Pages

Tuesday, November 25, 2014

MAHOJIANO: KUPITIA YOU TUBE.

JINSI NABII HEBRON ALIVYOITIKISA KUZIMU
NA KUMTOA ALIYE KUWA NGAZI YA TATU TOKA UFALME WA SHETANI
  SEHEMU YA  3.


MTUME:   Karibu tena katika  kipindi cha Nabii Hebron wa  Kanisa la YESU NI BWANA NA MOKOZI  WA  MATAIFA YOTE.  Somo ambalo nitakuwa nikifundisha kupitia ushuhuda ambapo nipo na Isaya, ambaye alikuwa anaitwa Maxwel sasa anaitwa Isaya, ambaye yeye alikuwa huko kuzimu na YESU alinituma nikamtoa huko, kwa hiyo nitaendelea leo katika mahojiano mengine tena. Ili kwamba, kuweza kuwafungua macho mjue ni nini mbinu za shetani na mjue mnatoka huko na mpone msidanganyike . Ameen!!

Mtume:   Karibu sana Isaya..

Isaya:    Asante , BWANA YESU asifiwe, kwa jina  naitwa Isaya ambaye jina langu la mwanzo nilikuwa nikiitwa Maxwel ni mtoto ambaye nabii alikuwa akinielezea, lakini kwa sasa hivi sipo tena katika huo ufalme, nimeokoka nampenda Bwana YESU na ninamtukuza na ninacho penda kuwaambia labda, ndugu zangu msije mkakubali tena kukaa kwa shetani kwa sababu mmeshaujua ukweli tayari. Mnatakiwa kumfuata MUNGU, kwa sababu shetani ni mbaya .
Na baada ya MUNGU kuona shetani anatamba ovyo ndio mana akaamua kumshusha Mtume na Nabii Hebon hapa duniani.
Kwa hiyo watu wasimuone mtume na nabii Hebron kuwa ni mtu wa kawaida, na tusiwe na mazoea na MUNGU, tunatakiwa kumuogopa MUNGU,kumuogopa Bwana YESU na pia madhabahu yake takatifu tuiheshimu na pia Mtume na Nabii tusimzoee tusimuone ni mtu wa kawaida.

Mtume:  Sasa si watu wataniogopa aisee…. Hehehe!!

Mtume: BWANA YESU asifiwe, aaa.. sasa siku ya leo kuna maswali ambayo nitakuuliza machache, japo mimi nayajua lakini ili tuweze kuwafundisha, ndugu watazamaji na watoto wa MUNGU, ambao wanamjua MUNGU ili warejee kwa YESU na watoto wa MUNGU  kile alichonituma YESU ni kuhakikisha kwamba wewe unamjua MUNGU , unaokoka nunakuwa mtoto wake ili kwamba usipelekwe huko ambako shetani alishaandaa kwa ajili yako wewe  na mwingine lakini  ipo neema  ya MUNGU leo , utaenda kutubu  na kuambatana na mimi  tuungane na YESU , utapona. Bwana YESU asifiwe,
Sasa siku ya leo Isaya nitakuuliza japo mimi nina yajua lakini ni kwa faida ya kuwafundisha wana wa MUNGU amen!!..
Mtume;   eee, Katika ofisi yako uliyokuwa nayo,wakati napambana na joka kuu na lusifa , nikitafuta yale mafail, nilielelezwa wewe ndie mwenye mafail ya dunia nzima.. sasa  embu tuelezee kwa ufupi hayo mafail yalikuwa na nini na nini  ulikuwa navyo..

Isaya:   BWANA YESU  asifiwe..

Mtume:  Ameen..

Isaya:     Yale mafail yalkuwa na baadhi ya majina ya wale waliokwenda kinyume na amri za MUNGU  na kila rekodi ya kila kitu kilichofanyika hapa duniani katika yale mafail, na pia kazi yake ilikuwa ni kurekodi kazi za kule kuzimu, kitu ambacho labda kimefanyika siku nzima na kwa masaa.
Na yale mafaili yalikuwa yana majina ya watu  wa shetani ambao wapo katika kile kitabu cha shetani ambacho ni kitabu cha hukumu na yalikuwa yana mambo mengi sana.

Mtume:  Lakini hayo mafaili kwa nini shetani na joka kuu walikukabidhi wewe  hayo mafaili yote  ya serekali ya kuzimu ambayo kwa sasa hivi nimekwisha yachukua?

