozi anayemuibia YESU je anakupeleka wapi? Jibu, anakupeleka kwa baba wa waizi shetani na wewe katika ulimwengu wa roho unakuwa baba yako wa kiroho ni mwizi na unaitwa mwana wa mnyang’anyi. Funguka sasa, uamue, utubu na uokoke YESU akuongoze yeye peke yake awe ndiye mchungaji wako na uisikilize sauti yake uachane na sauti  za wanyang’anyi ili upone sasa.

Sema BWANA YESU WA NAZARETI, naomba unisamehe, uniandike jina langu katika kitabu chako cha uzima wa milele niwe kondoo wako unichunge wewe. Niliibiwa sana pasipo kujua na hawa wanyang’anyi, nashukuru kwa kunifunulia sasa mimi nimekuwa huru amen. YESU awe mchungaji wako kuanzia sasa na uwakatae wanyang’anyi ili usije ukaangamia.

Zaidi karibu katika kanisa la YESU NI BWANA NA MWOKOZI WA MATAIFA YOTE, endelea kusoma blog hii yapo masomo mengi sana yatakuweka huru sababu mchungaji YESU amenituma niwaeleze habari zake na mumjue yeye awe BABA yenu na siyo tena baba yenu awe mnyang’anyi, chunguza matendo ya mnyang’anyi utaelewa zaidi. Ubarikiwe. Ingia katika website www.prophethebron.org, ingia katika YouTube ya prophet Hebron utasikiliza mengi utakuwa huru, na wewe uwatumie wengine kila mahali injili isonge mbele na wanyang’anyi wakome sasa.


NABII HEBRON.