HERI YA
KRISMASI!
MERRY
CHRISTMAS AND A HAPPY NEW YEAR 2015!
Nawasalimu watu wote wa mataifa yote kwa jina la YESU KRISTO
WA NAZARETI aliye hai. Krismasi hii iwe kweli na Krismasi ambayo utamtukuza
MUNGU kwa ajili ya kukumbuka ile siku ambayo YESU alizaliwa miaka 2000 iliyopita,
kama inavyotakwa na MUNGU na siyo miungu au mapokeo ya dini au mapokeo ya
mizimu. Kama nilivyokwisha elezea katika makala ya Nabii Hebron kuhusu father Christmas
ni nani? Na Christmas tree ni nini, na Christmas card ni nini? Wewe usome
utaelewa vizuri na endapo utashiriki na kuziweka hivi vitu nilivyovitaja basi
wewe utakuwa unashiriki Krismasi yako na mashetani na mizimu, na serikali ya kuzimu,
sababu na wao wanayo Krismasi yao na wanaye yesu wao wa uongo. Krismasi ya
kuzimu inaanza tarehe 23.12 hadi 27.12 kila mwaka na unapokuwa na hivyo vitu
basi na wewe unakuwa umeunganishwa katika krismasi ya kuzimu. Najua wengi
hamjui ila mimi ninayajua ili niwaeleze watu wote ukweli, sababu haya
yalifichika na hakuna binadamu aliyeyajua, zaidi soma katika blog www.prophethebron.blogspot.com,
uyasome hayo niliyo yaelezea hakika utafunguka.
Mwaka huu ninataka shetani asiwashirikishe watoto wa MUNGU
katika krismasi yake sababu na hao hawampendi ila hawaujui ukweli. Pia sikiliza
katika YouTube ya Prophet Hebron kuhusu masomo ya krismasi utaelewa zaidi, na
ukipiga picha katika ulimwengu wote utaona watu hawajui na ndiyo sababu
wanayapamda katika nyumba zao, makanisa, badala ya kumpamba YESU kwa kumpa
mioyo yao na kuokoka wengi wao wengi wanamtukuza shetani na masanamu pasipo
kupenda. Mfano huyu father Christmas siyo YESU wala hastahili yeye kuitwa baba
wa krismasi, wala yeye siyo baba yetu kama alivyo YESU, bali father Christmas ni
mzimu wa Saint Nicholas. Inasikitisha sana wakristo wanapigwa upofu hata
wakashindwa kuyajua haya na hii ni sababu watumishi wamemsaliti YESU siku
nyingi na YESU akakosa wa kumjulisha ili awaeleze watoto wake wapone.
Nawasihi kama unampenda YESU na unampenda MUNGU usiweke
father Christmas, Christmas tree, Christmas card, mambo haya yameanzia kuzimu
yakaletwa kwa wanadamu na unapoyashiriki tu basi na wewe unaunganishwa na
krismasi ya kuzimu. Nikuulize swali, je mbinguni wana father Christmas anayeitwa
Santa Claus? Jibu, hakuna. Mbinguni ipo siku ya kuzaliwa BABA yetu YESU peke
yake. Na pia nikuulize swali je mbinguni upo mti wa kuabudiwa? Jibu hakuna mti,
ni MUNGU peke yake ndiye anayeabudiwa, huu mti wa krismasi ndio mungu taamuzi,
mpaka hapo umenielewa. Shetani alivuruga Krismasi ya kweli akaileta ya uongo
ambayo ni ya kina Santa Claus. Sasa wewe unasherekea Santa Claus au YESU? Hapo uelewe
hayo yote ni machukizo mbele ya MUNGU na kwa shetani kwake ni furaha na
anashangilia wanadamu wanapigwa upofu wasimjue YESU wa kweli na Krismasi yake
inavyotakiwa iwe na ndiyo sababu watu wanakuw hawana baraka za kweli za
Krismasi bali wana za shetani, nuksi, balaa, mikosi, mateso, magonjwa, faraka
na mengineyo. Sasa umeijua siri hii na
usishiriki tena.
Na zaidi illuminati ndio wakati wa wao kuwaibia watu nyota
zao na vitu vyao kwa wale ambao wanashiriki vitu hivyo, na pia napenda muelewe,
joka anacho chama chake alichokianzisha. Chama hicho linaitwa illuminati. Sasa hata
katika sign za illumiati google utaona ipo picha ya father Christmas, Santa
Claus, hivyo na wewe katika ulimwengu wa roho unaunganishwa pasipokujua. Ila sasa
umtukuze YESU kwa kujua ukweli na ikuweke huru. Niliwaeleza shetani ameiteka
dunia 98%. Sasa hata kwa kupitia hii father Christmas, wewe chunguza utapata
picha na siyo ajabu na wewe ni mmoja wao au ndugu lakini ulikuwa haujui.
Jambo lingine, nawasihi muokoke ili muwe wakristo na muishi
maisha matakatifu, sababu ili uwe mkristo wa kweli ni lazima kumkiri YESU na
uokoke, sasa watu wengi wanajiita wakristo lakini hawajaokoka. Sasa kama hawajaokoka
waelewe ni wakristo jina tu siyo wakristo halisi, na YESU atakuja kuwachukua
wakristo halisi hatawachukua wakristo jina. Mkristo jina yeye ni mkristo
aliyeokoka katika giza na giza bado linamshikilia ambali ndilo shetani, bali
aliyeokoka na kuishi maisha matakatifu yeye ndiye mkristo halisi. Ila sasa
uokoke, sema:
BWANA YESU naomba unisamehe dhambi zangu zote, niandike
katika kitabu chako cha uzima niwe mkristo halisi. Natoka katika ukristo giza
nije katika nuru ambaye ndiye wewe. Amen.
NOTE:
Nawatakia wokovu watu wote wa ulimwengu, mumrejee YESU WA
NAZARETI, usishiriki krismasi kwa kupamba haya mapambo yao bali umpambe YESU
katika moyo wako na usherekee vizuri. Usimame imara katika wokovu wako ambao
ndiye nguzo ya ukristo. Zaidi mataifa yote karibuni katika kanisa la YESU NI
BWANA NA MWOKOZI WA MATAIFA YOTE, Arusha, Tanzania.
MERRY
CHRISTMAS AND A HAPPY NEW YEAR 2015.
NABII HERBON.