Isaya : Ni kwa sababu walifikiri kwamba mimi sitatoka tena kule..

Mtume :  MMh..
Isaya:   Na walishaniamini kwamba ile kazi naiweza lakini mpango wa MUNGU nimetoka  pasipo wao wenyewe kuamini nimetokaje.

Mtume:   kwa hiyo kuzimu yote ..siri zote hata joka kuu hana tena, yote yapo katika yale mafaili niliyayachukua na BWANA YESU ?

Isaya:   Ndiyo.
Mtume:  Sasa watoto wa MUNGU nawaambia ni wakati wa kufunguka! Hapa ipo neema ambayo mwana wa MUNGU anawaelezea….
Bwana YESU asifiwe!!.
Aaa nakuuliza ni namna gani hizi roho saba za shetani zinafanya kazi? Maana hata katika kanisa kuna roho saba lakini shetani nae anaroho saba na manabii wa uongo nao pia wana roho saba.. karibu..
Isaya;  Hizo roho saba !

Mtume:  Mmh..

Isaya:     Kazi yake inakuwa ni kuwapa manabii pamoja na mapepo na kundi la majini kule kuzimu kwa  hiyo hapa  ni kuwapulizia pumzi ya uhai kila siku. Nabii anapokuwa kule kuzimu  anapokuwa anapata zile roho saba, kufa kwake inakuwa .. labda inakuwa  tabu kidogo..

Mtume: Inakuwa hafi?

Isaya:  Ndiyo.

Mtume;  Lakini toka nimebomoa nini tena kinaendelea…?

Isaya :  Hakuna kitu.

Mtume: Bwana YESU asifiwe..

Isaya:  Amen.

Mtume:   Mmh.. tutaendelea katika jambo lingine..

Mtume:   Je, unamfahamu mtu aliyepo kuzimu anayeitwa amakuta?

Isaya:  Ndiyo.

Mtume: Embu tuelezee..

Isaya: Amakuta ni jinni kule kuzimu, na amakuta kitu anachokifanya ni kupotosha watu yeye pamoja na kusimamia majini mengine, huko kuzimu na ndote zote za uongo duniani na pia anakitengo chake kingine ambacho  alipewa na shetani ambaye ni lusifa, lakini kile kitengo nilikuwa sikifahamu kwa sababu sihusiki nacho.

Mtume: kwa hiyo kwenye upande wa injili  kama vile unavyoambiwa sadaka zisiandikwe majina, yeye anawaambia waandike majina, batiza ubatizo wa maji mengi ametoa ubatizo wa maji mengi ambayo ni kinyume na MUNGU . Bwana YESU asifiwe.
Mtume; Nitakuuliza, je, unaweza elezea njia ya shetani ambayo anaipitia peke yake?

Isaya; ndiyo

Mtume: Embu elezea..

Isaya: njia  ambayo shetani anapita ni njia ambayo ipo katika kijiji chake kinachoitwa freemason village, ile njia ipo ardhi ya million mia nane daraja la nne. Ndiyo njia ambayo yeye anaitumia kwenda katika kazi zake na kufanya mambo yake yeye mwenyewe.

Mtume. Na unaweza kuelezea njia ya joka kuu anayo pitia yeye peke yake?

Isaya :  Njia joka kuu anayoipitia  ni ardhi ya mwisho  kabisa ya milioni mia nane na pia yeye anapita daraja la sita.

Mtume.  Daraja la sita?

Isaya: ndiyo.

Mtume:  Na unaweza kuelezea na njia yako ilikuwa ya wapi?

Isaya: Bwana YESU asifiwe.

Mtume: Amen.

Isaya:  Njia yangu ilikuwa ardhi ya million mia nane daraja la tano.

Mtume: Je, unafahamu mti wenye matawi saba uliopo kwa joka kuu na kazi zake ambazo ndizo roho saba?

Isaya; Ndio

Mtume. Na ukoje huo mti embu elezea sababu watazamaji na wasikilizaji wangependa kuelewa kwa sababu walizoea kusoma tu, joka kuu itakuwa hivi mara vile, lakini kuna neema ya kumjua mpaka sura amen!!.

Isaya;  Bwana YESU asifiwe huo mti ni mkubwa sana labda tuseme  ni kama Tanzania nzima.

Mtume: Mmm..

