Pages

Wednesday, November 5, 2014

JE UNAJUA KUWA MAWIGI (WEAVE) NI NYWELE ZA SEHEMU ZA SIRI ZA MAJINI YALIYOPO KUZIMU?
ZAIDI SOMA HAPA….

BWANA YESU ASIFIWE watu wote wa mataifa yote na ambao mmeumbwa kwa mapenzi ya MUNGU na siyo shetani ila shetani hawapendi wanadamu kabisa na anataka waangamie na kuja kuchomwa naye moto kwa kumfanya mwanadamu amkosee MUNGU eiza kwa kujua mwanadamu mwenyewe au mwanadamu asijijue kuwa amemkosea MUNGU. Katika makala hii nitaelezea machache ya yale ambaye niliyaona kuzimu kwa macho yangu bila kuhadithiwa na mtu yeyote na zaidi ilikuwa ni mpango wa MUNGU mimi Hebron niende nikaone kila kitu ambacho shetani na serikali yake wanachokifanya na kwa ajili ya kuwateka wanadamu wamkosee MUNGU na wasifanikiwe sawa sawa na mpango wa MUNGU, na pia sikuonyehswa haya nije nikae kimya nilionyeshwa ili niwaeleze watu ili wapone na atakaye kaza shingo asije akamlaumu MUNGU Ufunuo Wa Yohana 3:6 (yeye aliye na sikio na asikie neno hili ambalo ayaambia makanisa, kanisa ni wewe mtu ambaye siku ya unyakuo YESU atakunyakuwa kama ukiwa umeokoka, batizwa ubatizo wa maji mengi na kuishi maisha matakatifu, ikiwa kinyume hautanyakuliwa.

Nilipofika kuzimu nilipelekwa sehemu za viwanda na viwanda vingi ambayo nilikuta kuzimu huku duniani vipo na viwanda hivyo vimeletwa ulimwenguni ili kuwadhoofisha wanadamu na kuwaharibu maisha yao, japo sasa nitaelezea kuhusu mawigi (weave) asili ya hizi nywele ya wigi, hizi nywele zinatoka kuzimu, kuna majini ambayo ni makubwa kuliko majini yote yanaitwa (GOLO) na yana manywele mengi sana, upana au unene wake ni kama mita nne kwa unene. Haya majini ndiyo yakisha nyolewa hizo nywele zao za siri ndizo zinazoletwa huku duniani kasha watu wanazivaa kichwani. Niliogopa sana na kushikwa na mshtuko na kuna salooni maarufu kuzimu ya kuwanyolea nywele za siri hawa majini hiyo salooni inaitwa YML saloon kirefu chake ni Yezebel, Makata, Lusifa. Katika hii salooni ndipo hawa majini wanaendaga kunyoa nywele zao kama vile hapa ulimwenguni watu wanapoenda salooni kunyoa nywele zao, ila tofauti hawatumii mashine ya kunyolea kama hizi ambazo watu hunyolea huku duniani wa hutumia mapanga makali sana na shoka kali kunyolea nywele zao za siri sababu ni nyingi kama kakichaka, na wakishazinyoa hizo nywele hukusanywa na hiyo salooni ya (YML) kisha zinaletwa huku duniani zinauziwa watu na wanazivaa katika vichwa, nilizidi kushtuka ila MUNGU akanitia nguvu sababu ni jambo la kutisha niliporudisha picha duniani, mamilioni ya watu wanavaa kitu wasichokijua asili yake ni nini? Na lango lake ni nini? Ndugu wasomaji ingekuwa labda ni wewe sijui ungejisikiaje japo nitaeleza kwa ufupi. Sasa unapoona haya mawigi (weave) kwanza uelewe siyo salama kwa mwanadamu, pili hizo ni nywele zilizotokea katika viungo vya siri vya majini ya kike na kiume, hivyo unapovaa ujue katika kichwa chako umevaa nywele za sehemu za siri za majini katika kichwa chako, na hata kama unafanya biashara ya kuvaa mawigi uelewe unafanya biashara ya kuuza nywele za siri za majini na hata kama unazo uelewe unazo nywele za majini katika miji yako.

MADAHARA YA KUVAA WIGI (WEAVE).

