Pages

Wednesday, November 5, 2014

JE UNAYAJUA MADAWA YA NYWELE AMBAZO ZIMETOKA KUZIMU NA ZINATUMIKA HAPA ULIMWENGUNI?
SOMA HAPA…

Kama nilivyokwisha elezea katika makala na vipindi mbali mbali ya redio na television, nasema tena wazi wazi shetani ni mpumbavu na hawapendi wanadamu wamtafute MUNGU na zaidi lengo lake ni kuyaharibu maisha ya watu peke yake yamkini unajua au haujui. Katika nchi ya kuzimu vipo viwanda vya mafuta ya nywele za wanadamu ambavyo hata mimi Hebron pasipokujuaga hapa ulimwenguni niliyapaka lakini namshukuru ROHO MTAKATIFU sana pale nilipoitwa na YESU nilipokea neema ya kubadilika na nilijikuta ghafla siyapendi mafuta ya nywele nikawa napaka mafuta ya kawaida.

Nakumbuka siku moja hata mke wangu aliniambia daddy mbona unajipaka body lotion mpaka kichwani kwani nywele si paka mafuta yake yapo na hayajaisha nikashangaa najipaka tu wala siyapaki, kumbe ROHO MTAKATIFU aliye ndani alikuwa ananiongoza, ila siku aliponipeleka YESU kuzimu na kunipa maelekezo ya kufanya nikapitishwa katika viwanda vya vipodozi, madawa ya nywele, nikaona yanavyotengenezwa na vitu vinavyowekwa huko na kasha viletwe huku duniani ili kuwaangamiza wanadamu. Mafuta haya ambayo hata mimi niliyatumiaga pasipo kujua nikakuta kule kuzimu yanachanganywa na mafuta ya mwili ya watu waliokufa na vitu vya ajabu ajabu, ila nitaelezea kwa ufupi.

a.      Mafuta yote ya curl yanatoka kuzimu na nimeyaona.
b.     Mafuta ya kuzifanya nywele ziwe nyeusi (mfano nywele za watu ni nyeupe halafu anapaka dawa zinakuwa ni nyeusi) anapopaka katika kichwa chake anayaweka mapepo na pia anauzuia utukufu wa MUNGU usishuke katika kichwa chake, na pia maisha yake yatakuwa nyeusi au yana giza siku zote, na akili zake na nyota imeibiwa na mapepo.
c.      Mafuta ya kubadilisha nywele rangi mfano zinakuwa njano, blue, nyeupe, au brown na rangi nyinginezo zote zimetoka kuzimu na madhara yake soma katika kifungu (b) yanafanana.
d.     Kwa jinsi nilivyoangalia na niliporudi ulimwenguni niliona mafuta ya nywele 95% yote ni ya kuzimu ikiwemo na vipodozi, madawa yote ya kujichubua.
e.      Mafuta ya kujifanyia scrub- mafuta ya aina yeyote ya scrub yanatoka kuzimu, unapofanyiwa na mafuta hayo, kwanza yanaondoka na uthamani wa ngozi yako na maisha yako, na kama unafanyiwa katika uso au kichwani unanyang’anywa macho ya rohoni, akili zako, sura yako, kibali chako ulichopewa na MUNGU na kuwekewa ya kipepo.
f.       Shampoo zote siyo salama, asili yake ni kuzimu. Shampoo ile nzito nzito iwe ya aina yeyote ila kule kuzimu ni makohozi ya majini yote vinavyotemewa yanahifadhiwa kisha wanayaleta kwa wanadamu wajipake, na madhara yake ni mikosi, kujipaka nuksi balaa. Na shampoo nyingine ni ile ambayo ni shampoo nyepesi, hiyo shampoo nyepesi kule kuzimu ni mbegu za kiume na kike za majini, unapoitumia huku ulimwenguni wewe binadamu unafanyika kuwa nyumba ya kuzaa majini pasipokujua, na inasababisha vijana na mabinti unakuta yeye haoi au kuolewa kumbe sababu moja wapo ni kuwa yeye ni chombo cha kuzalia majini hivyo akija mwanadamu ili watafute mtoto unakuta uzazi yaani yai lina majini vitoto, na kufanya mtu hazai kabisa katika maisha yake, na pia majini hukamata akili za wanadamu pale wanapopata mlango kisha wanawawekea kupenda vitu vyao na ukipata pesa utashangaa unaenda kuvinunua vitu vyao na kuvitumia na kwa njia hiyo, biashara ya kuzimu inayofanywa na majini ikashamiri duniani na viwanda kukua kumbe ni vya shetani vimeletwa ili kuharibu maisha ya wanadamu na ndiyo sababu watu wengi ni vigumu kumpenda MUNGU au kumfuata MUNGU ni sababu ya product za shetani wanazozitumia, watu wasingeijua siri hii naelewa hata shetani pamoja na wale wafuasi wake ambao ni wanadamu ambao wanashirikiana na shetani hawafurahi kabisa sababu waujua malengo yao yamefika mwisho na watu wa MUNGU hawatawapata tena na katika mitego hiyo YESU kaifichua siri. Sasa uamuzi ni wako wewe, pia sabuni asilimia kubwa ni makohozi ya majini, ila watu hawajui wanadanganyika na harufu za manukato yanayowekwa, ndio sababu watu nuksi na mikosi haziishi, faraka katika ndoa, magonjwa ya ngozi, sura kuharibika na mengineyo mengi ni sababu ya sabuni za kuzimu.