Isaya: Na ule mti kazi yake pia ni kutoa hizo roho kwa wale manabii pamoja na wale wote walioenda kinyume na MUNGU kule kuzimu.
Pia kazi yake ni kutoa zile roho ambazo manabii na wale wote walioenda kinyume na amri za MUNGU ambao wapo kule kuzimu.
Na ule mti unahusika na unaushirika na mapepo ambayo yanaruka duniani kila siku kwa muda wa saa sita usiku.  Yanaporuka yale mapepo yanaachilia zile roho za ule mti.
Kwa hiyo labda inaweza kupita Tanzania na kuziacha zile roho mkoa Fulani au Kenya zinaacha sehemu Fulani na p engine popote pale.
Na pia ule mti ulikuwa una ndege, ambayo ilikuwa inaitwa “air force one.”

Mtume: Ukubwa  wake hiyo ndege ni kama kiasi gani?

Isaya: Ni kama Arusha nzima,

Mtume: Ndege moja?

Isaya: Ndiyo.  Ile ndege pia inahusika katika kitengo cha ule mti cha kuachilia zile roho huku duniani kwa sababu yale mapepo yanaanza kazi saa sita yanapumzika siku ya kwanza, siku ya pili inaingia ile ndege inaachilia zile roho saba.
Mtume: Mmm.. Ndugu watazamaji mmeshaelewa ni kwa nini watu wanafanya dhambi wana ugua, ni kwa sababu  ilikuwepo ndege ambayo inamwaga roho za dhambi, ndiyo ndege kama alivyokuwa anatuelezea hapa ambayo kwa sasa imesha tunguliwa na watu ni wakati wa kuja kwa YESU sasa na watu waliookoka sasa watakwenda kusimama imara kwa Yule wanayempenda BWANA YESU , Ameen!

Mtume:  Jambo lingine nitapenda kukuuliza, hebu nieleze , kwa sababu ulikuwa mkuu wa kitengo  hiki na hayo makanisa ya kichawi yaliyopo yanatumia jina la YESU, wewe ndiwe kiongozi  na kuwapa nguvu na kuwapa pesa na kama ulivyowapa dola wale waliopo Tanzania, wenye mabenk embu naomba uelezee ndugu wasikilizaji na watazamaji, kwa nini makanisa mengine yanakuwa na picha ya msalaba, halafu yana alama ya dunia, halafu kuna  nyoka kwenye msalaba; na watu hawajijui wanaona wameokoka embu elezea maana yake ni nini?
Sasa unawaambiaje wasikilizaji na wanadamu wanaompenda YESU kuhusu hii habari ya huyu nyoka.
Huyu nyooka ninachowaambia ndugu watazamaji ni shetani, iweje leo kanisa la wokovu  lina nyoka kwenye nembo yake? Hiyo nembo huyo hapa  ndiye aliyekuwa anatoa mashariti ,.. sawa , sawa ..
Mtume: Bwana YESU asifiwe !  Ni masharti aiweke pale ili hawa washuke, wanaposhuka hapo… embu eleza  nini mnachokifanya katika kanisa.

Isaya: Unapoona ilea lama ya nyoka ndiyo inayotukaribisha sisi kushuka katika hilo kanisa na tunapokuwa tumeshuka  tunashuka kwa kuongozana,

Mtume: Ki vipi?

Isaya:  Mtu wa kwanza kushuka anakuwa ni joka kuu, mtu wa pili kushuka anakuwa ni shetani ambaye ni lusifa na mtu wa tatu kushuka alikuwa ni roho mtakatifu wa kuzimu ambaye ndiye  niliye kuwa naitwa maxwel. Na tunaposhuka, tunaenda kuchukua sadaka za watu, na wale watu tunachukua miili yao na pale kanisani tunaacha kopi, na pia joka kuu anaenda kumeza watu wote waliokuwepo katika hilo kanisa, na pia analimeza kanis azima, lusifa anaenda kuwaua watu wote, na mimi nilikuwa nikienda kuchukua pesa za watu.

Isaya: BWANA YESU asifiwe,

Mtume: Ameen..