1.     Kwanza kabisa uelewe katika kichwa chako unakuwa umevaa nywele za siri za majini na pia umevaa pepo.
2.     Madhara yake unakuwa umeuzuia utukufu wa MUNGU ushuke katika kichwa chako sababu tayari upo utukufu wa shetani katika kichwa chako yamkini unavaa pasipo kujua au kwa kujua.
3.     Akili yako na maono yako yanaibiwa na shetani na kasha shetani anakuwekea yak wake pasipo wewe kujua.
4.     Mawigi yanakufanya usiweze kusimama katika wokovu.
5.     Mawigi haya yanaletwa ulimwenguni ili kuwazuia wanawake wasiende mbinguni sababu shetani anajua kabisa katika mioyo ya wanawake wengi wanampenda YESU kama vile kipindi ambacho YESU aliuwepo ilionekana wanawake ndio waliokuwa wengi na hata sasa ukiangalia idadi kubwa ya wanawake ndio wengi waliookoka kuliko wanaume. Sasa alichokifanya shetani akabuni njia hii wanadamu wavae nywele za siri za majini kwa kuwapiga upofu wasielewe (huku ndiko kutekwa na shetani). Ila YESU atakaporudi kulinyakua kanisa wale waliookoka wakiwa wamevaa mawigi, wasiweze kunyakuliwa sababu katika vichwa vyao vitakuwa vimefunikwa na nguvu za giza ambazo ndizo nywele za majini yanayoitwa (GOLO). Ashukuriwe YESU aliyenipeleka na kunionyesha haya ili niwaeleze watu mpate kupona na niliporudi katika mwili akasema na mimi Hebron nimekufunulia haya uyaone na uyajue ili  uniandalie kanisa ambalo nitalinyakua katika unyakuo wangu, tazama wanadamu wananipenda ila mwovu amewatengenezea njia ili wasifike mbinguni, uwafundishe, uwaeleze ili wapone, na hata katika unyakuo niweze kuwanyakua.
6.     Ndani yako mizimu inaishi.
7.     Mapepo yanakuwa na uhalali wa kuishi ndani yako na wachawi hukuloga kwa urahisi na kukuibia vitu vyako.
8.     Unakuwa unayo alama ya mama wa makahaba (Yezebel) sababu unavaa vitu vyake.

NOTE: vitu vyte venye asili ya kuzimu ni vitu vya shetani hivyo havikomboleki wala havitakasiki, wala havibarikiki kwa jina la YESU WA NAZARETI sababu hauwezi ukazibariki kazi za shetani kwa jina la YESU, bali kazi za shetani huharibiwa kwa jina la YESU WA NAZARETI.
9.     Humfanya mwanamke kuwa na tabia za uzinzi, asiweze kutulia katika ndoa na huwaletea ndoto za uzinzi, na kuwaibia wanawake baraka zao walizoumbwa nazo na mwenyezi MUNGU.
10.                       Kila anayevaa nywele hizi katika ulimwengu wa roho yeye ni mke wa jini pasipo kujijua na wengine hujijua, haijalishi umeokoka au haujaokoka, ukweli ndio huo.
11.                       Katika ulimwengu wa roho jina lako unaitwa kahaba, na mfano rahisi tu angalia watu wenye tabia za ukahaba katika ulimwengu wote leo hii kwa upande wa watu weusi. Hata katika street wale wanaofanya uzinzi kujiuza mwili tazama katika kichwa utaona mawigi.
12.                       Mwanawake anapokufa akazikwa na wigi tayari anajifungia asinyakuliwe katika unyakuo sababu anacho cha kuzimu na MUNGU anaangalia haki amenituma niseme ukweli ili watu wapone, sababu shetani alishaona kuwa watu waliookoka hatawapata sasa akabuni njia hii ya mawigi, nikuulize swali labda umeokoka unampenda YESU na unaishi maisha matakatifu lakini katika kichwa chako umevaa mapepo je utukufu wa MUNGU utashuka katika maisha yako? Jibu hakuna na je MUNGU atakubarikije wakati unavaa kofia ya shetani?
13.                       Na majini haya ambayo yanayotoa nywele za siri ambazo ndizo wigi, majini haya nguo za ndani wale wa kiume wanavaa boxer na majini ya kike yanavaa BIKINI. Ukubwa wa size ya kiuno ni kama mita 4 kiuno.
14.                       Ufahamu unashikiliwa na shetani na anayeongoza maisha yako na hapo ndipo unapotea na kuacha njia za MUNGU pasipo kupenda hii ni sababu moja wapo ni hizi zinazovaliwa zinatoka katika viungo vya siri ya majini.

NOTE:
Yapo madhara mengi ila zaidi pata dvd na cd kutoka kwa kanisa la YESU NI BWANA NA MWOKOZI WA MATAIFA YOTE na usome makala ya Nabii Hebron Kisamo na katika YouTube sikiliza utayapata maelekezo zaidi na utapona roho yako ukiamua na kwa njia hii shetani anaitumia kuliteka kanisa 98%. Rudisha picha angalia makanisa utaona ni mawigi yamejaa, na watu wakifikiri ndio kujiremba kumbe ni kujipa cheo cha mama wa makahaba pasipokujua au kupenda. Nimewajulisha na mataifa yote sababu YESU aliyenituma ni wa mataifa yote na siyo nchi moja au kabila moja leo amenituma nikuletee habari hii na yeye anakuangalia wewe unayeupata ujumbe huu anasema na wewe. Amua na uchukie kabisa na uzivue katika kichwa chako ili akurejeshee akili zako na afunge milango ya kuzimu katika kichwa chako, na uokoke, sema BWANA YESU naomba unisamehe dhambi zangu zote, nimeamua kutovaa tena nywele za majini, nazitoa na nitazichoma, unikomboe YESU, unifunike sasa kwa uweza wako. Nilikuzuia muda mrefu, ila karibu ndani yangu uniandike na katika kitabu chako cha uzima wa milele, uniongozee wewe nisipotee tena kuvaa vitu vya kuzimu. Amen.

NABII HEBRON.