-       Mfano shetani akabuni njia ya kuwakamata au kuiba uthamani wa mikono yao na pesa zao, kila unapotumia hand wash kuoshea mikono hapo unaibiwa kila kitu, unabakia kulalamika pesa hazikai na hazifanyi kazi.
-       Kupiga deki na shampoo- unakuwa unaipaka makufuru nyumba yako au makohozi, mfano unamfahamu kono kono huyu ni kiumbe ambaye yeye hutumika na shetani kusambaza makufuru kwa ile njia ya kumwaga ule ute ambao ukiuangalia hauna tofauti na makohozi, kon kono akipita kwako uelewe ameacha makufuru, sasa cha ajabu watu wengine wanakula kono kono waelewe walikula makufuru au wanakula makufuru.

NOTE:
BWANA YESU namba unisamehe dhambi zangu, uniandike jina langu katika kitabu chako cha uzima simtaki kabisa shetani navikataa vipodozi vyake na mafuta yake sipaki tena unirejeshee vitu vyangu ili niwe nina vyote ulivyonipa na niishi katika utukufu siku zote za maisha yangu. Naomba ROHO MTAKATIFU anionyeshe mafuta yote ya kuzimu na vipodozi vyote nisitumie tena na nivichome, visikae tena katika nyumba yangu balaa ikanifuata sababu ni mlango. Nirejeshee uzuri wangu na sura yangu nipendeze zaidi.

Ili kuyajua mafuta yanaytokea kuzimu- yanaharufu kali na ukiona tu katika perfume ukasikia harufu ya ubani au harufu ya mchele mchele, iwe ni katika sabuni au perfume na mafuta yenye picha ya mwanamke ya curl, haya nimekufunulia uelewe yanatoka huko. ROHO MTAKATIFU akufunulieni zaidi awape macho myajue sababu ni aina nyingi hata nikiandika 100 days bila kupumzika sitayamaliza, ina maana maduka ya vipodozi 95% ni vitu vya kuzimu, hii ni katika ulimwengu wote. Hapo ndipo penye mtego kubwa wa shetani. Ila mshukuru MUNGU ambaye amekufunulia haya ili watu wapone. Sababu na MUNGU hapendi kabisa watoto wake wapake mafuta ya nyama za watu au vitu vya majini mfan makohozi, mikojo, jasho. Huduma za shetani sasa mwisho katika jina la YESU.

NABII HEBRON.