Isaya: Unapoona ile duara inamaanisha ni dunia,  ule msalaba, unamaana yake maana ya kwanza  ile ncha ya kwanza iliyo simama juu ni joka kuu, ya kulia ni shetani ambaye ni lusifa, ya kushoto ndiye maxwel ambaye ndiye nilikuwa mimi zamani kwa sasa hivi naitwa  Isaya. Ile ya chini inamaanisha kuzimu nzima.
Na Yule nyoka anayekuwa anazunguka ndiye joka kuu ambaye anazunguka na kuitawala dunia ameimeza.

Mtume.  Sasa ni kwa nini kanisa utakuta mchungaji ameokoka lakini nembo yake ipo nyoka?

Isaya:  Bwana YESU  asifiwe!

Mtume: Ameen..

Isaya: Unapoona hiyo nembo ya nyoka , maana yake ni watoto  wa joka kuu wametawala katika hilo kanisa lake, na wanakuwa wanaachilia nguvu zao, toka kuzimu katika hilo kanisa na pia wanaenda kuiba nafsi za wana wa MUNGU pamoja na vitu vyao vyote .

Mtume;  Wanaosali  mahali hapo?

Isaya; Ndiyo.

Mtume: Kwa hiyo watu kwenye makanisa hayo iwe hawajaokoka au wameokoka, mbinguni hawaendi?

Isaya: Ndiyo.

Mtume.  Na inakuwaje sasa unakuta anaitwa nabii, mtume , mchungaji  lakini anasema amepandishwa na YESU eti mpaka mbinguni hii ni teckique gani wakati unasema hapa kuwa alikuwa mtu wenu?

Isaya: kwanza anakuwa ni muongo anakuwa  anaongea kwa kinyume, anamaanisha ameshaenda kuzimu. Na pia anapokuwa anasema yeye ni nabii wa Mungu anamaanisha yeye ni nabii wa shetani na zile nguvu anazokuwa nazo ni mapepo yanakuwa katika kanisa lake na anakuwa na mapepo ya utambuzi utakuta anakuambia hivi na vile utoe pesa yako na unapoitoa pesa yako, tayari unakuwa umeshajiandikisha kwenye kitabu cha kuzimu.

Mtume: Swali jingine ulishanieleza japo nilikuwa najua, ulikuwa unawapa pesa , utashangaa kanisa hapa duniani linanyanyuka kumbe wewe ndie zile bank zilizokuwa zinaendeshwa na makanisa zilikuwa na maana gani?
Bwana YESU asifiwe embu naomba utuelezee ni kwa nini wengine  wanakuwa na benk na ulishanieleza kwamba, japo nilikuwa najua ulikuwa unawapa pesa, unashangaa kanisa linaendelea hapa duniani , utajiri hilo linaendelea limenyanyuka, kumbe wewe ndie ulikuwa unawapa pesa. Embu elezea zile pesa zilikuwa na maana gani?

Isaya:  BWANA YESU  asifiwe!

Mtume: Ameen..

Isaya:  zile benki zinapokuwa zinaongozwa na makanisa, zinanakuwa ni pesa za kwenu nyie nyie waumini, mnatoa sadaka katika lile kanisa, zile pesa zinakuwa zinapelekwa katika benki ya kuzimu, na kule kuzimu nilikuwa nazibadili zile pesa,  nakuwa nawapa manabii zinakuwa inawapa wale manabii zile pesa zao na kuwaambia wakajenge kitu Fulani, na mnapojenga, inakuwa hicho kitu wanajua lazima kitakamata watu sehemu Fulani, na zile pesa pia zinakuwa ninyi wenyewe waumini mnakuwa mmekwisha ingia agano pasipo nyie wenyewe kujielewa.

Mtume : Okey .. Jambo lingine , aa.. bank kuu ya shetani ambayo ni ya shetani, wewe ulikuwa ni partiner mmoja wapo?

Isaya: Ndiyo

Mtume:  na mlikuwa partiners wangapi katika  benki ya kuzimu?

Isaya: Watatu

Mtume: ehee  namba moja?

Isaya: Joka Kuu,

Mtume: namba mbili?

Isaya: Lusifa

Mtume; namba tatu?

Isaya: Maxwel

MTUME: Ambaye ndiye wewe hapo?

Isaya:  ndiyo

Mtume;  Sasa wewe ulikuwa director kule  ee.. !! ulikuwa gavana? sasa

Isaya;  nilikuwa gavana.

Mtume; Ulikuwa gavana na sasa umetoka kule, embu nieleze namna gani ulikuwa unawapa pesa? Badhi yao walikuwa  wanakuja  kuzitumia hapa duniani

Isaya:  Bwana YESU asifiwe,

Mtume; Ameen..

