Pages

Wednesday, December 3, 2014

JE UNAJUA KUWA UNAPOANDIKA SADAKA JINA LAKO NI KUMTUKUZA SHETANI?

Ukisoma katika injili ya Mathayo 6: 2-4
2Basi wewe utoapo sadaka, usipige panda mbele yako, kama wanafiki wafanyavyo katika masinagogi na njiani, ili watukuzwe na watu. 3 Amin, nawaambieni, wamekwisha kupata thawabu yao. Bali wewe utoapo sadaka, hata mkono wako wa kushoto usijue ufanyalo mkono wako wa kuume; 4 sadaka yako iwe kwa siri; na BABA yako aonaye sirini atakujazi.”

Maana ya neno hili alilolitoa YESU ni amri kutoka mbinguni akifundisha jinsi ya kumtolea MUNGU iwe ni siri yako, inapojulikana tayari umetupa chini au ukapita kanisani unazionyesha katika mikono yako ili uonekane umetoa nyingi, huo ni uchafu na ni dhambi na watu wafanyayo hivyo sadaka hizo hazipokelewi na MUNGU bali zinaenda kwa shetani na katika mtandao wa freemason katika ulimwengu wa roho. Ila makanisa yamemuasi mwenyezi MUNGU na kulivunja neno lake. Tazama sadaka zinavyotolewa katika makanisa halafu njoo katika kipengele hiki, je MUNGU hatukanwi? Jibu, ametukanwa na kudharauliwa na kazi hii inafanywa na viongozi wa makanisa.

Sasa waulize kama wanamheshimu MUNGU mbona wanavunja neno lake? Huko ndiko kulipindua neno la MUNGU. Sasa mtoto au watoto wa MUNGU madahara yake unapoandika sadaka jina lako au ukasema unatoa kiasi gani au ukapewa risiti au akaandika email yako na simu au mtaa au address yako, tayari hiyo siyo sadaka inayokwenda kwa MUNGU bali inakuwa umetoa kwa mashetani pasipo wewe kujua na wengine wanajua. Pia unakuwa umemtukuza shetani kwa kutii kuandika sadaka jina na ikawa siyo siri tena. Je ni wangapi mmefanya hivyo pasipo kujua? Jibu, inawezekana hata wewe ulitoa kwa mashetani au kwa wanyang’anyi ambao YESU aliwataja, muwe makini na wanaojiita ni watumishi.

Mfano kuomba pesa za vipindi vya TV au Redio au chochote, huko ni kumtukana YESU yeye ni masikini, hata ukitoa uelewe umeitoa kwa mashetani au wanyang’anyi. Hivyo mataifa yote msidanganyike tena watumishi wanatumia njia hii zaidi kuwafilisi, nyang’anya watu mali zao wakitumia jina la YESU na mwenyezi MUNGU na kuwafarakanisha wanadamu kwa njia hii. Unapoona hayo wewe endelea songa mbele YESU atakupigania, na wengine wanawaeleza watu wasaini katika nguo zao viwango vya pesa yaani huyo ni pepo sadaka, mnyang’anyi mkubwa aliyekomaa na yupo makini katika kunyang’anya watu pesa zao.

Nikuulize swali, tokea lini sadaka inaandikwa katika nguo ya mtumishi na ukapiga saini mgongoni au miguu katika suruali yake na akajipangia unaye saini juu unatoa zaidi na unayesaini miguuni kiwango kidogo? Huyo ni JAMBAZI wa kiroho. Amemtukuza shetani na mkitoa hapo pesa zote zimeenda kwa freemason na shetani na nyota zenu na Baraka zenu. Halafu yeye anastawi nyie mnabaki na mateso. Na pia kuhusu kapu la mama mchungaji au baba mchungaji unapotoa umemtukuza shetani. Nikuulize swali, je imeandikwa umtolee MUNGU sadaka au mke wa mchungaji au mchungaji? Jibu, umtolee MUNGU peke yake. Sasa hauoni tayari umefanyika kumtukana MUNGU na umuinue shetani? Wengi mmepotezwa na kudanganya na watumishi (wanyang’anyi) imefikia kipesa sasa hata wake wamenyang’anywa hata watoto, je utabisha? Kanisa halijatekwa na shetani? Na kumtukuza shetani na MUNGU akapuuziwa? Funguka ufahamu, tubu ili hiyo laana itoke kwako.

Sema YESU naomba unisamehe, niandike jina langu katika kitabu chako, najikabidhi kwako, nisamehe. Sitamtukuza shetani tena na sirudi huko wanapomtukuza shetani tena. Nakutukuza MUNGU WA IBRAHIM WA ISAKA NA YAKOBO.


NABII HEBRON.