Pages

Thursday, December 18, 2014

JE UNAJUA JINSI OFISI YA MBINGUNI ILIVYO?

BWANA YESU ASIFIWE, watu wengi wamekuwa wakijiuliza sana habari za mbinguni palivyo, mbinguni ipo ofisi kubwa sana ambayo katika ofisi hiyo inahusika na MUNGU BABA, ROHO MTAKATIFU na YESU WA NAZARETI katika ofisi hii. Aliponiita YESU ili nimtumikie nilifika katika ofisi hiyo na kunipa maagizo kwa ajili ya injili yake na kuukomboa ulimwengu na kumwandalia kanisa ili aje kulinyakua na mengine ni yangu peke yake.

Katika ofisi hiyo sijaona kitu kinaitwa msalaba wala mavazi yenye misalaba, wala ubani, wala mikuki, wala kofia za kuvaa kuhubiria, wala sijaona huduma ya askofu ndiye awe kiongozi wala hakuna kitabu cha injili tofauti na biblia hii takatifu peke yake. Na ilinichukua muda mpaka siku nilipokwenda kuibomoa serikali ya joka kuu nikaingia katika ofisi yake. Nilishangaa kuona katika ofisi ya joka kuu upo msalaba juu ya paa ni misalaba za dhahabu na ukubwa wake kwa urefu na upana ni kama 2 square kilomita. Akanieleza YESU pale ndipo penye siri zote za kuwaangamiza wanadamu na kuwasulubisha, hivyo hata katika ulimwengu unapoona mahali penye msalaba tayari uelewe Hebron hiyo madhehebu au jingo linaongozwa na head office ya joka kuu, hiyo ndiyo namna alivyoifanya joka kuu na kuwateka wanadamu, na niliwaita watumishi kila nilipokuwa nataka niwafunulie habari hizi walinisaliti na wengine hata sasa angalia majina yao yapok wa joka kuu tayari ni watumishi wake. Na majina niliyoyaona yalikuwepo majina ya watumishi wote maarufu katika nchi mbali mbali zote katika dunia hii 99.8% wote wapo kwa shetani na wengine wapo katika chama cha illuminati pastors, niliogopa sana sababu haikuwa ni jambo jepesi kwangu, hata mimi nilionaga msalaba na kitu kitakatifu na kinamfurahisha MUNGU, kumbe lilimfurahishaga shetani, nilitubu na kuomba rehema, na hata mlikula katika mkate kanisani kumbe mlikula laana, mauti, vifungo katika ulimwengu wa roho na kufungwa usiende mbinguni kupitia ule mkate wenye msalaba. Hilo ndilo lengo la joka kuu, sasa ufunguke na uamue. Unataka kushiriki katika kanisa lenye msalaba au kanisa lisilo na msalaba wala mavazi ya msalaba. Sababu hayapo katika ofisi ya mbinguni bali yapo katika ofisi ya joka kuu.

Zaidi fuatilia masomo yangu katika website www.prophethebron.org. Sema BWANA YESU naomba unisamehe dhambi zangu zote, naomba unisamehe na unifungue katika vifungo vya msalaba katika ulimwengu wa roho. Uniandike katika kitabu chako cha uzima wa milele. Kuanzia sasa mimi ni wa YESU WA NAZARETI na siyo wa misalaba tena katika ofisi ya joka kuu bali niwepo jina langu katika ofisi yake ya mbinguni.


NABII HEBRON.