Isaya; Mimi kama mimi binafsi nilikuwa nikitoa pesa kulingana na mtu kazi aliyokuwa ameifanya, kama mtu amefanya kazi nzuri ambayo shetani amemtuma aifanye anapokuwa ameifanya ile kazi sawasawa kama inavyotakiwa huwa nampa pesa lakini kama ameifanya kitu ambayo haijatakiwa ifanywe ,. Hapati kitu.

Mtume:  ni pesa za namna gani mlikuwa mnawapa?

Isaya;  Dola.

Mtume: na hizi dola? Haziwezi kuwa fake huku duniani?

Isaya: Haziwezi.

Mtume; Zinakuwa ni original?  Sasa bwana governer wa bank ya kuzimu enzi hiyo ambayo banki hiyo ilikuwa ni ya joka kuu, lusifa na maxwel bank sindio?

Isaya: ndiyo

Mtume:  ni nini sasa kinaendelea? Pesa watapata wapi?

Isaya:  Bwana YESU asifiwe,

Mtume: amen

Isaya; Kwanza katika ile bank pesa hakuna tena, ile bank ilishalipuliwa na hata manabii wa uongo wameshaporomoka kiuchumi, na pia ile bank kwa sasa hakuna pesa yeyote inayoingia wala kutoka.

Mtume: ni kwa nini?

Isaya: ni kwa sababu ile bank imeshalipuliwa haifanyi kazi tena.

Mtume: Ililipuliwa Lini?

Isaya: ililipuliwa wiki iliyopita.

Mtume: ilikuwaje?

Isaya: Bwana YESU asifiwe?

Mtume: amen

Isaya: Na hiyo bank ililipuliwa mwaka 2014 mwezi wa kumi wiki iliyopita

Mtume; Tarehe ngapi? Unaikumbuka

Isaya: tarehe siikumbuki, na aliyeilipua ni Mtume na Nabii Hebron peke yake.

Mtume: Sasa ni nini kinachoendelea  kama benki imelipuliwa?

Isaya: hakuna tena uchumi kuzimu wala hakuna tena pesa.

Mtume: Ndugu wasikilizaji hata vipo baadhi ya vyama vya siasa vilitegemea kuchukua pesa kuzimu, kule wapo waliokuwa wanapiga kampeni zile za urais, ubunge walikuwa wana mwaga pesa. Na watangazia hakuna pesa za kumwaga tena na uchaguzi kuanzia 2015 hakuna atakayetumia uchawi atakaye fanikiwa.
Bwana YESU asifiwe!

Mtume:  Kuna kitovu ambacho cha wokovu wa uongo utaweza kuelezea mana katika dunia hii utasikia mtu anasema lakini huyu hajaokoka wokovu wake ni wa uongo.. sasa shetani ndugu wasikilizaji na watazamaji naye alikuwa na kitengo chake cha wokovu  lakini makao yake yalikuwa Sri lanka na  bwana mkubwa zamani  sasa hivi  mtoto wa YESu embu tuelezee hicho kitovu kilichokuwepo Srilanka kilichowekwa na shetani na kazi zilizokuwa kinafanya.

Isaya: Bwana YESU asifiwe,

Mtume; amen

Isaya; Kile kitengo kilikuwa kinafanya kazi ya kuingiza roho za uovu duniani. Na pia kilikuwa na ushirika na joka kuu pamoja na majini na mapepo kule kuzimu.
Kwa hiyo kitu kilikuwa kinafanya kilikuwa kinaingiza wokovu wa uongo siku hadi siku na ule wokovu..

Mtume: Mmmh..

Isaya;   Na ule wokovu wa undio kama hivyo, ubatizo wa kikombe na maubarikio haya ya watu wazima na mambo mengine ambayo hayo ni dhambi.

Mtume: Ee.. Unaweza kuelezea watoto wa MUNGU na wana wa MUNGU kwa nini watumishi wana vaa nguo zenye nembo, mfano jumlisha, mzunguko, njiwa , mkuki, kondoo kwa sababu mimi YESU alishanifundisha nilipokuwa kule kuzimu japokuwa hayafanyi kazi tena.
Na unaweza kuniambia, nembo zake mlikuwa mnazifanyia nini? Na je? Hizo nembo ni mpango wa MUNGU au shetani?

Isaya: Bwana YESU asifiwe..

Mtume; Amen,

Isaya:  Nembo hizo sio mpango wa MUNGU, ni mpango wa shetani. Kwanza ningependa kuelezea ukiona kanisa lina alama ya mkuki, anakuwa anaua rohoa za wana wa MUNGU, wote mnakuwa tayari zimeshauliwa, na pia ile njiwa ina maana roho mtakatifu ambaye ni roho mchafu wa kuzimu, ambaye ndiye nilikuwa mimi kwa jina la maxwel.

Mtume: mmh..

Isaya: Na unapokuwa unaona kuna alama moja mfano labda ekaristi katika ekaristi kuna kaalama kama cha kikombe kilichowekwa chini, kile inamaana ni damu ya shetani pamoja na damu za wanadamu wenzako.  Kwa hiyo unapokuwa unakunywa unakuwa umekunywa damu ya wanadamu wenzako pasipo wewe mwenyewe kujielewa. Na pia kunai le kondoo ina maana watoto wa shetani ambaye ni baba wa kuzimu ambaye ni joka kuu.
Watoto wake wanakuwa wanashiriki mahali hapo na nyie pia mnaongozwa na watoto wa joka kuu.

Mtume:  Bwana YESU asifiwe

Mtume: Sasa tunaingia katika lengo lingine la sanamu, kwanza hizi zilizopo duniani zina maana gani?
                Karibu!!
Isaya: Bwana YESU asifiwe,

Mtume: Ameen,

Isaya;  Zile sanamu zilizowekwa duniani huko, zimewekwa kwa ajili ya kuteka fahamu za watu, waone wanamuabudu bwana YESU ambaye wanaweka picha za Yule Brian na kuna makanisa mengine unaweza ukasikia wanasema YESU ameshuka tumemuona, anakuwa haja shuka YESU ni ule mzimu wa Brian unakuwa unashuka mahali alipo kwa sababu hata mimi pia nilishashuka kwa mfano wa sura ile ile.

Mtume:   Sura hiyo hiyo

Isaya;   Ndiyo.

Mtume: ulishuka katika nchi gani?  Usitaje sehemu

Isaya; Nilishuka, nchi ni nyingi kama nchi tano hivi watu walikuwa wanasema  yesu ameshuka  na kumbe wao bila kuelewa ni mimi.

Mtume: Kwa sura kabisa?

Isaya: ndiyo, nilikuwa nimekuja duniani

Mtume: Ulishuka duniani watu wakaona ni YESU kabisa? Ilikuwa ni nchi gani?

Isaya: Nilishuka Tanzania

Mtume: Sehemu gani Mkoa?

Isaya: Nilishuka mkoa wa Dar es Salaam,

Mtume: Dar es salaam  ni maeneo gani?

Isaya; Dar es salaam ilikuwa ni maeneo ya mbezi pia maeneo ya temeke, na maeneo ya kunduchi.

Mtume: Ni katika makanisa pote

Isaya: Ndiyo.

Mtume; Na lengo ulivyoshuka ilikuwa ni nini?

Isaya; Ndiyo mara ya kwanza nimeshuka kuja kuiangalia dunia.

Mtume:  Na lengo ulivyoshusha ilikuwa ni nini?

Isaya: Ndio mara ya kwanza nimeshuka kuja kuiangalia dunia.

Mtume; Dunia..

Isaya:  Ndiyo

Mtume: Aaha..na  kwa nini ile sura ya YESU hamuwezi kuivaa kabisa muiecti, na yenyewe?

Isaya: Haiwezekani.

Mtume: haiwezekani, kwa hiyo watu wanavyo sema wamemuona YESU ni uongo, kumbe wamemuona Brian.
Hata mimi nimekwisha kuwaambia watoto wa MUNGU sura ya YESU duniani hakuna picha yake wala hakuna kumbu kumbu yake.
Bwana YESU asifiwe,
Lakini sasa tunapata shule na kuelewa maana mambo yameharibika, ila YESU amenituma niwaeleze habari njema.

Mtume; Kwenye habari za sanamu unakuta sanamu zipo kwenye mikoa, miji mbali mbali hizi zina maana gani kwenye ulimwengu wa roho?

Isaya: Sanamu pia kazi yake unapokuwa umeiangalia ile sanamu unapogeuka nyuma unakuwa umeacha kila kitu chako pale, unakuwa umeacha sura yako, maisha yako, uthamani wako pamoja na vitu vyako vyote.

Kuzimu pia kuna sanamu ambazo zina connection huku duniani hata ikiwa sanamu ya raisi yambunge au ya mtu yeyote hata kama ni ya mtumishi unayvyoiangalia hiyo sanamu unakuwa unaacha vitu vyako vyote katika ile sanamu wewe ukigeuka unakuwa unageuka boksi.

Mtume: Mmh.. kabla ya kumaliza kuna baadhi wana picha wanaziabudu picha za watumishi,

Isaya: Bwana YESU asifiwe..

Mtume: Ameen

Isaya: Zile Kwanza ningependa kuelezea katika upande wa stika zile stika maana yake?
Mtume;  Stika zipi hizo?

Isaya: Kwa upande wa stika ambazo zinakuwa zinatolewa makanisani. Zile stika unapokuwa unazichukua unakuwa tayari umeshachukua kumbukumbu za shetani ambaye ni lusifa na joka kuu pamoja na Yule roho mchafu wa kuzimu ambaye ni maxwel, unakuwa unawapeleka hao watu nyumbani kwako na unapo wapeleka hao watu nyumbani kwako tayari umekwisha wapa uhalali wa kushikilia kila kitu chako.

Mtume; mm..

Isaya: Kwa sababu hata huku duniani labda kwa upande wa nyumba huwezi kuwa na nyumba ukiwa hauna hati, hata mtu akiichukua ina maana hiyo nyumba sio ya kwako tena.
Hizo stika unapozichukua ukaenda kubandika nyumbani kwako tayari unawapa hao watu watatu uhalali pamoja na kuzimu nzima

Mtume; kwa hiyo na watu wengi naona wanaweka kwenye magari kwa hiyo wamemkaribisha shetani?

Isaya: Ndiyo

Mtume; kwa hiyo hizo ni hati za kumpa shetani mali yako na maisha yako? Lakini wao wanafikiri ni YESU

Isaya: ndiyo.

Mtume: Sasa niwaulize watoto wa MUNGU, je, YESU anatoa stika? Imeandikwa mniabudu katika roho lakini usichukie bali ufurahi, maana hizi ni habari njema alizonituma YESU WA NAZARETI, na siku ya leo nakufundisha kwa namna nyingine upate kuelewa. BWANA YESU ASIFIWE, sasa katika somo hili la shuhuda ambalo huyu ambaye nilikuwa namhoji, nafasi ya tatu kutoka kwa shetani, huyu hakuna mwanadamu alikuwa anamweza, hakuna mchawi anamweza. Huyu ndiye alikuwa anawapa mbinu zote, sasa YESU ni mjanja wa wajanja, amenituma mimi mjanja, nimemkamata, na sasa hivi mnaoendelea kuwa na uchawi mmeaibika YESU atainuliwa, huu ni wakati wa YESU WA NAZARETI peke yake kuinuliwa na shetani hana mamlaka tena katika jina la YESU KRISTO WA NAZARETI.

Zaidi ingia katika website yangu www.prophethebron.org, ingia katika blog www.prophethebron.blogspot.com utapata masomo mengi, na ingia katika YouTube ya prophet hebron utakuta vipindi vingi na zaidi karibu katika kanisa la YESU NI BWANA NA MWOKOZI WA MATAIFA YOTE. Shida yeyote inayokusumbua karibu tena njoo bure bila hata pesa, utafunguliwa ndio kazi YESU amenituma, BWANA YESU ASIFIWE. Na wengine wote mnayo nyanyaswa na shetani wakati wa kunyanyaswa umekwisha,wakati wa kudanganywa umekwisha, njoo usikilize ukweli na ukweli ukae ndani yako, watu wamedanganyika sana kwa habari ya makanisa, lakini sasa leo nimekuja kuwafundisha kwa njia hii japo mimi nilikuwa nayajua.

MUNGU WA IBRAHIM, MUNGU WA ISAKA awabariki, awatunze, nawafunika kwa damu ya YESU. Tutaonana muda mwingine wakati kama huu, karibuni sana katika siku za ibada mfunguliwe, mtukuze MUNGU, muwe na amani enyi mataifa yote, msidanganyike tena mambo yameharibika, ndio maana makanisa imemuacha MUNGU inatafuta pesa tu.